PICHA: Tofauti 17 kati ya matajiri na masikini

PICHA: Tofauti 17 kati ya matajiri na masikini

acha kupotosha mkuu ukiwa na laki 5 ukiugua si week tu imekata yote
Kama wewe ukiugua haikutoshi basi sio tajiri. Ila kama mtu akiugua akatumia sh elf 10 kwenye matibabu yake ikamtosha basi yeye ni tajiri
 
Kama wewe ukiugua haikutoshi basi sio tajiri. Ila kama mtu akiugua akatumia sh elf 10 kwenye matibabu yake ikamtosha basi yeye ni tajiri
Mkuu unaongea kumaanisha au kutania?
Ni matibabu gani hayo utafanya kwa elfu 10?
Hata kwa laki 5 tu, ukihitaji upasuaji mkubwa haitoshi chochote.
Cha muhimu ni kuacha kujidanganya kwamba utajiri ni kile unachoona kinakutosha, muhimu ni utajiri ni kile kinachowezesha maisha yako kwenda bila ya kukwamishwa na chochote, ikiwepo dharura mbalimbali unazoweza kukutana nazo.
 
Mkuu unaongea kumaanisha au kutania?
Ni matibabu gani hayo utafanya kwa elfu 10?
Hata kwa laki 5 tu, ukihitaji upasuaji mkubwa haitoshi chochote.
Cha muhimu ni kuacha kujidanganya kwamba utajiri ni kile unachoona kinakutosha, muhimu ni utajiri ni kile kinachowezesha maisha yako kwenda bila ya kukwamishwa na chochote, ikiwepo dharura mbalimbali unazoweza kukutana nazo.
Basi wewe sema ni kiasi gani kinachoweza kumtosha mwanadamu kwa kila dharula itakayo mkuta. Mi nimesema laki 5
 
😂😂😂
Eti wabongo ujuaji mwingi.

Wape story/fursa afu tulia uone muendelezo
 
Basi wewe sema ni kiasi gani kinachoweza kumtosha mwanadamu kwa kila dharula itakayo mkuta. Mi nimesema laki 5
Hakuna kiasi kimoja kinachoweza kuwatosha watu wote.
Lakini kanuni rahisi ni hii; kuwa na uwekezaji ambao unazalisha faida inayomtosha mtu kuendesha maisha yake bila ya kuhitajika kufanya kazi ya moja kwa moja.
Kwa mfano kama gharama zako za maisha ni milioni moja kwa mwezi basi uwe na uwekezaji ambao unaweza kukuingizia kipato hicho na zaidi kila mwezi bila ya wewe kuhitajika kufanya kazi.
Muhimu sana hapa ni uwekezaji na siyo kazi, maana kipato kikishakuwa kinategemea mtu ufanye kazi moja kwa moja, kinakuwa na ukomo.
 
Tafsiri ya utajiri ni pana sana na daima wanao itafsiri hawawezi kuwa na wazo moja. Mimi nitaendelea kukazia pale pale kiasi chochote kile ambacho ni fedha inayomtosheleza mtu kupata kila anacho kihitaji yeye tuu basi huyo mtu ni tajiri. Aweza kuwa na laki tano au laki 2 akawa tajiri mzuri tuu....

Naandika haya kwakuwa nawe umechanganya jambo hapo kusema kuwa utajiri ni kuwa na uwekezaji ambao haukulazimu kufanya kazi moja kwa moja mi naona haipo sawa... unaweza ukawa tajiri kwa kuingia shambani moja kwa moja na ukaongeza nguvu kazi nyingine
 
Ninakumbuka wajomba zangu wawili baada ya kupata mali za urithi kila mmoja alipata nyumba, yule Mmoja alianza kukodisha vyumba mpaka hii leo zaidi ya miaka 20 sasa maisha yake yamekua tegemezi hivyo. Yule mwengine aliuza nyumba ya kwanza akaanza kufanya biashara, Alilaumiwa sana na wanafamilia ila hakuwasikiliza, baada ya muda miaka kama mitatu mambo yakawa magumu biashara zilakwama akaamua kuuza na yapili, Kwa kweli jamii ilimuandama sana mpaka wakawa wanasema amerogwa, Ila jamaa hakurudi nyuma aliamini kwenye Biashara akiamini atafikia malengo yake. Hivi sasa jamaa ni MIlionea. Na yule kaka yake ambae aliekua anasambaza maneno kuwa jamaa amechanganyikiwa anauza nyumba sahivi kawa analalamika mitani kuwa Ndugu yake hamsaidii hali ya maisha ni ngumu.
 
Unauza kitabu Cha kutuelekeza njia za kua tajiri kwanini wewe usitumie hizo njia ili utajirike

Nauliza hivyo nikiwa Kama huyo mtu uliemchora ana kiraka kwa suruali
 
Unauza kitabu Cha kutuelekeza njia za kua tajiri kwanini wewe usitumie hizo njia ili utajirike

Nauliza hivyo nikiwa Kama huyo mtu uliemchora ana kiraka kwa suruali
Pata utajiri mkuu,
Utaacha kuuliza maswali ya kijinga.
 
so you need to learn more.
Learn more basi uwe tajiri baadaye ukiwa Kama mo ndio uje hapa utuambie. Mie nauliza wote waliosoma vitabu waliofanikiwa ndio. Samahani lakini Kama unajisikia vibaya Ila yabidi tutumie logic na sio emotions
 
Ninakumbuka wajomba zangu wawili baada ya kupata mali za urithi kila mmoja alipata nyumba, yule Mmoja alianza kukodisha vyumba mpaka hii leo zaidi ya miaka 20 sasa maisha yake yamekua tegemezi hivyo. Yule mwengine aliuza nyumba ya kwanza akaanza kufanya biashara, Alilaumiwa sana na wanafamilia ila hakuwasikiliza, baada ya muda miaka kama mitatu mambo yakawa magumu biashara zilakwama akaamua kuuza na yapili, Kwa kweli jamii ilimuandama sana mpaka wakawa wanasema amerogwa, Ila jamaa hakurudi nyuma aliamini kwenye Biashara akiamini atafikia malengo yake. Hivi sasa jamaa ni MIlionea. Na yule kaka yake ambae aliekua anasambaza maneno kuwa jamaa amechanganyikiwa anauza nyumba sahivi kawa analalamika mitani kuwa Ndugu yake hamsaidii hali ya maisha ni ngumu.
Halafu hili suala la kujenga nyumba limefanya watu wengi sana kuishia kuwa middle class au hata kuishi kwa shida.
 
Learn more basi uwe tajiri baadaye ukiwa Kama mo ndio uje hapa utuambie. Mie nauliza wote waliosoma vitabu waliofanikiwa ndio. Samahani lakini Kama unajisikia vibaya Ila yabidi tutumie logic na sio emotions
Daa jamaa we mmbishi kinyama,mpaka unatia huruma asee kwa hii fixed mindset
 
Back
Top Bottom