Peniela (Story ya kijasusi)

Peniela (Story ya kijasusi)

Inasikitisha sana kuona hizi nyumba 2 muhimu zinaunguzwa, pamoja na uzuri wa nyumba ya Peniela na vitu vingi vya thamani vilivyokuwemo, kuna kile kibox alichopewa na John Mwaulaya, hajakifungua kujua kuna nini sijui hatima ya hiki kibox.

Nyumbani kwa Mathew ilikuwa ni nyumba ya thamani nyumba ambayo Mathew aliamini kuwa ni sehemu salama kuliko sehemu yoyote.
Lakini kulikuwa na vitendea kazi muhimu hii ikiwa ni pamoja na magari yake, lakini kulikuwemo na kitu cha muhimu zaidi ambacho kiliwagharimu muda pamoja na uhai wa baadhi ya watu, kitu hiki ni zile nyaraka za siri zenye formula ya kutengeneza virus hatari, hii nayo sijui hatima yake.
Ngoja nione mtunzi atakavyo fix hii sintofahamu ya haya mambo pamoja na mengine.

Kitu kingine na ambacho nilikiona mapema ni Mathew kuwaamini sana washirika wake na kuwaonyesha mambo mengi ya siri pale nyumbani kwake, hili jambo limemgharimu.

Poor Elibariki.
 
Inasikitisha sana kuona hizi nyumba 2 muhimu zinaunguzwa, pamoja na uzuri wa nyumba ya Peniela na vitu vingi vya thamani vilivyokuwemo, kuna kile kibox alichopewa na John Mwaulaya, hajakifungua kujua kuna nini sijui hatima ya hiki kibox.

Nyumbani kwa Mathew ilikuwa ni nyumba ya thamani nyumba ambayo Mathew aliamini kuwa ni sehemu salama kuliko sehemu yoyote.
Lakini kulikuwa na vitendea kazi muhimu hii ikiwa ni pamoja na magari yake, lakini kulikuwemo na kitu cha muhimu zaidi ambacho kiliwagharimu muda pamoja na uhai wa baadhi ya watu, kitu hiki ni zile nyaraka za siri zenye formula ya kutengeneza virus hatari, hii nayo sijui hatima yake.
Ngoja nione mtunzi atakavyo fix hii sintofahamu ya haya mambo pamoja na mengine.

Kitu kingine na ambacho nilikiona mapema ni Mathew kuwaamini sana washirika wake na kuwaonyesha mambo mengi ya siri pale nyumbani kwake, hili jambo limemgharimu.

Poor Elibariki.

Kibox Paniela alikificha kule Makazi Mapya aliko pewa na Hon Rais
Ila zile nyaraka Ndo Basi tena

Kuanzia Sasa sito muamini Mtu humu Tofauti na Mathew Jaji alichofanya Sina ham kabisa
 
Kwa hapa story ilipofikia tafadhar lege naomba uweke vipande kama vitano pamoja na kwamba weng tupo makazi maana mda wote naona anitha ananililia nimwokoe baada ya dk nachungulia kwenye huu uzi kiona vp
 
Inasikitisha sana kuona hizi nyumba 2 muhimu zinaunguzwa, pamoja na uzuri wa nyumba ya Peniela na vitu vingi vya thamani vilivyokuwemo, kuna kile kibox alichopewa na John Mwaulaya, hajakifungua kujua kuna nini sijui hatima ya hiki kibox.

Nyumbani kwa Mathew ilikuwa ni nyumba ya thamani nyumba ambayo Mathew aliamini kuwa ni sehemu salama kuliko sehemu yoyote.
Lakini kulikuwa na vitendea kazi muhimu hii ikiwa ni pamoja na magari yake, lakini kulikuwemo na kitu cha muhimu zaidi ambacho kiliwagharimu muda pamoja na uhai wa baadhi ya watu, kitu hiki ni zile nyaraka za siri zenye formula ya kutengeneza virus hatari, hii nayo sijui hatima yake.
Ngoja nione mtunzi atakavyo fix hii sintofahamu ya haya mambo pamoja na mengine.

Kitu kingine na ambacho nilikiona mapema ni Mathew kuwaamini sana washirika wake na kuwaonyesha mambo mengi ya siri pale nyumbani kwake, hili jambo limemgharimu.

Poor Elibariki.
Kibox kilihifadhiwa ktk kasri jipya la Penny alilopewa na Mr Prezda....

Kuhusu nyaraka ila yenye formulas as kirusi yaweza patikana kwenye e - mail iliyotumwa Israel au underground siamini kama vitu muhimu Mathew angehifadhi panapofikika kwa urahisi.
 
Kibox kilihifadhiwa ktk kasri jipya la Penny alilopewa na Mr Prezda....

Kuhusu nyaraka ila yenye formulas as kirusi yaweza patikana kwenye e - mail iliyotumwa Israel au underground siamini kama vitu muhimu Mathew angehifadhi panapofikika kwa urahisi.
Nimekupata TaiJike, thanks.
 
