Picha: Ephrahim Kibonde wa Clouds FM atiwa nguvuni

Picha: Ephrahim Kibonde wa Clouds FM atiwa nguvuni

Ingekuwa wenzetu huko Ulaya kwa upuuzu alioufanya asingepata tena deal za kucheza matangazo maana kampuni makini haiwezi kujihusisha na watu wahuni, ila hapa Bongo eti hiyo ni kik
 
Habari JF lovers,
Hii ishu ya Kibonde ni kama ime kick sana, kwamba alijaribu kuvunja sheria huku akiwa amelewa,
The fact is Kibonde alikua anatengeneza Tangazo la Usalama Barabarani "TII SHERIA BILA SHURUTI"

Tangazo au SERIES kabisa........ Maana barabarani hadi kituo cha polisi na kuwekwa Mahabusu
 
Hayo yote waliyotaka ni makosa ila kosa moja hapo ambalo anaweza kuchomoka ambalo ni kubwa ni hilo kosa la kunywa pombe,kama walikuwa wamelewa na wakakataa kupimwa basi ni good advantage hata mahakamani wakiambiwa hivyo watawauliza police mna ushahidi gani.

Me mwenyewe endapo nimekamatwa nimelewa sikubali kupima....kupoteza ushahidi

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Habari JF lovers,
Hii ishu ya Kibonde ni kama ime kick sana, kwamba alijaribu kuvunja sheria huku akiwa amelewa,
The fact is Kibonde alikua anatengeneza Tangazo la Usalama Barabarani "TII SHERIA BILA SHURUTI"

Hilo "tangazo" hata likitoka litachosha sana watazamaji maana ni refu mno.

Kuanzia makumbusho,mwenge,ubungo mpaka lockup orstebay!
 
habari ya nyongeza kutoka kwa elizabeth hombo iliyopatikana hapa hapa jf inasema kuwa: Watangazaji maarufu wa redio nchini, ephraim kibonde na gadner g. Habash, wametiwa mbaroni katika kituo cha polisi cha oysterbay, jijini dar es salaam baada ya kudaiwa kusababisha ajali na kukaidi amri ya askari wa usalama barabarani. kibonde ambaye amejizolea umaarufu kupitia kipindi cha ‘jahazi’ kinachorushwa na kituo cha redio cha clouds fm akiwa na mtangazaji mwenzake wa radio times, gadner, walikutwa na mkasa huo jana saa 12 asubuhi katika eneo la makumbusho.

taarifa zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na kamanda wa polisi mkoa wa kinondoni, camillius wambura, zilieleza kuwa kibonde ambaye alikuwa dereva wa gari hilo aligonga kwa nyuma gari lililokuwa likiendeshwa na raia wa kigeni (mzungu).
akizungumza na gazeti hili kupitia simu yake ya kiganjani, kamanda wambura alisema baada ya kibonde kusababisha ajali hiyo, alikaidi amri ya askari wa usalama barabarani iliyomtaka asimame ili wapime na badala yake aliondoa gari kwa mwendo kasi hali iliyoashiria alikuwa amekimbia. alisema baada ya kukaidi amri hiyo, askari aliyekuwepo eneo la tukio naye alipanda gari jingine kwa nia ya kumfukuza na kwamba alipofika eneo la mwenge alifanikiwa kumsimamisha na kisha kupanda katika gari lake ili warudi eneo ilikotokea ajali.

kwa mujibu wa wambura, baada ya askari huyo kupanda kwenye gari la kibonde, mtangazaji huyo hakurudi kwenye eneo la tukio na badala yake aliendelea kukata mitaa mingine.
“bahati nzuri askari wetu huyo alikuwa anawasiliana na wenzake, walipofika eneo la ubungo mataa wakawawekea kizuizi kilichowasaidia kuwakamata. “…nilipata taarifa hizo za kibonde nikiwa kwenye kikao, ni kweli alisababisha ajali majira ya saa 12 asubuhi pale makumbusho na alimgonga mzungu ambaye hata hivyo sikuishika namba ya gari lake,” alisema kamanda wambura. alieleza kuwa baada ya askari wa ubungo kufanikiwa kuwakamata, waliwafikisha katika kituo cha polisi cha oysterbay na walibaini kuwa watangazaji hao walikuwa wamelewa. “walipofikishwa kituoni na kutakiwa kupimwa ulevi waligoma… kwa sababu kibonde alikuwa hana uwezo wa kuendesha tena gari na walikuwa wanatoa lugha chafu za matusi kwa askari wetu,” alisema.

