Tetesi: PhD aliyopewa Mwigulu Nchemba ipo kwenye hati hati ya kufutwa

Tetesi: PhD aliyopewa Mwigulu Nchemba ipo kwenye hati hati ya kufutwa


Mimi PhD ya Jafo ni Mungu tu anisamehe.

Hawa watu walikuwa mawaziri enzi ya Magufuli, Magufuli yule aliyetaka muda wote watu wafanye kazi. Walipata wapi muda wa kufanyia kazi hizo PhD?

Elimu za watu waliosoma baada ya kuwa viongozi zina mashaka
siku hizi pia kuna masters nyingi za voda fasta ambazo walizichukua watumishi wa umma ili waweze kupandishwa vyeo.ndo maana kwa sasa kuna wimbi kubwa la viongozi wa taasisi za umma ambao hawana maadili ya kazi.hizi masters zilipewa majina ya executive course ambapo unajisomea nyumbani halafu unaenda kufanya mtihani.je wewe mtumishi wa umma huo muda wa kujisomea nyumbani utaupata wapi?kwanza ukitoka kazini umechoka na ukirudi nyumbani unakutana na watoto hapa kuna kujisomea.waafrika tulilogwa tangu dunia inaanza.
makubwa sana.
 
Tumelalamika muda mrefu kuwa kuna PhD zinatolewa kwa baadhi ya wanasiasa wa Tanzania, kama njungu kupitia vyuo vikuu vya Tanzania

Kuna tetesi kuwa East Africa university quality assurance wanatarajia kuifuta PhD ya Mwigulu Nchemba baada ya kuonekana kukopy andiko la mtu mwingine.

Vyanzo vyetu pia vimefuatilia Phd ya Mh. Suleman Jafo nayo ipo matatani kufutwa.

Kwa kauli hii kaeni mkao wa kufuatilia yanayojiri na kwa sasa amepiga kimya kama mtu aliyefiwa na wazazi .
Duh! Siyo hao tu. Wako wengi sana.
 
Tumelalamika muda mrefu kuwa kuna PhD zinatolewa kwa baadhi ya wanasiasa wa Tanzania, kama njungu kupitia vyuo vikuu vya Tanzania

Kuna tetesi kuwa East Africa university quality assurance wanatarajia kuifuta PhD ya Mwigulu Nchemba baada ya kuonekana kukopy andiko la mtu mwingine.

Vyanzo vyetu pia vimefuatilia Phd ya Mh. Suleman Jafo nayo ipo matatani kufutwa.

Kwa kauli hii kaeni mkao wa kufuatilia yanayojiri na kwa sasa amepiga kimya kama mtu aliyefiwa na wazazi .
Kwa kumbukumbu zangu siyo jambo geni kwani huko majuu PhD ya aliyekuwa waziri katika serikali ya ujerumani ya mwanamama Angel Merkel ajulikanae kama Theodor Gotenberg kama sijakosea jina, ilifutwa baada ya kuonekana ame copy na ku paste kazi za watu wengine na hivyo kupelekea kujiuzulu. Kwa hiyo natarajia bwana madelu na Jaffo wangejiuzulu mara moja baada ya kuonekana PhD zao ni za mwendokasi aka. za mchongo......​
 
siku hizi pia kuna masters nyingi za voda fasta ambazo walizichukua watumishi wa umma ili waweze kupandishwa vyeo.ndo maana kwa sasa kuna wimbi kubwa la viongozi wa taasisi za umma ambao hawana maadili ya kazi.hizi masters zilipewa majina ya executive course ambapo unajisomea nyumbani halafu unaenda kufanya mtihani.je wewe mtumishi wa umma huo muda wa kujisomea nyumbani utaupata wapi?kwanza ukitoka kazini umechoka na ukirudi nyumbani unakutana na watoto hapa kuna kujisomea.waafrika tulilogwa tangu dunia inaanza.
Watu pekee wanaosoma kweli wakiwa kazini ni wakufunzi/walimu pekee, wengine wanaenda kuchukua vyeti.

Hao wote walienda kuchukua hizo PhDs kwakuwa waliona mzee anazipenda sana.
 
Watu pekee wanaosoma kweli wakiwa kazini ni wakufunzi/walimu pekee, wengine wanaenda kuchukua vyeti.

Hao wote walienda kuchukua hizo PhDs kwakuwa waliona mzee anazipenda sana.
Wakufunzi ni sehemu ndogo sana ya wanafunzi wa masters, wengi wanaomba ruhusa ya miaka miwili makazini wanarudi chuo na maarifa wanayopata ni yaleyale kama hao wakufunzi maana wanafundishwa na wahadhiri walewale na unakuta wamesoma pamoja kutokea degree ya kwanza na wanaweza kuwa bora zaidi yao. Tujaribu kuongea kwa uhalisia badala ya kufanya exaggerations ili kuponda kundi la watu fulani waonekane hawafai lolote.​
 
Tumelalamika muda mrefu kuwa kuna PhD zinatolewa kwa baadhi ya wanasiasa wa Tanzania, kama njungu kupitia vyuo vikuu vya Tanzania

Kuna tetesi kuwa East Africa university quality assurance wanatarajia kuifuta PhD ya Mwigulu Nchemba baada ya kuonekana kukopy andiko la mtu mwingine.

Vyanzo vyetu pia vimefuatilia Phd ya Mh. Suleman Jafo nayo ipo matatani kufutwa.

Kwa kauli hii kaeni mkao wa kufuatilia yanayojiri na kwa sasa amepiga kimya kama mtu aliyefiwa na wazazi .
Jaffo Sawa kabisa. binafsi nilikuwa na mashaka nayo tangu inatangazwa... jamaa ana presentation za undergraduate kabisa japo ni waziri afu uniambie ana PhD? Jafo hapana
mwingine ni Dotto biteko.... yule hana PhD Presentation za kitoto sana anafanya hazifanani na PhD
Futa futa futa
 
Back
Top Bottom