LGE2024 Pius Msekwa aeleza kutofurahia ushindi wa 99% wa CCM, asema anafurahia tu pale uchaguzi unapomalizika na pande zote zinaridhika

LGE2024 Pius Msekwa aeleza kutofurahia ushindi wa 99% wa CCM, asema anafurahia tu pale uchaguzi unapomalizika na pande zote zinaridhika

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Wenye akili wote wanaona wazi njia tunayoelekea siyo nzuri na tusipokuwa makini tutaiingiza nchi kwenye majanga lakini cha ajabu kuna wapumbavu wachache hawalioni hilo!
 
Magufuli ndio muasisi wa hizi siasa chsfu za kutaka ccm ishinde kwa kishindo kitu kisichoendana na ukweli. Wamaccm wanaojitambua wanajua ukweli kuwa ccm iko madarkani kwa shuruti na sio kwa ridhaa ya walio wengi.
Hakika.
 
Spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Pius Msekwa amesema hafurahii ushindi wa 99% wa CCM katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliomalizika kwani kuna mapungufu mengi. Pia amesema mtu mwenye akili timamu hawezi kufurahia ushindi huo.

Spika mstaafu ameyasema hayo leo alipohojiwa na Sauti ya Kiswahili ya Ujerumani. Spika amevitaka vyombo vya uchaguzi kuondokana na kasoro ikiwa ni pamoja na matumizi ya nguvu na kuwaengua wapinzani ambapo amesema hilo halikuwahi kutokea hapo zamani kwanini linatokea sana siku hizi? Amehoji Spika Mstaafu.

---------

View attachment 3170482
Naunga mkono hoja. Bora ushinde kihalali asilimia 51 kuliko kufanya ujambazi wa kura.
 
Kwani Msekwa anasema hii Katiba iliyopo imevunjwa wapi !
Kwani Katiba inasemaje kuhusu mambo ya Uchaguzi ??!!
Mimi naamini Mzee Msekwa anaijua vizuri hii Katiba na anajua kila kitu kilikwenda kwa mujibu wa Katiba !
Au nasema uongo ndugu zanguni ???!!!
😳🙄😳 !
Katiba haina tatizo,tatizo lipo kwenye Tume ya Uchaguzi,Rais,Makamu wa Rais,Waziri Mkuu,Spika na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
 
Ukimsikiliza kwenye hii clip, mzee Msekwa ni muoga.

Kaulizwa swali kwamba "Jana waziri mkuu mstaafu, jaji Joseph Since Warioba amelaani tabia ya kuvitumia vyombo vya dola kwenye chaguzi. Kwann ccm mnatumia vyombo vya adola kwenye chaguzi?"

Majibu ya mzee Msekwa anasema yeye hajawahi kuviona vyombo vya dola vikitumika ktk chaguzi. Majibu haya yamejaa marashi ya uwoga.
 
Naunga mkono hoja. Bora ushinde kihalali asilimia 51 kuliko kufanya ujambazi wa kura.
Huwezi kuwapumbaza watu wote muda wote, Vile vile ujinga ni kufanya jambo lile lile kwa namna ile ile halafu ukitegemea matokeo chanya ama kulazimisha watu wafikiri unavyotaka wewe hata kama una uwezo mdogo wa kufikiri
 
Spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Pius Msekwa amesema hafurahii ushindi wa 99% wa CCM katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliomalizika kwani kuna mapungufu mengi. Pia amesema mtu mwenye akili timamu hawezi kufurahia ushindi huo.

Spika mstaafu ameyasema hayo leo alipohojiwa na Sauti ya Kiswahili ya Ujerumani. Spika amevitaka vyombo vya uchaguzi kuondokana na kasoro ikiwa ni pamoja na matumizi ya nguvu na kuwaengua wapinzani ambapo amesema hilo halikuwahi kutokea hapo zamani kwanini linatokea sana siku hizi? Amehoji Spika Mstaafu.

---------

View attachment 3170482
Safi sana mzee Msekwa! Wazee hawapaswi kukaa kimya huku mambo yakienda kombo!
 
Back
Top Bottom