alipoulizwa kuwa ni sheria zipi walizozivunja, kamanda wambura aliyataja makosa matano, ambayo ni kusababisha ajali, kutokutii amri ya askari, kukimbia na kutoroka na askari, kutoa lugha chafu za matusi na kukataa kupimwa ulevi.
kamanda wambura alisema kwa sasa wanaendelea na upelelezi wa tukio hilo, na baada ya kuukamilisha watapeleka jalada kwa wakili wa serikali ili watangazaji hao washitakiwe. akiwazungumzia watangazaji hao, kamanda wambura alisema kuwa wao wanawaona kama wahalifu wa makosa ya jinai na kamwe hawatawachukulia kama watu maarufu.
“sisi hatutajali kama watangazaji hao ni watu maarufu, na kwamba mbele ya uso wa sheria hakuna umaarufu,” alisisitiza wambura ambaye hadi tunakwenda mitamboni jana jioni alisema watangazaji hao walikuwa bado rumande.

hebu njoeni sasa enyi wake zake kibonde mnaomtetea tangu jana eti ni tangazo la utii bila shuruti walilopewa kuliandaa. Kauli ya polisi ndo hii hapa. Kama vp ikanusheni na yenyewe, manake si ndo nyie mliompa kazi kamanda poti wambura!
 
Tatizo ni foleni wandugu. Tuko wengi tuna hasira kutokana na kucheleweshwa makazini na foleni ya magari jijini. Maaskari wa barabarani ni wasumbufu sana,mara nyingi wanachelewesha magari ya upande fulani,na kuruhusu ya upande mwingine kwa muda mrefu. Nafikiri jamaa alikuwa anawahi airport. Lakini kwa nini adhalilishwe hadharani kiasi hicho,askari wetu wanatumia maguvu zaidi,kichwani zero. Sikubaliani na kibonde kwa mengi,lakini kwa hili amedhalilihwa.

Unaambiwa askari katekwa, katukanwa bado unataka amkamate kwa kwa mahaba? Ok foleni inachelewesha watu, kwa hiyo unaamua kumgonga aliyembele yako kisha husimami unakimbia kwani huyo aliyembele yako ndiye kasababisha foleni.
Kitendo alichofanya Kibonde ni huo ulevi na majidai tuu kwa kujidhania ana umaarufu wa kumwezesha kufanya atakalo. Hapo kuna makosa ya faini na ya jela, ngoja sheria ichukue mkondo ndio watu watajifunza.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Hii post mnaihamisha sana jana mliitoa kule jukwaa la habari mchanganyiko mkaipeleka jamii photos leo tena mmeitoa na kuileta huku celebrity mnatuchanganya bana sisi mada yetu kwa wikiend hii ndo hii basi!mimi nimeitafuta kweli nikapagawa nikijua mods wameifuta!mambo gan haya ss!
Duu kumbe kuna updates nzuri kwamba wako na Gadner heeee imbombo ngafuuu!kutoka naona mpaka kesho!duuu bongo mapya yapo kila siku!
 
Invisible
mlituambia Jamii Media imeajili waandishi wake wa habari sasa wanafanya
nini hii thread tumeshaanza kulishana matango pori ni kwa nini
waandishi wa Jamii media polisi tupate usahihi wa habari hii?

kwani bado kuna utata?
 
Last edited by a moderator:
Sasa gadna anaunganishwaje kwenye kesi hyo?maana nijuavyo mm dreva ni kibonde, mtusaidie ili wengine tujue!

Inawezekana na yeye alihusika katika kutoa lugha za mauzi kwa askari wa barabarani.
 
Unaambiwa askari katekwa, katukanwa bado unataka amkamate kwa kwa mahaba? Ok foleni inachelewesha watu, kwa hiyo unaamua kumgonga aliyembele yako kisha husimami unakimbia kwani huyo aliyembele yako ndiye kasababisha foleni.
Kitendo alichofanya Kibonde ni huo ulevi na majidai tuu kwa kujidhania ana umaarufu wa kumwezesha kufanya atakalo. Hapo kuna makosa ya faini na ya jela, ngoja sheria ichukue mkondo ndio watu watajifunza.


Sent from my iPad using JamiiForums

Wafungwe tuuu na wakitoka hiyo kesho basi na mie namkata kerbu trafik.
 
