Polisi waanza kuonyesha zana za kupambana na wanaojipanga kufanya uhalifu wakati wa uchaguzi mkuu.

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Hakika jeshi limekuja kivingine, ukiweka ugoko wanaweka jiwe.

Hii ni moja ya zana ya kisasa ya kudhibiti wahuni kipindi cha uchaguzi, nyingine bado hazijaonyeshwa. Nasubiri nione dizaini ya rungu, nashauri kule Mbele ziwekewe kama miba miba hivi, ili zikigonga ugoko mtu asikilizie mpaka kwenye ubongo.

Pia gari za maji ya kuwasha yaongezwe ukali ili mtu ajikune kama Ndala Kasheba anapiga nyuzi za gitaa lake

 
Brand gani hii gari
 
SWAT TEAM imeingia katika jeshi letu la Polisi.

Toka maktaba: SWAT TEAM kazini nchini Marekani
 
Serikali inashindwa kuhudumia wajawazito ila pesa za kununua vifaa vya mauaji zipo
 
Kumbuka " Muosha huoshwa"
Akili za maccm wengi hudhani watanufaika na huu uhuni daima dumu.
 
Hawatoi bure, kwani in return anawagawia bandari, kia na ngorongoro
Nakumbuka mwaka 1994 Mrema akiwa waziri wa mambo ya ndani alienda kufanya shopping ya mabomu ya kisasa ya kutoa machozi huku akiwatukana wapinzani na kuwaita vichaa lakini mwaka 1995 akiwa mgombea wa Urais kupitia NCCR Mageuzi alikuwa wa kwannza kupigwa mabomu hayo kule Moshi na aliyekuwa RPC wa Kilimanjaro Omar Mahita karibu yampofue macho. Hawa hawa askari wanaowatumia kuteka na kuua wapinzani kuna siku watawageuzia hiyo mitutu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…