Inasikitisha sana kuona hizi nyumba 2 muhimu zinaunguzwa, pamoja na uzuri wa nyumba ya Peniela na vitu vingi vya thamani vilivyokuwemo, kuna kile kibox alichopewa na John Mwaulaya, hajakifungua kujua kuna nini sijui hatima ya hiki kibox.

Nyumbani kwa Mathew ilikuwa ni nyumba ya thamani nyumba ambayo Mathew aliamini kuwa ni sehemu salama kuliko sehemu yoyote.
Lakini kulikuwa na vitendea kazi muhimu hii ikiwa ni pamoja na magari yake, lakini kulikuwemo na kitu cha muhimu zaidi ambacho kiliwagharimu muda pamoja na uhai wa baadhi ya watu, kitu hiki ni zile nyaraka za siri zenye formula ya kutengeneza virus hatari, hii nayo sijui hatima yake.
Ngoja nione mtunzi atakavyo fix hii sintofahamu ya haya mambo pamoja na mengine. mkuu hakuna lililo haribika kile kibox alichopewa peniel umesahau kuwa hakukiweka nyumbani kwake bali alikihifadhi kulee kwenye nyumba iliyopo ufukweni aliyo pewa na dr JOSHUA?

nakuhusu karatasi zile haina shida kila kitu washakijua kilichopo kwenye zile karatasi na nzuri zaidi kopi alishazituma kwa jamaa zake waliomsaidia kutambua kuwa kunani??

kuhusu nyumba ya mathew kuteketea na vitendea kazi vyake hakuwezi kumzuia kufanya kazi. kumbuka john mwaulaya kamwachia mikoba yote mathew hivyo tegemea kuna mengi na siri nyingi sana kaachiwa pia.

mtunzi hakuna sehyem atakapo jichanganya kila tukio linapoishi ni mwanzo wa tukio jingine .

Kitu kingine na ambacho nilikiona mapema ni Mathew kuwaamini sana washirika wake na kuwaonyesha mambo mengi ya siri pale nyumbani kwake, hili jambo limemgharimu.

Poor Elibariki.
 
Yeahhhh...safi sana...sasa Mathew anaweza kufanya kazi vizuri

Waliokuja kumchukua watakuwa aidha watu wa Deus au Wasiri wa John

Kiufupi yeye ndiye amerithi mali zote za john....john was rich

Elibariki amefanya ujinga sana.....namsikitikia Anitha

Hadithi yote iko centred kwenye "Papuchi" na nguvu yake
 
PENIELA SEASON 3

SEHEMU YA 31

MTUNZI 😛ATRICK.CK


ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

“ Go away Vincent .I’ll fight this war alone”

“ Rose huwezi kushinda vita hii.Let me help you to find who did this to you” akasema Vincent.Rose akamuangalia kwa jicho la chuki kisha akauliza

“ Who killed Amos and why? Akauliza Rose

“ Siwezi kukutajia ni nani aliyemuua lakini ninaweza kukwambia ni kwa nini aliuawa.Alikuwa tayari kuvujisha siri ambayo hakutakiwa kuitoa” akasema Vincent
“ Ouh Amos nitakulilia kilio gani mimi jamani..!!..akasema Rose huku akimwaga machozi
“ Rose ninadhani sintakuwa na jambo lingile la kuzungumza nawe kwa usiku huu. Endelea kupumzika na tafadhali zingatia hayo niliyokueleza.Dont start war with Deus.Nitakutembelea tena kujua hali yako” akasema Vincent
“ Vincent don’t show your face here again you monster !! akasema Rose kwa ukali .Vincent akaufungua mlango akatoka .
“ Aaaagggghhhh.!!!!! Akalia kw auchungu Rose na mara Dr Imelda akaingia na kumchoma sindano ya usingizi ili aweze kulala



ENDELEA………………………



Anitha alifumbua macho na kujikuta akiwa katika kiza kinene.
“ Where am I? akajiuliza lakini hakupata jibu la mahala alikokuwa.Akajaribu kuinua mkono ili aweze kupapasa akastuka baada ya kugundua kuwa mikono yake imefungwa pingu.
“ Nimefungwa pingu ! ? Niko wapi hapa? Akajiuliza Anitha na kugundua kwamba hata miguu yake pia ilikuwa imefungwa pingu

“ Hapa niko wapi? What happened? Akawaza Anitha na kujaribu kurudisha kumbukumbu nyuma na ndipo alipokumbuka kile kilichokuwa kimetokea

“ Elibariki did this !!.Ni yeye ..ouh my God why him??.. akajiuliza

“ Ninakumbuka alinifuata ofisini akaniomba anitengenezee kahawa nikakataa. Muda huo huo Mathew akanipigia simu nikapokea lakini nilipoanza kuongea naye ghafla nikapigwa na kitu kigumu kichwani nikapoteza fahamu.Lazima ni Elibarki ndiye aliyenipiga na kitu kile nikapoteza fahamu.Dhumuni lake lilikuwa nini ? Kama ni yeye lazima ndiye aliyenileta hapa.Anataka nini toka kwangu? Anitha akaendelea kujiuliza maswali yaliyokosa majibu
“ Mathew hivi sasa atakuwa katika matatizo na anahitaji sana msaada wangu.Naomba Mungu huko aliko awe salama.” Anitha akaanza tena kukumbuka kila kilichotokea usiku ule nyumbani kwa Mathew

