POMBE ‘Ganzi yenye maumivu’ (Safari yangu ya kuacha pombe)

POMBE ‘Ganzi yenye maumivu’ (Safari yangu ya kuacha pombe)

My dear bottle !

Chanzo cha yote ni pombe. Unaamka asubuhi unaenda kuoga uende kwenye mitikasi unashangaa kuona wapangaji wenzako wanakuangalia kwa huruma. Kumbe jana usiku ulikuja upo kiwingu ukaanza kumtongoza mama mwenye nyumba wako, mpangaji mwenzako wa kiume akakutoa.😁

My dear bottle!

Unakopa hela iende kwenye biashara, unasema wacha kwanza niende matako bar nistue moja baridi. Alafu nikadake mazaga, imeisha hiyoo.

Mpe pombe masikini asahau shida zake! Sababu bilion 1 madhara ya ulevi kupitiliza. Drink Responsibly!
 
Si muda mrefu sana ni miezi mitano tu sasa tangu niache naimani sitarudi tena
Ngoja niweke comment hapa ili mwakani tukuulize kwa mwaka mmoja pesa uliyookowa umefanyia nini? Itabidi utuoneshe nyumba au gari.
 
Nashukuru sana mkuu, kweli wanawake wanaoishi na walevi wanavumilia mengi sana hata wale wanaojiita walevi wastaarabu nao ni shida tupu nimekaa nao mimi unaweza kumuona mstaarabu sana kumbe kuna mambo ya kishenzi anayafanya gizani

Ni kwamba inapunguza ustaarabu wa wengi.

Wanasahau ahadi zao. Afya zao, familia zao, biashara, kazi zao, heshima zao. Wakipitiwa.

Wengi ni kero kubwa kwa familia, koo zao. Sababu wakilewa muda huo mchache unafuata wanafikiria pombe tu. Zikiisha ni watu wazuri. Tunaishi nao.
 
Mkuu Hongera sana.

Mimi pia kwa sasa namaliza mwezi wa pili baada ya kuachana na ulevi wa namna hiyo

Na naomba nikuunge mkono kuwa ni kweli pombe inaingiza watu kwenye matatizo mengi hasa Madeni, Uzinzi, migogoro ya ndoa, kupoteza kazi, kupoteza mali na kadhalika. Ni vigumu sana watu wengine kuelewa maana kuhusu ulevi it's all about levels, yaani mtu kafikia ulevi wa aina gani na amepata uwezo wa aina gani wa kujitambua.

Pombe ni mbaya sana. Tunywe kistaarabu kama tunakunywa , na imiwezekana tuache na tuwakimbie marafiki hawa wa pombe na tuwakemee

Asanteni sana
 
Umeongea ukweli 100% yaani hata wenye pesa nyingi za kuchezea, akichezea pesa kwasabab ya pombe na wanawake ni kawaida na lazima ataamka asubuh roho inamuuma nafsi inamsuta kwa upuuzi aliofanya jana yake...
Kuna watu humu mnajifanya walevi wastarabu lakini ukweli ni kwamba pombe inamaliza pesa, hata kama unakunywa bia mbili kusema kwamba unamatumiz mazuri ya pesa ni upumbav na kujipa moyo ujione unazimudu pombe...
All in all pombe ni tam sana ila zinatuCost sana kwa namna nyingi
 
Umeongea ukweli 100% yaani hata wenye pesa nyingi za kuchezea, akichezea pesa kwasabab ya pombe na wanawake ni kawaida na lazima ataamka asubuh roho inamuuma nafsi inamsuta kwa upuuzi aliofanya jana yake...
Kuna watu humu mnajifanya walevi wastarabu lakini ukweli ni kwamba pombe inamaliza pesa, hata kama unakunywa bia mbili kusema kwamba unamatumiz mazuri ya pesa ni upumbav na kujipa moyo ujione unazimudu pombe...
All in all pombe ni tam sana ila zinatuCost sana kwa namna nyingi
Keleleee nyiingii, sasa mbona wanywaji pombe ndio wenye maendeleo?

Ndinga kali zinapaki bar sijawahi kuona vijiwe vyenu wacheza karata, bao na draft kuna mtu kapaki hata Sn Lg tu.

