Polisi wakamata dhahabu ya Sh milioni 140 ikitoroshwa, mtuhumiwa atokomea, atelekeza gari

Polisi wakamata dhahabu ya Sh milioni 140 ikitoroshwa, mtuhumiwa atokomea, atelekeza gari

Mwanadamu ata umuwekee tozo elfu 2 atafanya jitihada akwepe tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Nope unakuta hawa wengi wanaokwepa kama asilimia lukuki ya kina TRA plus rushwa na red tapes za hapa na pale.....unakuta mtu anatoa hata robo tatu ambayo angetoa kama kodi anatoa Rushwa sasa kama unadhani Kodi na Tozo zingekuwa hata hio robo tatu au chini kidogo ya hapo wasingejipeleka wenyewe kutoa ?, unakuta pesa wanazotoa hongo za hapa na pale zile mtu angeweza kulipa kama zingekuwa na uhalisia...
 
Shida ipo wapi maana masoko ya madini yamewekwa karibu kila mkoa, sasa ni vyema serikali ikae tena. Chini na hawa wafanya biashara wa madini na wachimbaji ili wao wachimbaji pamoja na serikal.waje na maamizi ambayo ni win to win

Imaonekana soko la nje lina dhamani zaid au nini shida
 
Ina maana jamaa kwenye kizuizi akaacha gari akaanza kutoka mbio vichakan 😀😀😀😀
Uhalif sio mzur ila jamaa kama kapewa mzigo sio wake atakua sio mzoef
Mzigo zaidi ya 140mil unakamatwa tu kama kuku
 
Anatorosha kwenda wapi?Mtu bado yupo Mbeya ndani ya Tanzania useme anatorosha?.Kama alikuwa anaenda kutafuta soko zuri mkoa mwingine?

Polisi siwamini kabisa,ni majambazi yanayolipwa kwa kodi zetu.
Nakazia
 
Huenda polisi wa Japan wamekamata dhahabu ya milioni 600 ila wakafanya yao.


Tunawajua asilani hawawezi kuacha mzigo kirahisi.

Huyo wamemwmambia aseepe tu
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Maafisa Madini Wilaya ya Chunya limefanikiwa kukamata madini aina ya dhahabu yenye thamani zaidi ya Tsh milioni mia arobaini (140).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ulrich Matei, ameeleza kuwa Februari 9, 2022 majira ya saa 19:30 usiku katika kizuizi cha Polisi Chalangwa kilichopo Kata ya Chalangwa, Tarafa ya Kiwanja, Wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya, Askari Polisi kwa kushirikiana na Maafisa Madini Wilaya ya Chunya walikamata Gari T.948 DTM aina ya Toyota Crown iliyokuwa ikiendeshwa na mtu aliyefahamika kwa jina BARAKA SINGU @ NYODA, ambaye baada ya kusimamishwa kwenye kizuizi hicho alikimbia na kutelekeza gari hiyo.

Katika upekuzi uliofanywa kwenye gari hiyo vilikutwa vipande 36 vya madini aina ya dhahabu vyenye uzito wa gramu 1367.07 vyenye thamani ya Tshs. 147,694,961.83/= na fedha taslimu Tshs. 504,600/=, lengo ni kukwepa kodi na tozo za serikali.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na msako wa kumtafuta mtuhumiwa kwa hatua zaidi za kisheria.

Aidha, linatoa rai kwa wafanyabiashara kutambua kuwa mkono wa serikali ni mrefu hivyo ni vyema kufanya biashara halali kwa kufuata sheria na taratibu zilizopo ili kuepuka kukinzana na sheria.

View attachment 2114949
Usikute alipewa achaguwe kutimka yaishe au sheria ichukuwe mkondo wake
 
Unaacha madini yote hayo,kisa mrahaba wa 4% duu,sasa serikali inayauza na hela inaingia huko
Una uhakika baada ya tozo zote na makato yote total ni 4% pekee ?, Na huyo mununuzi huwa akienda kuuza huko dunia ya mbali faida yake huwa ni asilimia ngapi ?

Sio kwamba najua ninauliza tu kwa mwenye ufahamu breakdown ya hii kitu mnunuzi wa hapa analipia kiasi gani na mwisho wa siku akiuza anapata ngapi na serikali inapata ngapi....

Na ni ipo tofauti kuuzia kwenye soko lao la dhahabu au masoko ya nje, na je unaweza kuuza tu au mpaka uje na vielelezo ni wapi umeyatoa na Je hauhitaji leseni yoyote ?

Sababu kama hizi double taxation zilizopo huku kitaa na huko pia zipo basi black market haitaisha kamwe....
 
Hapo Polisi washapiga panga/wamesunda,hizo ndiyo wakakabidhi😀
😀
 
Back
Top Bottom