Hahahahahaha[emoji23][emoji28][emoji28]Keleleee nyiingii, sasa mbona wanywaji pombe ndio wenye maendeleo?
Ndinga kali zinapaki bar sijawahi kuona vijiwe vyenu wacheza karata, bao na draft kuna mtu kapaki hata Sn Lg tu.
Sasa mtu unasema pombe inamaliza hela kwani kazi ya pesa ni nini?
Kila mtu na vipaumbele vyake, wengine pesa zao zinaliwa kwenye ushirikina, wengine pesa zao zinaliwa makanisani na mitume na manabii kwa kuwatishia moto feki ahera wakati wao wenyewe hawajui majaliwa yao ya life after death.
Umeacha piga kimya njoo baada ya miaka mitatu utupe ushuhuda uliacha pombe na umalaya ukafanikiwa kusave na ukafanya moja mbili tatu, au show us your Ferari tutakuelewa, otherwise hizi nyenyenyenye hatuzitaki hazina tija.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji2][emoji1787][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]Hii kitu ikiingia kwenye damu kuacha ni inshu,baada ya kujua mke wangu kazalishwa nje na mtoto sio wangu,hapa ndipo nilipoanzia kua chapombe,mwaka mmoja na nusu sijagusa pombe na sitak tena.
Wamejaa porojo tu kufundisha watu maisha wakati kila miaka inavyokwenda ndio wanazidi kupigika tu.Hahahahahaha[emoji23][emoji28][emoji28]
Afuu kweli asee, sijawahi ona wanywa soda wamepaki X6
Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
kuna wasiokunywa pombe waliofanikiwa,pia kuna wanywa pombe waliofanikiwa na ambao hawajafanikiwa piaWamejaa porojo tu kufundisha watu maisha wakati kila miaka inavyokwenda ndio wanazidi kupigika tu.
Amekudanganya nani? Hayo magonjwa ni life style za binadamu wenyewe, unywe pombe, usinywe pombe mtindo wako wa maisha utakufikisha hapo.Umeongea ukweli mtupu,achilia mbali hayo matumizi mabaya na uasherati,pia inashawishi hata kuiba sehemu yako ya kazi kama kuna hiyo mianya,lakini pombe ina madhara sana kwenye afya zetu,walevi wengi au wanywaji wasio na mipaka wameishia kuugua Pressure,kisukari,ini,Figo,uchizi n.k...
InshaAllah!... Hii nimeacha kwa nia moja mkuu na sio kwamba namaisha magumu sasaivi, kama ni pesa ya matumizi hainipigi chenga kama ningekuwa na nia ya kulewa nisingeshindwa kunywa kila sikuAllah azidi kukuongoza ndugu yangu katika imani fanya toba ya kweli kabisa na udhamirie haswa kuacha Pombe
Lakini ndugu yangu isijekua umeacha kisa mambo yapo kombo ila maisha yakirudi katika hali nzuri unarudi huko
Cha mwisho cha kukushauri tafuta darsa uwe unasoma ili ujiweke karibu na mola wako
kuhusu Madhambi ya Pombe uloyafanya usikhofu sana kwani Allah anasema maovu atayabadilisha kua mema soma aya 2 za chini hapo utaona View attachment 2212006
Endelea tu kunywa babu yangu,fainali ni uzeeni,utanitafuta siku moja na kunipa beer moja ya baridi ya Carlsberg kuniunga mkono ninayoyasema...Amekudanganya nani? Hayo magonjwa ni life style za binadamu wenyewe, unywe pombe, usinywe pombe mtindo wako wa maisha utakufikisha hapo.
Mtu pombe hunywi halafu unakula hovyo kama nguruwe wewe unadhani kati yako na anayekunywa pombe nani mwenye hatari ya kupata hayo maradhi? Kwanza hicho kisukari ni magonjwa ya kurithi hayo.
Sasa si mpaka ufike uzeeni? Unaweza kufa mapema tu kwa pneumonia.Endelea tu kunywa babu yangu,fainali ni uzeeni,utanitafuta siku moja na kunipa beer moja ya baridi ya Carlsberg kuniunga mkono ninayoyasema...
