Picha adimu za TANU, Julius Nyerere na wazalendo waliosahaulika katika Historia ya kudai Uhuru


Kitabu cha Mzee Sykes na simulizi zake za mdomo kwa waliobahatika kuongea naye ..kiko biased kiasi Fulani ....Kama ilivyo historia rasmi ya NCHI Hii nayo Ina mapungufu ...LENGO la kitabu cha Sykes linajulikana Pamoja na mengi mazuri yaliyomo ....
Mimi nafikiri historia ya NCHI Hii inatakiwa kuandikwa UPYA Sasa na watafiti Huru wasiopendelea upande wowote

Mfano mchango wa Watu waMikoani kwenye kupambana na uokoloni kwenye vitabu hata historia rasmi haujaandikwa ...kwa kuwa tu Hapakuwa na "kamera ..." lakini waliukataa ukoloni ....

Kuna Watu wana LENGO la kudanganya Watu kuwa wao pekee ndio walipigania Uhuru
 
Nnahisi kwa kuwa hilo ni baraza la wazee, Ali Sykes siku hizo ni kijana.

Hakuna wa kuleta pingamizi la kumpinga Sheikh Mohamed Said. Wataishia kutukana, kukashifu na maneno mengine yanayofanana na haya.
Lakini kuleta ushahidi wa kutetea kile anachokizungumzia Sheikh Mohamed Said kama anavyofanya sasa, upande wa pili hawataweza kufanya. Wataishia kututukana tu na kutukashifu.
Nawakubali sana Wajapan Polisi wake,wanapokukamata kwa kukutilia shaka kwa jambo fulani, kwenye maswali yao utaruka ruka wee, mwisho wanakupiga nyundo na picha zako za matukio.
Kutoka hapo tena unakuwa mpole.
Ndicho anachofanya Sheikh Mohamed Said, kadiri wanavyotukana na kumuita muongo yeye analeta vitu tu,upande wa pili vyao hatuvioni tulinganishe mambo, wanaishia kutukana tu.
Mwenyezimungu akupe umri mrefu Sheikh Mohamed Said, akufanyie wepesi kila penye uzito ili upate kutuletea zaidi hivi.UKWELI HUWA UNACHELEWA TU, LAKINI KUJULIKANA HUWA LAZIMA.
 

Tena ukiwaambia tupeni basi historia za wazee wenu, ndiyo wanatokwa povu kila namna, watajibu nini?
 
Uhuru ulitafutwa maeneo ya Pwani na kidogo Tabora mjini kwa maustaz pia wala sio huko kwa Wamasai na Wasukuma.

Huo ndio uongo ambao wewe na wenzio mnataka uwe ukweli.

Kwa kufurahisha roho yako, ngoja nikubaliane nawe:Uhuru ulitafutwa na waislam tu wa pwani na Tabora, wengine hawakushiriki.
 
Huo ndio uongo ambao wewe na wenzio mnataka uwe ukweli.

Kwa kufurahisha roho yako, ngoja nikubaliane nawe:Uhuru ulitafutwa na waislam tu wa pwani na Tabora, wengine hawakushiriki.

Nanren,
Harakati zilipangika kama ilivyo hapo chini:

[TABLE="width: 601"]
[TR]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]· Central Province, 1955 (Omari Suleiman na Haruna Taratibu)

[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]· Southern Province, 1955 (Sheikh Yusuf Badi, Chembera, Salum Mpunga)

[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]· Western Province, 1955 (Bilali Rehani Waikela, Abdalla na Maulid Kivuruga)

[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]· Tanga Province, 1956 (Sheikh Rashid Sembe, Rashid Makoko)

[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]· TANU in Mombasa, Kenya, 1957 (Ismail Bayumi)

Nimekuwekea majina machache tu kwani huko Kilimanjaro kulikuwa na Yusuf Olotu, Mwanza Saadan Abdu Kandoro nk. nk.[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 

