Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi (kwamba Katiba Mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi) siyo msimamo wa Kanisa Katoliki

Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi (kwamba Katiba Mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi) siyo msimamo wa Kanisa Katoliki

Mhashamu Askofu Kardinali Pengo amesema kuwa kauli iliyotolewa na askofu Niwemugizi kuwa katiba mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi sio msimamo wa kanisa kwa sababu kanisa lina taratibu zake za kuishauri serikali au kuzungumzia masuala ya jamii.

Pia amesema kwake yeye katiba ni kitu kije baadaye si cha haraka.

chanzo: gazeti la Mwananchi via facebook.
Huyu mzee ana mahaba na JPM na msimamo wake umekuwa wazi tangu kampeni za urais hadi sasa. Sasa anataka awape maneno ya kusema maaskofu wenzake. Hata hivyo na yeye aliyoyasema, kama kweli kayasema, ni maoni yake na si ya kanisa.
 
Kwa mujibu wa taratibu za kanisa katoliki,askofu pengo sio msemaji wa kanisa,Msemaji ni Rais wa Baraza la maaskofu Tanzania,

Rais wa Baraza la Maaskofu ndio Bosi wa Maaskofu wote nchini na hata askofu pengo anakuwa yuko chini yake, pia kama askofu pengo hakiutumwa na Rais wa Baraza la Maaskofu,na yeye pia hana mamlaka ya kulisemea kanisa katoliki na alichosema ni maoni yake


Ukadinali wake ni kwa ajili ya kupiga kura kumchagua Papa tu,ila yeye akiwa Tanzania kicheo ni Askofu wa Jimbo la Dar es Salaam,anataka watu waone kwamba Ukadinali ndio Ukubwa wa kanisa,Mkubwa wa kanisa ni Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania,na ni askofu wa Iringa Askofu Ngalalekumtwa na anayefatia kwa Cheo ni huyo Niwemugizi, Pengo yuko chini yake Rais wa Baraza

"first among equals" Pengo hamzidi Askofu yeyote kwa cheo,ni sawa na rafiki yangu sheikh mkuu wa mkoa wa Dar ajione mkubwa kuliko mashehe wa mikoa mingine
Kiukweli huyu jamaa nilitokea kumchukia Sana, ni Kati ya viongozi WA kanisa wanaosababisha nisiende kanisani siku hizi, nikiamini ni wapiga dili tu.
 
Hivi wewe bwanamdogo unasimamia nini hasa ?
Najiuliza hivi huyu Yehodaya ni muumini wa dini yeyote? kama ndio, ni dini ipi hiyo ambayo miongozo yake inaruhusu waumini wake kufanya hiki anachokishauri huyu member hapa kwenye hizi comment zake hapo chini, kwenye hiyo thread inayomuhusu mh Lissu?

YEHODAYA said:
Waziri huwa anasaini mikataba ya tender iwe ya ujenzi au yoyote? Magufuli Kill these idiots

YEHODAYA said:
Usijali hata the hague wanipeleke kichwa cha lisu kikikatwa I don't mind najitoa muhanga heri mtu moja afe Kuliko taifa liangamie magufuli Kill lisu ruksa kunisingizia Mimi. Taifa ni LA muhimu kuendelea kuwepo kuliko kichwa cha Lisu Kill him now if you can.

Tundu Lissu: Aliyevunja Mkataba wa ESCEL ni rais Magufuli
 
Huyu mzee ni mnafiki sana shida yake ni udini tu kipindi ambacho ikulu inakuwa na viongozi wa dini nyengine.
 
Mhashamu Askofu Kardinali Pengo amesema kuwa kauli iliyotolewa na askofu Niwemugizi kuwa katiba mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi sio msimamo wa kanisa kwa sababu kanisa lina taratibu zake za kuishauri serikali au kuzungumzia masuala ya jamii.

Pia amesema kwake yeye katiba ni kitu kije baadaye si cha haraka.

chanzo: gazeti la Mwananchi via facebook.