Sasa mtu unasema pombe inamaliza hela kwani kazi ya pesa ni nini?

Kila mtu na vipaumbele vyake, wengine pesa zao zinaliwa kwenye ushirikina, wengine pesa zao zinaliwa makanisani na mitume na manabii kwa kuwatishia moto feki ahera wakati wao wenyewe hawajui majaliwa yao ya life after death.

Umeacha piga kimya njoo baada ya miaka mitatu utupe ushuhuda uliacha pombe na umalaya ukafanikiwa kusave na ukafanya moja mbili tatu, au show us your Ferari tutakuelewa, otherwise hizi nyenyenyenye hatuzitaki hazina tija.
 
Sijakataa watu wa design yako kama wapo? Ila elewa na wa design hii wapo pia tena wengi. Huwa tuna hesabu na maamuzi mazuri kabla ya kulewa lakini tukishakuwa tumelewa maamuzi hayo huyeyuka. Unaweza usikope lakini ukatumia zaidi ya ulichokuwa umepanga yote ni ufujaji wa pesa
Kwa hiyo ukiwa na laki tano yote unaenda nayo bar mkuu badala ya kuchukua elfu 30 au 40 na nyingine kuacha home??
 
Mimi ndio maana baa huwa naenda kama mchawi huwa sipendi kampani za kidwanzi unawanywesha watu kwa pesa yako ila wao hawazungushi raundi
Au unakaa kaunta.. Ukiondoka kaunta unampa bia moja na mnakuwa marafiki hata siku ukisahau kitu anakutunzia na pia hata ulewe vipi hakuzidishii bili
 
Mi niliacha pombe baada ya kupiga mzinga wa K Vant mwenyewe tena kavu,asubuhi nilipoamka nikawa naumwa na koromeo siwezi kumeza kitu zaidi ya maji na soda ,week mbili nilikuwa mgonjwa mi mtu wa uji tu . Nilipopona nikasema haya yote ya nini miye? Starehe gani inakuwa mateso ,nilipopona sikuendelea tena nilitumia mwanya huo kuacha pombe kabisa
Daaah lile lichupa likubwa ukalikata?? [emoji12] [emoji12] Haukuzima?? Maana ndiyo moja ya side effects za hiyo Kitu...
 
Kama ulishawahi kusoma nyuzi zangu mbili tatu hapa JamiiForum utagundua kabisa mimi ni cha pombe. Nikwambie tu mada zote nlizowahi kuzileta hapa ni za ukweli isipokuwa huwa nabadili kidogo maudhui ili kuepuka wazee wa kuunga dots, bado sijawa tayari kujiweka wazi mimi ni nani maana mengi ni ya aibu kwangu na jamii inayonizunguka na mengi nilikuwa nayafanyia gizani ukija mtaani kwangu mimi ni mtu mstaarabu na mpole sana.

Leo nimekuja tena na mada hii ya pombe lakini si kwa kuipa sifa za kijinga kama ilivyokuwa kwenye mada zile bali kuelezea jinsi nilivyoamua kuacha pombe, naamini sitarudi tena huko kwa bidii zangu na uwezo wake Allah (SW).

Kuna sababu nyingi zimenifanya kuacha pombe lakini kubwa zaidi ni madeni. Pombe iliniingiza kwenye madeni makubwa sana ambayo hadi leo hii bado kuna ambayo sijayamaliza, bado kuna watu nawalipa taratibu maana yalikuwa ni madeni haswa sio videni, kwa kipato changu kudaiwa 3,000,000 (milioni tatu) ya riba kubwa na mtu au watu ni jam kubwa sana na hapa sijaweka deni la taasisi ambalo natembea nalo mwaka wa pili huu sasa, nafikiri kwa sasa ngoma itakuwa bado inasoma kama 30 something million hivi au chini kidogo ya hapo.

Waajiriwa wengi na wafanyabiashara huchukua mikopo bank na huwa na manufaa sana kwao kwani husaidia kutimiza malengo yao kwa wakati lakini kwangu imekuwa kimeo sababu mkopo niliochukua nilitimiza malengo machache sana ya msingi na kubwa kuuza sura kwenye maeneo ya starehe na kulipa madeni (yani deni kwa deni!)

