Polisi kuua mlinzi wa bar Dar: Je, Chalamila anakwepaje kuwajibika?

Polisi kuua mlinzi wa bar Dar: Je, Chalamila anakwepaje kuwajibika?

Watanzania sijui wanatatizo gani na nguo fupi .... Yaani mwanamke kuvaa nguo fupi au suruali linawasumbua sana Wataznania wengi .... what's wrong with us. Watu wajue kuwa ni fashion tu na itapita. Huwezi mukuta mtu na kamin kake bar basi unaasume kuwa anajiuza .....!!
Viongozi walio wengi ni wanafiki. Wanachokitenda siyo kilichopo moyoni mwao, ni usanii wa kutaka kujionyesha. Nenda kakague simu na computer zao utawakuta wamejaza picha za ajabu, lakini kwenye jamii wanajifanya watakatifu.

Tanzania si kisiwa, kwa utandawazi tulionao huwezi kuwachagulia watu mavazi. Je, huyo RC atafungia TV na mitandao dunia nzima watu wasione hayo mavazi mafupi? Hii tabia ya kuvamia nyumba za watu kwa kisingizio cha kuwasaka machangudoa siyo sahihi. Inawezekana kabisa hata yeye akawa miongoni mwa wateja wazuri wa hii biashara, maana machangudoa wapo kwasababu wanapata wateja.
 
Kumbe Chalamila ndio aliye fyatua risasai, 🥴🥴.
Aliwatuma askari akijua wanakuwaga na chamoto wakati dadapoa wanabebada kondomu tu, alishindwa nini kumtuma mtendaji wa mtaa akaenda na mgambo ambaye anafimbo tu,
 
Tumeshuhudia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akivalia njuga wanawake wanaojiuza almaarufu makahaba. Zoezi lilianzia kwenye kuvamia na kuvunja vibanda maarufu vijjlikanavyo kama Vibanda vya Wahaya na kuwatia mbaroni baadhi yao.

RC Chalamila anayesifika kwa tabia za ufyatu ambapo aliwahi kusikika akisema kuwa akimkuta kibaka nyumbani kwake anamuua na hata aliwahi kusema hivi karibuni kuwa akiliamsha dude hakuna wa kumfanya lolote (hata sheria), amenadi kuwa ataendelea kuwasaka wanaojiuza miili yao kila kona ya mkoa wa Dar.

Juzi tu kumetokea mauaji mjini Dar es salaam kwenye Bar moja iliyopo Sinza iitwayo Boardroom (mlinzi wa bar hiyo aliuawa kwa risasi kutoka bunduki ya askari wetu), chanzo cha mauaji hayo yaliyofanywa na Askari Mbumbumbu ni kwenda kuwasaka makahaba hapo Bar!

Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa chini ya mwenyekiti wake wanawajibika na tukio hili la kinyama. Serikali inaendaje kuwasaka wanawake wanaojiuza kwa kutumia mtutu?

Chalamila ni mteule wa Rais, na kama inavyozoeleka mama huwalinda wale anaowapenda. Tunaamini kuwa Chalamila akiendelea kuwepo ofisini inapelekea jamii kuamini kuwa mteuzi anaridhika na mwenendo na maadili ya RC Chalamila.

Tunataka uwajibikaji na sheria ichukue mkondo wake kwa sababu maagizo ya Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoa yamepelekea mauaji ambayo yangeweza kuepukika endapo busara zingetumika. Kuanzia muuaji na wote wanaohusika na sakata hili wanapaswa kufikishwa mbele ya sheria ili haki ipatikanike.

Maadili ya viongozi wengi wa CCM imepelekea chama hiko kuwa kichaka cha wahalifu

Pia Soma Boniface Jacob: Polisi walioua Mlinzi wa Bar ya Boardroom Sinza wadaiwa kutumwa na RC Chalamila kukamata Wanaojiuza
Kauli ya RC Chalamila iliyochangia mauaji ya raia kule Sinza inalindwa na mamlaka ya uteuzi?

Kesi ya yule askari muuaji imeisha vipi?
 
Back
Top Bottom