Askofu Niwemugizi alitoa mawazo yake kama yeye na siyo kama TEC na it was crystal clear. Sasa Kardinali Pengo anaposema alichosema siyo msimamo wa Kanisa Katoliki ana maana gani au hakuwahi kusikia alichosema Askofu Niwemugizi? Otherwise, ninachoona ni kama kuna mgawanyiko wa kifikra kwenye TEC kati ya wale wanaotaka Katiba Mpya na wale ambao wanaridhika na Katiba ya 1977 na hawaoni umuhimu wa kuwa na Katiba Mpya. Kama hii ni kweli tafsiri yake ni kwamba TEC inaweza kuwa katika mgawanyiko kati ya maaskofu ambao ni "conservative" na "progressive".
 
Thread closed...wanaomshambulia mkuu pengo wasome hapa...

Siyo kweli. Askofu alionyesha kabisa yalikuwa mawazo yake labda kama kila anachosema askofu huwa ni tamko la TEC au jimbo lake kitu ambacho siyo kweli pia.
 
Mhashamu Askofu Kardinali Pengo amesema kuwa kauli iliyotolewa na askofu Niwemugizi kuwa katiba mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi sio msimamo wa kanisa kwa sababu kanisa lina taratibu zake za kuishauri serikali au kuzungumzia masuala ya jamii.

Pia amesema kwake yeye katiba ni kitu kije baadaye si cha haraka.

chanzo: gazeti la Mwananchi via facebook.
Nafikiri, hata hicho alichosema yeye kwamba Katiba IJE BAADAE nao usiwe msimamo wa RC,bali msimamo wake binafsi
 
Hamjamuelewa Pengo. Kasisitiza kuwa kuna utaratibu wa kanisa kuhusu kutoa matamko ya kisiasa. Sasa wapinga kila kitu wanakuja na mipash yao. Kwani pengo kasosea wapi? kwani Pengo kasema hataki katiba mpya?
Awe Pengo awe mwanya katiba kwanza
 
Swali kwa kadinali je katiba na bombadia kipi kinafanya watu wafe njaa na kukosa elimu? Kipi ni cha muhimu zaidi?
 
Hamjamuelewa Pengo. Kasisitiza kuwa kuna utaratibu wa kanisa kuhusu kutoa matamko ya kisiasa. Sasa wapinga kila kitu wanakuja na mipash yao. Kwani pengo kasosea wapi? kwani Pengo kasema hataki katiba mpya?
Dragoon, nafahamu misimamo na itikadi zako kuhusu siasa zetu na sishangai kwa ulichosema.

Kadinali Pengo amezungumzia hili kama nani? Ask.Niwemugizi alikuwa wazi kwa kusema 'haya ni maoni yangu binafsi, sio ya Kanisa', wananchi na vyombo vya habari tulimwelewa vizuri.

Sasa shangaa, Pengo anaibukia wapi kwa suala ambalo halijaleta mkanganyiko wowote. Kama maoni ya Ask. Niwemugizi yangekuwa yameleta mkanganyo Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) kupitia Katibu wake au Rais wake Askofu Ngalalekumtwa wangekuwa wameshalitolea ufafanuzi. Sasa Pengo anaibuka ghafla na anapata mwanya wa kupenyeza maoni yake! Ningemwelewa Ask. Pengo kama angetoa maoni yake binafsi kuhusu Katiba mpya bila kuzungumzia hoja ya Ask. Niwemugizi.

Vv
 
Askofu Niwemugizi alitoa mawazo yake kama yeye na siyo kama TEC na it was crystal clear. Sasa Kardinali Pengo anaposema alichosema siyo msimamo wa Kanisa Katoliki ana maana gani au hakuwahi kusikia alichosema Askofu Niwemugizi? Otherwise, ninachoona ni kama kuna mgawanyiko wa kifikra kwenye TEC kati ya wale wanaotaka Katiba Mpya na wale ambao wanaridhika na Katiba ya 1977 na hawaoni umuhimu wa kuwa na Katiba Mpya. Kama hii ni kweli tafsiri yake ni kwamba TEC inaweza kuwa katika mgawanyiko kati ya maaskofu ambao ni "conservative" na "progressive".
Na iko ndo kinaonekana wazi kabisa
 
Mhashamu Askofu Kardinali Pengo amesema kuwa kauli iliyotolewa na askofu Niwemugizi kuwa katiba mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi sio msimamo wa kanisa kwa sababu kanisa lina taratibu zake za kuishauri serikali au kuzungumzia masuala ya jamii.