Mtu unaweza kujiuliza pombe inasababishaje kuingia kwenye madeni ya mamilioni?! Kama wewe ni mlevi, mpenda starehe na sifa bila kujali kipato chako huwezi kunishangaa ila kama wewe una sifa hizi na bado unanishangaa basi mshukuru Mungu kukupa uwezo huo wewe ni mlevi mwenye kujitambua. Hapa sijakataa kuwa wapo walevi wastaarabu wasiofuja pesa japokuwa hata kwao huwa haikosekani hata ile kidogo ya kujilaumu kutumia pesa tofauti na malengo.

Lakini usilewe sifa kimsingi walevi wengi ni wa hasara sema tu walevi huwa na tabia moja; Maumivu na mateso wanayopitia huwa hawapendi yawe wazi, maranyingi hupenda kuonekana wao ni watu wanaofurahia maisha kuliko yeyote hapa duniani na siku zote utawasikia “Basi pombe inamaliza hela ndugu yangu!... Mimi nikiwa hata na elfu kumi nalewa na nnarudi zangu nyumbani”. Weeeee!!!.... usijaribu ndugu yangu hakunaga mlevi wa hivyo na kama rafiki yako mlevi anakuambiaga yuko hivi anakudanganya.

Pombe imebeba mzigo mkubwa sana nyuma yake, usione mtu bar na bia yake mezani akinywa huku akitabasamu pekeake, akipiga story kwa uchangamfu na rafiki zake au akisimama na kucheza kwa furaha ukadhani mtu huyo ni mwenye kufurahia sana maisha na pombe inaishia hapo tu. Elewa kabisa nyuma ya pazia kuna mengi. Uzinzi, ufujaji pesa, kutoa ofa hovyo hata kwa usiowafahamu, kula hovyo (barbeque) hatakama huna njaa na kukopa hovyo ilimradi siku hiyo utimize lengo. Vyote hivi vipo nyuma ya pombe.

***Uko nyumbani kama mgonjwa sababu ya kuwaza pesa uliyoharibu jana kwenye pombe, huna raha kabisa maana unawaza ile pesa uliyochezea ungeweza hata kufanya kitu fulani cha maana. Mara inaingia simu toka kwa swahiba wako mlevi mwenzako.

“We Gee uko wapi?” inasikika sauti ya kilevi.

“Home Mazee” unajibu kinyonge kama mgonjwa sababu upo kitandani huna usingizi ila umelala na kujipindua pindua ukiwa umesongwa na mawazo.

“Aaaaah hahahaaa!!!.... we mjinga umelala nini? Acha ujinga wewe njoo hapa Machakani Lounge tupige vitu” anaongea jamaa yako akionekana mwenye furaha sana huku pembeni ukisikia shangwe la kutosha toka kwa wadau wengine.



Kwakuwa unajua shoo za mdau wako huyu unakurupuka kitandani bafuni fasta piga mswaki unaoga na kuvaa chap huku ukijiliwaza.

“Bora niende huko nipunguze stress maana nikikaa hapa nyumbani nazidi kuchanganyikiwa”

Unatoka ukimuaga mkeo na kumuomba akuazime 20 (toka kwenye hela za matumizi ya nyumbani) maana unaona kwenda mikono mitupu kabisa ni aibu lolote linaweza kutokea.

Unafika bar kweli jamaa wamewaka, vibe la kutosha kwenye meza ya duara kuna watoto wakali kama wanne hivi na washkaji wapo watatu tu, baada ya utambulisho unagundua kabisa mmoja umeachiwa wewe na kawaida ya walevi utasikia;

“We vuta kiti pale, wewe njoo huku alafu huyu akae hapa”

Unasogezewa zigo kiulaini bila hata kutumia nguvu, niwaambie tu jamani walevi maranyingi huwa hawatongozani mambo huwa yanajipanga yenyewe kama game tu. Ukiwa hujalewa vitendo hivi utaona vya kawaida kabisa wala havikuchukulii muda sana tena kuna wakati unajisemea moyoni

“Leo mimi nimekuja kulewa habari za wanawake sitaki, kwanza sina hela kabisa sitaki mambo mengi leo”

