Dah! Umetisha mwanang!Mkuu hapo tusiwalaumu hawa architects wetu kwa kutokujibu unavyohitaji, kwa nijuavyo mimi hapo fundi akikupa makadirio atakuwa anakudanganya maana makadirio huwa yanatokana kwa vipimo unless just unataka makadirio yasiyo ya kitaalam.
Ila kama makadirio ya huyo mnigeria ni 16M ikiwa na garage,kwa kuwa room itakuwa na mahitaji ya material zaidi ya hapo garage tegemea zaidi ya 16M.
Dah! Umetisha mwanang!
Kwamba sixteen millions inateketea kwenye Garage pekee....noma sana, then hiyo Garage itakuwa ya kupark gari ngapi? Au hiyo garage itakuwa imebeba room ya ukubwa gani?
Wewe kama mtaalamu Chukua hiyo picha then tengeneza ramani kupitia hiyo Design ya nje ili tupate migawanyo ya vyumba na vipimo baada ya hapo utaniambie cost zake kupitia hivyo vipimo....deal?Mkuu Ni kweli imetokana na ramani. Kwa hiyo leta na hiyo ramani pamoja na hiyo picha yako watu waifanyie kazi.
Ramani ina migawanyo ya vyumba na vipimo.
Okay, I got you. Kuondoa garage lengo ni kupunguza gharama sasa kama kuondoa ndio kuongezeka kwa gharama Wacha tu ikae vile ikoHujanielewa, nimesema kama 16M ni kwa ramani ikiwa na garage, ila wewe unataka modify garage kuwa room…so budget itaongezeka maana room itahitaji materials zaidi.Soma vizuri.
Mkuu huoni hiyo slab?32 millions of TZS nayo haitoshi?
Kwa hiyo wewe ukienda hospital unataka Dr ahisi ugonjwa wako? Mkuu tusirahisishe maisha namna hiyo. Vitu makini vinahitaji analysis za uhakika.Okay, Dr anaweza kuhisi unaumwa nini kutokana na maelezo yako pasipo ata kukupima Damu
Actually sitaki kusema kuwa narahisisha bali nasema kuwa nyie mnafanya Mambo yawe mengi sana
Wewe kama ni fundi au mchora ramani huwezi kupata shida kiasi hicho unless otherwise uwe huna uzoefu kabisa
Kama ni mzoefu basi utajua kabisa vyumba katika nyumba za kisasa let's say waga vina ukubwa wa 12*16, dining 20*25,Choo cha ndani 2*3, kitchen 8*8 and so on
Sasa hapo unashindwa kumpa simple analysis kulingana na uzoefu wako na pia jicho la kiufundi baada ya kuangalia mfano wa picha na kusikiliza matakwa yake? Kwanini usimpe mtu roughly sketch ata 3 ambazo yeye atachagua?
Na ndomana mara nyingi wateja waga wanapenda kutumia mafundi wa kawaida Kwa sababu waga wako straight na sio architecture au engineers Kwa sababu always Wana complicate Mambo
Naira 1 ni sawa na Tsh 3.20 kwa hiyo 5Mill Naira ukizichange kwa madafu inakua 16 Million Tsh yuko sahihi mkuu !!Alie kwambia naira million 5 ni Sawa na million 15 tzs ndio kakuingiza chaka. Hiyo ni zaidi ya million 30 ya kibongo tupende kufatilia mambo
Sent from my SM-A025U using JamiiForums mobile app
Nakupa mfano,Vyumba viwili, ukubwa miguu 15 Kila upande
Sitting room na dinning ipo ukubwa wake wa kawaida tu
Kila chumba kiwe na choo then choo Cha public hakuna
Mbona imeporomoka hivyo mwezi uliopita ilikuwa 5.23 kweli yuko sahiiNaira 1 ni sawa na Tsh 3.20 kwa hiyo 5Mill Naira ukizichange kwa madafu inakua 16 Million Tsh yuko sahihi mkuu !!
Labda imeshuka kwa sababu ni sera ya nchi wameamua kushusha thamani ya pesa yao !!Mbona imeporomoka hivyo mwezi uliopita ilikuwa 5.23 kweli yuko sahii
Sent from my SM-A025U using JamiiForums mobile app
Umepiga kwa rate gani? Wewe ndio ufuatilie mamboAlie kwambia naira million 5 ni Sawa na million 15 tzs ndio kakuingiza chaka. Hiyo ni zaidi ya million 30 ya kibongo tupende kufatilia mambo
Sent from my SM-A025U using JamiiForums mobile app
Okay, so hapo budget yake ni ngapi kwa makadirio yako hadi nyumba isimame kama hivyoNakupa mfano,
1. Nyumba ya two bedrooms, dining, sitting, kitchen ina wastani wa 6windows, 6doors.
Tutengeneze grills sita kwa lowest price (dar), @90,000x6 = 540,000
Grills mbili za milango ya nje na vitasa vyake kwa lowest price @150,000x2 = 300,000
Tuweke aluminium 6 kwenye madirisha at a very low price kwa sasa @250,000x6= 1,500,000. Tuweke aluminium kwenye milango ya chooni, @200,000x2= 400,000
Tuweke milango ya nje miwili na vyumbani, standard panels kwa sasa ni around (bei ya chini)@450,000×4 =1,800,000. Milango na madirisha tu vinaweza kufika 4m kiwango cha chini.
2. Bati ni la kujificha, wastani wa bati 40 kwa design za kisasa na tuchukue mabati kwa bei za kizalendo @25,000×40 = 1,000,000, mbao za kench, 2x4 70 @ 5,500= 385,000 , 2x2 35 @2,500= 87,000.
Blundering 2x2 90 @2,500 = 225,000, misumari na ufundi utajua mwenyewe. Kupaua na ufundi wake fanya 3m makadirio ya chini.
3. Umeme c.pipe 80pcs @2,000(africab)= 160,000, kuna cable 2.5, 1.5, sockets, main switch 70,000, sq boxes za kutosha nk. Ufundi utajua mwenyewe. Ila materials na ufundi 1.5 hadi 2.5m inakata kutegemeana na materials ulizoweka, ukifunga ac tutarajie zaidi.
4. Plumbing materials na ufundi 1m inakata
5. Hatujazungumzia boma, plastering, gypsum board, skimming, tiles, rangi, maji ya kujengea(wengi hawaweki makadirio), landscaping, mashimo ya choo.
Umetaka kitu kizuri, 16m ni utani. Kwanza kuna slab humo.