“ lazima ni Elibariki aliyenipiga na kitu kile kichwani nikapoteza fahamu. Kwa nini afanye hivi wakati anajua kwamba sisi ndiye wakombozi wake?.Pale nyumbani kwa Mathew ndiyo sehemu pekee ambayo salama kwake.Mwenzetu Noah alipoteza uhai wake wakati akimuokoa Elibariki katika shambulio kwa hiyo sisi ni watu wake wa muhimu sana ,kwa nini basi atufanyie hivi? Kwa nini ametusaliti? Tulimuamini sana Elibariki lakini kumbe katika kipindi hiki chote tulichokaa naye kumbe alikuwa anatuchunguza.Ouh my God sikutegemea kama Elibarikianaweza akatufanyia hivi.Who is he working with? Anyway ngoja nisubiri ili nijue sababu iliyomfanya atugeuke katika dakika hizi za mwishoni.Kinachoniumiza kichwa zaidiamenileta na kunifunga huku katika wakati ambao Mathew anahitaji sana msaada wangu.Nitafanyaje kumsaidia kwani ananitegemea sana katika kuifanikisha mpango mzima wa kuichukua package toka kwa Dr Joshua na tayari tumekwisha fanya kazi kubwa na tulikuwa tunaelekea mwishoni .Ee Mugu nisaidie niweze kutoka humu ndani salama na kumsaidia Mathew.Bila ya mimi kuwepo kila kitu tulichokihangaikia kitakuw akazi bure.” Akawaza Anitha na kuumia sana.

“ Sifahamu dhumuni la kuletwa hapa na sijui nitakaa hapa kwa muda gani .Lazima nitafute akili ya kuweza kunitoa hapa lazima nikaonane na Mathew .Siwezi kukubali kile tulichokipigania Kwa nguvu zote kishindikane wakati tunakaribia sana kufika mwisho.Tusipokuwa makini kirusi kile kitatua mikononi mwa watu wabaya na juhudi zetu zote za kulizima shambulio hili zitakwenda bure.Sitaki kukubali hilo litokee.I cant die in here while Mathew needs me.I must find a way out of here.I better die trying” akawaza Anitha
Katika chumba cha pili jaji Elibariki alikuwa amefungwa pingu kama alivyofungwa Anitha.Kchwa chake kilijaa mawazo

“ Kwa nini Rosemary anifanyie hivi hata baada ya kumsaidia kumuweka huru? Nimewasaliti wenzangu kwa kumsaidia yeye lakini haya ndiyo malipo yake? Nilikosea sana.Ninakijutia kitendo nilichokifanya.Hii ni dhambi kubwa sana ya kuwasaliti wenzangu na hii itanitafuna hadi siku ninaingia kaburini.My plan failed and I don’t know what to do anymore.” Akawaza
“ Ni bora ningeendelea kukaa pale pale kwa Mathew kuliko kufanya usaliti kama huu ambao haujanisaidia lolote na umeniweka pabaya zaidi.Nimeruka jivu nimekanyaga moto.Kinachoniumiza zaidi ni ukatili alioufanya Rose kwa kuichoma moto nyumba ya Mathew.Hii imeniumiza sana na sikutegemea kabisa kama Rose angeweza kufanya jambo kama lile .Sijui Mathew atakuwa katika hali gani akikuta nyumba yake aliyoijenga kwa mamilioni ya fedha imeungua moto na kila klichomo ndani kimegeuka majivu.Sijui sura yangu nitaiweka wapi Mathew akigundua kwamba ni mimi ndiye niliyefanya usaliti huu mkubwa.Naomba hata Rosemary aniue tu ili niepukane na mateso hjaya makubwa ninayoyapata hivi sasa.Sioni tena hata thamani ya kuendelea kuishi.Imefikia hatua sasa ambayo ninatamani kufa kuliko kuendelea kuishi .Akili yangu imechoka na haina tena uwezo wa kupata ufumbuzi wa kudumu wa matatizo yanayonizunguka” akawaza jaji Elibariki na kuanza kuikumbuka historia ya maisha yake.
“ Maisha yangu yalianza kubadilika nilipofunga ndoa na Flaviana.Japokuwa kwa nje tulionekana tunapendana lakini maisha yetuya ndani ni Mungu tu ndiye anayejua namna tulivyokuwa tunaishi.Ghafla Peniela akajitokeza katika picha nikatokea kumpenda hapo ndipo kila kitu kilipokwenda chini.Laiti peniela asingejitokeza katika maisha yangu ningeendelea na maisha yangu ya kukwaruzana na mke wangu Flaviana na wala tusingefika hapa tulipofika sasa hivi.Kwa ajili ya kumpenda Peniela nilitaka kulisafisha jina lake na ndiyo maana nikamuajiri Mathew ili aweze kumsaka muuaji halisi wa Edson lakini badala yake yameibuka mambo mengi makubwa na kunifikisha hapa nilipofika. Nimempoteza mke wangu Flaviana,nimemkosa Peniela,nimewapoteza ma rafiki Mathew na Anithana hili inainuma sana.Mathew ni rafiki yangu mkubwa ambaye aliyatoa maisha yake kunisaidia lakini kwa kutokufikiri kwa umakini nikamsaliti kwa kutegemea kwamba ninatengeneza njia ya kunisaidia kumbe ninabomoa na sasa nimekwama.Now where to run.Ouh my Lord please show me the way..” akaendelea kuwaza Elibariki akiwa amekata tamaa kabisa.
“ Anitha na Naomi nao wamechukuliwa pia .Sikujua kama angemchukua na Anitha .Yule ni msaada mkubwa sana kwa Mathew.Shughuli nyingi za Mathew zinamtegemea sana Anitha .Kwa kutokuwepo anitha kila kitu walichokuwa wanakifanya kitakwama. Huu ni mwisho wa kila kitu ila ninachokiomba Rose asimuue Anitha.Ni bora aniue mimi lakini amuache Anitha.Halafu kuna Yule paka shume Naomi.Yeye ndiye amechangia kwa kiasi kikubwa mimi kupatwa na mawazo haya ya kuwasaliti wenzangu kwa kumuachia Rosemary.Yeye ndiye aliyenishawishi nikafanya naye mapenzi na tukakutwa na akina Mathew na mimi kupata abu kubwa kwa watu ambao wananiheshimu sana.Ni yeye ambaye amesababisha nikamkosa Peniela kwani baada ya kushuhudia kitendo kile hakutaka tena kuendelea na mahusiano na mimi.Nilijaribu sana kumbembeleza lakini alinitolea maneno machafu na sitaki hata kuyakumbuka .” akaendelea kuwaza jaji Elibariki na taratibu macho yakaazna kuwa mazito akalala




