Elections 2015 Picha: Tulichokishuhudia katika mapokezi ya Magufuli Jijini Mwanza, upinzani unafutika

Elections 2015 Picha: Tulichokishuhudia katika mapokezi ya Magufuli Jijini Mwanza, upinzani unafutika

Hao watu walikusanyana sehemu moja, ushabiki unakupofua!
kwani magufuli kafanya nini,picture inajisema...na imepigwa na kuletwa hapa na mtu aliyekuwa akitamani hata kw akudanganya aonyeshe wingi wa watu.Pikipiki na mibendera tuu imechukua nafsi sana huku pembeni na nyuma pakiwa hakuna watu..na palipokuwa na watu ni skiasi gani waandishi,usalama, green guards na wanachama wa ccm,
 
Ccm kwenye kampeni zao huwa wanapata shida sana inawalazimu waanze kukodi watu wahudhulie mikitano yao hii inaosheja kiasi gani hawa kubariki na hilo nao wanalijua vizuri Mm kuna jamaa yangu mmoja wa ccm alilazimishwa akachukue fomu ya kugombea ubunge ccm Yule jamaa nilivyo muuliza jamaa kwanini umeamua hivyo na haugopi kuabika kwa kwasababu kwa namna yoyote huwezi kupita piga ua hata iweje Jamaa kaniambia mm mwenyewe kinaniuma sana kijana kama mm kuwepo ccm mm kwa nje naonakana ccm lakini roho yangu yote ipo chadema nafanya yote haya ili kuwafurahisha mabosi wangu na kulinda kibarua Hapo kwenye huo mkutano sio wote wanaipenda ccm ila wengi tu wamelazimishwa. Na usione matabasamu yote hayo ni matabasamu ya kununuliwa.
hao walio changanyikiwa ndio wazuri kwani huwa tunawaita undecided ila dkk za mwisho huwa wanadecide vizuri sana kwa kufuata mkumbo.
 
Asante kwa kuniwahi ukiangalia picha zake 80% wamevaa kijani ikiwa na maana ni wale wale wanaobebwa na malori kijaza viwanja. Na hili ndilo kosa Maccm wanafanya, kununua watu ili kujifariji. Mbona hawaangalii wenzao Cdm wanafanyaje mikutano bila gharama za kununua watu??Yaani mara hii UKAWA hawapotezi jimbo hata moja zaidiya kuongeza.
CCM hawana akili km Lowasa anafanya kazi ya CDM kwa ufanisi kwa gharama zake na CCM kuliko ZZK na ACT walivyfanya kwa CDM kwa gharama za CCM na serikali yote.Yoote haya kwa CDM ni bure.
 
Shughuli za usafirishaji jana zilisimama kwa zaidi ya saa mbili, baada ya msafara wa mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi(CCM), Dk. John Pombe Magufuli, kupita jijini hapa.

Licha ya kusimama kwa usafiri, msafara huo pia ulizuiwa kwa muda na wananchi katika eneo la Pasiansi, Kona ya Bwiru na Makongolo, wakishinikiza kusalimiana na mgombea huyo.

Magufuli ambaye aliongozana na viongozi mbalimbali wa CCM, serikali, madhehebu ya dini na wananchi wengine kutoka ndani na nje ya mkoa wa Mwanza alitua Uwanja wa Ndege saa 7:50 mchana.

Baadhi ya viongozi wa CCM taifa waliokuwa wameongozana na Dk. Magufuli ni pamoja na Katibu wa Siasa na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Tanzania Bara, Rajabu Luhavi.

Kadhalika, Dk. Magufuli alikuwa amefuatana na mkewe, mama Janet Magufuli. Msafara wa Magufuli kuelekea ofisi za CCM mkoani hapa uliondoka uwanja wa ndege Mwanza majira ya saa 8:30.