Ganzi ikianza kukuingia upuuzi unaanza pia. Dem ulikuwa unamuona wa kawaida mara unaanza kumuona Cleopatra na hivi wakati huo kakulalia pegani kichwa kinakujaa mwanaume unaanza kupiga hesabu kichwani. Mfukoni una 20 tu kuna watu wanakunywa wine hapo, 20 haitoshi. Fasta unamcheki mdau wako wa pesa za moto (za riba umiza) na walivyo hawa jamaa huwa wanaamini sana walevi (wenye vyanzo) hata ukimuomba laki3 wakati huohuo anakuletea, hii inanikumbusha jamaa mmoja aliwahi comment kwenye uzi wangu akisema kwamba alipokuwa mlevi alikuwa hakosi pesa kabisa tofauti na alipoacha. Huu ndio ukweli walevi huwa na mipango mingi ya pesa sema pesa zenyewe huwa za moto[emoji1787] . Mzigo ukifika bata linaendelea....***

Unafikiri asubuhi utaamkaje tena? Juzi umechezea pesa ukaamka unajilaumu, jana rafiki zako wanakushawishi ukanywe unaona ni sawa ili upunguze mawazo lakini baada ya kulewa unajikuta unafuja tena pesa!! Umeamka pombe imeisha na pesa imeisha na deni juu! Kweli pombe ni ganzi yenye maumivu tena maumivu makali sana.

Hii ni sababu kubwa iliyonifanya kuacha pombe, rafiki zangu wengi hawajaamini kama nimeacha na wengine wanafikiri nimetumia dawa au nilipewa dawa na ndungu zangu bila mimi kujua lakini ukweli ni kwamba nimeamua mwenyewe kuacha na InshaAllah sitarudi tena huko. Ili kukaa mbali na pombe nikaamua kuwa karibu na Allah sasaivi nafanya ibada maana ibada hutuweka mbali na maasi. Ukiwa na hofu ya Mungu utafata maamrisho yake.

Makosa yetu na ya watu wanaotuzunguka yawe funzo na si kuzidi kujaza kurasa chafu kwenye kitabu cha maisha yetu.

Wasalaam.View attachment 2210931
Allahuma Ameen.
Don't look back bruda.
 
Hii kitu ikiingia kwenye damu kuacha ni inshu,baada ya kujua mke wangu kazalishwa nje na mtoto sio wangu, hapa ndipo nilipoanzia kua chapombe, mwaka mmoja na nusu sijagusa pombe na sitaki tena.
 
Mkuu Mungu anitie nguvu nmeipiga chini sababu ya aibu inayoniletea ,nikirudia hakika ntakuwa nunda nmechoka na sumu acha niwe huru.
 
Kama ulishawahi kusoma nyuzi zangu mbili tatu hapa JamiiForum utagundua kabisa mimi ni cha pombe. Nikwambie tu mada zote nlizowahi kuzileta hapa ni za ukweli isipokuwa huwa nabadili kidogo maudhui ili kuepuka wazee wa kuunga dots, bado sijawa tayari kujiweka wazi mimi ni nani maana mengi ni ya aibu kwangu na jamii inayonizunguka na mengi nilikuwa nayafanyia gizani ukija mtaani kwangu mimi ni mtu mstaarabu na mpole sana.

Leo nimekuja tena na mada hii ya pombe lakini si kwa kuipa sifa za kijinga kama ilivyokuwa kwenye mada zile bali kuelezea jinsi nilivyoamua kuacha pombe, naamini sitarudi tena huko kwa bidii zangu na uwezo wake Allah (SW).

Kuna sababu nyingi zimenifanya kuacha pombe lakini kubwa zaidi ni madeni. Pombe iliniingiza kwenye madeni makubwa sana ambayo hadi leo hii bado kuna ambayo sijayamaliza, bado kuna watu nawalipa taratibu maana yalikuwa ni madeni haswa sio videni, kwa kipato changu kudaiwa 3,000,000 (milioni tatu) ya riba kubwa na mtu au watu ni jam kubwa sana na hapa sijaweka deni la taasisi ambalo natembea nalo mwaka wa pili huu sasa, nafikiri kwa sasa ngoma itakuwa bado inasoma kama 30 something million hivi au chini kidogo ya hapo.

