Polisi wazuia ndoa ya utotoni, muoaji na muolewaji wote wakiwa chini ya miaka 18

Polisi wazuia ndoa ya utotoni, muoaji na muolewaji wote wakiwa chini ya miaka 18

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na maofisa maendeleo ya jamii halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, wamezuia ndoa ya utotoni aliyokuwa akifungishwa mtoto wa miaka 15 kwa mahari ya ng'ombe kumi na fedha Sh200, 000 kwa mtoto mwenzake mwenye miaka 17.

Tukio la kufungishwa ndoa hiyo lilikuwa lifanyike jana Jumanne Agost 16, 2022 katika kijiji cha Manyada, Kata ya Usanda, ambapo askari polisi pamoja na maofisa maendeleo ya jamii walifika eneo la tukio na kuzuia ndoa hiyo kufungwa.

Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Deus Mhoja, alisema walipata taarifa ya kufungishwa ndoa ya mtoto huyo kutoka kwa wasamariawema ndipo wakapanga mikakati ya kwenda kuizuia kufungwa.

Mhoja amesema mtoto huyo (jina lake limehifadhiwa) inaelezwa amemaliza darasa la saba mwaka jana katika Shule ya Msingi Manyada na hakuendelea na masomo, ndipo wazazi wake wakachukua uamuzi wa kumuozesha.

“Sisi kama halmashauri, tutaona namna ya kumsaidia mtoto huyu ili aendelee na masomo na kuweza kutimiza ndoto zake, sababu bado ni mdogo sana na hatakiwi kuingia kwenye ndoa,” alisema Mhoja.

Kwa upande wake, mkuu wa dawati la jinsia na watoto wilaya ya Shinyanga kutoka Jeshi la Polisi Brihtone Rutajama ambaye alikuwa eneo la tukio alisema katika sherehe hiyo wamewakamata bibi harusi, mshenga, mama mzazi na mjomba wake huku wahusika wengine wakikimbia.

Aidha, alisema taarifa nyingine zaidi zitatolewa na Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani humo Janeth Magomi juu ya hatua zaidi ambazo zinafuata kwa wazazi hao.

Source: Mwananchi
 
Uzungu umeleta shida kubwa sana.

Mtoto wa miaka 15 ambaye shule ameshamaliza kuolewa na mtoto mwenzake wa miaka 17 nini cha ajabu. Wote wamesha balehe na wanaishi maisha ya kimila.

Hao walioenda kuwakamata wajiulize bibi zao waliolewa wakiwa na miaka mingapi na babu zao walioa wakiwa na miaka mingapi?

Ndoa ya kimila mnakataza kisa wadogo huku mnaruhusu uzinzi kwa jina la kizungu watiane kwa njia ya u boyfriend na u girlfriend. Sababu wote wamebalehe wana mahitaji ya kimwili. Watayapataje bila ndoa,

Kutunza mke sio ngumu maana mwanaume anapewa mashamba na mifugo na wazazi wake ndipo anaozeshwa.. kama hapo mahari ngombe 10 na hizo hela wazazi wake wamemlipia
 
Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na maofisa maendeleo ya jamii halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, wamezuia ndoa ya utotoni aliyokuwa akifungishwa mtoto wa miaka 15 kwa mahari ya ng'ombe kumi na fedha Sh200, 000 kwa mtoto mwenzake mwenye miaka 17.
Msiwaache waliochagua mchele, wapiga ngoma, shehe au mchungaji na mwenyekiti wa kijini, wote tupa ndani.
 
Wamuache binti wa watu aolewe. Mi nilidhani wanaenda kumtoa kafara.
Kumbe kutimiza agizo la kuzaa na kuongezeka?
Akifikisha miaka 30 bila mme wataanza kumsema.
Sometimes sheria za kikoloni zinaturudisha nyuma.
 
Eti tutamsaidia asome ili atimize ndoto zake, kwani kawaambia kama ana ndoto zozote kwenye elimu,, darasa la saba tu limemshinda mwacheni aolewe

Ustawi wa jamii wameona wivu maana pale kuna mimama huwa haiolewi na wakiolewa wiki wanaludi kwao.
 
Hivi wazungu wanaoana wakiwa na umri Gani?

1660737536326.png
 
Wanaenda kumpoteza binti wa watu maskini daaah.

Huyo akienda shule atapigwa rungu na walimu wake, wanafunzi wake mwisho adake mimba akiwa shule.

