PICHA: Hili jengo linalojengwa Kariakoo kwa PPP ni balaa ni zaidi ya Mlimani City unaambiwa Serikali itajizolea zaidi ya TZS 2.5bn kila mwaka

PICHA: Hili jengo linalojengwa Kariakoo kwa PPP ni balaa ni zaidi ya Mlimani City unaambiwa Serikali itajizolea zaidi ya TZS 2.5bn kila mwaka


Hatimaye PPP ya David Kafulila iliyoanzishwa kwa mujibu wa sheria namba 103 ya mwaka 2010 ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2014, 2018 na 2023 imeanza kuzaa matunda chanya kwa Watanzania hasa baada ya kuanza kutumika kwa marekebisho mapya ya ya mwaka 2023 ya Sheria hiyo.

PPP kwa kumtumia mbia mzawa toka kampuni ya Tosh Logistics Limited wanajenga jengo kubwa huenda ikawa ni zaidi ya lile la Mlimani City kwa gharama ya TZS 36.7bn wakati matumizi yatagharimu kiasi cha TZS 13.3bn litakalokuwa na wapangaji zaidi ya 900 lenye ghorofa 10 kwenda juu.

Mkurugenzi Mtendaji wa PPP-Centre Bw. David Kafulila ameiambia kamati ya Bunge ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kuwa Dar es Salaam City Council's Economic and Development Corporation (DDC) katika wakati wote wa Ujenzi wa mradi huo kila mwaka watajizolea kiasi cha TZS 2 bilioni na baada ya mradi huo kukamilika watalipwa kiasi cha TZS 2.5 bilioni kama kodi ya jengo tu bila kuhesabu kodi za TRA pamoja na shuru zingine mbalimbali lakini kubwa zaidi baada ya muda wa mkataba kuisha jengo hilo litakuwa ni mali halali ya serikali ya Tanzania.

Mkurugenzi huyo ameiambia kamati hiyo ya Bunge kuwa Ujenzi wa mradi huo ni miongoni mwamiradi yenye mikataba bora zaidi ya uwekezaji na Ubia kuwahi kushuhudiwa hapa kwenye ardhi ya Tanzania.

Mkurugenzi huyo ameishukuru na kuipongeza kamati hiyo ya Bunge kwa kutembelea mradi huo wa Ubia huku akiomba ushirikiano zaidi kati ya TAMISEMI na PPP ili kwa pamoja waweze kuvuta mitaji toka sekta binafsi ili kujenga miradi yenye tija na thamani halisi ya fedha kwa manufaa ya Taifa kwani miradi hii itaipatia Serikali Kodi pamoja na tozo mbalimbali na hivyo kuchochea ukuaji wa Uchumi endelevu huku Serikali ikiachwa ifanye miradi ile tu ambayo haina sura ya kibiashara na hivyo kuipa nafuu zaidi Serikali katika kutafuta Mikopo na misaada mbalimbali toka kwa wahisani na mashirika mbalimbali nje na ndani ya nchi.
Hongera sana Rais SAMIA
 
Kwa akili yako kiasi gani kinapaswa kulipwa? Hata mimi naona ni ndogo ukizingatia jengo litakuwa na wapangaji 900! Kwa K/koo unit ya biashara si chini ya Tshs 1,000,000 kwa mwezi! Hili jengo lingepaswa litengeneze Tshs 900,000,000 kwa mwezi na si chini ya Tasha 10 bln kwa mwaka
Pesa zote ni za mwekezaji, serikali katoa kiwanja tu hapo na analipwa. 2.5bn kwa mwaka, hahusiki na chochote kingine. Unadhani mwekezaji anagenerate faida gani? Na hayo mapato ya serikali ni nje ya kodi zitazotozwa hapo.

Tusome na tuache kupayuka
 

Hatimaye PPP ya David Kafulila iliyoanzishwa kwa mujibu wa sheria namba 103 ya mwaka 2010 ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2014, 2018 na 2023 imeanza kuzaa matunda chanya kwa Watanzania hasa baada ya kuanza kutumika kwa marekebisho mapya ya ya mwaka 2023 ya Sheria hiyo.

PPP kwa kumtumia mbia mzawa toka kampuni ya Tosh Logistics Limited wanajenga jengo kubwa huenda ikawa ni zaidi ya lile la Mlimani City kwa gharama ya TZS 36.7bn wakati matumizi yatagharimu kiasi cha TZS 13.3bn litakalokuwa na wapangaji zaidi ya 900 lenye ghorofa 10 kwenda juu.

Mkurugenzi Mtendaji wa PPP-Centre Bw. David Kafulila ameiambia kamati ya Bunge ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kuwa Dar es Salaam City Council's Economic and Development Corporation (DDC) katika wakati wote wa Ujenzi wa mradi huo kila mwaka watajizolea kiasi cha TZS 2 bilioni na baada ya mradi huo kukamilika watalipwa kiasi cha TZS 2.5 bilioni kama kodi ya jengo tu bila kuhesabu kodi za TRA pamoja na shuru zingine mbalimbali lakini kubwa zaidi baada ya muda wa mkataba kuisha jengo hilo litakuwa ni mali halali ya serikali ya Tanzania.

Mkurugenzi huyo ameiambia kamati hiyo ya Bunge kuwa Ujenzi wa mradi huo ni miongoni mwamiradi yenye mikataba bora zaidi ya uwekezaji na Ubia kuwahi kushuhudiwa hapa kwenye ardhi ya Tanzania.

Mkurugenzi huyo ameishukuru na kuipongeza kamati hiyo ya Bunge kwa kutembelea mradi huo wa Ubia huku akiomba ushirikiano zaidi kati ya TAMISEMI na PPP ili kwa pamoja waweze kuvuta mitaji toka sekta binafsi ili kujenga miradi yenye tija na thamani halisi ya fedha kwa manufaa ya Taifa kwani miradi hii itaipatia Serikali Kodi pamoja na tozo mbalimbali na hivyo kuchochea ukuaji wa Uchumi endelevu huku Serikali ikiachwa ifanye miradi ile tu ambayo haina sura ya kibiashara na hivyo kuipa nafuu zaidi Serikali katika kutafuta Mikopo na misaada mbalimbali toka kwa wahisani na mashirika mbalimbali nje na ndani ya nchi.
Baada ya muda wa mkataba kuisha..litakuwa jengo la Serikali . Muandishi kanjanja wa kusifu na kuabudu akashindwa kuuliza swali jepesi kabisa HUO MUDA WA MKATABA NI MUDA GANI!!?
 
Back
Top Bottom