Akijitambulisha mbele ya maelfu ya wakazi wa mkoa wa Mwanza waliofurika nje ya ofisi ya CCM mkoani hapa, Dk. Magufuli aliwapongeza wananchi kwa mapokezi yao makubwa, huku akiwataka Watanzania wote kuendelea kulinda umoja wao kwa nguvu zao zote.

“Ninawashukuru sana kwa mapokezi yenu makubwa…lakini pia ninawaomba muulinde umoja wetu na tuendelee kushirikiana bila kujali itikadi za vyama wala rangi zetu,”Dk. Magufuli.

Aliahidi kuisimamia kwa kikamilifu Ilani ya CCM. Alisema atahakikisha wafanyabiashara ndogo ndogo hawanyanyaswi.
Awali akimkaribisha, Dk. Magufuli, Nnauye alisema CCM hakitasita kuwashughulikia wanachama wake ambao hulalamika kwamba mchakato wa kuwapata mgombea urais kupitia chama hicho ulikiuka taratibu.

“Ninapenda kuwaambia kuwa mchakato wa kumpata mgombea urais ndani ya chama uliisha salama na tulimaliza salama ingawa kuna baadhi ya watu wanalalamika lalamika,” alisema.

Alisema wanaCCM hao watashughulikiwa na chama iwapo wataendelea na malalamiko hayo ambayo alisema hayana ukweli wowote.

“Wakiendelea tutawajibu, hasa wazee wetu.” alisema huku akishangiliwa.
Hii ni mara ya kwanza kwa Dk. Magufuli kufika Mwanza tangu achaguliwe na CCM kupeperusha bendera ya chama hicho kuwania nafasi ya urais kupitia uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, mwaka huu

chanzo nipashe
 
hii ndo raha ya kuwa madalakani na tume ya uchaguzi na wafanya kazi wake wakitegemea mshahara wao ww ndo uwalipe na hii ndo raha ya kuwa mtawala kwani ndege za serikali na magari ya serikali ndo yameguka ya chama cha mapinduzi na ccm wanamesha anza kufanya kampeni wakati mda wa kampeni bado na tume ya uchaguzi ikiwa kimya na msajili wa vyama wote wamevaa miwani za mbao
naamini ukiwasachi mfukoni zaidi ya kitambulisho na fedha utakuta pia kadi za chama cha mapinduzi mfukoni mwao
 
hii ndo raha ya kuwa madalakani na tume ya uchaguzi na wafanya kazi wake wakitegemea mshahara wao ww ndo uwalipe na hii ndo raha ya kuwa mtawala kwani ndege za serikali na magari ya serikali ndo yameguka ya chama cha mapinduzi na ccm wanamesha anza kufanya kampeni wakati mda wa kampeni bado na tume ya uchaguzi ikiwa kimya na msajili wa vyama wote wamevaa miwani za mbao
naamini ukiwasachi mfukoni zaidi ya kitambulisho na fedha utakuta pia kadi za chama cha mapinduzi mfukoni mwao

hiyo ndiyo CCM mkuu
 
Shughuli za usafirishaji jana zilisimama kwa zaidi ya saa mbili, baada ya msafara wa mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi(CCM), Dk. John Pombe Magufuli, kupita jijini hapa.

Licha ya kusimama kwa usafiri, msafara huo pia ulizuiwa kwa muda na wananchi katika eneo la Pasiansi, Kona ya Bwiru na Makongolo, wakishinikiza kusalimiana na mgombea huyo.

Magufuli ambaye aliongozana na viongozi mbalimbali wa CCM, serikali, madhehebu ya dini na wananchi wengine kutoka ndani na nje ya mkoa wa Mwanza alitua Uwanja wa Ndege saa 7:50 mchana.

Baadhi ya viongozi wa CCM taifa waliokuwa wameongozana na Dk. Magufuli ni pamoja na Katibu wa Siasa na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Tanzania Bara, Rajabu Luhavi.