Na huko kijijini kwao sijui kama ataeleweka.
Wamwache dogo avute jiko mapema si ndo mila zao zilivyo, miaka 15 sio mtoto kiasi hicho
 
Hongera sana kwa jeshi la polisi Shinyanga
Kama hakuwa tayari kuolewa hapo sawa lakini kama ni sheria tu imembana, ipo siku atajutia.
Elimu ipo tu.
Binafsi kwa Sasa nina miaka zaidi ya 35 na sina mme wala mtoto. Nilikataa kuolewa kwa kigezo cha kusoma na kupata kazi kwanza.
Kweli nina kazi ila sina mme. Maisha nayaona hayana faida.
Maana kusoma hakuna umri wala mipaka, ila kuolewa kuna umri ukifika, yaani maombi ya kufunga kama yote kama sio kupishana kwa akina kalumanzila!😔

Nikiona binti anakatazwa kuolewa kwa kigezo cha umri, napata hasira sana. Labda kama hajapenda yeye binafsi.
Duniani tulikuja kuzaa na kuongezeka. Hizi elimu ni mfumo tu na ustaarabu wa kikoloni!

Mambo ninayoyapinga kwa nguvu zangu zote, ni ubakaji na ulawiti. Kumuingilia binti kwa lazima bila ridhaa yake au kinyume na maumbile. Lakini kuolewa, aolewe tu,azae!
 
Wanaenda kumpoteza binti wa watu maskini daaah.

Huyo akienda shule atapigwa rungu na walimu wake, wanafunzi wake mwisho adake mimba akiwa shule.

Na huko kijijini kwao sijui kama ataeleweka.
Wamwache dogo avute jiko mapema si ndo mila zao zilivyo, miaka 15 sio mtoto kiasi hicho
Tanzania ina maajabu sana aisee
 
Wanaenda kumpoteza binti wa watu maskini daaah.

Huyo akienda shule atapigwa rungu na walimu wake, wanafunzi wake mwisho adake mimba akiwa shule.

Na huko kijijini kwao sijui kama ataeleweka.
Wamwache dogo avute jiko mapema si ndo mila zao zilivyo, miaka 15 sio mtoto kiasi hicho

😆😆😆
 
Kama hakuwa tayari kuolewa hapo sawa lakini kama ni sheria tu imembana, ipo siku atajutia.
Elimu ipo tu.
Binafsi kwa Sasa nina miaka zaidi ya 35 na sina mme wala mtoto. Nilikataa kuolewa kwa kigezo cha kusoma na kupata kazi kwanza.
Kweli nina kazi ila sina mme. Maisha nayaona hayana faida.
Maana kusoma hakuna umri wala mipaka, ila kuolewa kuna umri ukifika, yaani maombi ya kufunga kama yote kama sio kupishana kwa akina kalumanzila![emoji17]

Nikiona binti anakatazwa kuolewa kwa kigezo cha umri, napata hasira sana. Labda kama hajapenda yeye binafsi.
Duniani tulikuja kuzaa na kuongezeka. Hizi elimu ni mfumo tu na ustaarabu wa kikoloni!
Pole. Aisee ningekuwa na umri wa miaka zaidi yako ningekuoa sema niko kwenye mid 20s. Dah ningekusitiri mkuu
Samahani kwa hilo.
 
Kama hakiwa tayari kuolewa hapo sawa lakini kama ni sheria tu imembana, ipo siku atajutia.
Elimu ipo tu.
Binafsi kwa Sasa nina miaka zaidi ya 35 na sina mme wala mtoto. Nilikataa kuolewa kwa kigezo cha kusoma na kupata kazi kwanza.
Kweli nina kazi ila sina mme. Maisha nayaona hayana faida.
Maana kusoma hakuna umri wala mipaka, ila kuolewa kuna umri ukifa yaani maombi ya kufunga kama yote kama sio kupisha kwa akina kalumanzila!

Nikiona binti anakatazwa kuolewa kwa kigezo cha umri, napata hasira sana. Labda kama hajapenda yeye binafsi.
Duniani tulikuja kuzaa na kuongezeka. Hizi elimu ni mfumo tu na ustaarabu wa kikoloni!
Lakini bado ni mtoto, she is only 16 kama sikosei, unadhani mtoto wa miaka 16 anaweza kumudu majukumu ya ndoa?

Dont blame yourself dear, kila kitu kinakuja kwa wakati wake, you should be greatful umepata elimu na una kazi nzuri, kuna watu wameolewa wapo majumbani hata mia ya kununua sabuni ya kuogea hawana na mume hana hata habari, sasa hapo unadhani anaona raha ya hiyo ndoa?

Atlist you can manage your life, Mungu atakupatia mume kwa muda wake
 
Back
Top Bottom