PM Majaliwa: Watanzania tunaomba mtuamini (kuhusu uwekezaji Bandarini)

PM Majaliwa: Watanzania tunaomba mtuamini (kuhusu uwekezaji Bandarini)

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731

Waziri Mkuu ameomba Watanzania waiamini Serikali kwenye uwekezaji unaotaka kufanyika Bandari, akidai kuwa sio uwekezaji wa kwanza wala sio jambo jipya bali kulikuwa na mwekezaji ambaye walimpa vipindi vya kumfanyia tathmini hadi akafika miaka 22 na ameondoka Novemba mwaka 2022; hivyo DP World nao watampa vipindi kama aliyekuwepo.

Waziri Mkuu Majaliwa anasema Mwekezaji huyu mpya hajauziwa bandari, ila atapewa kuwekeza.

Kuhusu ukomo wa muda, amesema wanaodai DP World kapewa miaka 100 au milele sio kweli kwani hapajaandikwa popote juu ya ukomo ila akija ndio watakubaliana juu ya suala hilo.

Ameongeza kuwa Mwekezaji hajauziwa ardhi kwani hata sheria za nchi haziruhusu ila mwekezaji atapewa kibali cha kukaa juu ya ardhi na atalipa kodi, pia mkataba utazingatia maslahi ya nchi kama wengi wanavyodai.


Pia soma: Dodoma: Bunge lapitisha azimio la kuunga mkono mkataba wa Tanzania na DP World
 
Huyu PM sidhani kama kuna mtanzania mwenye akili timamu ambaye bado anamuamini. Kauli zake nyingi zina utata tangu aliposema JPM ni mzima anaendelea na kazi!
Atatumia nguvu nyingi sana watu kumuamini tena kauli zake
 
Watu wanalalamikia IGA iliyopitishwa na bunge na sio HGA zitakazoingiwa ili kutekeleza IGA. Mapungufu katika IGA hayawezi kutatuliwa katika HGA.

Kama IGA haina ukomo ni kwamba serikali itatakiwa kuingia HGA moja baada ya nyingine bila kikomo. Na kwa vile IGA inasema bayana kuwa haiwezi kufutwa kwa sababu yeyote ile, serikali haitakuwa na pa kutokea. Haya ndio mambo yanayowatia watu hofu.

Amandla...
 
Utaratibu mzima wa uwekezaji unapaswa kubadilika!. Hata kama huko nyuma Serikali iliwekeza lakini yote ilikuwa kwa manufaa ya Serikali na mafisadi walioko kwenye mfumo. TICTS kwa mfano, ilimnufaisha vipi mwananchi wa kawaida?
Inashangaza sana kuona viongozi tunaowachagua wenyewe, wanageuza rasilimali za taifa kama mali zao binafsi.

Viongozi wameshindwa kusimamia rasilimali za taifa badala yake wanatafuta njia ya mkato.... Kutafuta mwekezaji !!
Umiliki wa Serikali kwenye mashirika yote ya umma, hata yale yaliyojifia yanapaswa kufanyiwa uthamini, hisa zinazomilikiwa na Serikali kwa asilimia 100, zinapaswa kupunguzwa- Serikali iwe na asilimia 25% TU.

Hisa za TPA zilizobaki ambazo ni asilimia 75 (baada ya kutoa 25%za Serikali kwenye bandari kama kuwekeza ni lazima) zigawanywe kwa mwekezaji wa kimkakati 49%, wafanyakazi bandarini 5%, na wananchi na makampuni binafsi 21%. Baada ya mgawanyo huu wa awali, TPA ijiorodheshe kwenye soko la hisa la DSE, Pesa itakayopatikana itumike kuwekeza kwenye bandari, Hii inawezekana kabisa pale wananchi wakipewa fursa ya kununua hisa na baadaye wataweza kuisimamia vizuri TPA maana ni mali yao, na maamuzi yoyote yatadhibitiwa kila mwaka kwenye mikutano ya kila mwaka.

Hivi kuna ubaya gani Serikali ikiupiga chini huu mpango wa uwekezaji wa DPW kwenye bandari yetu,ikafanya hayo niliyoshauri hapo juu? Kuna ulazima gani wa kulazimisha wananchi waiamini Serikali kwenye deal ambayo wameisha isitukia? kwa nini Serikali inatumia nguvu nyingi sana kuwashawishi watu kuwa wao wako sahihi na wengine wanaopinga ni wapotoshaji? DPW imekuja wakati sahihi kabisa, itatusaidia kunyoosha mambo mengi yasiyoeleweka kama ulivyo muungano wa "Tanzania na Zanzibar"
 
Back
Top Bottom