PM Kassim Majaliwa piga kazi, achana na ndoto za Urais, umemponza SG Dk. Bashiru Ally

PM Kassim Majaliwa piga kazi, achana na ndoto za Urais, umemponza SG Dk. Bashiru Ally

KooZito

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2020
Posts
397
Reaction score
1,377
Wanabodi heshima kwenu!

Taarifa zilizonifikia kutoka chanzo ninachokiamini ni kwamba ziara za Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mikoani pamoja na mambo mengine anazitumia kujiweka sawa kwa ajili ya kumrithi Rais Magufuli.

Duru za siasa mikoani zinaeleza kwamba, sehemu kubwa ya Wabunge waliopitishwa na CCM na hatimaye kuwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano ni mipango mahsusi iliyopangwa na PM Kassim na kuratibiwa na Katibu Mkuu Dk. Bashiru Ally kama hatua ya kwanza ya kujiweka sawa kwa 2025.

Hatua ya pili kupitia wabunge hao ni kupanga safu katika Uchaguzi Mkuu wa ndani ya Chama 2022 ambapo "wabunge wa PM" wamepewa jukumu la kushawishi wajumbe mikoani na wilayani kuunga mkono harakati hizo butu.

Taarifa zinaeleza kwamba, harakati hizo zinam-keep busy Waziri Mkuu kiasi kwamba utendaji wake kuwa shakani au dhaifu.

Hata hivyo, taarifa kutoka kwenye korido za Lumumba zinaeleza kuwa mamlaka za juu zimepata taarifa na hivyo hatua kadhaa zimeanza kuchukuliwa dhidi ya SG na PM likiwemo uteuzi wa Polepole Ubunge kufuatilia nyendo za PM bungeni.

My Take! Kutamani Urais si dhambi. Lakini tamaa hiyo inapokuondoa katika utendaji kazi basi ni kheri kujiuzulu ili kuwa huru kusaka Urais. Lakini pia ikumbukwe Waziri Mkuu naye ni Mkulu kiprotokali. Anaishi Ikulu. Kuutamani Urais ni kutaka kuishi Ikulu kwa miaka 20 tofauti na Rais aliyeishi 10 years. Hawezi kuruhusu ajali hiyo kutokea. Huu ni muda wa kujenga nchi si kusaka madaraka.

Ni ushauri tu!
 
Acha umbea wewe; jamaa huyu tangu awe waziri mkuu mwaka 2015 amekuwa anatembelea mikoni siku zote katika kutekeleza moja ya majukumu yake ya kufuatilia miradi mbalimbali ya serikali, halafu leo wewe unaanza kugeuza nia ya safari hizo kuwa ni za kutafuta urais! Hii ni kutaka kuchonganisha watu tu.
 
acha umbea wewe; jamaa huyu tangu awe waziri mkuu mwaka 2015 amekuwa anatembelea mikoni siku zote katika kutekeleza moja ya majukumu yake ya kufuatilia miradi mbalimbali ya serikali, halafu leo wewe unaanza kugeuza nia ya safari hizo kuwa ni za kutafuta urais! Hii ni kutaka kuchonganisha watu tu.
Ni suala la muda tu, tutaweka hadharani vikao vyote vya mikakati hiyo kama ushahidi.
 
Hapana alisema anataka kijana achukue viatu vyake, Lukuvi na Kabudi waliambiwa hata wafanyeje hawapati kitu, huu mzigo wa Bashungwa tu

Marais wote waliomtangulia walikuwa na akili na wabobezi wa siasa kuliko Jiwe lakini walishindwa kuwachagulia wabongo warithi wao!!! Mkwere alimtaka Membe , sasa yuko wapi? Hata Mwalimu alishndwa kumuachia Salim!!! Kama ana akili kidogo ataelewa kuwa kama ana mpango wa kumuachia msukuma mwenzie afadhali auache.
 
Marais wote waliomtangulia walikuwa na akili na wabobezi wa siasa kuliko Jiwe lakini walishindwa kuwachagulia wabongo warithi wao!!! Mkwere alimtaka Membe , sasa yuko wapi? Hata Mwalimu alishndwa kumuachia Salim!!! Kama ana akili kidogo ataelewa kuwa kama ana mpango wa kumuachia msukuma mwenzie afadhali auache.
Bashungwa sio Msukuma
 
Ni suala la muda tu, tutaweka hadharani vikao vyote vya mikakati hiyo kama ushahidi.

Ni mtu kama Nape Mnauye tu ndio anaweza kuanza kuandika fitina kama hizi kwani alikatazwa kuzunguka zunguka kufanya kampeni kwenye sehemu nyingine tofauti na constituency yake!!! I am told he also has presidential ambitions!.

Jiwe has lowered the bar of the presidency to such a low such that even fools believe they can be presidents.
 
Back
Top Bottom