Pigo la mwisho kwa Thadei Ole Mushi: Katoliki wakataa kumzika kwa kuwa aliwapinga TEC kuhusu DPW

Pigo la mwisho kwa Thadei Ole Mushi: Katoliki wakataa kumzika kwa kuwa aliwapinga TEC kuhusu DPW

Mkuu ni sahihi kabisa, watu ni wanafiki sana humu. Utakuta mtu anaanzisha uzi wa kupinga kushiriki jumuiya akidai zinawachangisha hela, halafu mtu huyo huyo anakuja kuanzisha uzi kuwa Kanisa linazingua kukataa kumzika marehemu. Sasa kama wewe unahitaji huduma, kwa nini ukiwa hai hautaki kushiriki na wenzako? Ukiamua kujitenga hutakiwi kuja kuomba huruma siku watakapokukana kuwa sio mwenzao. Yaani wakiwa wanakuhitaji unawakana, wewe ukiwa unawahitaji wakikukana iwe nongwa? Kimsingi unatakiwa kujua umejitenga mwenyewe, wala hujatengwa
Nimakupa like. Hawa jamaa kama wana moyo mzuri, hawajui kuzika ni ibada, mbona hawaendi kusomba miili isiyo na ndugu mochwari wakazike.
 
Sijawahi kuona waislam wanamsusia marehemu. Wana ushirikiano sana kwenye misiba, taarifa zikitolewa chaap wamefika shughuli inaanza.
Utaskia tu Inalillahi wa inailahi rajiun, Mungu amjalie mapumziko mema inshaallah yani fasta tu mtu analamba udongo.
 
Hakuwa na pesa. Kama anapesa maaskofu wangaligombea mwili kuuombea. Au nasema uongo wadau?

KANISA KATOLIKI LAGOMA KUMZIKA BILIONEA MREMA

Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Arusha jana lilikataa kuendesha misa ya mazishi kwaajili ya marehemu Faustine Mrema, mmiliki wa hotel za Ngurdoto, Impala na Naura springs kwavile hakuwa na sakramenti ya ndoa na mke wake wala kipaimara.

Paroko Msaidizi wa Parokia ya Mt. Theresia, Mtoto Yesu, Jimbo Kuu la Arusha, Padri Festus Mangwingi amethibitisha hilo na kusema marehemu hakuweka heshima kwa kanisa.

"Marehemu ni mkatoliki wa kuzaliwa lakini hakuwahi kuwa na sakramenti ya ndoa na mke wake aliyezaa nae watoto wala kupata kipaimara hivyo kanisa haliwezi kabisa kumzika. Kwa kawaida, mazishi ya Kanisa Katoliki hutolewa tu kwa mkristu anayestahili. Huyu marehemu hakuwahi kufunga ndoa kanisani na alijitenga na kanisa. Hivyo kusema Kanisa limemtenga si kweli kwani yeye ndiye alilitenga kanisa, hakutaka kuonesha heshima yake kwa kanisa kama mkristu. Aidha, marehemu hakuwahi kuhudhuria misa za jumuiya ambazo ni muhimu kwa Mkristu. Jumuiya ni utaratibu wa Kanisa unaowataka waumini wawe na usharika wa karibu na kufahamiana. Marehemu alikuwa hashiriki kabisa kwenye jumuiya sasa unaanzaje kumzika mtu kama huyo kwa heshima za Kanisa Katoliki?" alihoji padri Mangwingi.

Baada ya Kanisa hilo kujivua, ilibidi Askofu Dr. Eliud Issangya wa Kanisa la Kimataifa la Kiinjili kuokoa jahazi na akaendesha ibada hiyo ya mazishi iliyofanyika hoteli ya Ngurdoto, wilaya ya Arumeru, Arusha.
 
Sijawahi kuona waislam wanamsusia marehemu. Wana ushirikiano sana kwenye misiba, taarifa zikitolewa chaap wamefika shughuli inaanza.
Mbona mochwari miili mingi tu haina ndugu hao waislam hawaendi kuibeba wakaizike kwa ibada? Unadhani kuzika ni kitu chepesi sana?
 
Kanisa Katoliki lagoma kuendesha Ibada ya misa ya mazishi ya Thadei Ole Mushi kwa sababu ALIPINGA WARAKA WA BARAZA LA MAASKOFU WA KANISA KATOLIKI TANZANIA (TEC) Uliopinga uuzwaji wa Bandari, uliotolewa tarehe 18 August 2023 na TEC.

Thadei Ole Mushi alipinga hadharani waraka wa TEC, kupitia andiko lake la tarehe 18 August 2023 lenye kichwa cha Habari "WARAKA WA MAASKOFU SIO ITHIBATI ZA MAONI YA WATANZANIA"

Juzi ndugu na msemaji wa familia Bwana Victor Tesha, alitangazia dunia kwamba ibada ya mazishi ya kumuaga ndugu yetu Thadei Ole Mushi kwa Dar es Salaam ingefanyika katika kanisa la St. Peter - Oysterbay.

Lakini watu wengi ikiwemo mimi tulipofika kanisa la St. Peter's Oysterbay, tulikuta milango ya kanisa imefunga na hakuna dalili ya kuwepo kwa misa yoyote.