Pia amesema kwake yeye katiba ni kitu kije baadaye si cha haraka.

chanzo: gazeti la Mwananchi via facebook.
Na majibu ya pengo siyo ya kanisa pia
 
Hakika.Maana niliuliza hapa mtu akivunja katiba nini kinafuata?Hakuna aliyejibu.Kama iliyopo tu inavunjwa na ni kawaida wala anayevunja hashtuki,hata ikiwekwa katiba gani haitasaidia kitu.
Ndio maana tunataka katiba ili akivunja achukuliwe hatua sahivi rais yuko juu ya katiba
 
Kwa mujibu wa taratibu za kanisa katoliki,askofu pengo sio msemaji wa kanisa,Msemaji ni Rais wa Baraza la maaskofu Tanzania,

Rais wa Baraza la Maaskofu ndio Bosi wa Maaskofu wote nchini na hata askofu pengo anakuwa yuko chini yake, pia kama askofu pengo hakiutumwa na Rais wa Baraza la Maaskofu,na yeye pia hana mamlaka ya kulisemea kanisa katoliki na alichosema ni maoni yake


Ukadinali wake ni kwa ajili ya kupiga kura kumchagua Papa tu,ila yeye akiwa Tanzania kicheo ni Askofu wa Jimbo la Dar es Salaam,anataka watu waone kwamba Ukadinali ndio Ukubwa wa kanisa,Mkubwa wa kanisa ni Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania,na ni askofu wa Iringa Askofu Ngalalekumtwa na anayefatia kwa Cheo ni huyo Niwemugizi, Pengo yuko chini yake Rais wa Baraza

"first among equals" Pengo hamzidi Askofu yeyote kwa cheo,ni sawa na rafiki yangu sheikh mkuu wa mkoa wa Dar ajione mkubwa kuliko mashehe wa mikoa mingine
Ni sawa na makonda anavyo jiona kuwa yeye ndo Maui wa wakuu wa mikoa yote tanzania
 
Uingereza haijawahi kuwa na katiba na haina mpango wa kuwa na katiba lakini ni nchi iliyoendelea.Katiba sio kipaumbele cha maendeleo
Umewahi kuona uingereza video ya rushwa inasambaa na mty bado anateuliwa kuwa kiongozi kwenye chama?
 
Nafikiri,hata hicho alichosema yeye kwamba Katiba IJE BAADAE nao usiwe msimamo wa RC,bali msimamo wake binafsi

Kama yeye anaweza kusema hivyo, kwa nini wengine wakitoa mawazo yao binafsi anaibuka ibuka?
 
Kwa ufupi


Kutokana na nafasi ya Uaskofu aliyonayo Askofu Niwemugizi, kauli yake inaweza kutafsiriwa kuwa ndio msimamo wa Kanisa Katoliki au wa Jimbo la Rulenge, Ngara



Dar es Salaam. Mwadhama Kadinali, Polycarp Pengo amesema kwamba kauli iliyotolewa hivi karibuni na Askofu wa Jimbo la Rulenge mkoani Kagera, Severine Niwemugizi kwamba Katiba mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi ni maoni binafsi siyo msimamo wa Kanisa Katoliki nchini.

Pengo alisisitiza hilo wakati akitoa ufafanuzi juu ya sintofahamu iliyojitokeza miongoni mwa Watanzania na waumini wa kanisa hilo kutokana na kauli ya Askofu Niwemugizi.

