Picha: Ephrahim Kibonde wa Clouds FM atiwa nguvuni

Picha: Ephrahim Kibonde wa Clouds FM atiwa nguvuni

It's a shame kwa mtu kma yeye. Kwanza ni ushamba kukimbia trafiki. Simama, mmalize tatizo. Pumbavu
 

Attachments

  • 1407675855928.jpg
    1407675855928.jpg
    60.3 KB · Views: 1,218
Shame on u Kibonde sikutegemea unaweza kufanya vitu kama ulivyofanya leo pale ubungo asbh uuuuh ivi nn maana ya public figure ya Tz hii mnatuonyesha nn duh Polen clouds maana jamaa kachemsha.

Jamani mshasema ni KIBONDE.. Jina tu linasadifu akili yake.. Yani huyu ni kibonde wa akili na busara... Tehhhhhh
 
Shame on u Kibonde sikutegemea unaweza kufanya vitu kama ulivyofanya leo pale ubungo asbh uuuuh ivi nn maana ya public figure ya Tz hii mnatuonyesha nn duh Polen clouds maana jamaa kachemsha.


attachment.php


UPDATES:






Jamani mshasema ni kibonde Jina lake linasadifu akili na busara zake .. Yan huyu ni kibonde haswa tehhh
 
Jamaa(Kibonde)sio kwamba alikuwa anategemea kukwaa ukuu wa wilaya moja hapa nchini?.....najua utaachiwa soon broda kwani uliitetea sana serikali ya CCM kupitia media!
 
attachment.php

Kayanda anaenda kumtoa kama nani? Ni mwana-sheria wao?
 
Tupeane updates jamani, huyu jamaa bado anakojoa kwenye ndoo mpaka sasa?
 
na si kama mdhaniavo


acha kupotosha watu.

pole sana. Soma hapa mchini
elizabeth hombo watangazaji maarufu wa redio nchini, ephraim kibonde na gadner g. Habash, wametiwa mbaroni katika kituo cha polisi cha oysterbay, jijini dar es salaam baada ya kudaiwa kusababisha ajali na kukaidi amri ya askari wa usalama barabarani.
Kibonde ambaye amejizolea umaarufu kupitia kipindi cha ‘jahazi' kinachorushwa na kituo cha redio cha clouds fm akiwa na mtangazaji mwenzake wa radio times, gadner, walikutwa na mkasa huo jana saa 12 asubuhi katika eneo la makumbusho.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na kamanda wa polisi mkoa wa kinondoni, camillius wambura, zilieleza kuwa kibonde ambaye alikuwa dereva wa gari hilo aligonga kwa nyuma gari lililokuwa likiendeshwa na raia wa kigeni (mzungu).
Akizungumza na gazeti hili kupitia simu yake ya kiganjani, kamanda wambura alisema baada ya kibonde kusababisha ajali hiyo, alikaidi amri ya askari wa usalama barabarani iliyomtaka asimame ili wapime na badala yake aliondoa gari kwa mwendo kasi hali iliyoashiria alikuwa amekimbia.
Alisema baada ya kukaidi amri hiyo, askari aliyekuwepo eneo la tukio naye alipanda gari jingine kwa nia ya kumfukuza na kwamba alipofika eneo la mwenge alifanikiwa kumsimamisha na kisha kupanda katika gari lake ili warudi eneo ilikotokea ajali.
Kwa mujibu wa wambura, baada ya askari huyo kupanda kwenye gari la kibonde, mtangazaji huyo hakurudi kwenye eneo la tukio na badala yake aliendelea kukata mitaa mingine.
"bahati nzuri askari wetu huyo alikuwa anawasiliana na wenzake, walipofika eneo la ubungo mataa wakawawekea kizuizi kilichowasaidia kuwakamata.
"…nilipata taarifa hizo za kibonde nikiwa kwenye kikao, ni kweli alisababisha ajali majira ya saa 12 asubuhi pale makumbusho na alimgonga mzungu ambaye hata hivyo sikuishika namba ya gari lake," alisema kamanda wambura.
Alieleza kuwa baada ya askari wa ubungo kufanikiwa kuwakamata, waliwafikisha katika kituo cha polisi cha oysterbay na walibaini kuwa watangazaji hao walikuwa wamelewa.
"walipofikishwa kituoni na kutakiwa kupimwa ulevi waligoma… kwa sababu kibonde alikuwa hana uwezo wa kuendesha tena gari na walikuwa wanatoa lugha chafu za matusi kwa askari wetu," alisema.
Alipoulizwa kuwa ni sheria zipi walizozivunja, kamanda wambura aliyataja makosa matano, ambayo ni kusababisha ajali, kutokutii amri ya askari, kukimbia na kutoroka na askari, kutoa lugha chafu za matusi na kukataa kupimwa ulevi.
Kamanda wambura alisema kwa sasa wanaendelea na upelelezi wa tukio hilo, na baada ya kuukamilisha watapeleka jalada kwa wakili wa serikali ili watangazaji hao washitakiwe.
Akiwazungumzia watangazaji hao, kamanda wambura alisema kuwa wao wanawaona kama wahalifu wa makosa ya jinai na kamwe hawatawachukulia kama watu maarufu.
"sisi hatutajali kama watangazaji hao ni watu maarufu, na kwamba mbele ya uso wa sheria hakuna umaarufu," alisisitiza wambura ambaye hadi tunakwenda mitamboni jana jioni alisema watangazaji hao walikuwa bado rumande.
 
Ni tangazo, kuna rafiki yangu yuko Clouds Media ameniambia.
 
Utii wa "SHERI" bila shuruti ni jina la movie,kampuni au nini hasa!
 
Back
Top Bottom