Uamuzi wa haraka kutaarifu watu waelekee Muhimbili katika kanisa la Pamoja (siyo Katoliki) ukafanyika na pakaendeshwa ibada na mapadre ambao ni marafiki wa karibu wa Thadei Ole Mushi na siyo Paroko anayehusika katika parokia yake ya Muhimbili.

Leo familia imekwaa tena kisiki kingine Mkoani Kilimanjaro, Uru nyumbani kwa Thedei Ole Mushi baada ya Parokia ya Uru nyumbani kwa marehemu kugomea kuendesha mazishi na kufunga milango kiasi cha kupelekea kutafutwa kwa wachungaji wa madhehebu ya Kipentekoste pale Uru.

Baadae ibada ikaendeshwa na kasisi akiwa amevaa t-shirt nyeusi na sio mavazi halisi ya ibada kwa mujibu wa taratibu. Na wala hakukuwa na kwaya ya Kanisa.

Wajuzi na wasomi wa kanisa Katoliki wanasema ukipinga Waraka wa Maaskofu ni sawa na kuasi kanisa kwa kukataa mafundisho yake, hivyo kama utafariki kabla ya kurudishwa kundini utakuwa umefariki kama muasi nje ya kanisa na hivyo kanisa halitohusika na mazishi yako.

Hili ni Somo kubwa na funzo kwa wanasiasa na watu wote ambao tulikuwa hatujui uzito na maana ya waraka wa baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) ambao hutolewa na kusomwa makanisa yote ya waumini wao.

Kama na wewe ni muuumini wa kanisa katoliki na unajua uliropoka na kupinga lolote kuhusu waraka ule wa TEC fanya haraka urudishwe kundini.

VIJANA🙄
Ni sahihi, warudishwe kundini. Hususani viongozi.
 
Ni kweli mkuu kanisa Katoliki hailimtengi mtu ila halilazimishi mtu kulifuata. Kama alijitenga akiwa hai, kwa nini kanisa limlazimishe akiwa ameshakufa na bila kujua sababu ya yeye kujitenga huko.

Suala la Waraka inaweza isiwe sababu ila maisha yake ya ukatoliki, ndoa n.k hatuyajui yanaweza kuwa ni sababu pia.

Wapo wengi mfano bilionea Mrema wa Arusha (Ngurudoto na Nauru Spring) nae hakupata ibada ya mazishi ya kanisa Katoliki. Nyie mnaosema haina umuhimu wowote kwa nini mnalalamika na kuleta uzi?

Ile ni Ibada/ Misa ya kuonesha ushindi katika kuiishi imani katoliki (Ukristo) katika maisha yako hapa duniani. Kwamba "Nimevipiga vita vilivyo vizuri mwendo nimeumaliza na Imani nimeilinda."
Ona hii ilichoandika
images%20(6).jpg
 
Hapa ndio dini yangu huwa inanichosha kabisa!

Hata wakatae kumsalia, what difference does it make to a dead man?🧟‍♂️ AbsoFREAKINGlutely NONE!!!!
Dead man wangapi umeenda kuwazika, ambao hata huwafahamu? Unadhani kanisa ni tofauti?
 
Hakuna Dola na Taasisi ya Kidkteta hapa ulimwenguni kama Kanisa Katoliki na Vatican[holy see] kwa ujumla.

Hivi, taasisi inayohimiza Uhuru wa Maoni and yet inaadhibu wenye maoni tofauti nayo, is it not dictatorial in it's own form!?

Ajabu Kanisa hili hili, linataka Mashoga wabarikiwe, in spirit ya kukumbatia tofauti zetu.

Organized religions zote ni shida zinapigania zaidi maslahi ya taasis and not an expected prime role ya kulea watu kiroho.
 
Katika eneo Uislam nina usifu ni Mazishi. Yeyote mwenye elimu na ujuzi wa kusalia maiti, anazika. Hii mambo ya kuweka taratibu kuwa hadi kiongozi, ni kutumia mwanya huu kuweka mambo ambayo sio ya kiimani kabisa kwa waumini. Yaani kanisa haliziki Muumini wake, kwa sababu ya utofauti wa mitazamo ya Kisiasa. Thadei anaadhibiwa na Kanisa kwa mambo ya Kaisari na Sio Mungu.
 
Kuna msiba uliokuwa na hela kama wa Ruge Mutahaba kwa siku za hivi karibuni? Muulize ndugu yake yeyote kama alizikwa kikatoliki. Ukiishi bila ndoa umejitenga na Kanisa, utazikwa na wahuni
Ruge Mutahaba ni cha mtoto, bilionea Mrema wa Arusha, pamoja na ubilonea wake hakuzikwa na kanisa Katoliki. Usicheze na Kanisa Katoliki katika kufuata taratibu zake.
 
Mbona mochwari miili mingi tu haina ndugu hao waislam hawaendi kuibeba wakaizike kwa ibada? Unadhani kuzika ni kitu chepesi sana?
Katika uislam kuzika ni Sanda tu tena kitambaa chepesi hakizi elf 20, kumsalia bure na kumzika bure. Hao waliokuwa munchuwari waislam labda uongozi wa hospital hawajatoa tu Taarifa kwa uongozi wa msikiti uliokaribu dakika miili yote itazikwa kiislam
 
Back
Top Bottom