******


Kumekucha tena Tanzania .Habari kubwa iliyotawala katika vyombo vyote vya habari asubuhi hii ni matukio makubwa mawili ya nyumba kuteketea kwa moto.Taarifa zilisema kwamba Jeshi la polisi linaendelea kufanya utafitiwa vyanzo vya moto huo navile vile taarifa ziliongeza kwamba mmiliki wa mojawapo ya nyumba iliyongua anatafutwa na jeshi la polisi kwani katika nyumba yake kulitokea milipuko inayosaidikiwa kuwa ni mabomu. Kingine kilichochukua nafasi katika vyombo vya habari hususan magazeti ni kurejeshwa nchini kwa mwili wa Flaviana mtoto wa rais aliyepelekwa nchini afrika ya kusini kwa matibabu baada ya kushambuliwa katikashambulio linalosadikiwa kupangwa na mumewake jaji Elibariki.Taarifa hiyo pia iliambatana napicha kubwa ya jaji Elibariki na ilimuelezea kama mtu anayesakwa kila kona kwa kusababisha kifo kile cha mtoto wa rais.
Saa mbili na nusu za asubuhi Dr Imelda,akaingia chumbani kwa Rosemary akamuamsha.

“ hallow madam unaendelaje?
“ Ninaendelea vizuri ila maumivu bado ni makali sana hasa miguuni Yule kijana alikonikata vidole.Waliniumiza sana wale jamaa.Sijawahi fanyiwa hivi toka nizaliwe.”akasema Rosemary
‘Pole sana madam utapona tu.kwa sasa nitakusafisha majeraha na kisha nitakucho masindano .” akasema Imelda
Baada ya zoezi lile kukamilika Rosemary akaomba kuonana na Fernando mlinzi mkuu wa nyumba yake.

“ Fernando nataka uwaandae wale watu nahitaji kuonana nao mmoja mmoja.Nataka kwanza kuonana na Yule mwanaume halafu Yule mwanamke na kisha kale ka binti”akasema Rose na Fernando akatoka mle chumbani.Baada ya Fernando kutoka akaingia Celine katibu wa Rose.Wakasalimiana na baada ya maongezi machache Rose akasema .
“Celine naomba ufute kabisa ratiba zangu zote kwa muda wa wiki mbili hadi hapo nitakapopona kabisa .” Akasema Rose
“ sawa madam .lakini nimepokea simu kadhaa za watu maarufu wanaotaka kuja kukupa pole.Kuna mawaziri,wafanyabiashara n.k . Sijawapangia chochote kwanza ninasubiri ruhusa toka kwako” akasema Celine

“ Vizuri.Sihitaji kuonana na mtu yeyote Yule siku ya leo.Nitakutaarifu sikuya kuonana nao .Kikubwa ninachokihitaji siku ya leo,andaa ni mkutano na waandishiwa habari.Andaa sehemu ya kukutana nao kule bustanini na nitaonana nao saa nane za mchana wa leo.Hakikisha waandishi toka redio na televisheni zote wanafika na andaa vle vile posho zao ilitaarifa zangu zipewe kipaumbele cha juu .Nina jambo kubwa na la muhimu sana la kuzungumza nao naambalo ninataka litawale katikakila chombo cha habari kwa siku nzima ya leo na kesho.bada ya kulikamilisha hilo,nitakupa tena maelekezo mengine ” akasema Rose