“Napenda kutamka moja kwa moja kwamba huo siyo msimamo wa kanisa na hauwezi kuwa msimao wa kanisa kwa sababu sisi tuna taratibu zetu za kuishauri Serikali au kuzungumzia masuala ya jamii,” alisema.

Alifafanua zaidi kwamba kutokana na nafasi ya Uaskofu aliyonayo Askofu Niwemugizi, kauli yake inaweza kutafsiriwa kuwa ndio msimamo wa Kanisa Katoliki au wa Jimbo la Rulenge, Ngara lakini kimsingi kauli ile imekosa vigezo vya kuichukulia kama msimamo wa kanisa au jimbo anakotoka.

Kadinali Pengo alisema yeye binafsi kipaumbele chake ni kuona huduma za jamii kama zile elimu na afya zinaendelea kuboreshwa kwa kasi kama ambavyo Serikali ilivyoanza kufanya.

“Mtu akiniambia priority (kipaumbele) ya Tanzania ni Katiba mpya inabidi anithibitishie huo ukipaumbele maana siwezi kuona mtoto anakufa kwa njaa au kwa kukosa dawa eti kwa sababu ya Katiba mpya. Kwangu mimi Katiba ni kitu ambacho kije baadaye, si cha haraka.

“Wanasiasa wasiache watoto wetu wafe kwa njaa kisa malumbano ya Katiba. Wasiache watoto wakose shule kwa sababu hela zote zimeishia kwenye malumbano juu ya Katiba,” alisisitiza Kadinali Pengo.

Kwa upande wake Balozi wa Vatican nchini Tanzania, Askofu Marek Solczynski hakutofautiana na kauli ya Kadinali Pengo kwa kusema pamoja na kwamba Askofu Niwemugizi ana haki ya kutoa maoni yake lakini tatizo linakuja pale watu wakaposhindwa kung’amua kuwa ni maoni binafsi au ni ya kanisa.

Amesisitiza kwamba kanisa lina taratibu zake za kutoa maoni kwa masuala ya kijamii na kwa Serikali. “Hayo ni maoni yake binafsi na wala yasihusishwe na kanisa katoliki,” alisema Balozi Askofu Merek.

Hivi karibuni Askofu Niwemugizi alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kipaumbeke cha kwanza cha Watanzania ni Katiba mpya na kuongeza yeye binafsi ni miongini mwa watu walioipinga Katiba Inayopendekezwa.

Hata hivyo, wachambuzi wa mambo walisema, pamoja na mjadala mkubwa ulioibuka na baadhi ya wanasiasa kususia mchakato wa kukamilisha Katiba mpya, wataalamu wa sheria wanasema Katiba inayopendekezwa ilikuwa ni bora kuliko ya sasa ikiwemo kuruhusu wagombea kuhoji mahakamani matokeo mbalimbali ikiwemo ya urais.

“Hata mimi ukiniuliza leo tuache kufanya mageuzi ya msingi katika jamii ili kuwa na uchumi imara au tuanze kushughulika na Katiba mpya, nitakwambia tuachane na Katiba.

“Nakumbuka ile Katiba Inayopendekezwa ilikuwa na masuala makubwa yenye maslahi kwa nchi ikiwemo kipengele cha kupinga matokeo ya urais lakini kwa kuwa kuna watu walikuwa na maslahi yao binafsi, wakatoka nje ya Bunge na kukwamisha mchakato ule sioni uharaka wa leo tuache mengine yote turejee kwenye mchakato huu,” alisema Wakili wa Mahakama Kuu, James Nandonde.

Tutamwitia Gwajima, ndiye anamuweza huyu mzee
 
Mhashamu Askofu Kardinali Pengo amesema kuwa kauli iliyotolewa na askofu Niwemugizi kuwa katiba mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi sio msimamo wa kanisa kwa sababu kanisa lina taratibu zake za kuishauri serikali au kuzungumzia masuala ya jamii.

Pia amesema kwake yeye katiba ni kitu kije baadaye si cha haraka.

chanzo: gazeti la Mwananchi via facebook.

Naona kama Kardinali alikuwa out of context kabisa!
 
Back
Top Bottom