Waajiriwa wengi na wafanyabiashara huchukua mikopo bank na huwa na manufaa sana kwao kwani husaidia kutimiza malengo yao kwa wakati lakini kwangu imekuwa kimeo sababu mkopo niliochukua nilitimiza malengo machache sana ya msingi na kubwa kuuza sura kwenye maeneo ya starehe na kulipa madeni (yani deni kwa deni!)

Mtu unaweza kujiuliza pombe inasababishaje kuingia kwenye madeni ya mamilioni?! Kama wewe ni mlevi, mpenda starehe na sifa bila kujali kipato chako huwezi kunishangaa ila kama wewe una sifa hizi na bado unanishangaa basi mshukuru Mungu kukupa uwezo huo wewe ni mlevi mwenye kujitambua. Hapa sijakataa kuwa wapo walevi wastaarabu wasiofuja pesa japokuwa hata kwao huwa haikosekani hata ile kidogo ya kujilaumu kutumia pesa tofauti na malengo.

Lakini usilewe sifa kimsingi walevi wengi ni wa hasara sema tu walevi huwa na tabia moja; Maumivu na mateso wanayopitia huwa hawapendi yawe wazi, maranyingi hupenda kuonekana wao ni watu wanaofurahia maisha kuliko yeyote hapa duniani na siku zote utawasikia “Basi pombe inamaliza hela ndugu yangu!... Mimi nikiwa hata na elfu kumi nalewa na nnarudi zangu nyumbani”. Weeeee!!!.... usijaribu ndugu yangu hakunaga mlevi wa hivyo na kama rafiki yako mlevi anakuambiaga yuko hivi anakudanganya.

Pombe imebeba mzigo mkubwa sana nyuma yake, usione mtu bar na bia yake mezani akinywa huku akitabasamu pekeake, akipiga story kwa uchangamfu na rafiki zake au akisimama na kucheza kwa furaha ukadhani mtu huyo ni mwenye kufurahia sana maisha na pombe inaishia hapo tu. Elewa kabisa nyuma ya pazia kuna mengi. Uzinzi, ufujaji pesa, kutoa ofa hovyo hata kwa usiowafahamu, kula hovyo (barbeque) hatakama huna njaa na kukopa hovyo ilimradi siku hiyo utimize lengo. Vyote hivi vipo nyuma ya pombe.

***Uko nyumbani kama mgonjwa sababu ya kuwaza pesa uliyoharibu jana kwenye pombe, huna raha kabisa maana unawaza ile pesa uliyochezea ungeweza hata kufanya kitu fulani cha maana. Mara inaingia simu toka kwa swahiba wako mlevi mwenzako.

“We Gee uko wapi?” inasikika sauti ya kilevi.

“Home Mazee” unajibu kinyonge kama mgonjwa sababu upo kitandani huna usingizi ila umelala na kujipindua pindua ukiwa umesongwa na mawazo.

“Aaaaah hahahaaa!!!.... we mjinga umelala nini? Acha ujinga wewe njoo hapa Machakani Lounge tupige vitu” anaongea jamaa yako akionekana mwenye furaha sana huku pembeni ukisikia shangwe la kutosha toka kwa wadau wengine.



Kwakuwa unajua shoo za mdau wako huyu unakurupuka kitandani bafuni fasta piga mswaki unaoga na kuvaa chap huku ukijiliwaza.

“Bora niende huko nipunguze stress maana nikikaa hapa nyumbani nazidi kuchanganyikiwa”

Unatoka ukimuaga mkeo na kumuomba akuazime 20 (toka kwenye hela za matumizi ya nyumbani) maana unaona kwenda mikono mitupu kabisa ni aibu lolote linaweza kutokea.

