Philosophy of Religion: Uthibitisho wa uwepo wa Mungu kwa hoja ya Ufunuo na maandiko matakatifu

Philosophy of Religion: Uthibitisho wa uwepo wa Mungu kwa hoja ya Ufunuo na maandiko matakatifu

Atheists wa jamii ya wapi hao wanaoamini hakuna Mungu?
Wale ambao wenye madai ya kudai kuwa hakuna Mungu au miungu, madai hayo yamejengwa kwenye msingi wa imani. Kama sivyo basi niambie hayo madai ya kusema hakuna Mungu or miungu mmeyajenga kwenye msingi upi au hoja ya msingi yenye kufanya mdai kuwa hakuna God or gods?
 
MUNGU YUPO , kuwepo kwa Mungu hakuthibitishi kwa maandiko ya dini yoyote ila maandiko yamemtaja Mungu, wengi kwa kuamgalia maandiko wamekuja na hoja pinzani kwani vitabu hivyo haviwezi kujibu hoja kwani vipo kuelezea hasa maisha ya mwanadamu na sio kuleta majibu ukitaka kuthibitisha Mungu kwa maandiko ya dini utakwama

Mungu ni kiswahili lakini neno halisi ni muumbaji
Kwa kizungu the creator kwa maana mtengenezaji wa ulimwengu

Kwa formula ya kisayansi hakuna kitu kinachoweza kujitengeneza chenyewe lazima awepo aliye kibuni na kuiunda
Wanadamu hawawezi kutokea tu ghafla ulimwengu umepangika kwa hesabu kamili
Wanasayansi wamechunguza mambo mengi na kugundua yamefanyika kwa hesabu kamili hivyo inatoa uthibitisho kuwa alikuwepo aliyefanya kazi hii kwa umakini zaidi yani mtengenezaji (ndio watu wanamuita Mungu)

Bila hata dini hizi zetu ambazo nyingi zimekuja huku kutoka kwa wazungu na waarabu ma Babu zetu alitambua Mungu yupo ndio wakampa jina
Karibu kila kabila lina jina la Mungu kwa rugha yake hata waleta dini waliendelea kutumia majina
Tofauti tu zizopo ni namna na taratibu za kumwabudu ndio zilitofautiana na hasa hapa ndio huwa msingi wa kitu kinaitwa imani

Imani katika dini kwa rugha nyepesi ni mtazamo wa mtu au kikundi cha watu juu ya taratibu na kanuni za namna ya kufanya katika kuabudu

Mungu yupo kwa sababu yupo na sio yupo kwa imani ,imani ni mlango wa kuwasiliana naye
Hata kama hakuna wa kumwabudu bado atabaki kuwa muumbaji
Mungu ni mkuu sana binadamu ni kama sisimizi tu mbele zake uamini usiamini kwake huwezi kumuongezea chochote

Wanadamu wanamhitaji Mungu kwa faida yako na sio Mungu kumhitaji binadamu kwani akitaka kwa sekunde moja anaweza kufuta kila kiumbe akaanza upya kama wewe unavyo weza kubomoa majengo yako ukajenga upya
Mungu yupo na anatisha kama nini huyu aliyemuumba binadamu kwa ufahamu wa hali ya juu sana ukiusoma mwili wa binadamu kuna maajabu makubwa sana jicho tu la binadamu ni sayansi ya hali ja juu bado mfumo ya moyo sensor za mwili mfumo wa ulinzi ,figo nk

Wengi kwa sababu ya kuvimbewa tu ndio uja na hoja ya hakuna Mungu ,
Wenye akili walifikili na kuja na majibu ya kwamba ni "mpumbavu tu usema moyoni hakuna Mungu"

Kama ulivyo mfumo wa mwili unafanya kazi Mungu alisha maliza mambo yote kwa sasa yupo na mengine haya unayo yaona ni kanuni tu zinatenda kazi ukiamini utaona nguvu za Mungu usipoamini utaona nguvu za shetani mambo yote yanaendelea na kubadilika kwa kwanini yeye alisha maliza hana kazi nyingine ya kufanya kwetu kama ilivyo majira ya mvua kupanda na kuvuna ndiyo yalivyo maisha yote alipanga na kumaliza
Sawa ila kumbuka hujathibitisha huyo Mungu yupo
 
Wale ambao wenye madai ya kudai kuwa hakuna Mungu au miungu, madai hayo yamejengwa kwenye msingi wa imani. Kama sivyo basi niambie hayo madai ya kusema hakuna Mungu or miungu mmeyajenga kwenye msingi upi au hoja ya msingi yenye kufanya mdai kuwa hakuna God or gods?
Hiyo ni rejection sio imani

Hata wewe unapinga yesu sio Mungu

Kwa mantiki hiyo una imani mbili

Moja ya kuamini Allah na nyingine uliyoipata baada ya kuamini Yesu sio Mungu
 
Hiyo ni rejection sio imani

Hata wewe unapinga yesu sio Mungu

Kwa mantiki hiyo una imani mbili

Moja ya kuamini Allah na nyingine uliyoipata baada ya kuamini Yesu sio Mungu
"Kama sivyo basi niambie hayo madai ya kusema hakuna Mungu or miungu mmeyajenga kwenye msingi upi au hoja ya msingi yenye kufanya mdai kuwa hakuna God or gods ni ipi?"
 
