Polisi inawakamata Waratibu wa LBL lakini Watu wanaendelea kupigwa hela kwenye mfumo huohuo

Polisi inawakamata Waratibu wa LBL lakini Watu wanaendelea kupigwa hela kwenye mfumo huohuo

Mbona mimi naona kama jamaa aliweka hela tena 227,000/= ili aweze kulog in ili kutoa pesa, lakini ameletewa tena ujumbe kuwa bado wapo kweny majadiliano na BOT, pesa za wateja zitatolewa kwa pamoja
Watu wanapenda kujipa matumaini hewa, ndo imetoka hiyo
 
Mbona mimi naona kama jamaa aliweka hela tena 227,000/= ili aweze kulog in ili kutoa pesa, lakini ameletewa tena ujumbe kuwa bado wapo kweny majadiliano na BOT, pesa za wateja zitatolewa kwa pamoja
Waaminishe ujinga
 
Kuna story nikihadithia mtacheka sana!
Kuna kanisa la walokole wamepigwa kuanzia mchungaji hadi waumini.
Walitangaziwa kanisani🤣
Lbl wamepigwa wengi wengine hawasemi ila wamenuna balaa si shuleni si kazini si kanisani.
 
Licha ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa tangazo linaloeleza kuwa haihusiki na jambo lolote linalohusu Kampuni inayoitwa Leo Beneath London (LBL) ambayo inavyoonekana kilio chetu ni cha Watu wengi, lakini nimeamua kuandika hapa kwa kuwa najua kuna wenzetu ambao wana msongo wa mawazo wanaendelea kama mimi wanaendelea kupigwa.

Ipo hivi wale ambao tulikuwa Wanachama, kila tukiingia kwenye mfumo huo kwa nia ya kuangalia nini kinaendelea, tunakutana na jumbe mbalimbali, mojawapo ni kuwa inatutaka kulipia hadi Tsh. 270,000 ili kuweza kuingia katika Akaunti husika na kufanya mchakato wa kunasua fedha zetu zilizokwama ndani.
Nafikisha ujumbe huu kupitia JamiiForums naamini ujumbe huu utafika sehemu nyingi kwa kuwa mimi siwezi kuwafikia BoT.

Ukifungua kwenye akaunti yako ya LBL kuna ujumbe ambao unakuja ukikuelekeza kulipa kulingana na kiwango cha fedha ambacho ulilipia wakati unajiunga.

Mfano levo ya P3 kiwango cha kujiunga ni Tsh. 540,000 hivyo unatakiwa kulipia nusu ya kiasi hicho ambacho ni 270,000 ili wakuwezeshe kufungua akaunti yako na uweze kutoa fedha zako zote zilizosalia kwenye Wallet uhamishe katika mitandao ya simu.

Kinachofanyika ni kuwa hasara inaongezeka kwa Watu kuendelea kuliwa zaidi licha ya juhudi nzuri za Serikali na Jeshi la Polisi linawakamata Watu.

Pia soma:
~
Jeshi la Polisi Morogoro lawakamata maofisa saba wa LBL kwa tuhuma za biashara haramu ya fedha

~ Benki Kuu (BoT): Hatujatoa leseni wala kuruhusu shughuli za LBL
Sijui kwanini mamlaka hua zinaingilia kati haya mambo? Ifike kipindi tuache ili wapumbavu wapigwe hadi akili zikae sawa. Eti hadi leo watu bado wanaamini kuna kuweka hela na kupata faida mara tatu nne ndani ya mwezi 🚮🚮🚮🚮🚮🚮
 
Huu upumbavu wa LBL ni nini hasa? Inawahusu nani, ni DECI au uchafu gani inaitwa LBL?
 
Waaminishe ujinga
Nilikuwa nawafafanulia wagumu kuelewa ambao hawajamuelewa mleta mada.

Mleta mada nilivyomuelewa amepigwa mara mbili pesa yake na LBL.

Mara ya kwanza aliweka mzigo akashindwa kulog in, then LBL wamewataka wateja waweke hela ili waweze kulog in, ameweka hiyo 227,000/= then wanaambiwa wasubiri pesa zitatolewa kwa pamoja wapo kwenye majadiliano na BOT
 
Back
Top Bottom