Unafika bar kweli jamaa wamewaka, vibe la kutosha kwenye meza ya duara kuna watoto wakali kama wanne hivi na washkaji wapo watatu tu, baada ya utambulisho unagundua kabisa mmoja umeachiwa wewe na kawaida ya walevi utasikia;

“We vuta kiti pale, wewe njoo huku alafu huyu akae hapa”

Unasogezewa zigo kiulaini bila hata kutumia nguvu, niwaambie tu jamani walevi maranyingi huwa hawatongozani mambo huwa yanajipanga yenyewe kama game tu. Ukiwa hujalewa vitendo hivi utaona vya kawaida kabisa wala havikuchukulii muda sana tena kuna wakati unajisemea moyoni

“Leo mimi nimekuja kulewa habari za wanawake sitaki, kwanza sina hela kabisa sitaki mambo mengi leo”

Ganzi ikianza kukuingia upuuzi unaanza pia. Dem ulikuwa unamuona wa kawaida mara unaanza kumuona Cleopatra na hivi wakati huo kakulalia pegani kichwa kinakujaa mwanaume unaanza kupiga hesabu kichwani. Mfukoni una 20 tu kuna watu wanakunywa wine hapo, 20 haitoshi. Fasta unamcheki mdau wako wa pesa za moto (za riba umiza) na walivyo hawa jamaa huwa wanaamini sana walevi (wenye vyanzo) hata ukimuomba laki3 wakati huohuo anakuletea, hii inanikumbusha jamaa mmoja aliwahi comment kwenye uzi wangu akisema kwamba alipokuwa mlevi alikuwa hakosi pesa kabisa tofauti na alipoacha. Huu ndio ukweli walevi huwa na mipango mingi ya pesa sema pesa zenyewe huwa za moto[emoji1787] . Mzigo ukifika bata linaendelea....***

Unafikiri asubuhi utaamkaje tena? Juzi umechezea pesa ukaamka unajilaumu, jana rafiki zako wanakushawishi ukanywe unaona ni sawa ili upunguze mawazo lakini baada ya kulewa unajikuta unafuja tena pesa!! Umeamka pombe imeisha na pesa imeisha na deni juu! Kweli pombe ni ganzi yenye maumivu tena maumivu makali sana.

Hii ni sababu kubwa iliyonifanya kuacha pombe, rafiki zangu wengi hawajaamini kama nimeacha na wengine wanafikiri nimetumia dawa au nilipewa dawa na ndungu zangu bila mimi kujua lakini ukweli ni kwamba nimeamua mwenyewe kuacha na InshaAllah sitarudi tena huko. Ili kukaa mbali na pombe nikaamua kuwa karibu na Allah sasaivi nafanya ibada maana ibada hutuweka mbali na maasi. Ukiwa na hofu ya Mungu utafata maamrisho yake.

Makosa yetu na ya watu wanaotuzunguka yawe funzo na si kuzidi kujaza kurasa chafu kwenye kitabu cha maisha yetu.

Wasalaam.View attachment 2210931
Allah azidi kukuongoza ndugu yangu katika imani fanya toba ya kweli kabisa na udhamirie haswa kuacha Pombe

Lakini ndugu yangu isijekua umeacha kisa mambo yapo kombo ila maisha yakirudi katika hali nzuri unarudi huko
Cha mwisho cha kukushauri tafuta darsa uwe unasoma ili ujiweke karibu na mola wako

kuhusu Madhambi ya Pombe uloyafanya usikhofu sana kwani Allah anasema maovu atayabadilisha kua mema soma aya 2 za chini hapo utaona
20220505_070142.jpg
 
Yaani nikope pesa kwa ajili ya pombe? Aisee mimi ni mlevi lakini siwezi kuingia madeni sababu niendelee kulewa, Nilijifunza kwenda bar na kiasi fulani cha pesa, kikiisha ni nduki home hata kama nina access ya kukopa labda kama kutakuwa na washkaji ambao watalendeleza libeneke.
Bado muda utafika
 
Kama ulishawahi kusoma nyuzi zangu mbili tatu hapa JamiiForum utagundua kabisa mimi ni cha pombe. Nikwambie tu mada zote nlizowahi kuzileta hapa ni za ukweli isipokuwa huwa nabadili kidogo maudhui ili kuepuka wazee wa kuunga dots, bado sijawa tayari kujiweka wazi mimi ni nani maana mengi ni ya aibu kwangu na jamii inayonizunguka na mengi nilikuwa nayafanyia gizani ukija mtaani kwangu mimi ni mtu mstaarabu na mpole sana.