Kadhalika, Dk. Magufuli alikuwa amefuatana na mkewe, mama Janet Magufuli. Msafara wa Magufuli kuelekea ofisi za CCM mkoani hapa uliondoka uwanja wa ndege Mwanza majira ya saa 8:30.

Akijitambulisha mbele ya maelfu ya wakazi wa mkoa wa Mwanza waliofurika nje ya ofisi ya CCM mkoani hapa, Dk. Magufuli aliwapongeza wananchi kwa mapokezi yao makubwa, huku akiwataka Watanzania wote kuendelea kulinda umoja wao kwa nguvu zao zote.

“Ninawashukuru sana kwa mapokezi yenu makubwa…lakini pia ninawaomba muulinde umoja wetu na tuendelee kushirikiana bila kujali itikadi za vyama wala rangi zetu,”Dk. Magufuli.

Aliahidi kuisimamia kwa kikamilifu Ilani ya CCM. Alisema atahakikisha wafanyabiashara ndogo ndogo hawanyanyaswi.
Awali akimkaribisha, Dk. Magufuli, Nnauye alisema CCM hakitasita kuwashughulikia wanachama wake ambao hulalamika kwamba mchakato wa kuwapata mgombea urais kupitia chama hicho ulikiuka taratibu.

“Ninapenda kuwaambia kuwa mchakato wa kumpata mgombea urais ndani ya chama uliisha salama na tulimaliza salama ingawa kuna baadhi ya watu wanalalamika lalamika,” alisema.

Alisema wanaCCM hao watashughulikiwa na chama iwapo wataendelea na malalamiko hayo ambayo alisema hayana ukweli wowote.

“Wakiendelea tutawajibu, hasa wazee wetu.” alisema huku akishangiliwa.
Hii ni mara ya kwanza kwa Dk. Magufuli kufika Mwanza tangu achaguliwe na CCM kupeperusha bendera ya chama hicho kuwania nafasi ya urais kupitia uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, mwaka huu

chanzo nipashe

nimependa hii sentensi ya mwisho
eti hii ni mara ya kwanza kwa dr magufuli kufika mwanza tangu achaguliwe na ccm kugombea urais.
dah ulivoandika utadhani jamaa kachaguliwa miaka mitano ilopita na sasa ndo anakuja mza kumbe ni juzi tu kachaguliwa.
ila hongera upambe mwema
 
nimeangalia picha najaribu kutafuta umati uko kwa upande gani sion!
Hizo picha zinaonyesha akiwa njiani na si kwenye mkutano. Ina maana watu walijitokeza kuanzia Airport kumlaki hadi anaingia ofisi ya CCM. Imenikumbusha enzi zile tunawapokea Marais wa nje wakipitia pugu road, port access na uhuru kuelekea ikulu wakiwa gari la wazi na mwenyeji wao JKN. Watu walikuwa wakijipanga toka Airport hadi ikulu lakini wakati huo kwa kulazimishwa. Ila naona hao ni kwa utashi wao
 
Mapokez siyo kigezo cha kudhihirisha kuondoka upinzani, tambua watu wengi hawaendi kudhihirisha kwamba wanahama chama bali wanaenda kumuona mtu nasio kuhama chama, lazima uwe nafikra pevu ktk hoja zakisiasa, ukijumlisha watu wasiomjua mtu huyo nawengine wanataka tu kusikia atasema nini, hivyo wingi wa watu siyo kigezo cha kuondoa upinzani
 
Hizo picha zinaonyesha akiwa njiani na si kwenye mkutano. Ina maana watu walijitokeza kuanzia Airport kumlaki hadi anaingia ofisi ya CCM. Imenikumbusha enzi zile tunawapokea Marais wa nje wakipitia pugu road, port access na uhuru kuelekea ikulu wakiwa gari la wazi na mwenyeji wao JKN. Watu walikuwa wakijipanga toka Airport hadi ikulu lakini wakati huo kwa kulazimishwa. Ila naona hao ni kwa utashi wao
Ndugu,
Hata habari imejieleza lakini kwa vile wana fikra hasi hawawezi kusoma na kuelewa.