......mustakabar different.👏👏😄😄Usiache pombe sababu ya umaskini acha pombe sababu umeamua nakuhakikishia yeyote anaecha sababu amekosa pesa siku akizipata itakuwa hatari mara 11.....mimi mlevi hayo yote nayapitia sio siri ila life goes on......drink responsible
Hongera sana mkuu.Kama ulishawahi kusoma nyuzi zangu mbili tatu hapa JamiiForum utagundua kabisa mimi ni cha pombe. Nikwambie tu mada zote nlizowahi kuzileta hapa ni za ukweli isipokuwa huwa nabadili kidogo maudhui ili kuepuka wazee wa kuunga dots, bado sijawa tayari kujiweka wazi mimi ni nani maana mengi ni ya aibu kwangu na jamii inayonizunguka na mengi nilikuwa nayafanyia gizani ukija mtaani kwangu mimi ni mtu mstaarabu na mpole sana.
Leo nimekuja tena na mada hii ya pombe lakini si kwa kuipa sifa za kijinga kama ilivyokuwa kwenye mada zile bali kuelezea jinsi nilivyoamua kuacha pombe, naamini sitarudi tena huko kwa bidii zangu na uwezo wake Allah (SW).
Kuna sababu nyingi zimenifanya kuacha pombe lakini kubwa zaidi ni madeni. Pombe iliniingiza kwenye madeni makubwa sana ambayo hadi leo hii bado kuna ambayo sijayamaliza, bado kuna watu nawalipa taratibu maana yalikuwa ni madeni haswa sio videni, kwa kipato changu kudaiwa 3,000,000 (milioni tatu) ya riba kubwa na mtu au watu ni jam kubwa sana na hapa sijaweka deni la taasisi ambalo natembea nalo mwaka wa pili huu sasa, nafikiri kwa sasa ngoma itakuwa bado inasoma kama 30 something million hivi au chini kidogo ya hapo.
Waajiriwa wengi na wafanyabiashara huchukua mikopo bank na huwa na manufaa sana kwao kwani husaidia kutimiza malengo yao kwa wakati lakini kwangu imekuwa kimeo sababu mkopo niliochukua nilitimiza malengo machache sana ya msingi na kubwa kuuza sura kwenye maeneo ya starehe na kulipa madeni (yani deni kwa deni!)
Mtu unaweza kujiuliza pombe inasababishaje kuingia kwenye madeni ya mamilioni?! Kama wewe ni mlevi, mpenda starehe na sifa bila kujali kipato chako huwezi kunishangaa ila kama wewe una sifa hizi na bado unanishangaa basi mshukuru Mungu kukupa uwezo huo wewe ni mlevi mwenye kujitambua. Hapa sijakataa kuwa wapo walevi wastaarabu wasiofuja pesa japokuwa hata kwao huwa haikosekani hata ile kidogo ya kujilaumu kutumia pesa tofauti na malengo.
Lakini usilewe sifa kimsingi walevi wengi ni wa hasara sema tu walevi huwa na tabia moja; Maumivu na mateso wanayopitia huwa hawapendi yawe wazi, maranyingi hupenda kuonekana wao ni watu wanaofurahia maisha kuliko yeyote hapa duniani na siku zote utawasikia “Basi pombe inamaliza hela ndugu yangu!... Mimi nikiwa hata na elfu kumi nalewa na nnarudi zangu nyumbani”. Weeeee!!!.... usijaribu ndugu yangu hakunaga mlevi wa hivyo na kama rafiki yako mlevi anakuambiaga yuko hivi anakudanganya.
Pombe imebeba mzigo mkubwa sana nyuma yake, usione mtu bar na bia yake mezani akinywa huku akitabasamu pekeake, akipiga story kwa uchangamfu na rafiki zake au akisimama na kucheza kwa furaha ukadhani mtu huyo ni mwenye kufurahia sana maisha na pombe inaishia hapo tu. Elewa kabisa nyuma ya pazia kuna mengi. Uzinzi, ufujaji pesa, kutoa ofa hovyo hata kwa usiowafahamu, kula hovyo (barbeque) hatakama huna njaa na kukopa hovyo ilimradi siku hiyo utimize lengo. Vyote hivi vipo nyuma ya pombe.