Sawa. Asante kwa ufafanuzi.
Hao uliowataja kwa provinces, walikuwa ni kama waratibu-coordinators. Je waliokuwa chini yao wote walikuwa wa dini moja? Hawakuwepo wapagani, christians, bohora? Kama walikuwepo, je ipo haja ya kulalamika kwamba hawapo kwenye "limelight"?
Miaka uliyotaja hapo kwanzia 1955-1957, harakati zilipangiliwa kama ulivyoonesha.
Je miaka mingine hakukuwa na harakati? Au miaka mingine ilikuwa ni ya majina ya upande wa pili ndio maana inabidi isioneshwe?
Vyama vya ushirika vilikuwepo kabla ya miaka hiyo kwenye baadhi ya mikoa, na vilishiriki kwa namna fulani kwenye vuguvugu za uhuru, mbona huvitaji? au vilikuwa na majina ambayo ni "SIYO"?
 
Ni kweli Nyerere alikuwa na wazee wa TANU.
Inawezekana chama kilikuwa cha kieneo zaidi , yaani Pwani na dhahiri wakapatikana hao wazee wa awali.

Lakini jambo lolote ni mchakato na mabadiliko hutokea kutokana na kasi.

Si ajabu baada ya uhuru changamoto zilikuwa tofauti na ndivyo game ya siasa ilivyo , wanakuja watu wapya kabisa.
 

Nanren,
Soma kitabu cha Abdul Sykes nimeanza na African Association kuanzia 1929.
Hiyo hapo chini ni picha ya ofisi mpya ya CCM imeunganishwa na ofisi ya zamani.

Mbele ya ofisi hizo ambazo ndipo ilipoasisiwa TANU kutoka TAA ni ''glass house,''
ni nyumba ya akina Maalim Faiza na Faiza kakulia hapa akimuona Nyerere toka utoto wake.

 

Soma kipande hiki:

By Mohamed Said

Nanren,
Harakati zilipangika kama ilivyo hapo chini:

[TABLE="class: cms_table, width: 601"]
[TR]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]· Central Province, 1955 (Omari Suleiman na Haruna Taratibu)
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]· Southern Province, 1955 (Sheikh Yusuf Badi, Chembera, Salum Mpunga)
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]· Western Province, 1955 (Bilali Rehani Waikela, Abdalla na Maulid Kivuruga)
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]· Tanga Province, 1956 (Sheikh Rashid Sembe, Rashid Makoko)
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]· TANU in Mombasa, Kenya, 1957 (Ismail Bayumi)

Nimekuwekea majina machache tu kwani huko Kilimanjaro kulikuwa na Yusuf Olotu, Mwanza Saadan Abdu Kandoro nk. nk.
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Wazee wetu walikuwa nadhamira ya dhati kujitolea na kujengea nchi , cyo sasa ufisafi mtupu c mkubwa wala mdogo wote mlemle
 

Kila jambo na kila kitu kina tafsiri mbili.
Tafsiri mbaya na tafsiri nzuri sasa ni wajibu wa muhusika kuamua vipi atafsiri ww umetafsiri hoja ya mzee MS kuwa ya udini lakini sidhani kama mzee Ms nia yake na tafsiri yake kuwa ni udini.
Nadhani kama mzee Ms ingekuwa nia yake ni udini asingesita kuandika WAISLAM WALIOGOMBANIA UHURU WALIO SAHAULIKA.
Mm nadhani ww ndio mdini ambae ulie kereka na bandiko la mzee Ms.
Na ndio ulie tafsiri vibaya na kwa mtazamo wa udini aidha kwa kuwa alie leta hoja mzee Ms ni muislam au kwa kuwa anaezungumziwa ni muislam.
Angalizo langu kama unaona wapo watz wengine ambao mzee Ms hawazungumzii aidha kwa kuwa si waislam tu basi tumia fursa hiyo kutuletea tuwajue na tujadili kwa heshima na adabu.
 

Salahsahim4,
Wakati naandika kitabu hiki cha historia ya uhuru wa Tanganyika haikunipitikia
hata kwa mbali sana kuwa kitabu hiki kitakuja kuumiza baadhi ya jamii kwa kiasi
hiki ninachoshuhudia.