Muda wa kufanya mkutano ulimalizika kabla ya kufika kwenye viwanja vya furahisha kutokana na wananchi kukaa katikati ya barabara ili kumzuia kwa nguvu wakitaka wasikie hata neno moja kutoka kwake.

Nilichikiona kuanzia Dodoma, Dar, Zanzibar na Jijini Mwanza kinasema Magufuli anasubiri kuapishwa kuwa Rais wa Tanzania wa Awamu ya Tano.

Ukitaka kufahamu yaliyotokea Geita, pitia thread hii,
 
Ndugu,
Hata habari imejieleza lakini kwa vile wana fikra hasi hawawezi kusoma na kuelewa.

Muda wa kufanya mkutano ulimalizika kabla ya kufika kwenye viwanja vya furahisha kutokana na wananchi kukaa katikati ya barabara ili kumzuia kwa nguvu wakitaka wasikie hata neno moja kutoka kwake.

Nilichikiona kuanzia Dodoma, Dar, Zanzibar na Jijini Mwanza kinasema Magufuli anasubiri kuapishwa kuwa Rais wa Tanzania wa Awamu ya Tano.

Ukitaka kufahamu yaliyotokea Geita, pitia thread hii,

mkuu hiyo ya Geita nimeiona. Nimeona Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita, Bwana Musukuma, amerejea kundini!
 
mkuu hiyo ya Geita nimeiona. Nimeona Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita, Bwana Musukuma, amerejea kundini!
Mkuu kuna umbali mrefu kutoka airport ya Mwanza mpaka ofisi za CCM ni msururu mrefu wa magari naona wakazi wa Ilemela, Igombe, Pansiansi, Nyamanoro, Kirumba wamejitokeza kumpokea Dr.Magufuli.
 
mkuu hiyo ya Geita nimeiona. Nimeona Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita, Bwana Musukuma, amerejea kundini!
Ndugu,
Kauli mbiu yetu tunasema Umoja ni Ushindi.

Wana CCM wameamua kuvunja makundi na kama kuna mwana CCM bado anataka kuendelea na makundi, chama kimesema lazima akipishe ili aende kwenye siasa za makundi kati ya mwenye chama na wanachama wa kawaida.

CCM kwa sasa ni moja baada ya Mkutano Mkuu.
 
Wingi wa watu haimaanishi wote watampa kura
Subirini lowassa atakavokipasaua chama.
Ndugu,
Unatuambia sisi tusubiri au wewe ndiyo usubiri.

Wana CCM kwa sasa wanaendelea kutambulisha Mgombea Urais wa Tanzania na kutoa fomu za kugombea Ubunge na Udiwani.

Hoja ya kutafuta mgombea Urais imefungwa ndani ya CCM.
 
"Insanity: doing the same thing over and over again and expecting different results."...mi sio chizi CCM hampat kura yangu hata moja....
 
Hakika UKAWA wanayo kazi!
Ndugu,
Mimi nadhani CCM imewarahisishia kazi kwa sababu kwa sasa hawahitaji kufikiri sana kama watashinda nafasi ya Urais wa Tanzania.

Magufuli anasubiri kuapishwa awe Rais wa Awamu ya Tano.

Kazi ya wapinzani kwa sasa ni ubunge.
 
Ndugu,
Mimi nadhani CCM imewarahisishia kazi kwa sababu kwa sasa hawahitaji kufikiri sana kama watashinda nafasi ya Urais wa Tanzania.

Magufuli anasubiri kuapishwa awe Rais wa Awamu ya Tano.

Kazi ya wapinzani kwa sasa ni ubunge.
Hakika wamechanganyikiwa hadi hawana la kufanya..
 
Back
Top Bottom