***Uko nyumbani kama mgonjwa sababu ya kuwaza pesa uliyoharibu jana kwenye pombe, huna raha kabisa maana unawaza ile pesa uliyochezea ungeweza hata kufanya kitu fulani cha maana. Mara inaingia simu toka kwa swahiba wako mlevi mwenzako.
“We Gee uko wapi?” inasikika sauti ya kilevi.
“Home Mazee” unajibu kinyonge kama mgonjwa sababu upo kitandani huna usingizi ila umelala na kujipindua pindua ukiwa umesongwa na mawazo.
“Aaaaah hahahaaa!!!.... we mjinga umelala nini? Acha ujinga wewe njoo hapa Machakani Lounge tupige vitu” anaongea jamaa yako akionekana mwenye furaha sana huku pembeni ukisikia shangwe la kutosha toka kwa wadau wengine.
Kwakuwa unajua shoo za mdau wako huyu unakurupuka kitandani bafuni fasta piga mswaki unaoga na kuvaa chap huku ukijiliwaza.
“Bora niende huko nipunguze stress maana nikikaa hapa nyumbani nazidi kuchanganyikiwa”
Unatoka ukimuaga mkeo na kumuomba akuazime 20 (toka kwenye hela za matumizi ya nyumbani) maana unaona kwenda mikono mitupu kabisa ni aibu lolote linaweza kutokea.
Unafika bar kweli jamaa wamewaka, vibe la kutosha kwenye meza ya duara kuna watoto wakali kama wanne hivi na washkaji wapo watatu tu, baada ya utambulisho unagundua kabisa mmoja umeachiwa wewe na kawaida ya walevi utasikia;
“We vuta kiti pale, wewe njoo huku alafu huyu akae hapa”
Unasogezewa zigo kiulaini bila hata kutumia nguvu, niwaambie tu jamani walevi maranyingi huwa hawatongozani mambo huwa yanajipanga yenyewe kama game tu. Ukiwa hujalewa vitendo hivi utaona vya kawaida kabisa wala havikuchukulii muda sana tena kuna wakati unajisemea moyoni
“Leo mimi nimekuja kulewa habari za wanawake sitaki, kwanza sina hela kabisa sitaki mambo mengi leo”
Ganzi ikianza kukuingia upuuzi unaanza pia. Dem ulikuwa unamuona wa kawaida mara unaanza kumuona Cleopatra na hivi wakati huo kakulalia pegani kichwa kinakujaa mwanaume unaanza kupiga hesabu kichwani. Mfukoni una 20 tu kuna watu wanakunywa wine hapo, 20 haitoshi. Fasta unamcheki mdau wako wa pesa za moto (za riba umiza) na walivyo hawa jamaa huwa wanaamini sana walevi (wenye vyanzo) hata ukimuomba laki3 wakati huohuo anakuletea, hii inanikumbusha jamaa mmoja aliwahi comment kwenye uzi wangu akisema kwamba alipokuwa mlevi alikuwa hakosi pesa kabisa tofauti na alipoacha. Huu ndio ukweli walevi huwa na mipango mingi ya pesa sema pesa zenyewe huwa za moto[emoji1787] . Mzigo ukifika bata linaendelea....***
Unafikiri asubuhi utaamkaje tena? Juzi umechezea pesa ukaamka unajilaumu, jana rafiki zako wanakushawishi ukanywe unaona ni sawa ili upunguze mawazo lakini baada ya kulewa unajikuta unafuja tena pesa!! Umeamka pombe imeisha na pesa imeisha na deni juu! Kweli pombe ni ganzi yenye maumivu tena maumivu makali sana.
Hii ni sababu kubwa iliyonifanya kuacha pombe, rafiki zangu wengi hawajaamini kama nimeacha na wengine wanafikiri nimetumia dawa au nilipewa dawa na ndungu zangu bila mimi kujua lakini ukweli ni kwamba nimeamua mwenyewe kuacha na InshaAllah sitarudi tena huko. Ili kukaa mbali na pombe nikaamua kuwa karibu na Allah sasaivi nafanya ibada maana ibada hutuweka mbali na maasi. Ukiwa na hofu ya Mungu utafata maamrisho yake.