“ Sawa madam,nitalishughulokia suala hilo.Kuna ambo lingine lolote la kufanya madam? Akauliza Celine.
“Kwa sasa ni hilo tu celine.Kama nina jambo lingine ninahitaji nitakujulisha “akasema Rose na Celine akatoka mle chumbani.
“ Hakuna ambaye anaweza akaniambia chochote nikamuelewa kwamba eti Dues hakuhusika katika tukio lile la mimi kutekwa nyara.Najua amekwisha pata taarifa kwamba ninatarajia kuwania urais kwa hiyo jambo hili limemstua sana kwani anafahamu fika nguvu niliyonayo na anafahamu kabisa kwamba nina uhakika mkubwa wa kuweza kushinda uchaguzi.Ameogopa na kusudio la kuwatumia wale vijana ni kuniogopesha ili nisiweze kuendelea na mpango wangu .Alikose a sana kwani badala ya kniporomosha yeye atazidi kunijenga na nitaitumia fursa hii kujijenga kisiasa.”akawaza Rose na kuichukua simu yake iliyokuwa inaita.Akataarifiwa na mlinzi wake kwamba kamandawa polisi wa kanda maalum ya Dare s salaam anahitaji kumuona.Bila kipingamizi akaomba kamanda aruhusiwe kungia ndani

“ Wote hawa niwatu ambao wananipa sapoti kubwa sana.Ameachakazizake zote na amekuja kunitembelea.” akawaza Rose huku akivaa na kujiandaa kuonana na kamanda Yule Ezekiel msonobari
Walitumia zaidi ya dakika thelatjini kwa maongezi na kikubwa kamanda alimuhakikishia Roseary kwamba uchunguzi unaendelea ili kuwabaini wale wote waliofanya kitendo kile kiovu.Kamanda wa polisi alipoondoka Rosemary akamuita Fernando na kumtaka ampeleke akaonane na jaji Elibariki.Fernando akamtegemeza wakatembea taratibu hadi katika chumba alimofungwa jaji Elibariki.
“ Rose is this how you repay me?akauliza jaji Elibariki kwa ukali mara tu Rosemary alipoingia mle ndani

“ jaji ni jadi yetu mnapoonana kwanza mnasalimiana kisha mambo mengine yafuate.Unaedelaje? akasema Rosemary
“ Unategemea niseme ninaendelea vizuri?Kwa nini umenifanyia hivi Rose? Nilijitoa mhanga kukusaidia lakini malipo yake ndiyo haya?.Nashukuru sana Rose.Ninachokuomba ninataka uniue tu ili niepukane na haya mateso niliyonayo.Kill me Rose..Kill me right now !!”akafoka jaji Elibariki
“ jaji usihamaki namna hiyo.Sijakuleta hapa kukuua na kwa nini nifanye hivyo? Siwezi kukuua mtu kama wewe.kwanza ninakushukuru sana kwa kunisadia nikaweza kutoka katikaile jehanamu.Lakini pamoja na msaada mlionisaidia naombanikuweke wazi kwamba sikuamini hata chembe na siwezi kufanya hivyo.Ninazifahamu mbinu zenu zote mnazotumia .Baada ya kuona mmeshndwa kupata kile mlichokuwa mnakihitaji toka kwangu mkapangana wenzako kwamba ujifanye umewasaliti na ili nikuamini na halafu muendelee kunichunguza.Mamboyote haya nimekwisha yapitia kwa hiyo ninayafahamu vizuri sana na hamuwezi kunidanganya kitu.”akasema Rosemary

“ Rose you’re a monster !!..akasemaElibariki
“ Pamoja na maamuzi yale magumu niliyoyafanya bado tu huniamini? Nimewasaliti wenzangu walioniamini sana pamoja na kuivuruga mipango yetu yote bado tu huniamini ? Nifanye nini ili uniamini?
“ Do you think I can easily trust you? No I cant..” akasema Rosemary

“ I betrayed my friends because of you !! !Nifanye nini zaidi ili uniamini? If you don’t tyrust me then kill me..akasemajaji Elibariki.Rosemary akamfanyia ishara Fernando asogee karibu akamnong’oneza kitu kisha Fernando akatoka na baada ya muda akarejea akiwa ameongozana na Anitha.Jaji Elibariki akastuka sana alipogonganisha macho na Anitha

“ Elibariki?!! Rosemary?!! Akasema Anitha kwa mshangao

‘ Jaji uliniambia kwamba una matatizo na unahitaji msaada wangu kwa hiyo ukawasliti wenzako na kuniachia huru ili nikusaidie kutatua matatizo yako lakini bado siamini kama unachoniambia ni kweli.Ili nikuamini kwamba kweli unahitaji msaada wangu ,ninataka umpige risasi huyu mwenzako ambaye ulikuwa unashirikiana naye ,mbele yangu.Ukifanya hivyo utanithibitishia kwamba ni kweli unahitaji msaada wangu na nitakusaidia”akasema Rose kisha akampa ishara fernandoamfungue jai Elibariki.
“ Rosemary ina maana haya yote nliyoyafanya kukuweka huru haujaniamini hadi nimuue mwenzangu? Hapana siwezi kufanya kitu kama hicho”akasema Elibariki

