Polepole: Hii sio awamu ya Sita bali ni ya Tano kipindi cha pili, aliyeondoka ni Magufuli peke yake

Polepole: Hii sio awamu ya Sita bali ni ya Tano kipindi cha pili, aliyeondoka ni Magufuli peke yake

Wakuu,

Mbunge wa kuteuliwa na mtunga Sheria Humphrey Polepole, anadai hii awamu ya rais Samia sio awamu ya sita.

Rais Samia alisema yeye ndiye rais ya awamu ya Sita. Kwamba ni awamu ya sita kipindi cha kwanza.

"Hii serikali sio mpya,haikupigiwa kura, huwezi ukaita awamu ya sita, awamu lazima iwe na miaka10, ilani na Sera zinazopaswa kutekelezwa ni zile tulizozinadi 2020, asiwadanganye mtu kuwa hii ni awamu ya sita,Kwa sababu aliyeondoka ni Magufuli peke yake" kasema polepole.

RAIS SAMIA ANASEMA UFISADI ULIFANYIKA AWAMU ZILIZOPITA SIO AWAMU YAKE YA SITA
"Kuna makundi wanajua wanayoyafanya ndani ya serikali, na yanageuka kusema serikali ya awamu ya 6 ufisadi umerudi mambo yako hovyo kumbe wao ndio wako hovyo, mambo hayo yalifanyika huko nyuma, gari bovu linaangushiwa awamu ya 6 sitakubali"
Rais Samia Suluhu akiwa Bandarini.

Je, nani yupo sahihi na Sheria inasemaje?

View attachment 2041066
Dah mwendazake alikaa kipindi kimoja tu, hii inawaumiza sukuma gang mpaka kufa
 
Wewe kubali tu tuko awamu ya 5. 2020 tumemchagua magufuli wewe jitahidi kuendeleza msimamo wa kimagufuli ndio watu walimchagua. Ukifanikisha hilo hakika watu watakupenda sana. Mungu akubariki mama yetu.
Hivi magufuli aliwahi kushinda uchaguzi wote tangu akiwa mbunge ??
 
Mbona hili liko wazi kabisa ,halihitaji hata tochi,awamu Ni mtu na Wala so miaka Wala vipindi,so hii Ni serikali ya awamu ya sita
 
Hata ikiwa ni awamu ya kumi hiyo itatusaidia nini sisi?
Kwangu mimi awamu maana yake ni kipindi cha mtawala akiwa madarakani, na hapa Tz mtawala ni rais.
Rais=awamu
Nyerere (awamu ya kwanza)
Mwinyi (awamu ya pili)
Mkapa (awamu ya tatu)
Kikwete (awamu ya nne)
Magufuli (awamu ya tano)
Samia (awamu ya Sita)
Chakubanga (awamu ya saba?!)🤣
... wanagombea awamu! Ajabu kweli kweli! Mama hataki kujinasibisha na awamu ya 5; wao wanajaribu kum-drag arudi awamu ya 5! Sijajua kila upande una siri gani ila kama unavyosema to common mwananchi awamu is immaterial or better call it NONSENSE!
 
Polepole anatakiwa kujua Samia ni Amiri Jeshi Mkuu!

Anaesema hii ni awamu ya Sita ni Rais Samia Mwenyewe! Sasa kama anapinga hii sio awamu ya Sita ajue anapingana na Rais Samia mwenyewe!

Kifupi anatakiwa ajue sonono aliyokuwa nayo juu ya Rais Samia sasa itaenda kumuonesha kuwa Samia ni Rais Kweli na Amiri Jeshi Mkuu
Unapotumia neno AMIRI JESHI maana yake ni kama unamtisha asitoe maoni yake
 
Polepole yupo sahihi, ishu ni kuwa alishajipaka sana matope enzi za godfather kiasi hakuna Mtanzania anayemtilia maanani sasa...
 
Polepole hataki ubunge, ... msimlazimishe!
... kama eye hataki ubunge atuachie nasisi sasa tuchukue ubunge! (kwa sauti ya Gwajiboy!😅)
 
HII NI AWAMU YA SITA, NA TUNAYE RAIS WA AWAMU YA SITA, HII SIO AWAMU ILE YA UDHAMU, UHUNI WA KUPIGA WATU RISASI, KUPOTEZA WATU, WAKO WAPI AKINA BEN SAANANE?, MAMA HATAKI KUJIHUSISHA NA UDHALIMU WA KIONGOZI ALIYEPITA, KWANI AKISEMA HII NI AWAMU YA SITA, MNAUMILIA NINI?
 
