Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi (kwamba Katiba Mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi) siyo msimamo wa Kanisa Katoliki

Hamjamuelewa Pengo. Kasisitiza kuwa kuna utaratibu wa kanisa kuhusu kutoa matamko ya kisiasa. Sasa wapinga kila kitu wanakuja na mipash yao. Kwani pengo kasosea wapi? kwani Pengo kasema hataki katiba mpya?
Yale ni maoni binafsi kwani alisema ni ya Kanisa?
 
Sioni hoja yako ni ipi hasa. Potelea mbali, iwe vyovyote vile iwavyo: huyu pengor afahamishwe kwamba yeye kama mchungaji mkuu wa kanisa la Tanzania anayo kura yake kwenye uchaguzi wa Papa. Na huko Roma yeye kweli ndiye mwenye veto ya kuamua (kuunga mkono, kupinga, kuhoji, etc) chochote kwa niaba ya Tz

1. Hapa kwetu yeye kazi yake ni kukemea dhambi (uovu) na kuwaongoza waamini kwenye toba. Full stop.

2. Sio kazi yake kuongoza kanisa lijadili hoja ipi ya kijamii na ipi isipewe umuhimu. Hana sifa hiyo kwasababu hawezi na alidhathibitisha kushindwa na alishukiwa vikali (rejea kauli "kala Maharage ya wapi").
 
Huyu askufu wangu ananiabisha ila tumsamehe kwani afya yake ina mgogoro na amebakisha miaka michache astaafu tutue zigo hili
 
Uingereza haijawahi kuwa na katiba na haina mpango wa kuwa na katiba lakini ni nchi iliyoendelea.Katiba sio kipaumbele cha maendeleo
Umenichokoza kwny field yng ewe mwanalumumba usiye na upeo, kwanza usidhani katiba ni kitabu, katiba ni makubaliano ya watawala na watawaliwa jinsi ya kuendesha taifa. Uingereza wana katiba na katiba yao inakuwa categorized kama "UNCODIFIED CONSTITUTION" aina ya katiba hii huwa inafuata mila na desturi za maamuz ya nchi yao tangu miaka ya zaman. Yan kama walipanga uchaguz uwe baada ya miaka minne bas wataifuata sheria hiyo miaka yote.

Kihistoria uingereza iliwah kuwa na katiba ya kuandikwa kama ss miaka ya 1215 ikijulikana kama "MAGNA CARTA" na pia mwaka 1717 walikua na kitu kinaitwa TREATY OF UNION. Waingereza huwa wanatumia busara kama hizo kufanya maamuz yao ya kikatiba, siku nyingine usithubutu kuongea uongo kwny jukwaa lililosheheni manguli wa kila kitu.
 
Kwani alisema ndio msimamo wa kanisa au mahitaji ya wananchi!!
 
Huo ukatoliki umeingia lini mjahidina wewe
 
Automata, mkuu mimi ni Mkatoliki na nitafia kwenye Ukatoliki,Tatizo kubwa nalo liona Pengo sio rais wa TEC,hata kuna kipindi alijitokeza hadharani baada ya mjadala wa mahakama ya Kadhi,na kutoa msimamo wake kama yeye,nashangaa yeye leo anamkandia Niwemugizi aliyetoa mawazo yake binafsi na si kuhusisha baraza la TEC, Pengo amekuwa na misimamo yake nje ya TEC kitu kinachochanganya Waamini wa kanisa.
 
Kinchowaua watoto ni nini kama sio utekelezaji mbovu wa Sera ambazo zinatekelezwa bila kuthibitiwa na taratibu ikiwemo katiba!!
 
Pamoja na kujaza maneno ya kuokoteza ya kilatini na kiingereza uliyoweka conclusion ni kuwa Uingereza haina katiba. Hayo mengine umejaza porojo zenye maneno ya kilatini na kiingereza
 
Mkuu nadhani kunawatu humu wanafanya makusuditu kupost mambo ambayo unaweza kuita ni kama ya kitoto kwa makusudi.

llimraditu aonekane amepinga kitu bilakujali hata anachopinga ninini.

We have long way to go.
 
Kwani Askofu Niwemugizi alisema ni msimamo wa kanisa?
 
Pamoja na kujaza maneno ya kukoteza ya Kilatini na Kiingereza uliyoweka conclusion ni kuwa Uingereza haina katiba. Hayo mengine umejaza porojo zenye maneno ya Kilatini na Kiingereza

Wanalumumba wengi mlikimbia umande, ndo mana mm mtaalam nlianza kwa kudadavua kuwa katiba sio kitabu, Uingereza hawana kitabu kimoja kinachoitwa katiba kama sisi ila wana sheria zinazoongoza maamuzi ya kikatiba, kitaalam tunaita "CONSTITUTIONAL STATUTES"

Mfano wa hizo constitutional statutes ni "THE ACT OF HUMAN RIGHTS ya mwaka 1998 na THE FREEDOM OF INFORMATION ACT ya mwaka 2000. Vitu kama hivyo kwa Tanzania vimewekwa katika katiba moja huku kwa wenzetu ni sheria zinazojitegemea

Nafurahi kukunyanyasa kwny huu ulimwengu wa kitaaluma ww mwanalumumba uliekimbia umande
 
Pengo yuko sahihi, Msimamo wa kanisa katoriki unatolewa na baraza la maaskofu hii ni kauli ya pili kuitoa aliitoa wakati ule askofu Kilaini aliposema Kikwete ni chaguo la Mungu wakosoaji wameangalia kwa mtazamo binafsi badala ya uhalisia
 
Pengo na masheikh wa Bakwata wote wanajulikana kutumiwa na serikali. Sasa kama kachukia basi amfute huyo askofu.
 
Pengo yuko sahihi, Msimamo wa kanisa katoriki unatolewa na baraza la maaskofu hii ni kauli ya pili kuitoa aliitoa wakati ule askofu Kilaini aliposema Kikwete ni chaguo la Mungu wakosoaji wameangalia kwa mtazamo binafsi badala ya uhalisia
Hawajui protocol kuwa alichoongea askofu niwemugizi hata kijimbo anakoongoza tamko lile halitambuliki sababu hakuna kikao cha jimbo cha kanisa kilichokaa na kumpa go ahead ya kusema alichosema. Niwemugizi ajiandae kuhamishiwa Vatican
 
Msimamo wa kanisa hutolewa mara baada ya Baraza la maaskofu kuketi,so wote hao kila mmoja ametoa maano yake binafsi.
Na kwa inshu ya ukubwa sijaelewa unamaanisha nini kwani kwa mujibu wa kanisa daraja ni la upadri tu hivyo vingine ni vyeo tu vinavyowekwa ili kuwepo kwa usimamizi na kardinali ndio msemaji wa mwisho wa kanisa ktk inchi husika so acha kupotosha watu.
 
Bora mwakani aondoke zake anazingua sana huyu siku hizi. Huyu ndo kamfanya mfalme kuwa hakanyiki maana ndiye aliye mwambia ni heri mmoja apotee kuliko wengi wapotee ilihali anajua fika ubovu wa katiba tuliyo nayo.Mmoja wa kupotea hawawezi isha maadam tunafikiria kwa kutumia vichwa.

Apumzike imetosha sasa ipo siku atamshauri vya ajabu zaidi pasi na kutegemea. Pia ni ujinga kutaka kizazi cha sasa kiishi ujinga wa kizazi cha zamani. Ukitaka kujua amechoka kufikiri;hata kama jpm atafanya vizuri kiasi gani kama hakuna katiba inayoweza kudumisha ulichofanya ni kujilisha upepo.Kwa katiba yetu kila rais anajifanyia na kuchukua mwelekeo anaoutaka.Bila kuwa na katiba madhubuti tutacheza mchezo wa kitoto au kazi ya ujinga hauishi.

Pengo lazima ajue,kizazi cha sasa kina wajibu wa kuandalia mazingira bora ya kuishi kizazi kijacho. Wao walitumia muda mrefu wa wakati wao kujijenga binafsi mpaka wakafika walipo fika leo anapopinga nchi kuchukua mwelekeo mpya kwa kigezo cha huduma za jamii anapotosha maana ya kuwa na katiba mpya.Kwani hata hii tunayo na huduma ni nusu mfu. Hivyo hoja yake haina mashiko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…