Leo nimekuja tena na mada hii ya pombe lakini si kwa kuipa sifa za kijinga kama ilivyokuwa kwenye mada zile bali kuelezea jinsi nilivyoamua kuacha pombe, naamini sitarudi tena huko kwa bidii zangu na uwezo wake Allah (SW).

Kuna sababu nyingi zimenifanya kuacha pombe lakini kubwa zaidi ni madeni. Pombe iliniingiza kwenye madeni makubwa sana ambayo hadi leo hii bado kuna ambayo sijayamaliza, bado kuna watu nawalipa taratibu maana yalikuwa ni madeni haswa sio videni, kwa kipato changu kudaiwa 3,000,000 (milioni tatu) ya riba kubwa na mtu au watu ni jam kubwa sana na hapa sijaweka deni la taasisi ambalo natembea nalo mwaka wa pili huu sasa, nafikiri kwa sasa ngoma itakuwa bado inasoma kama 30 something million hivi au chini kidogo ya hapo.

Waajiriwa wengi na wafanyabiashara huchukua mikopo bank na huwa na manufaa sana kwao kwani husaidia kutimiza malengo yao kwa wakati lakini kwangu imekuwa kimeo sababu mkopo niliochukua nilitimiza malengo machache sana ya msingi na kubwa kuuza sura kwenye maeneo ya starehe na kulipa madeni (yani deni kwa deni!)

Mtu unaweza kujiuliza pombe inasababishaje kuingia kwenye madeni ya mamilioni?! Kama wewe ni mlevi, mpenda starehe na sifa bila kujali kipato chako huwezi kunishangaa ila kama wewe una sifa hizi na bado unanishangaa basi mshukuru Mungu kukupa uwezo huo wewe ni mlevi mwenye kujitambua. Hapa sijakataa kuwa wapo walevi wastaarabu wasiofuja pesa japokuwa hata kwao huwa haikosekani hata ile kidogo ya kujilaumu kutumia pesa tofauti na malengo.

Lakini usilewe sifa kimsingi walevi wengi ni wa hasara sema tu walevi huwa na tabia moja; Maumivu na mateso wanayopitia huwa hawapendi yawe wazi, maranyingi hupenda kuonekana wao ni watu wanaofurahia maisha kuliko yeyote hapa duniani na siku zote utawasikia “Basi pombe inamaliza hela ndugu yangu!... Mimi nikiwa hata na elfu kumi nalewa na nnarudi zangu nyumbani”. Weeeee!!!.... usijaribu ndugu yangu hakunaga mlevi wa hivyo na kama rafiki yako mlevi anakuambiaga yuko hivi anakudanganya.

Pombe imebeba mzigo mkubwa sana nyuma yake, usione mtu bar na bia yake mezani akinywa huku akitabasamu pekeake, akipiga story kwa uchangamfu na rafiki zake au akisimama na kucheza kwa furaha ukadhani mtu huyo ni mwenye kufurahia sana maisha na pombe inaishia hapo tu. Elewa kabisa nyuma ya pazia kuna mengi. Uzinzi, ufujaji pesa, kutoa ofa hovyo hata kwa usiowafahamu, kula hovyo (barbeque) hatakama huna njaa na kukopa hovyo ilimradi siku hiyo utimize lengo. Vyote hivi vipo nyuma ya pombe.

***Uko nyumbani kama mgonjwa sababu ya kuwaza pesa uliyoharibu jana kwenye pombe, huna raha kabisa maana unawaza ile pesa uliyochezea ungeweza hata kufanya kitu fulani cha maana. Mara inaingia simu toka kwa swahiba wako mlevi mwenzako.

“We Gee uko wapi?” inasikika sauti ya kilevi.

“Home Mazee” unajibu kinyonge kama mgonjwa sababu upo kitandani huna usingizi ila umelala na kujipindua pindua ukiwa umesongwa na mawazo.

“Aaaaah hahahaaa!!!.... we mjinga umelala nini? Acha ujinga wewe njoo hapa Machakani Lounge tupige vitu” anaongea jamaa yako akionekana mwenye furaha sana huku pembeni ukisikia shangwe la kutosha toka kwa wadau wengine.



