Wengi tulioko JF tunatumia IDs fake (wengi), comments na mitazamo yetu most likely siyo fake kama ID zetu zilivyo.
Utu wa mtu unausoma kwenye maandishi yake (ingawa kuna maandishi fake pia), nikukumbushe kitu kimoja mdogo wangu, wanaume kokote waliko hawapendi mtu mwenye ligi kama zako.
Jifunze kuwasoma utafanikiwa, watu walioko humu ndo hawa hawa walioko mtaani, makazini, makanisani na kwingineko.
Kama baadhi ya wadau walivyoshauri, tunapomwomba Mungu hatumwambii nilitee mume/mke katika mfumo huu, yeye anajibu kadri anavyoona ni sahihi, na huwezi jua inawezekana kaamua kujibu kwa namna ulivyoileta humu, na kama ungejipa muda wa kuchunguza, kwenye hao walioku-PM kuna aliyeletwa na Mungu.
Ushauri mwingine; kuna mtu umemjibu kuwa asubiri kushuhudia kwa sababu ni lazima uwe umepata mtu mwisho wa mwaka 2016, Mungu hapewi timeline, anajibu muda wowote anaoona kwamba unafaa, usilazimishe sana ukajikuta unaangukia mahali ambapo siyo kwa sababu shetani naye anacheza na desparation zetu kutujaribu. Hivyo kuwa makini kwenye machaguo, kwenye maneno yako na kwenye matendo yako pia.
All the best.