Picha ya Rais vs Rais wa Picha

Picha ya Rais vs Rais wa Picha

Lini lilipitishwa hili? Mkuu usiniabishe kuwa hata civics ya form two ilikupitia mbali. Picha ni nembo ya nchi?! Hakika tutafika tukiwa tumechoka sana kiakili🤔
Kwahy jamaa kwann amefungwa?
 
Picha ya rais pamoja na yeye mwenyewe rais ni nembo ya nchi
Hapana! Rais ni binadamu na mtumishi wa umma kama wengine. Nembo za nchi ni Bendera, tuzo, rakili, ngao za taifa, majengo au ofisi kuu inayotambulika kisheria kuwa makao ya nchi na Serikali.

Rais au kiongozi mkuu wa nchi juu yake kimamlaka ni Mungu, kumtambua Rais kama nembo ya nchi ni sawa na kutengezeza mazingira ya kuwa Mungumtu.
 
Waafrika, hasa Watanzania..tunapenda sana utukufu..kitu kinachompasa Mungu pekee. Pengine ndio maana hatustawi sana.
 
Hapana.
Ichukue hiyo picha ya ku-'down-load'; halafu itisha kikundi cha watu na ku-download' mahasira yako kwenye picha hiyo na kuichoma moto. Ni lazima pawepo na tendo la aina hiyo.
Binafsi bado sikubaliani ni huo ujinga wa kushtaki watu kwa mambo ya kipuuzi kama hilo.
Hili la rais naliona kuwa tofauti na tendo la kuchoma bendera ya nchi kwa mfano.
je dhamira ya kuchoma picha ya Rais ilikuwa ni nini,kudhalilisha au nini hapa lazima nia,kusudio na dhamira ithibitishwe mahakamani
 
je dhamira ya kuchoma picha ya Rais ilikuwa ni nini,kudhalilisha au nini hapa lazima nia,kusudio na dhamira ithibitishwe mahakamani
Hasira; hamaki, ghadhabu, taharukii soi lazima viwe na nia ya "kudhalilisha."
 
Back
Top Bottom