Kwakuwa unajua shoo za mdau wako huyu unakurupuka kitandani bafuni fasta piga mswaki unaoga na kuvaa chap huku ukijiliwaza.

“Bora niende huko nipunguze stress maana nikikaa hapa nyumbani nazidi kuchanganyikiwa”

Unatoka ukimuaga mkeo na kumuomba akuazime 20 (toka kwenye hela za matumizi ya nyumbani) maana unaona kwenda mikono mitupu kabisa ni aibu lolote linaweza kutokea.

Unafika bar kweli jamaa wamewaka, vibe la kutosha kwenye meza ya duara kuna watoto wakali kama wanne hivi na washkaji wapo watatu tu, baada ya utambulisho unagundua kabisa mmoja umeachiwa wewe na kawaida ya walevi utasikia;

“We vuta kiti pale, wewe njoo huku alafu huyu akae hapa”

Unasogezewa zigo kiulaini bila hata kutumia nguvu, niwaambie tu jamani walevi maranyingi huwa hawatongozani mambo huwa yanajipanga yenyewe kama game tu. Ukiwa hujalewa vitendo hivi utaona vya kawaida kabisa wala havikuchukulii muda sana tena kuna wakati unajisemea moyoni

“Leo mimi nimekuja kulewa habari za wanawake sitaki, kwanza sina hela kabisa sitaki mambo mengi leo”

Ganzi ikianza kukuingia upuuzi unaanza pia. Dem ulikuwa unamuona wa kawaida mara unaanza kumuona Cleopatra na hivi wakati huo kakulalia pegani kichwa kinakujaa mwanaume unaanza kupiga hesabu kichwani. Mfukoni una 20 tu kuna watu wanakunywa wine hapo, 20 haitoshi. Fasta unamcheki mdau wako wa pesa za moto (za riba umiza) na walivyo hawa jamaa huwa wanaamini sana walevi (wenye vyanzo) hata ukimuomba laki3 wakati huohuo anakuletea, hii inanikumbusha jamaa mmoja aliwahi comment kwenye uzi wangu akisema kwamba alipokuwa mlevi alikuwa hakosi pesa kabisa tofauti na alipoacha. Huu ndio ukweli walevi huwa na mipango mingi ya pesa sema pesa zenyewe huwa za moto[emoji1787] . Mzigo ukifika bata linaendelea....***

Unafikiri asubuhi utaamkaje tena? Juzi umechezea pesa ukaamka unajilaumu, jana rafiki zako wanakushawishi ukanywe unaona ni sawa ili upunguze mawazo lakini baada ya kulewa unajikuta unafuja tena pesa!! Umeamka pombe imeisha na pesa imeisha na deni juu! Kweli pombe ni ganzi yenye maumivu tena maumivu makali sana.

Hii ni sababu kubwa iliyonifanya kuacha pombe, rafiki zangu wengi hawajaamini kama nimeacha na wengine wanafikiri nimetumia dawa au nilipewa dawa na ndungu zangu bila mimi kujua lakini ukweli ni kwamba nimeamua mwenyewe kuacha na InshaAllah sitarudi tena huko. Ili kukaa mbali na pombe nikaamua kuwa karibu na Allah sasaivi nafanya ibada maana ibada hutuweka mbali na maasi. Ukiwa na hofu ya Mungu utafata maamrisho yake.

Makosa yetu na ya watu wanaotuzunguka yawe funzo na si kuzidi kujaza kurasa chafu kwenye kitabu cha maisha yetu.

Wasalaam.View attachment 2210931
Hongera Sana Mkuu Kwa hatua hiyo,ni uamuzi unaohitaji ujasiri mkubwa, Mimi mwenyewe ni mnywaji sana lkn sio mlevi maana nakunywa kwa viwango vyenye mipaka,na sijawahi kufuja pesa kiasi ambacho wewe umeelezea.
 
Daaah lile lichupa likubwa ukalikata?? [emoji12] [emoji12] Haukuzima?? Maana ndiyo moja ya side effects za hiyo Kitu...
sikuzima ,hata hivyo nilikunywa nikiwa nyumbani,aisee nilipoamka ndo hivo chakula chochote hakiliki
 
Back
Top Bottom