Ph.D bila kupata Master

Ph.D bila kupata Master

Paschal Matubi

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2008
Posts
235
Reaction score
303
Wanandugu,

Je, duniani kuna utaratibu wowote unaoweza kukufanya ukapata Ph.D bila kulazimika kupitia kwanza Masters? Kama inawezekana, ni institutions zipi zinao utaratibu huo?
 
Upo vyuo vingi tu, Ila inahitaji uwe umefaulu vizuri sana kwenye shahada ya kwanza, ili wakuruhusu ujiandikishe kama mwanafunzi wa Ph.D, kwa maana ya kuanza kuwa mtafiti mbobevu!.Nadhani hili haya UDSM linawezekana.

Au kwa vyuo, vinavyo value papers kuliko final document eg thesis au dessertation unaweza pata Ph.D direct badala ya masters kama umeandika papers zinazohitajika. Hili vyuo vingi vya south africa wanafanya.
 
nenda UDSM ila uwe kichwa sio mvivu a kusoma na bingwa wa kucopy and paste
 
UDSM upande wa Sheria kulikuwa na offer kwa atakayepata first class ataenda moja kwa moja kusoma Phd. Sijui kama bado ipo au iliondolewa.
 
It z pocble, unaweza ukapata hata Prof; bila ya kupitia masters na Phd.
 
Kwa madaktari wa binadamu ni rahisi zaidi kwenda phd moja kwa moja
 
Ukiwa Bachelor yenye (4years) ukaweza pia kumaliza COURSE WORK na PAPERS ZOTE requred for Masters, unaweza kuunganisha PhD ukitokea bachelor degree.Mara nyingi PhD ya aina hii si chini ya miaka minne.
 
Hiyo inaitwa research degree ambacho ukiwa na bachelor unasomea PhD hasa vyuo vya nje wanafanya sana. Kwa hapa Tanzania utatibu huo upo lakini hautumiki sana
 
UDSM upande wa Sheria kulikuwa na offer kwa atakayepata first class ataenda moja kwa moja kusoma Phd. Sijui kama bado ipo au iliondolewa.
first class ya mwisho UDSM SCHOOL OF LAW(Formely Faculty of Law) ni 1988 nafikiri ni ya Asha Rose Migiro...so sidhani kama hiyo offer bado iko valid...i stand to be corrected...yooo
 
Unaweza ndugu. Wewe pata first class kwenye chuo maarufu duniani utakwenda kusoma PhD. Vile vile waweza kuwa professor bila kupata PhD. Prof. Wamba dia Wamba hakusoma PhD.
 
Wanandugu,

Je, duniani kuna utaratibu wowote unaoweza kukufanya ukapata Ph.D bila kulazimika kupitia kwanza Masters? Kama inawezekana, ni institutions zipi zinao utaratibu huo?

Ndio inawezekana. Uingereza wanao utaratibu huo siku nyingi sana. Mfano, Prof. Mwandosya (Waziri) nadhani alikiuka Masters pale University of Birmingham, UK na kupata Ph.D. Lakini sasa lazima uwe unapasua vizuri. Kilaza unaweza kupata hata Masters 10 kabla ya kupata Ph.D. Kuna watu ninaowajua bali sitaki kuwataja ambao wamechukua miaka zaidi ya 15 (this is not a joke) kufanya Ph.D zao baada ya kuwa na Masters.

Ph.D. study is a trainning in research. If you are ready, YOU ARE READY. There is no requirement that you have to have a Masters first.
 
Inategemea na mfumo wa elimu ya nchi. Kwenye nchi zinazotumia credits sio lazima uwe umepasua sana. Unaweza kuingia lakini itabidi uchukue Credits nyingi kuliko yule wa aliyeingia na Masters.
 
Upo vyuo vingi tu, Ila inahitaji uwe umefaulu vizuri sana kwenye shahada ya kwanza, ili wakuruhusu ujiandikishe kama mwanafunzi wa Ph.D, kwa maana ya kuanza kuwa mtafiti mbobevu!.Nadhani hili haya UDSM linawezekana.

Au kwa vyuo, vinavyo value papers kuliko final document eg thesis au dessertation unaweza pata Ph.D direct badala ya masters kama umeandika papers zinazohitajika. Hili vyuo vingi vya south africa wanafanya.

uwe umefaulu vipi mkuu? only first class au inakuwaje? nikifanikiwa hivi ntafurah sana,...
 
Unaweza ndugu. Wewe pata first class kwenye chuo maarufu duniani utakwenda kusoma PhD. Vile vile waweza kuwa professor bila kupata PhD. Prof. Wamba dia Wamba hakusoma PhD.

Duu, shortcut is always a right cut...lol
 
Samahani nipo nje ya mada, Naomba kuuliza mtu akipata division 1 form six, anaweza kuomba scholarships kwenye vyuo kama harvard, duke, vya marekani na kufanikiwa, au siri hasa ya kupata hizo scholarships ni nini au vigezo gani hasa wanahitaji?
 