CCM si huwa wanasema kuwa endapo makada wao wakigombana, basi huwa wanatafuta suluhu kuhusu tofauti zao ndani ya vikao vyao rasmi vya chama. Sasa mbona hawa waliokuwa makatibu waenezi kila siku hawaachi vituko vya kupigana vijembe pasipo hata kusuluhishwa?

Hiyo lugha ya awamu za uongozi katika nchi ziliasisiwa na CCM yenyewe. Wao waliamini kuwa baada ya kupita awamu ya uongozi wa Baba wa Taifa, awamu zitakazofuata ziwe za Rais atokanaye na chama chao, apishwe na kutawala vipindi viwili vya uchaguzi vyenye jumla cha miaka 10.

Kwa muktadha huo, ili kumtafuta mpeperusha bendera katika kinyang'anyiro cha nafasi ya urais, Rais aliyepo madarakani hapaswi kushindanishwa na kada mwingine katika kipindi chake cha kwanza cha miaka mitano. Hivyo basi hupewa nafasi ya kutawala mpaka amalizie kipindi chake cha pili.

Kwa mantiki hii, awamu ya utawala ndani ya CCM huendana na dhamana pamoja na ridhaa ambayo kada wa chama hicho amepewa fursa ya kuwa Rais na Mwenyekiti Taifa. JPM pamoja na kutokuweza kukamilisha muda wake wa utawala wa miaka 10, bado aliweza kupitishwa kuwa mgombea na hatimaye kuwa Rais atokanaye na chama chake.

Baada ya mauti kumfikia, hapo ndipo ilikuwa mwisho wa awamu yake. Awamu huusishwa na mtu na wala siyo muda wa utawala, na pia awamu humuangalia Rais na Mwenyekiti Taifa aliyepo madarakani. Rais SSH yupo sahihi kabisa, yeye ndiye Rais wa awamu ya 6.
Hii aya ya mwisho imeonesha ni namna gani CCM hii nchi mejitwalia aisee. Inasikitisha sana!
 
Polepole anasema yupo anawafuatilia watu fulani. Ambao hakuwataja kwa jina ila amesha wapa warning kuwa wakivurunda atawaambia wazi wazi kuwa umevurunda. Inaonesha kuna watu wanataka waachane na ile miradi mikubwa ya awamu ya magufuli
Kwani nchi hii ni ya Magufuli.?
 
Nchi haiendeshwi kwa ilani ya chama bali Katiba na sheria, ilani inaweza kutupiliwa mbali kabisa na nchi ikaendelea. Kikwete alijenga UDOM na haikuwa kwenye ilani, Magufuli kajenga Bwawa la Stiglers na Daraja la Kigongo Busisi bila kuwepo kwenye ilani.
Mang'ula amesema ilani ya uchaguzi ilizunguzia kujenga gati bagamoyo huyu rais atuonyeshe ilani yake aliyoingia nayo kwenye uchaguzi
 
Nyerere aliyetawala Tanzania kwa miaka 21 alitawala kwa awamu ngapi?
Inawezekana polepole yuko sahihi kwa maana kwamba aliyebadilika ni rais peke yake. Kwa hiyo tunaweza kusema Samia ni rais wa sita katika awamu ya tano
 
Hili tulilo nalo ni bunge la kumi na mbili.
Ila ulifanyika uchaguzi..kupata serikali mpya na wabunge wapya chini ya mwinyi kama rais..hivyo ikaitwa awamu ya pili mwinyi akiwa rais wa pili..nikuulize wewe mchumia tumbo..baada ya JPM kufa kuna uchaguzi uliofanyika? ili kuharalisha kua hii ni awamu nyingine..au ni kumalizia awamu ya 5 kwa mujibu wa katiba?

#MaendeleoHayanaChama
 
Hujui chochote kuhusu katiba, katiba haina propoganda za awamu.
Katiba inasemaje..au tunaedeshwa ni mtu mmoja kwa mawazo yake..kwahiyo angesem awamu ya 10 mngekenua meno tu..njaa ya kichwani mbaya sana.

#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom