Penye nia pana njia: Ni wiki ya 5 sasa sijatia soda mdomoni, kumbe inawezakana kabisa

Kitu usichokielewa ni bora ukae kimya, mimi spice huwa nanunuwa kwa Muhindi karibu na Co cabs pale kuna mashine wanasaga wao wenyewe natural, spice nyingi zinapatikana hapo.
Ni vizuri kama ni natural, ila anachosema ni kwamba kuna spices za kuchanganya madawa viwandani, na hizo ndizo nyingi madukani
 
Mimi matumizi yangu makubwa Ni maji, kwa 24 hrs nakunywa 1.5 lt chupa 6 au 7. Kwenda kwa watu lazima nibebe maji kwenye begi. Safarini napata tabu Sana maana nalazimika kutokunywa maji ili kuzuia kukojoa Mara kwa Mara. Je hii nayo Ni addiction?
Hiyo haijawekwa kwenye addiction, pengine ndio mahitaji yako sahihi ya maji mfano labda wewe washikaji hukuona kama pande la jitu.
 
Hongera mkuu, tuendelee kupeana moyo, tutafanikiwa na hii kadhia, nimejidhatiti kweli kweli
Mimi sijaacha ila ukitaka kuacha ni rahisi tu ,ukifanya hivi
1) chakula chako kiwe ugali ,kama mjuavyo ugali ni "mboga" basi fanya mboga ya kulia ugali ziwe nzuri ,pia ugali ni adui no 1 wa soda tofauti na vyakula vyote duniani ,mungu katujalia waafrika kwa kuwa na hichi chakula cha ugali .
Njia ya pili
2)kila unapo sikia kiu au hamu ya soda kunywa maji kwanza ukiona hamu ya soda bado ipo ndiyo nunua soda unywe ,mm niligundua kuwa asilimia 80% ya hamu ya kunywa soda tunayo ipata huwa siyo halisi na ukitaka kujua kuwa siyo halisi basi kabla ya kuamua kunywa soda nunua maji unywe kiu ikate kisha sikilizia kama hamu ya soda bado ipo
Hizi njia mbili zinatosha kabisa kuzitumia kuacha soda ,tena ni nyepesi
 

Maamuzi tu ndugu yangu
 
We jamaa naona unakusudia kuharibu hali ya hewa.
Ngoja tusubiri.
 
Mimi matumizi yangu makubwa Ni maji, kwa 24 hrs nakunywa 1.5 lt chupa 6 au 7. Kwenda kwa watu lazima nibebe maji kwenye begi. Safarini napata tabu Sana maana nalazimika kutokunywa maji ili kuzuia kukojoa Mara kwa Mara. Je hii nayo Ni addiction?
Napenda maji pia , japo sjiafika kiwango chako ila nakunywa wastani wa lita 5 kwa siku.
Kuna madhara ya kunywa maji mengi pia ,niliambiwa na mtaalamu mmoja kuwa unaweza kupoteza nutrients muhimu kupitia mkojo kama utakuwa unakojia mara kwa mara , japo hili sijawahi kulijua kitaalamu ila naamini wapo humu kutuelimisha .
 
Unafanya hayo yote..na bado unagonga kavu.hhaahhahaha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Soda ni hatari kuliko Bia, fanyeni utafiti.
 
Mimi matumizi yangu makubwa Ni maji, kwa 24 hrs nakunywa 1.5 lt chupa 6 au 7. Kwenda kwa watu lazima nibebe maji kwenye begi. Safarini napata tabu Sana maana nalazimika kutokunywa maji ili kuzuia kukojoa Mara kwa Mara. Je hii nayo Ni addiction?
Kwamba unakunywa 9lts kwa siku? Hilo nalo ni tatizo mkuu, hizo kidney zako zinapiga mzigo zaidi ya kawaida. Lakini pia unapoteza nutrients nyingi kupitia filtration, 9lts per day, unafanya shughuli gani mkuu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…