Pendekezo: Itungwe sheria ya upimaji wa DNA kwa mtoto. Sheria iwe lazima pindi tu mtoto anapozaliwa

Endelea kuficha hivyo hivyo ila siku ukibainika, ukipona sana ni kuivunja familia yako, yaani hayo yatakuwa ni madhara yenye haueni kwako.
Weeeh tumewaheshimisha kwa kuwapa watoto halafu bado mnatusimanga! Mara paaap DNA imekosewa, ya Khamis kapewa Juma! Msitafute matatizo nyie viumbe, leeni watoto wenu.
 
Mmeamua kumtesa shemeji yenu kisakolojia!!
 
Siyo kwamba mtoto hakuhusu,mtoto anakuhusu sana hata ukitaka maji ya kunywa unaweza mtuma si umemlea mwenyewe, sema DNA inakuonesha hiyo siyo damu yako yaani huyo mtoto hajatoka kiunoni mwako! Hayo sijui ya majina ya mtoto DNA hayamuhusu,DNA yeye ana deal na damu kwa damu,tena DNA huwa hataki kabisa hata kujua majina ya wahusika,maana inaweza leta conflict of interest!!
 
Maboresho hayo ni mazuri ila sasa kile kipengere cha kwamba mwanaume au baba wa mtoto anaapishwa mahakamani ETI KWAMBA HATA KAMA MTOTO ATAJULIKANA SIO WANGU BASI NITAMUHUDUMIA MAHITAJI YAKE YOTE.
Hiki kipengele kimetubana na hata umekosekana umuhimu wa PARTENITY TEST
 
Mantiki nzima ya hii comment yako ni nini hasa? maana nimesoma mara mbili mbili kujua ulichokusudia kulenga lakini nimetoka kapa..

Kuhusu suala la mtoto kutokukuhusu pale mama mtoto anapoamua Hilo linawezekana sana na huna la kufanya...

Yaani unaambiwa kabisa "huyu mtoto baba yake ni Fulani Wala sio wewe, na kwanzia sasa nampeleka kwa baba yake wa kumzaa sitaki aendelee kuteseka kwenye mikono yako(na hapo unakuta hujawahi hata kumtesa), na kweli anaenda wewe unabaki unalia tu hapo huku ukiigusa psychological trauma...

Endelea kujidanganya kwamba eti kwa sababu umemlea basi wewe ndio utakuwa na mamlaka naye siku zote....
 
Tunatakiwa kuwasanua madogo sasa hivi
Utakuwa tagged kama adui mkubwa wa jamii kwanzia kwa hao madogo mpaka kwa mishangazi kwamba unawaharibia vijana wao wa kiume kwa kuwafundisha "toxic masculinity"

Wewe acha tuendelee kuushudia tu jamii ikitengeneza kizazi Cha wanaume wanaokuja kuwa watumwa wa wanawake na watakaoteswa na wanawake mpaka basi...
 
Naunga mkono hoja. Na nikikuta nimechomekewa naomba gharama zangu zote zirudi, siui mtu wala nini!
 
Ni vyema sana sana kukaa kimachale, kwa sisi tuliotendwa vibaya na ndoa, mioyo yetu ipo na status ya “auto pilot” yani hata usipodhamiria, inamwangalia mwanamke kwa Machame!
Mkuu kama ulitendwa na Mwanamke kwa kubambikiziwa mtoto, basi kaa ukijua kwa asilimia kubwa na wwe una mtoto wako wa damu sehemu kapewa mwanaume mwingine anamlea bila kujua kama wake! Ni swala la muda tu mtakutana, wwe mshukuru Mungu kwa kila jambo!!
 
kabisa mkuu tena huduma itolewe bure ili iwe haki kwa wote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…