Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sasa mwamba mbabe namna hiyo, kugusishwa ncha ya sindano tu ndiyo akatawanyika kama karatasi!Hapana mkuu mimi nimewasilisha mawazo tu..!
Utakuwa mmoja wa wafanyakazi/wanufaika wake. Ni mawazo yangu tu lakini, hivi vyeti vya bashite ulishaviona? Au hilo halikuhusu kama la Lisu....Makonda Kijana Mzalendo Wa Taifa letu.....
Tunakukumbuka Sana kwa kuwa ICON wetu sisi vijana hasa wa CCM......
Tunakukumbuka Sana kwa KUPAMBANA KWAKO na Vita dhidi ya MADAWA YA KULEVYA.....
Makonda umetupunguzia VIJANA WANAOBEMBEA NA BWIMBWI HADHARANI......
Nikiwa Kama MUISLAM...hakika SITOKUJA KUKUSAHAU ulivyotupigania tuwe na MSIKITI MKUBWA NA BORA KULIKO YOTE TANZANIA.....
Waislam HATUTOKUSAHAU kwa sababu OFISI ZETU ZA BAKWATA hazikuwa na UBORA wenye KUSTAHILI.....
Makonda hilo hapo JUU SI DOGO......
Makonda Hilo la kutufanyia HISANI waislam hususani wa DAR si jepesi hata kidogo.....
Nitaendelea KUKUOMBEA DUA kila uchao,aaaamin.
Makonda your too zeal,patriotic and perseverant,I wish you the best in achieving your political goals aaaaamen aaaaamen.
Kila Mtu Ana Ndoto Zake.
Makonda Nae Ana Ndoto Zake.
Jumbe Brown,
Kijana Muuza Al Kasus
Kijiweni Tandale Kwa Mtogole
Mkuu, kuna namna mtu akifanya anakua bora kuliko jana katika muktadha wa utu (siyo uchumi, utu) mojawapo ni namna ya kujua kuwasiliana na wanaomzunguka.Leo Ngojea Niseme...
Makonda ANAKAANGWA na UWEZO WAKE MKUBWA WA KIUONGOZI.
Nyota Nyota Nyota ya Makonda imemfanya awe na UADUI na kila Mmoja mwenye roho ya korosho katika haya Mambo yetu ya SIASA......
Huko Nyuma Wako waliopendwa Sana na MARAIS waliokuwepo madarakani kwa KUSIFIWA NAO na kutaka WAWE MIFANO kwa wengine juu ya uchapa kazi wao ULIOTUKUKA....hayo yalipelekea WAKAKEBEHIWA KUZODOLEWA KUKASHIFIWA KUVUNJIWA HESHIMA na hata kutishwa kuhujumiwa nafsi zao....MIFANO iko MINGI mno.....
Mifano IPO.....ya kutosha.
Nyota ya KIUONGOZI ya Makonda ni kubwa Sana ZAIDI ya UMRI WAKE na pengine hata zaidi ya UWEZO WAKE UPSTAIRS(intelligence).......
Kipindi Cha marehemu mzee Sitta(mola amlaze pema peponi Amin) Makonda alikuwa na MAADUI wakubwakubwa kisiasa........
Watu wakasema labda ni kwa sababu AMEKUWA na UKARIBU wa kirafiki na MAADUI wa "watu"......
Hali hiyo haikupunguza UKALI WA NYOTA YAKE na pamoja ya yote HAIKUMRUDISHA nyuma.....Kuna wakati alisimama peke Yake.....
Huko TAHLISO ameshawahi kusimama peke Yake....
Huko SHIRIKISHO LA CCM VYUO VIKUU ameshawahi kusimama peke Yake......
Kwenye VITA DHIDI YA MADAWA YA KULEVYA NA SHISHA ZENYE BANGI alisimama peke Yake......
Akinamama waliotelekezwa na wazazi wenzao,alisimama peke Yake.....
......,..,.,..............
.........................
........................
..............,.........
List ya ALIYOFANYA ni NDEFU............nako alisimama peke Yake.
Sishangai na sitomshangaa AKIZISIMAMIA NDOTO ZAKE...NDOTO ZAKE PEKE YAKE......
Paul Christian Makonda anaponzwa na Nyota yake Kali na Kaliba yake Kuu KIUONGOZI.
Siempre Siempre CCM
Hasta la Victoria CCM.
Muuza Al Kasus Tandale kwa Mtogole.
Mkuu acha ARGUMENTUM AD HOMINEM basi...Utakuwa mmoja wa wafanyakazi/wanufaika wake. Ni mawazo yangu tu lakini, hivi vyeti vya bashite ulishaviona? Au hilo halikuhusu kama la Lisu....
Swadakt mkuu Wangu We acha tu...Yaani hata hili HAWALIONI analiona Sky Eclat TU?!!!Sina chuki kwa Makonda amefanya uhalifu Dar I mepungua.
Mkuu, kuna namna mtu akifanya anakua bora kuliko jana katika muktadha wa utu (siyo uchumi, utu) mojawapo ni namna ya kujua kuwasiliana na wanaomzunguka.
Mfano: Wewe waweza kua una akili kunizidi na mimi ninajua kua umenizidi akili lakini ikatokea siku ukaniambia "Castr nimekuzidi akili" ujue wazi sitafurahia hiyo kauli ingawa ni kweli na ninajua kua ni kweli.
Watu wengi wenye madaraka wanakwama hapo, kuanzia baba mwenye nyumba, bosi ofisini, kaka yako, wabunge, mawaziri n.k.
Na hapo tu kwenye communication ndiyo kumesababisha watu waone sawa Mwakyembe kutemwa "Nina degree nne siwezi kusikiliza ushauri wa la saba" na Makonda (Ana kauli nyingi ambazo alilenga zidisplay ni namna gani hayupo level moja na anaowaongoza/ anaowatawala.
Mkapa amefariki atakumbukwa kwa mengi umeona jingine ambalo watu wanamkumbuka nalo? Neno malofa na wapumbavu. Na hili alitamka mwanadiplomasia.
Hivyo wewe hapa utaweza hisi anachukiwa kisa nyota, kisa madawa, kisa akili n.k. lakini mzizi upo hapo. Amina Chifupa alipigania drugs pia uliwahi sikia anachukiwa?
Anyway usiku mwema.
Kajijaza upepo kama futuzaSasa mwamba mbabe namna hiyo, kugusishwa ncha ya sindano tu ndiyo akatawanyika kama karatasi!
Watu wanavituko nyie!