Habari ya nyongeza kutoka kwa ELIZABETH HOMBO iliyopatikana hapa hapa JF inasema kuwa: Watangazaji maarufu wa redio nchini, Ephraim Kibonde na Gadner G. Habash, wametiwa mbaroni katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, jijini Dar es Salaam baada ya kudaiwa kusababisha ajali na kukaidi amri ya askari wa usalama barabarani. Kibonde ambaye amejizolea umaarufu kupitia kipindi cha ‘Jahazi’ kinachorushwa na kituo cha redio cha Clouds Fm akiwa na mtangazaji mwenzake wa Radio Times, Gadner, walikutwa na mkasa huo jana saa 12 asubuhi katika eneo la Makumbusho.

Taarifa zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, zilieleza kuwa Kibonde ambaye alikuwa dereva wa gari hilo aligonga kwa nyuma gari lililokuwa likiendeshwa na raia wa kigeni (mzungu).
Akizungumza na gazeti hili kupitia simu yake ya kiganjani, Kamanda Wambura alisema baada ya Kibonde kusababisha ajali hiyo, alikaidi amri ya askari wa usalama barabarani iliyomtaka asimame ili wapime na badala yake aliondoa gari kwa mwendo kasi hali iliyoashiria alikuwa amekimbia. Alisema baada ya kukaidi amri hiyo, askari aliyekuwepo eneo la tukio naye alipanda gari jingine kwa nia ya kumfukuza na kwamba alipofika eneo la Mwenge alifanikiwa kumsimamisha na kisha kupanda katika gari lake ili warudi eneo ilikotokea ajali.

Kwa mujibu wa Wambura, baada ya askari huyo kupanda kwenye gari la Kibonde, mtangazaji huyo hakurudi kwenye eneo la tukio na badala yake aliendelea kukata mitaa mingine.
“Bahati nzuri askari wetu huyo alikuwa anawasiliana na wenzake, walipofika eneo la Ubungo Mataa wakawawekea kizuizi kilichowasaidia kuwakamata. “…Nilipata taarifa hizo za Kibonde nikiwa kwenye kikao, ni kweli alisababisha ajali majira ya saa 12 asubuhi pale Makumbusho na alimgonga Mzungu ambaye hata hivyo sikuishika namba ya gari lake,” alisema Kamanda Wambura. Alieleza kuwa baada ya askari wa Ubungo kufanikiwa kuwakamata, waliwafikisha katika kituo cha Polisi cha Oysterbay na walibaini kuwa watangazaji hao walikuwa wamelewa. “Walipofikishwa kituoni na kutakiwa kupimwa ulevi waligoma… kwa sababu Kibonde alikuwa hana uwezo wa kuendesha tena gari na walikuwa wanatoa lugha chafu za matusi kwa askari wetu,” alisema.

Alipoulizwa kuwa ni sheria zipi walizozivunja, Kamanda Wambura aliyataja makosa matano, ambayo ni kusababisha ajali, kutokutii amri ya askari, kukimbia na kutoroka na askari, kutoa lugha chafu za matusi na kukataa kupimwa ulevi.
Kamanda Wambura alisema kwa sasa wanaendelea na upelelezi wa tukio hilo, na baada ya kuukamilisha watapeleka jalada kwa wakili wa serikali ili watangazaji hao washitakiwe. Akiwazungumzia watangazaji hao, Kamanda Wambura alisema kuwa wao wanawaona kama wahalifu wa makosa ya jinai na kamwe hawatawachukulia kama watu maarufu.
“Sisi hatutajali kama watangazaji hao ni watu maarufu, na kwamba mbele ya uso wa sheria hakuna umaarufu,” alisisitiza Wambura ambaye hadi tunakwenda mitamboni jana jioni alisema watangazaji hao walikuwa bado rumande.

Et Tangazo la kutii sheria bila shuruti!
 

Attachments

  • Kibonde.jpg
    Kibonde.jpg
    8.7 KB · Views: 293
Et Tangazo la kutii sheria bila shuruti!
Kama ni tangazo litavunja record ya matangazo dunian kote kwa kufuatiliwa na watu wengi, ila najua pombe sa iv zimekwisha so anaomba msmaha wayamalize na aliyemgonga, kama namuona anavyo;!!
Ooo afande samahan ujue shetan alinipitia,
Afnde;- alikupitia kwenda wapi?
Kibonde!:-ujue afande npo silias, ntalipa garama zote w nhurumie tu, m ntamalizana nae yele hata gari ntamnunua lingine!!

Jaman mnaokunywa maji ya mande kazi kwenu!
 
Back
Top Bottom