Tetesi: PM, Philips, Foreign na February wamekalia kuti kavu?

Tetesi: PM, Philips, Foreign na February wamekalia kuti kavu?

Sababu ulizotoa zote hazina mashiko. Tatizo la uchumi kuporomoka sio kosa la philipo ni magufuli mwenyewe. Swala la korosho nalo sio la PM ni magufuli mwenyewe kuchanganya biashara na siasa za kutaka utukufu. Mambo ya nje nayo hahusiki hata kidogo, mahusiano yetu na nch za nje kavurugwa magufuli mwenyewe na mwanaye kwa kauli zao zisizokuwa na vichwa wala miguu.
Sote tunajua katika wote hao hakuna mwenyewe tatizo, tatizo ni boss mwenyewe. Lakini katika nchi zenye mifumo ya kusadikika, mabosi huwa ni miungu watu, huwa hawapaswi kuonekana wamekosea, na hilo ili litokee inabidi tambiko la kafara lifanyike. Sasa hao wote ni kafara tu ili kuondoa nuksi za mizimu.

Lini tambiko litafanyika, sote tunasubiri, huku tukijua mbuzi wa kafara wapo tayari.
 
Wa fedha sitashangaa sana ili abaki inabidi apige kazi kweli maana elimu ya kodi kwa wananchi bado hajatoa vya kutosha, kunakipindi walijitahidi sana ila sasa kimya.

Ni kiri wazi mimi sio mtaalumu wa maswala ya kodi ila ninakauelewa kadogo kuhusu umuhimu wa kodi., Sasa inapofikia mahali makusanyo ya kodi yanapungua wakati ukinunua bidhaa baadhi ya maduka makubwa na baadhi ya min supermakert ukidai risiti za EFD hawana, kidogo hii linashangaza kama kweli taifa kimedhamiria kukusanya kodi na kutekekeza miradi mikubwa kama ya ujenzi wa SGR.

Mheshimiwa raisi anania nzuri sana na nchi hii ila atakwamishwa na baadhi ya watendaji
wake aidha kwa kujua au kuto kujua.
 
PM siyo rahisi hivyo ww kumtoa pale, hao wengine wanaweza kutupwa chini anytime...


Wizara ya viwanda ni ngumu sana, yule waziri atapata angalau mda wa kupumzika...

Makyembe nae akapumzike sasa, anataka kufia serikalini au
 
Juz ndo nilijua PM anasukumwa tu..hili la wafanya biashara kumbe alipigiwa awape siku 4
 
February yeye anajua tayari yuko kwenye blacklist, hatakiwi kuwepo kwenye baraza, anatuhumiwa kuwa ana ndimi mbili, haaminiki kabisa, anatajwa kama ndiye mjumbe mkuu wa yule adui ndani ya serikali. Kwake ni suala la muda tu, uamuzi ulishafanyika toka kitambo na mwenyewe anajua hilo. Ni
Jiwe anaogopa kumtumbua maana Mange alishasema kwamba Marope atatumbuliwa na MAGU kwahiyo anataka kumprove wrong.
 
Kama atamtema PM basi atakuwa amefanya kosa kubwa sana la kiufundi. Itamgharimu zaidi ya anavyodhani.

PM ni very dedicated katika kila anachokifanya. Pia PM anajitofautisha na bosi wake katika matumizi sahihi ya kuweka mizania ya maamuzi.

PM anajua ni wakati gani awe mwanasiasa na ni wakati gani asicheke na mtu aliye mbele ya uso wake. Hao wengine haswa february, anaweza kupigwa chini muda wowote, kwa sababu keshaonyesha kejeli za zile katuni zake.
Tatizo sio mkurupukaji na hana ngebe na maneno ya kashfa,kwahyo anakuwa haendani na modus operandi ya Awamu ya tano.
 
Madaraka yalikabidhiwa kwa mshamba, bas tabu tuupu!!
 
Hii tabia ya kutumbuana natamani ingeshuka hadi vyeo vya chini. Nadhani hii itasaidia Wafanyakazi wa umma kutambua zile nafasi siyo permanent wala guaranteed hadi ustaafu kupitia hiyo mentality labda wataanza kushawishi na kutunga sera na sheria zilizo rafiki kwa watu sekta binafsi na zile ambazo hazitambuliki wakitambua na wao siku yeyote wanaweza kuhamia kwenye hizi sekta kabla hawajastafu na wakiwa na watoto ambao hawajamaliza shule. Tukifanikiwa hivyo natarajia kodi na ukiritimba zitapungua na serikali Itakuwa inahusisha wadau kwenye sekta uhusika kabla hawajafanya maamuzi. Naamini ukitaka kuona mtu anachapa kazi mtoe kwenye comfortable zone yake.
 
