Polisi: Tunawashikilia Niffer na Diva kwa mahojiano na hatua nyingine za Kisheria

Ni banana state wanaowashikilia watuhumiwa kabla ya upel3lezi kukamilika.

Hapo Polisi washaanza kuwahukumu kabla ya mahakqma kusoma hukumu
 
Kwa miaka mingi kama nchi tumekuwa na tatizo la uongozi kutua kwa wasiostahili now tatizo lingine ni pesa kutua kwa wasiostahili kuwa nazo
 
A good Police Officer is only a dead Police Officer.

Jeshi la Polisi badala ya kuwakamata Watu waliohusika katika kusababisha ajali na kisha kuwafikisha Mahakamani wao wanahangaika na Watu waliokusanya michango ya maafa.
Yaani hovyo kabisa.
Huna Akili....
…....….................
...........................
Napenda kutoa ushauri ufuatao kwa watu wenye ushawishi kwa jamii;

1. Kukitokea maafa/janga la kitaifa, usichangishe fedha. Sheria ya usimamizi wa maafa ya mwaka 2022, kifungu cha 26(2) inasema jukumu la kuchangisha litafanywa na Kamati ya maafa iliyo chini ya ofisi ya Waziri mkuu, kupitia akaunti maalumu.

2. Ukichangisha fedha kwa matatizo mengine ambayo si maafa (eg matibabu, elimu, yatima) usitumie namba/akaunti binafsi. Ni kosa kisheria. Tumia taasisi (NGO) iliyosajiliwa.

Kwa mujibu wa Sheria ya NGO namba 24 ya mwaka 2002, kifungu cha 32, michango ya kibinadamu (charitable initiatives) inaratibiwa na mashirika yaliyosajiliwa na sio mtu binafsi. Lengo la sheria ni kuweka "Check & Balance" ili kudhibiti ubadhirifu kwa sababu NGO inafanyiwa auditing angalau mara 2 kwa mwaka (internal & external).

3. Kama unataka kumsaidia mtu na huna NGO, tumia namba za mhusika mwenyewe, lakini kwanza upate kibali kutoka ofisi ya Mkuu wa wilaya. Kifungu cha 122 cha sheria ya serikali za mitaa ya mwaka 1982 inataka michango inayokusanywa na mtu binafsi kwa ajili ya "charity" ipate kibali kwa DC.

#Swali: Je watu wanafahamu haya?

#Jibu: Hapana. Kuna watu wanachangisha pesa kwa nia njema kabisa (utmost good faith) lakini hawajui utaratibu wa kisheria ulivyo.

#Swali: Je nini kifanyike?

#Jibu: Wapewe elimu. Hawapaswi kutishwa, kubezwa au kukatishwa tamaa. Kama mtu amechangisha fedha kupitia akaunti yake binafsi ili aokoe maisha ya mgonjwa kwanini umshtaki? Ni kweli hajafuata utaratibu lakini kafanya jambo jema. Kwahiyo kunaweza kuwa na "actus reus" lakini kusiwe na "mens rea" na hivyo ikawa ngumu kuestablish jinai.

#Points3ZaKukariri;
1. Michango ya maafa/majanga inakusanywa na serikali tu.

2. ⁠Michango ya "charity" inakusanywa na taasisi/NGO iliyosajiliwa na inayowasilisha auditing report wizarani.

3. ⁠Ukitaka kuchangisha na huna NGO tumia namba/akauti za mhitaji mwenyewe kwa kibali cha DC.

#UshauriKwaSerikali: Watanzania wanapendana sana, lakini wengi hawana imani na serikali kuhusu michango. Wanakumbuka kuchangia wahanga Kagera pesa zikabadilishwa matumizi. Kwahiyo tumieni watu wenye ushawishi kuhamasisha (eg wasanii, viongozi wa dini, wanamichezo, wanahabari etc).!

Credit.... Malisa GJ. Facebook.
 
A good Police Officer is only a dead Police Officer.

Jeshi la Polisi badala ya kuwakamata Watu waliohusika katika kusababisha ajali na kisha kuwafikisha Mahakamani wao wanahangaika na Watu waliokusanya michango ya maafa.
Yaani hovyo kabisa.
Unadhani hawajakamatwa?
 
Wasanii Niffer na Diva wanapaswa kuburutwa Kortini kwa kutakatisha pesa " money laundering". Ili fundisho kwa wengine. Shobo sio dili.
 
Wapi lini? Unaushahidi gani hapo ulipo bando umekopa acha kuropoka chamsingi waache vimberembere kujifanya mama upatu
 
Wivu kama wivu mwingine

Mimi binafsi siwezi kushawishika kuchangia mfuko wa serikali ila nimechangia pesa kwa nifer
Sababu. Namuamini

Kila mtu ana mawazo yake na uhuru na utashi wa kutoa maoni watu wengi Imani ya kifedha hatuna na watu wa huko tunawaamini Hawa watu wa mtaani
 

Attachments

  • 1731954395535.jpg
    217.1 KB · Views: 1
Binti mdogo wa miaka 25 ana trend kwa kuchangisha michango ya maafa, huyu si ndio angepongezwa kwa kufanya hivyo chapchapu wakati mamlaka husika imelala? cha ajabu ananakamatwa. itungwe sheria ya msamaria mwema
Msamaria mwema au tapeli tu. Si angetoa mchango wake ye mwenyewe, si ana maduka kibao. Alaf hata kwny hilo tukio hajafika, mtu yupo dodoma anafurahi kufungua duka lake, eti anachangisha. Asee watz sijui ujinga utawaisha lini.
 
Wajinga ndio waliwao.
 
CCM izuie mjadala iwe iweje? Katika nchi ambayo uongozi wa nchi hauna pressure ya kuogopa mijadala ya wananchi basi ni Bongo. Wananchi wenyewe siku mbili tu wanakuwa wameshasahau kila kitu. N kama majoka ya kibisa tu, hawana madhara.
Kuna wana flan nipo nao job, yan hawa jamaa tokea lile tukio la kariakoo litokee cjawah kuwaskia wakizungumzia kwny mazungumzo yao. Yani kila mda ni mipira tu. Mpk nikajisemea tu kwel hii nchi acha watawala waeendelee kutuburuza, maana wananchi wengi bado ni wajinga sana.
 
Vipi wazembe waliosababisha hii dhahama ya Jengo kudondoka wameshakamatwa na Kuhojiwa ?
Watuhumiwa wa kwanza na muhimu kabisa hawajahojiwa.

Labda usikute kuna kiongozi mkubwa ndiye mhusika mkuu wa jengo hilo...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…