Penati nane za Rais Samia katika maslahi ya watumishi

Penati nane za Rais Samia katika maslahi ya watumishi

Nyabukika

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2022
Posts
1,440
Reaction score
1,046
Hakika, Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni! Ni ile kauli ya Mama Anaupiga Mwingi usidhani ni msemo tu, sasa hebu tazama jinsi Mama alivyoweka historia katika maslahi ya watumishi wa umma ndani ya muda mfupi tu tangu ashike hatamu.

Uchumi wa Dunia unapoyumba hakuna nchi inayobaki salama. Baada ya athari za COVID19, tayari Dunia imeingia katika suala la mgogoro wa Urusi na Ukraine. Licha ya changamoto hizi kiuchumi Rais

Rais Samia ameweza kuonyesha umahiri mkubwa kwa kufanya haya katika sekta ya utumishi wa umma;

1. Nyongeza ya mshahara kwa asilimia 23.3 kwa watumishi wote wa umma ikiwemo wa kima cha chini.

2. Kupunguza kodi(PAYE) kwa kuifikisha 8% na kupandisha kiwango cha chini cha kukatwa kodi, suala hili lilipoteza kiwango cha takribani Bilioni 14 ya fedha zilizopaswa kukusanywa na serikali.

3. Katika mifuko ya hifadhi ya jamii kupandisha kiwanga cha malipo ya mkupuo kwa kufikia asilimia 33 kutoka 25% iliyokataliwa na wadau mwaka 2018.

4. Kupandishwa madaraja WATUMISHI laki moja tisini elfu na miatano sitini na mbili~ 190,562 (Kwa wasioelewa, hii imeigharimu Serikali kiasi cha takribani TZS BILIONI 39.6).

5. Taasisi zote zenye uhitaji wa wafanyakazi kupewa vibali vya ajira mpya na kutolewa vibali kwa watumishi walioomba kubadilisha vituo na kwenda kuongeza taaluma kwa mujibu wa taratibu na sheria za utumishi wa umma.

6. Kuanzia Mwezi March 2021 hadi January 2022, Rais Samia amewezesha ulipwaji wa madeni na malimbikizo ya watumishi wa umma wapatao 65,391, madeni yenye thamani ya takribani TZS BILIONI 90.7.

7. Kuondolewa kwa mzigo wa tozo ya 6%(VALUE RETENTION FEE) kwa watumishi waliokuwa wanufaika wa mikopo ya Elimu ya juu (HESLB). Kiwango hiki cha 6% kimekuwa mzigo mzito kwa watumishi hususani vijana wanaotoka Vyuo Vikuu, Rais Samia atakumbukwa sana kwa hili.

8. Kuboreshwa kwa mazingira ya kazi ya watumishi. Hii inatupa hamasa watumishi kutoa huduma bora na kuhakikisha wananchi wanapewa wanachostahiri.

Itoshe kusema kwamba Rais Samia Suluhu Hassan ameweka rekodi ya aina yake kama Mkuu wa nchi anayejali watumishi wa umma. Tumuunge mkono tujenge nchi yetu.
 
Tuliokwishaona pay rolls za mwezi wa saba zenye asilimia 23.3% za nyongeza tunaruhusiwa kukomenti kwenye huu uzi?
 
Katiba mpya itasimamia haki za watumishi wa umma Ili wasidhulumike kama ilivyo Sasa ambapo utashi wa mtu unaamua malipo ya WATUMISHI yaweje na kwa WAKATI GANI wapande vyeo na uchawa kuwaumiza WATUMISHI kama ilivyo Sasa HIVI!!!

"Rasimu ya Warioba irudi mezani SASA iwe KATIBA MPYA!
 
Think twice vinginevyo umetoroka Milembe.

1. Miradi mikubwa haikamiliki mfano bwawa la Nyerere, daraja la Busisi, SGR

2. Gharama za maisha kupaa

3. Watu wa kawaida wanafaidikaje

4....
20220715_201048.jpg
 
Ongezea,
1. Machinga kutimuliwa na mamalishe kuporwa wali
2 . Diesel kupanda kutoka 1250 hadi 3390
3. Bei ya nguzo ya umeme kutoka elfu 27 hadi elfu 570
4. Mchele kutoka 950 kwa kilo hadi 2400
5. Watoto kutumia laki tano kujiunga form five
6. Bei ya pamba kushuka kutoka 2700 hadi 1800 kwa kilo
7. Nyumba za nyasi kupewa majiko hatarishi ya gesi ya LPG
8. Kubambikwa kesi wana ccm kama Sabaya na Makonda
9. Kulala chumba cha milioni 65 kwa siku kwa wiki mbili
10. Kuchezewa kwa mfumo wa kutoza ushuru
11. Kutozwa elfu mbili kwa kumtumia bibi elfu tano
12. Gari jipya Kutozwa kodi sawa na chakavu
13. Nauli ya China mil 11 huku walijua mahemezi yako China
14. Mkandarasi aliye shinda kujenga ofisi ya wilaya ya Magu kupewa kujenga SGR
15. Niongeze?
 
Think twice vinginevyo umetoroka Milembe.

1.Miradi mikubwa haikamiliki mfano bwawa la Nyerere, daraja la Busisi, SGR

2.Gharama za maisha kupaa

3.Watu wa kawaida wanafaidikaje

4....View attachment 2293331
Hiyo miradi mikubwa kama inaathiri maslahi yetu Watumishi bora isikamilike tu.

Nakumbuka Magufuli alituchana live Mei Mosi Iringa kuwa eti hawezi kutuongeza mishahara kisa stiglaz goji sijui.

Mama piga chini hayo mamiradi watakuja kujenga wajukuu zetu, kwani hata kina Nyerere wenyewe walishindwa
 
Hiyo miradi mikubwa kama inaathiri maslahi yetu Watumishi bora isikamilike tu.

Nakumbuka Magufuli alituchana live Mei Mosi Iringa kuwa eti hawezi kutuongeza mishahara kisa stiglaz goji sijui.
Mama piga chini hayo mamiradi watakuja kujenga wajukuu zetu, kwani ht kina Nyerere wenyewe walishindwa
Aliigeuza Tanzania kuwa Ethiopia iliyo karibu na Zambia.Ujeuri wa madaraka wakati mwingine hugeuka kuwa uwendawazimu. 😂😂😂😂
 
Hakika, Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni! Ni ile kauli ya #MamaAnaupigaMwingi usidhani ni msemo tu, sasa hebu tazama jinsi Mama alivyoweka historia katika maslahi ya watumishi wa umma ndani ya muda mfupi tu tangu ashike hatamu.

Uchumi wa Dunia unapoyumba hakuna nchi inayobaki salama. Baada ya athari za COVID19, tayari Dunia imeingia katika suala la mgogoro wa Urusi na Ukraine. Licha ya changamoto hizi kiuchumi Rais

Rais Samia ameweza kuonyesha umahiri mkubwa kwa kufanya haya katika sekta ya utumishi wa umma;
1. Nyongeza ya mshahara kwa asilimia 23.3 kwa watumishi wote wa umma ikiwemo wa kima cha chini.

2. Kupunguza kodi(PAYE) kwa kuifikisha 8% na kupandisha kiwango cha chini cha kukatwa kodi,
suala hili lilipoteza kiwango cha takribani Bilioni 14 ya fedha zilizopaswa kukusanywa na serikali.

3. Katika mifuko ya hifadhi ya jamii kupandisha kiwanga cha malipo ya mkupuo kwa kufikia asilimia 33 kutoka 25% iliyokataliwa na wadau mwaka 2018.

4. Kupandishwa madaraja WATUMISHI laki moja tisini elfu na miatano sitini na mbili~ 190,562 (Kwa wasioelewa, hii imeigharimu Serikali kiasi cha takribani TZS BILIONI 39.6).

5. Taasisi zote zenye uhitaji wa wafanyakazi kupewa vibali vya ajira mpya na kutolewa vibali kwa watumishi walioomba kubadilisha vituo na kwenda kuongeza taaluma kwa mujibu wa taratibu na sheria za utumishi wa umma.

6. Kuanzia Mwezi March 2021 hadi January 2022, Rais Samia amewezesha ulipwaji wa madeni na malimbikizo ya watumishi wa umma wapatao 65,391, madeni yenye thamani ya takribani TZS BILIONI 90.7.

7. Kuondolewa kwa mzigo wa tozo ya 6%(VALUE RETENTION FEE) kwa watumishi waliokuwa wanufaika wa mikopo ya Elimu ya juu (HESLB). Kiwango hiki cha 6% kimekuwa mzigo mzito kwa watumishi hususani vijana wanaotoka Vyuo Vikuu, Rais Samia atakumbukwa sana kwa hili.

8. Kuboreshwa kwa mazingira ya kazi ya watumishi. Hii inatupa hamasa watumishi kutoa huduma bora na kuhakikisha wananchi wanapewa wanachostahiri.

Itoshe kusema kwamba Rais Samia Suluhu Hassan ameweka rekodi ya aina yake kama Mkuu wa nchi anayejali watumishi wa umma. Tumuunge mkono tujenge nchi yetu.
Hiyo namba 3 mwambie arudishe kile kikokotoo cha zamani. Kamwe asifikirie watumishi wa serikali ni mambumbumbu! Wanamuangalia tu kwa jicho kali la husda. Atambue pia hana haki ya kuwapangia watu wazima, matumizi ya fedha zao walizokatwa kwenye mishahara yao kwa miaka lukuki kupitia mifuko ya hifadhi ya jamii.

Na kama anaona ana huruma sana na watumishi wa umma, basi huruma hizo hizo zihamie pia kwa Wabunge! Nao wapewe 33% baada ya kumaliza utumishi wao pale bungeni! Badala ya kupewa milioni zaidi ya 250 kila baada ya miaka 5!
 
Back
Top Bottom