Inawezekana manake kuna Dr Padri yeye alisomea Biblia sasa hivi anajiita Dr
 
Wanandugu,

Je, duniani kuna utaratibu wowote unaoweza kukufanya ukapata Ph.D bila kulazimika kupitia kwanza Masters? Kama inawezekana, ni institutions zipi zinao utaratibu huo?

Mbona utaratibu huo upo sana ninamfahamu binti mmoja mtoto wa mkubwa hapa bongo alisoma UK degree yake ya kwanza akafaulu vizuri sana wazungu wa kule Sussex wakamwita aende kusoma PHD bila kusoma Masters na tunapoongea binti aliishafaulu na amerudi na Phd yake anafanya kazi hapa bongo kwenye Bank moja naihifadhi jina.
Habari ndio hiyo
 
Swali zuri. Unaweza kupata PhD bila masters kama ambavyo unaweza kupata masters bila bachelor!. Southampton university kwa mfano wana kitu kinaitwa integrated degree(sio course zote) yaani mtu anaingia kuanza kusoma bachelor ya four years but kiukweli bachelor yake inakuwa ni three years ila mwaka wa nne unakuwa wa masters. At the end anapata masters but hapewi cheti cha bachelor anakuwa na cha masters tu (so inakuwa kama vile hajasoma bachelor). However, kuna baadhi ya vyuo ulaya unaweza kusoma masters ukiwa na diploma na mara nyingi ni zile za diploma za three years although za miaka miwili pia waweza kusoma masters kulingana na "content" ya diploma yako. I think journalism and mass comm ina-lead katika hizi degree.

Suala la kuruka kwenda PhD bila masters linawezekana si tu ulaya bali hata UDSM. Sio kweli kwamba ukiwa na first class pekee ndiyo utasoma PhD (a case of law pale UDSM kwa mfano) ila ni pale tu unakuwa umeregister kama mwanafunzi wa masters especially under thesis (not coursewok and dissertation) na wakati wa kuandaa thesis yako ukaona imekaa ki-PhD PhD (imevuka viwango vya masters masters) then utaipeleka department na department wakiipitia waka-confirm wanaipeleka senate na senate itakuruhusu ''kuvuka'' na kuwa PhD candidate (sio kukupa PhD hapohapo). Baada ya kukupa candidacy ya PhD, chuo kinafuta registration ya masters palepale (automatic cancellation). Kazi yako wewe ni kufanya thesis yako ya PhD na ukifanya viva ikapita wanakuaward PhD kama wanafunzi wengine wa PhD. Hivyo, at the end utakuwa na PhD bila masters.

Kwa vyuo vingine hasa South wao wakishakuona umefanya vizuri thesis yako ya masters wanaweza kukutongoza ili upublish paper kadhaa kama tatu hivi na vi-conference proceedings paper kadhaa then wanakwambia uvifanye viwe kitu kimoja (monography) then unapata PhD yako hata after 1 year. Ingawa hili linawezekana pia hata kama umeshakuwa awarded masters yako (hasa pia kama ulipublish zaidi ya paper walizokuwa wanazihitaji masters). This is also applicable hata EU na sehemu nyingine.

Kuhusu swala la division one form six (I assume ni NECTA na sio cambridge au IB) kupata admission havard, duke na vyuo vingine vya marekani inategemea na vitu vingi sana. Vyuo vya wenzetu wanaangalia mambo mengi sana ikiwemo lugha, uwezo wako kulingana na course unayokwenda kuchukua, cousre husika (masharti yanatofautiana), competition etc. Si division one pekee, hata two shida inakuwa competition hasa kwenye admission ya ''best'' universities kama Havard, MIT, Stanford, Princeton, Yale, Columbia, California Berkeley etc. But ukiwa na one yako nzuri, TOEFL nzuri sana, admission exam yao ukapass vizuri sana (incase wanataka ufanye paper), halafu ukawa financially muscular, unaweza kupata. Shida nyingine ni pale ambapo nafasi ni chache na unacompete na watu kutoka states zote za US, wako safi kila angle na hawajasoma system zaidi ya US inakuwa shida. Kumbuka mnacompete dunia nzima etc.

Sina experience ya bachelor but admission ya PhD economics havard au leading university in the world kama MIT huwa wanapokea 30 students au wakizidi sana 33 wakati walio-apply na wana sifa ni 900 kutoka kila sehemu duniani. GMAT yao kwa mfano ukitaka kusoma PhD au masters katika business huwa ni si chini ya score 730, au 740 na kuendelea kati ya 800!. Sasa hao ni wa maana kweli mdogo wangu?!!. BUT ASK GOD.YEYE NI KILA KITU.
 
Back
Top Bottom