"Kama sivyo basi niambie hayo madai ya kusema hakuna Mungu or miungu mmeyajenga kwenye msingi upi au hoja ya msingi yenye kufanya mdai kuwa hakuna God or gods ni ipi?"
Ni rejection tu
 
Ni rejection tu
Mkuu hapo kuna madai ya kuwa hakuna Mungu wala miungu, kwahiyo sio suala tu la kukataa kuamini uwepo wa Mungu bali mnadai hakuna Mungu wala miungu na huo ndio msimamo wenu ambao nataka kujua msingi wa hayo madai ni upi?
 
Mkuu hapo kuna madai ya kuwa hakuna Mungu wala miungu, kwahiyo sio suala tu la kukataa kuamini uwepo wa Mungu bali mnadai hakuna Mungu wala miungu na huo ndio msimamo wenu ambao nataka kujua msingi wa hayo madai ni upi?
Kukiwa kuna madai ya hakuna Mungu ndio inakuwa ni imani?
 
Kukiwa kuna madai ya hakuna Mungu ndio inakuwa ni imani?
Hayo madai yenu yapo kwenye mfumo wa imani ndiyo maana nikasema kama sio imani tu basi eleza msingi wa hayo madai ni upi?
 
Hayo madai yenu yapo kwenye mfumo wa imani ndiyo maana nikasema kama sio imani tu basi eleza msingi wa hayo madai ni upi?
Ni rejection sio imani

Atheism ni ukosefu wa imani, ukosefu wa imani sio aina fulani nyingine ya imani
 
Ni rejection sio imani

Atheism ni ukosefu wa imani, ukosefu wa imani sio aina fulani nyingine ya imani
Mkuu mie nazungumzia hilo dai la kusema hakuna Mungu wala miungu, huo si ukesefu wa imani kwamba hamuamini tu bali mnadai kuwa hakuna Mungu.

Sijui kama unaona tofauti.
 
Mkuu mie nazungumzia hilo dai la kusema hakuna Mungu wala miungu, huo si ukesefu wa imani kwamba hamuamini tu bali mnadai kuwa hakuna Mungu.

Sijui kama unaona tofauti.

Sasa kama unasema tunadai Mungu hayupo kivipi tena uhusishe dai hilo na mfumo wa imani?

Dai la kusema hakuna Mungu hiyo ni rejection ya dai linalosema kuna Mungu ambaye hajathibitishwa
 
Kwanini haiingii wakati iko based kwenye imani?

Hujui kwamba kuweka alarm ikuamshe asubuhi huku ukiamini kuwa hapo katikati hutapatwa na mauti bali utaamka salama ni imani?
Hii sio sahihi. Kwa sababu kuamka salama hakuhusiani na imani; na hali hiyo haiwezi kuwa ndio imani.
 
Kama lugha ya kiswahili bado ni changa, basi hoja yako ya kusema hakuna imani zaidi yamoja itakuwa invalid
Kwa namna gani uchanga wa lugha ya kiswahili unafanya hoja ya kwamba "hakuna imani zaidi ya moja kuwa invalid"?
 
Kwa namna gani uchanga wa lugha ya kiswahili unafanya hoja ya kwamba "hakuna imani zaidi ya moja kuwa invalid"?
Interpretation, kutumia neno moja kwenye sentensi zinazotofautina kimaana

Nina imani kesho yanga itagungwa, na kwa hivyo naibetia timu pinzani

Hata mtoto unapomrusha juu na kumdaka halafu akawa nacheka, ile pia ni imani kuwa ana amini huto mdondosha

Kuamini taarifa ya mamlaka ya hewa kuwa kesho kutakuwa na mvua kubwa halafu asubuhi nikaamka kwenda kazini nikiwa nimebeba mwavuli, hiyo ni imani kuwa nimeamini walichokisema mamlaka ya hewa kitatokea
 
Interpretation, kutumia neno moja kwenye sentensi zinazotofautina kimaana

Nina imani kesho yanga itagungwa, na kwa hivyo naibetia timu pinzani

Hata mtoto unapomrusha juu na kumdaka halafu akawa nacheka, ile pia ni imani kuwa ana amini huto mdondosha

Kuamini taarifa ya mamlaka ya hewa kuwa kesho kutakuwa na mvua kubwa halafu asubuhi nikaamka kwenda kazini nikiwa nimebeba mwavuli, hiyo ni imani kuwa nimeamini walichokisema mamlaka ya hewa kitatokea
Nafikiri hujaelewa maana ya imani. Mifano yote uliyoitoa haiendani na maana ya imani.

Kwa mfano, kwa namna gani taarifa ya mamlaka ya hali hewa iwe imani? Imani haishughuliki na mambo kama hayo ulioyatolea mfano.
 
Back
Top Bottom