Msimu wa kutumbua tumbua katika utawala wa mtukufu hautakoma kamwe. Kila baada ya muda kuna kigogo ndani ya utawala anatumbuliwa. Ndio mtindo wake, hivyo tunapaswa kuuelewa na kuuzoea tu.

Wadadisi wa mambo wameshaweza kumsoma mtukufu na kuweza kutengeneza baadhi ya tabiri ambazo mara kadhaa zimekuwa kweli kabisa. Na JF ndio imekuwa kinara wa kuweza kuzisoma Codes na kuunganisha mambo.

Ukitazama kauli kadhaa za mtukufu kuhusiana na PM wake utagundua kabisa ipo siku atatemwa tu. PM huenda ameshachokwa na bosi wake na kilichobakia ni kutengenezewa sababu nzito ya kwenda na maji. Hili la korosho ndio lilikuwa jaribio la pili, limewakumba wenzake na kumuacha salama PM, lakini kwa jicho la karibu sana, linaonekana bado bichi mnoo, hivyo PM akae kwa umakini.....

Upande wa Philips nako hali si hali, uchumi umeyumba, makusanyo ya kodi anadai yameshuka, hakuna vyanzo vipya vya mapato, mambo hayaendi, lugha zinagongana tu na bosi wake au mtoto wa bosi. Lazima mchawi atafutwe tu. Waswahili wanasema mchawi ndio alipewa alee mtoto, na mtoto ameshaangamia, kitakachofuata ni mchawi naye kuangamizwa. Philips hawezi kukwepa mtego tena. Ni suala la muda tu.....

Foreign naye huenda ameshachoka, amebanwa mnoo, hana pakusimamia, diplomasia ya Tz imepwaya mno, uwaziri kwake umegeuka kuwa shubiri, anatamani huo mzigo autue lakini anaona aibu na woga umemjaa, hana ujanja, msimamo wa bosi hauwezi kuivusha nchi kimataifa, mabalozi wamelala fofofo, hawana mbinu mbadala. Mtego uliopo mbele yake kwa sasa ni kuwa dalali wa kuuza korosho kimaitaifa. Huo ni mtihani kwake, Kitakachofuata ni kwenda na maji tu...

February yeye anajua tayari yuko kwenye blacklist, hatakiwi kuwepo kwenye baraza, anatuhumiwa kuwa ana ndimi mbili, haaminiki kabisa, anatajwa kama ndiye mjumbe mkuu wa yule adui ndani ya serikali. Kwake ni suala la muda tu, uamuzi ulishafanyika toka kitambo na mwenyewe anajua hilo. Ni

Hizo zote ni ndoto za Zanzibar-ASP.
Tatizo ni jamaa mwenyewe dish linaonekana kuyumba sana
 
Bosi ukiwa mkali sana utawachanganya walio chini yako mpaka kazi ulizowatuma wataziharibu kwa hofu
 
Nimesoma uzi wako kwa umakini. Nakubaliana na wewe kwa PM hapo, huyu bwana anaonekana majukumu yamemzidi uwezo na kutemwa ni suala la muda tu,

Filipo bado yuko salama kwa sasa kama hatatoa kauli tata kama alizotoa Bungeni juzi hivi majuzi,

Mwisho ni bwana Februari, Huyu nadhani yuko salama kabisa kwa sababu wizara yake haina relevance kiivo ktk nchi, (sio wizara nyeti) kwahyo hakuna sababu yoyote ya kumwondoa.
 
Wa fedha sitashangaa sana ili abaki inabidi apige kazi kweli maana elimu ya kodi kwa wananchi bado hajatoa vya kutosha, kunakipindi walijitahidi sana ila sasa kimya.

Ni kiri wazi mimi sio mtaalumu wa maswala ya kodi ila ninakauelewa kadogo kuhusu umuhimu wa kodi., Sasa inapofikia mahali makusanyo ya kodi yanapungua wakati ukinunua bidhaa baadhi ya maduka makubwa na baadhi ya min supermakert ukidai risiti za EFD hawana, kidogo hii linashangaza kama kweli taifa kimedhamiria kukusanya kodi na kutekekeza miradi mikubwa kama ya ujenzi wa SGR.

Mheshimiwa raisi anania nzuri sana na nchi hii ila atakwamishwa na baadhi ya watendaji
wake aidha kwa kujua au kuto kujua.
Kampuni na biashara nyingi zinakufa makusanyo ya kodi yatapandaje unafikili? Kweli ukipewa ukuu kwenye hii awamu ni sawa umebebeshwa gunia la misumali.
 
Back
Top Bottom