“ Ukikataa utanifanya niamini kwamba unanidanganya na nitakufanyia kitu kibaya sana.Nitakutesa na kukuua taratibu sana”akasema

“ Rose I cant do that”akasema jaji Elibariki

“ Fernando give him the gun !! akasema Rose na fernandoakampatia Rosemary bastora.
“ Shoot her.Prove to me that you are not lying to me .Iwill cont to three..

“ One..! akasema Rose..jaji Elibariki jasho lilikuwa linamtoka .

“ Two !..akahesabu tena Rose.Jaji Elibarikihukuakilengwa na machozi akainukana kuchukua ilee bastora akainua mkono na kumuelekezea Anitha

“ Elibariki are you sure you want to kill me? Akauliza anitha
“ I’msorry Anitha !! akajibu Elibariki
“Ok go ahead traitor,shoot me but I’ll haunt you to the grave..!! akasema Anitha huku macho yake yamejaa machozi.

“ I’m sorry Anitha I have to do this”akasema jaji Elibariki na kuilenga bastora ile kichwani kwa Anitha

“ Three !!..
Jaji Elibariki akaizinga bastora ile na ukatokea mlipuko.




TUKUTANE SEHEMU IJAYO
 
SEASON 3

SEHEMU YA 32

MTUNZI 😛ATRICK.CK


ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

“ Fernando give him the gun !! akasema Rose na fernandoakampatia Rosemary bastora.
“ Shoot her.Prove to me that you are not lying to me .Iwill cont to three..
“ One..! akasema Rose..jaji Elibariki jasho lilikuwa linamtoka .

“ Two !..akahesabu tena Rose.Jaji Elibarikihukuakilengwa na machozi akainukana kuchukua ilee bastora akainua mkono na kumuelekezea Anitha

“ Elibariki are you sure you want to kill me? Akauliza anitha
“ I’msorry Anitha !! akajibu Elibariki
“Ok go ahead traitor,shoot me but I’ll haunt you to the grave..!! akasema Anitha huku macho yake yamejaa machozi.
“ I’m sorry Anitha I have to do this”akasema jaji Elibariki na kuilenga bastora ile kichwani kwa Anitha

“ Three !!..
Jaji Elibariki akaizinga bastora ile na ukatokea mlipuko.



ENDELEA……………



“ hahahahaha..!! akacheka Rosemary

“ I’m impressed with you judge ! kidogo sasa nimeanza kukuamini.Hiyo bastora haikuwa na risasi halisi bali ni risasi baridi kwa ajili ya kuogofya.” Akasema Rosemary na kumgeukia Fernando

“ Fernando take thegun” .Uso wa Jaji Elibariki ulikuwa umeloa jasho na midomo ilikuwa inamtetemeka.
“ Fernando take her out of here” akaamuru Rosemary na Anitha akatolewa mle chumbani alikuwa anatetemeka mwli mzima kwa woga.Hakuamini kama bado alikuwa hai.
“ Jaji kitendo ulichotoka kukifanya kimenithibitishia kwamba ni kweli una tatizo na unahitaji sana msaada wangu na ndiyo maana hukusita kuachia risasi ile ambayo kama ingekuwa ni risasi halisi basi mwenzako angekufa.Lakini pamoja na hayo kuna mambo ninataka kufahamu toka kwako.Nataka kufahamu wale wenzako ni nani aliye nyuma yao? Ni nani aliyewatuma kwangu? Akauliza Rosemary
“ No one” akajibu jaji Elibariki
“ Jaji bado hatima yako iko mikononi mwangu.Ni mimi ndiye nitakaye kusaidia na kukutoa katika matatizo yako uliyonayo kwa hiyo ninapokuuliza swali naomba unijibu bila kunificha Ni nani aliyewatuma wale wenzako kwangu? Ni nani aliyewapa taarifa zangu?
“ Nitakueleza ukweli Rose .Hakuna mtu yeyote aliyetutuma kwako lakini ulijitokeza katikati ya uchunguzi aliokuwa anaufanya Mathew na ndipo alipoanza kukufuatilia.”
“ Nilitokea katikati ya uchunguzi? Ni uchunguzi gani huo alikuwa anaufanya ?

“ Mathew alikuwa anachunguza kuhusiana na kifo cha Edson aliyeuawa na kisha Peniela akaangushiwa kesi ile ya mauaji.Mimi ndiye niliyemuachia huru Peniela baada ya kuridhika kwamba hakuwa amefanya mauaji yale ya Edson kama ilivyokuwa imedaiwa.Baada ya hukumu ile kulikuwa na maneno mengi sana yaliyoongelewa kwa hiyo nikataka kukata mzizi wa fitina kwa kumtafuta muuaji halisi wa Edson na ndipo nilipomkodisha Mathew aweze kuifanya hiyo kazi.Katika uchunguzi huo Mathew alibaini kwamba kuna nyaraka za siri ziliibwa ikulu na Edson ndiye aliyeeziiba akishirikiana na Captain Amos.Baada ya kulicghimba kwa undani suala hili akabaini kwamba wewe ndiye uliyekuwa nyuma ya wizi huo na ndiyo maana akaanza kukufuatilia.Hakuna mtu yeyote aliye nyuma yetu.”
“ damn you !!!!. akasema Rose kwa hasira.
“ Mathew anafanya kazi idara gani? Ni polisi?

“ Ni mpelelezi wa kujitegemea. “akajibu Elibariki.Rose akamtazama na kusema
“ Pamoja na maelezo hayo bado ninaamini lazima kuna mtu aliye nyuma yenu.Nieleze ukweli nani amewapa taarifa zangu ? akauliza Rose
“ Hakuna mtu aliyetutuma kwako Rose.kwa nini hutaki kuniamini? Akauliza Elibariki
“ That guy Mathew !alinitesa sana nani wazi kuna kitu alichokuwa anakitaka toka kwangu na ninaamini alikuwa anafuata maelekezo aliyopewa na mtu Fulani.Nataka kumfahamu huyo mtu ni nani? akasema Rose.Elibariki akamtazama kwa hasira na kusema

“ Mimi na Mathew ni marafiki wakubwa na tumekuwa tunasaidiana katika mambo mengi na hata nilipomuomba anisaidie kumtafuta muuaji wa Edson hakusita kukubali.Niko hai leo hii kwa sababu yake.lakini pamoja na hayo yote bado nimekubali kumsaliti kwa kukuachia huru.Unadhani Mathew angethubutu kukuacha huru? Nakuhakikishia ule ndio ungekuwa mwisho wako.Wewe ni mtu hatari sana na asingethubutu kukuachia huru..Wewe na wenzako mnafahadhili makundi ya kigaidi afrika mashariki .Fedha za kufadhili ugaidi zinapitia kwako .Yote haya tayari wanayafahamu unadhani wangekuachia huru? Katu usingeachiwa huru.Lakini pamoja na kufahamu kwamba weweni mtu hatari bado nimeamua kukuachia huru.Nilikua tayari kumuua mshirika wangu Anitha muda mfupi uliopita yote hii ni katika kukufanya uniamini. Unataka nifanye nini kingine ili uniamini? Kama hutaki kunisaidia ninaomba uniue tu.Kill me now.Kill me!! Akasema jaji Elibariki kwa hasira
“ Mathew ni rafiki yako mkubwa na umemsaliti? Unadhani kwa kitendo ulichokifanya akikutana nawe leo hii atakuacha hai?akauliza Rose

“ Sina namna nyingine ya kufanya zaidi ya kutafuta msaada wa kunikamua katika matatizo niliyonayo.Nimechoka kukimbia,nimechoka kujificha.Nataka niwe huru na ndiyo maana nikawasaliti wenzangu ili niweze kupata msaada toka kwako”
“ Ni jambo gani linakufanya ukimbie? Umefanya nini? akauliza Rose
“ Hivi sasa ninasakwa kila kona ya nchi hii kwa kusababisha kifo cha mke wangu Flaviana ambaye ni mtoto wa rais .“

“ You killed her?
“No I didn’t”

“ who killed her then”

“ watu waliotumwa na rais”
“kama wewe hukumshambulia mke wako na kusababisha kifochake kwa nini basi ukimbie?Kwa nini usieleze ukweli?
“ Nimenusurika kuuawa mara moja nikalazimika kuingia mafichoni lakini nikiwa mafichoni nimebambikiwa tena kesi ya kusababisha kifo.Hakuna ninayeweza kumueleza chochote akanielewa..”
“ kwa nini ulitaka kuuawa? Nani anayetaka kukuua? Kwa nini ubambikiwe kesi wakati wewe siye uliyesababisha kifo cha mkeo? Jaji unaonekana unataka kucheza na akili yangu .Mimi si mtu wa kudanganywa hovyo”
“ Wamenibambikia kesi kwa sababu wanataka kuniondoa duniani”
“ Akina nani hao wanaotaka kukuondoa duniani?
“ Rais Dr Joshua na wenzake”
“ kwanini Joshua atake kukumaliza wewe jaji? Umemfanya nini?
“ Kuna jambo nimeligundua ambalo sikupaswa kuligundua”