Kuwa Waislam mchango wao katika kupigania uhuru wa Tanganyika hauna kifani
huu ndiyo ukweli na kwa bahati mbaya sana hapa ndipo kilipo chanzo cha baadhi
yetu kukerwa na kitabu hiki.

Lakini haya niliyoandika mimi zaidi ya miaka 18 sasa watoto wa wazalendo ambao
baba zao ndiyo waliokuwa mstari wa mbele kupanga mipango ya kuung'oa ukoloni
nao sasa wanazungumza.

Hawa watoto wote wanasikitika kuwa wazee wao hawajapewa na taifa hili ile
heshima wanayostahili baba zao.

Kwa faida ya Majlis naweka hivi viungo hapa chini msomaji asome:
Mohamed Said: RAIA TANZANIA: KLEIST ABDULWAHID SYKES AMZUMGUMZIA BABA YAKE KATIKA HISTORIA YA UHURU WA TANGANYIKA
Mohamed Said: FB: JUMA MWAPACHU AMZUNGUMZIA BABA YAKE KATIKA HISTORIA YA UHURU WA TANGANYIKA

Naunga mkono hoja yako kuwa ikiwa kuna mtu anaona kuna baadhi ya wazalendo
ambao walistahili kuelezwa khabari zao katika kitabu changu nami sikuwaeleza
ni vyema habari zao zikaandikwa ili zisomwe na kuhifadhika.
 

Mzee ms huyu kleist alikuwa na urafiki mkubwa na mzee Robat Makange unaweza kumzungumziaje mze Makange na familia hiyo na kleist na uhuru wa tanganyika?
 

Sheik Mohamed Said,
Is Yusuf Olotu not the father of the famous actor Ahmed Y. Olotu a.k.a. Mzee Chilo?
 
Mzee ms huyu kleist alikuwa na urafiki mkubwa na mzee Robat Makange unaweza kumzungumziaje mze Makange na familia hiyo na kleist na uhuru wa tanganyika?

Salahsahim4,
Robert Makange na Kheri Rashid Baghdelleh walikuwa wahariri wa gazeti
la Mwananchi wakati wa kupigania uhuru.

Wazalendo hawa wawili walifungwa jela na Waingereza kwa kosa la ''uchochezi.''
Robert Makange ni katika wanachama wa mwanzo kabisa katika TANU.

Hii picha hapo chini inamuonyesha Makange mwaka 1955 akiwa katika kundi
lilomsindikiza Nyerere Uwanja wa Ndege alipokwenda UNO:



Kushoto: Rashid Sisso, Robert Makange, Zuberi Mtemvu, Iddi Faiz Mafongo, Julius Nyerere, John Rupia, Bi. Titi Mohamed
 
Nakusoma Mudir Mohamed Said.
 
Last edited by a moderator:

Shukran mzee wangu MS nafurahia jibu lako zuri.
Mm binafsi namfaham marehem mzee makange na klest.
 
Shukran mzee wangu MS nafurahia jibu lako zuri.
Mm binafsi namfaham marehem mzee makange na klest.

Salahsahim,
Mimi sikupata kufahamiana na Mzee Makange ila ni mtu nikimuona tu.

Kleist mimi tunafahamiana toka utoto kwa kuwa kwanza babu yangu Salum
Abdallah
alikuwa akifanya kazi na babu yake Kleist Tanganyika Railways kisha
wakiishi jirani Mtaa wa Kipata na walikuwa pamoja katika siasa za mji.

Bibi yangu Zena bint Farjallah na bibi yake Kleist Bi. Mluguru biti Mussa walikuwa
mashoga.

Baba zetu walikuwa marafiki na mama yake Klest Bi. Mwamvua na mama yangu
Bi. Baya walikuw apia mashoga.

Uhusiano huu wa miaka mingi kati ya wazee wetu ulinirahisishia sana kuaminika na
kuweza kupewa nyaraka za familia kuzisoma.

Kleist ni mkubwa kwangu kwa miaka miwili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…