Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi (kwamba Katiba Mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi) siyo msimamo wa Kanisa Katoliki

Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi (kwamba Katiba Mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi) siyo msimamo wa Kanisa Katoliki

Pengo alisema kuwa maoni ya Askofu yule wa Karagwe ni maoni yake binafsi lakini hata yeye akashindwa kuwa mkweli kuwa 'katiba kutokuwa kipaumbele', ni maoni yake binafsi kama Pengo, na siyo ya Catholic Church. Pengo siyo msemaji wa Kanisa Katoliki. Msemaji wa Kanisa Katoliki Tanzania ni Mwenyekiti wa Baraza la maaskofu.

Pengo kama kadinali, ni mjumbe wa Baraza la Papa kule Vatican. Kwa hapa nafasi yake ni Askofu Mkuu sawa na maaskofu wakuu wengine.
 
Wewe unalijua Kanisa Katoliki kuliko Kardinali Pengo ambaye anakaa meza moja na Papa? Pengo ana kiti chake Roma kwenye Meza moja na Papa, Pengo anaweza kuongea na Papa kwa Simu, wewe takataka unaweza kumpigia nani Simu hata akapokea?
Kwa hiyo sifa ya unafiki Vatican kwa papa inakubalika? Kwani Niwemugizi sio Askofu wa Katoliki? Tena Niwemugizi ni Makamu Mwenyekiti wa TEC, kwa hiyo ukizungumzia Kanisa Katoliki Tanzania TEC ndio hasa wenyewe sio Pengo wala Papa. Usipindishe hoja tafadhali.

Vv
 
Acha ubabaishaji bwana kama Wewe ni RC FAKE

Mimi nimezaliwa mkatoliki, baba, mama na ndugu zangu wote ni RC

Lakini kwa hiii tabia ya Pengo kulinajisi kanisa...hapa mzee hafai na Mungu amuadhibu kwa kadri ya matendo yake maovu.

Mnataka kila mtu awe mropokaji ndani ya kanisa kama walivyo viongozi wa cdm? Wewe sio mkatoriki, ungeyajua haya.
 
Hivi swala la katiba halipo kwenye ilani ya ccm? Kama lipo kwanini lisipewe kipaumbele? Na kama halipo ccm haioni kuwa imechezea pesa za watanzania kwa kina Warioba kukusanya maoni yetu sisi wananchi? Na kama katiba mpya haitakuwepo kwa sababu ya maslahi ya ccm. Je si ni dharau kwa wananchi? Nauliza tu jamani!
 
Kardinali sio askofu wa kawaida. Ujue kwanza ni askofu wa Raisi wa nchi. Magufuli askofu wake ni pengo
.pili kardinali ana Siri za kanisa katoliki za dunia nzima na za Vatican ambazo askofu mwingine wa kawaida Hana sababu ni mjumbe wa vikao vizito vya Vatican ambavyo husimamia Mambo Ya kanisa. Pengo ni mtu wa Karibu na Papa. Magufuli akitaka kitu cha kumwambia Papa anaongea na pengo ambaye ni mtu wa karibu na Papa akamwambie hawezi kuongea na Niwemugizi ambaye mwisho wake ngara
Rais akitaka kuongea na Papa anawasiliana na Balozi wa Vatican hapa Tanzania,sio Pengo
 
Wakuu natanguliza salamu .

Maelekezo makuu ya Mungu kwa wanadamu ni kuishi katika kweli iliyojaa haki tupu , kutenda mema na kukataa maovu , hivyo tunategemea kiongozi yeyote wa dini ya kweli aishi na atende kama Mungu alivyoelekeza .

Kardinali Pengo anatenda kinyume na Maagizo haya ya Mungu , ni wazi ameamua kujipambanua kuukumbatia unafiki , Amejipachika usemaji wa Kanisa kinyume cha utaratibu .

Ni vema sasa Kwa kulinda heshima yake lililojiwekea miaka mingi , kanisa Katoliki linapaswa KUMTIMUA kardinali Pengo ili akaendeleze harakati zake za kupinga katiba mpya ndani ya chama chake cha ccm .

Naomba kuwasilisha .
Bavicha mnahitaji kuwa Na daktari wa akili.
 
Wakuu natanguliza salamu .

Maelekezo makuu ya Mungu kwa wanadamu ni kuishi katika kweli iliyojaa haki tupu , kutenda mema na kukataa maovu , hivyo tunategemea kiongozi yeyote wa dini ya kweli aishi na atende kama Mungu alivyoelekeza .

Kardinali Pengo anatenda kinyume na Maagizo haya ya Mungu , ni wazi ameamua kujipambanua kuukumbatia unafiki , Amejipachika usemaji wa Kanisa kinyume cha utaratibu .

Ni vema sasa Kwa kulinda heshima yake lililojiwekea miaka mingi , kanisa Katoliki linapaswa KUMTIMUA kardinali Pengo ili akaendeleze harakati zake za kupinga katiba mpya ndani ya chama chake cha ccm .

Naomba kuwasilisha .
Tatizo la kardinal pengo ni mahaba yake na ccm,inaana pengo angekuwa yeye ni nyerere asingeruhusu mfumo wa vyama vyingi,kwa kisingizio cha kuwa sio kipaumbele cha wananchi?
 
Utakufa unawaza hivyo!Vi vyama vya kijinga km VYENU laiti ningekuwa magu...vingeishia....pamoja na watu wake!Upuuzi tupu!Na mtakufa bila kushika dola!
Magufuli hata kama akiamua vipi hawezi abadani kufuta mfumo wa vyama vyingi,labda vyama vimfute yeye
 
esitena tetena,

Kwani muadam kadinali naomba nikukumbushe kuwa KATIBA kwa SERIKALI ni kama ilivyo BIBLIA. kwa KANISA.

Leo hii mtu akikuambia kuwa BIBLIA sio muhimu kwa kanisa bali kilicho muhimu ni HUDUMA bila shaka utamuona ni mwendawazimu
 
Wakuu natanguliza salamu .

Maelekezo makuu ya Mungu kwa wanadamu ni kuishi katika kweli iliyojaa haki tupu , kutenda mema na kukataa maovu , hivyo tunategemea kiongozi yeyote wa dini ya kweli aishi na atende kama Mungu alivyoelekeza .

Kardinali Pengo anatenda kinyume na Maagizo haya ya Mungu , ni wazi ameamua kujipambanua kuukumbatia unafiki , Amejipachika usemaji wa Kanisa kinyume cha utaratibu .

Ni vema sasa Kwa kulinda heshima yake lililojiwekea miaka mingi , kanisa Katoliki linapaswa KUMTIMUA kardinali Pengo ili akaendeleze harakati zake za kupinga katiba mpya ndani ya chama chake cha ccm .

Naomba kuwasilisha .
Mkuu ungeelewa kardinali anapatikana vipi usingeandika upuuzi kama huu uliouandika.

Ungeelewa heshima yake kidini usingejisumbua kuandika mambo ambayo huyafahamu.

Kardinali sio mtu mdogo sana kama unavyodhani, kama mnavyoongea mkiwa kijiweni kwenu.
 
Back
Top Bottom