“ Jambo gani hilo? Akauliza Rose.Jaji Elibariki akabaki kimy

“ You want my help? Tell me everything!!..akasema Rose
“ Niligundua kwamba alimuua mkewe “
“ Dr Flora?!! Aliuawa na Dr Joshua?..Rosemary akashangaa
“ Ndiyo aliuawa na Dr Joshua kwa kumtumia Captain Amos.”
“ Ninawafahamu Dr Joshua na Dr Flora walikuwa wanapendana sana.Hainiingii akilini eti Dr Joshua amuue mke wake !!
“ Flora aligundua jambo kubwa la hatari alilokuwa anataka kulifanya Dr Joshua na ndiyo sababu akauawa.”
“Ni jambo gani hilo?
“ Kuna kirusi hatari kinaitwa Aby ambacho Dr Joshua anataka kukiuza.Nina hakika unalifahamu jambohili kupitia kwa Amos ambaye alikuwa ni mshirika wa karibu wa rais na walikuwa pamoja katika suala hili.Nina hakika hata wewe pia ulikuwa unaifuatilia package yenye kirusi hicho kwani tuliyanasa mawasiliano yako na mtu mmoja anaitwa Samir ,ukimuahidi mtu mmoja aitwaye Samir kwamba muda si mrefu utaupata mzigo kwa kuwa ulikuwa na mawasiliano na mtu wa karibu na rais.”

“ I hate that guy Mathew !!..nitamsaka kila kona mpaka nimpate lakini ninashukuru kwa taarifa uliyonipa kuhusu Dr Joshua kumuua mke wake “ akasema Rosemary
“ Dr Joshua I’ve got you now.Wewe ndiye utakayeikamilisha ndoto yangu .You are going to make me the next president of the united republic of Tanzania.”akawaza Rose na kutabasamu halafu akamgeukia Elibariki
“ I will help you judge!!..
“ Thank you Rose.” Akajibu Elibariki
“Unataka nikusaidie nini?

“ Niligundua kwamba Dr Flora aliuawa kwa sumu kwa hiyo nikawa adui mkubwa wa Dr Joshua kwani aliamini kwamba ningeweza kulitumia jambo hilo kumchafua kwa hiyo lengo lake lilikuwa ni kuniua.Kwa bahati mbaya mpango wa mara ya kwanza wa kuniua ulishindikana kwa hiyo toka wakati huo wamekuwa wakinitafuta kwa kila nguvu waliyonayo.Nimejiuliza maswali mengi kwamba nitajificha mpaka lini? Nitaendelea kukimbia hadi lini? Jibu nililolipata ni kwamba vita hii imenishinda.Siwezi kupambana na Dr Joshua kwani yeye ana nguvu kubwa kunishinda mimi.Nimeinua mikono kwa hiyo ninachohitaji ni kujisalimisha kwake ili mambo haya yaweze kuisha.Nisipofanya hivyo maisha yangu yataharibika na nitakosa kila kitu.Siwezi kukubali maisha yangu yaharibike na ndiyo maana niko tayari kufanya jambo lolote lile kwa ajili ya kuyajenga upya tena maisha yangu.Msaada ninaouhitaji toka kwako ni kunikutanisha na Dr Joshua ili niweze kuongea naye” akasema jaji Elibariki.Rose akamtazama kwa makini kisha akauliza
“ Una hakika Dr Joshua atakubali kukusamehe?
“ Nina uhaika huo kwani niko tayari hata kumsaidia katika mpango wake wa kuiuza package ili ufanikwe.Ninaifahamu mipango yote waliyoipanga Mathew na wenzake na kwa sasa baada ya nyumba ya Mathew kuungua moto hakuna tena kitakachoendelea.”
“ Unasema uko tayari kumsaidia Dr Joshua kuuza kirusi Aby? Are you out of your mind? Akauliza Rosemary
“ Kama kwa kufanya hivyo atanisamehe na kuniweka huru basi niko tayari.Rose hii ni fursa kwako na kwangu ambayo tunatakiwa kuitumia.Endapo tutaitumia vizuri fursa hii kila mmoja atafaidika.Rose tunaweza kuwa washirika na tuk……………..”

“ Stop that judge..! akasema Rosmeary mkozumi kwa ukali
“ Usiongelee kabisa suala la mimi na wewe kuwa washirika.Siwezi kamwe kushirikiana na mtu kama wewe ambaye nimekushuhudia ukiwasaliti wenzako.Kwa ajili ya maslahi yako unaweza ukamsaliti mtu yeyote Yule.Wewe si mtu wa kuamini hata kidogo lakini hata hivyo itakusaidia ingawa kwa sharti moja kubwa.”
“ Sharti gani hilo Rose? akauliza Elibariki

“ Promise me that you will help me find Mathew”akasema Rose
Bila kupepesa macho jaji Elibariki akasema
“ I will help you find Mathew.I promise”akasema jaji Elibariki.
“ Thank you.I will help you.Dr Joshua atakapomaliza mazishi ya mwanae nitakukutanisha naye”akasema Rose

“ Naomba unisaidie suala hili kwa haraka zaidi ili niweze kushiriki mazishi ya mke wangu Flaviana” akaomba Elibariki
“ Nitajitahidi kadiri nitakavyoweza “
“Fernando I’m done with Mr Judge,Take me to the next room to see that woman ” akasema Rose na kisha Fernando akamsaidia kuinuka akamshika mkono akamsaidia kutembea wakatoka mle chumbani.


TUKUTANE SEHEMU IJAYO……
 
Back
Top Bottom