Makosa yetu na ya watu wanaotuzunguka yawe funzo na si kuzidi kujaza kurasa chafu kwenye kitabu cha maisha yetu.
Wasalaam.View attachment 2210931
Pombe siyo jela ila pombe si kwa ajili ya kila mtu.Hongera sana mkuu.
Inawezekana kabisa kuacha pombe moja kwa moja na ukafurahia maisha kwa njia nyengine.
Nami nilikuwa mlevi pia ingawa sikufikia kiwango hicho ulichoelezea lakini bado hali haikuwa ya kujivunia hata kidogo na kwa namna fulani najutia maisha yale.
Namshukuru Mungu huu ni mwaka wa nne sasa nimeshaachana na pombe na kwa sasa najiona nipo huru sana.
Allah akusimamie katika maamuzi yako haya uweze kufanikiwa na akuongoze katika kheri.
Pia unapoleta uzi kama huu inabidi ujiandae kwa kejeli na dhihaka za kila namna kutoka kwa wale wanaojiita 'wanywaji'.
Hivyo wewe jikite kwenye maudhui ya uzi wako kwani naamini una faida kwa wengi ambao bado wamefungwa kwenye jela ya pombe na wanatamani kuachana nayo,na hao ndio wengi.
Wewe jamaa kama vile ili bandiko ni lakwangu linanihusu kwa kila kilichopo kwenye hu uzi, nami nimekata shauri naelekea kufikisha mwezi Sasa. Kikombe noma sana wakuu kinaharibu future mazimaKama ulishawahi kusoma nyuzi zangu mbili tatu hapa JamiiForum utagundua kabisa mimi ni cha pombe. Nikwambie tu mada zote nlizowahi kuzileta hapa ni za ukweli isipokuwa huwa nabadili kidogo maudhui ili kuepuka wazee wa kuunga dots, bado sijawa tayari kujiweka wazi mimi ni nani maana mengi ni ya aibu kwangu na jamii inayonizunguka na mengi nilikuwa nayafanyia gizani ukija mtaani kwangu mimi ni mtu mstaarabu na mpole sana.
Leo nimekuja tena na mada hii ya pombe lakini si kwa kuipa sifa za kijinga kama ilivyokuwa kwenye mada zile bali kuelezea jinsi nilivyoamua kuacha pombe, naamini sitarudi tena huko kwa bidii zangu na uwezo wake Allah (SW).
Kuna sababu nyingi zimenifanya kuacha pombe lakini kubwa zaidi ni madeni. Pombe iliniingiza kwenye madeni makubwa sana ambayo hadi leo hii bado kuna ambayo sijayamaliza, bado kuna watu nawalipa taratibu maana yalikuwa ni madeni haswa sio videni, kwa kipato changu kudaiwa 3,000,000 (milioni tatu) ya riba kubwa na mtu au watu ni jam kubwa sana na hapa sijaweka deni la taasisi ambalo natembea nalo mwaka wa pili huu sasa, nafikiri kwa sasa ngoma itakuwa bado inasoma kama 30 something million hivi au chini kidogo ya hapo.
Waajiriwa wengi na wafanyabiashara huchukua mikopo bank na huwa na manufaa sana kwao kwani husaidia kutimiza malengo yao kwa wakati lakini kwangu imekuwa kimeo sababu mkopo niliochukua nilitimiza malengo machache sana ya msingi na kubwa kuuza sura kwenye maeneo ya starehe na kulipa madeni (yani deni kwa deni!)
Mtu unaweza kujiuliza pombe inasababishaje kuingia kwenye madeni ya mamilioni?! Kama wewe ni mlevi, mpenda starehe na sifa bila kujali kipato chako huwezi kunishangaa ila kama wewe una sifa hizi na bado unanishangaa basi mshukuru Mungu kukupa uwezo huo wewe ni mlevi mwenye kujitambua. Hapa sijakataa kuwa wapo walevi wastaarabu wasiofuja pesa japokuwa hata kwao huwa haikosekani hata ile kidogo ya kujilaumu kutumia pesa tofauti na malengo.
Lakini usilewe sifa kimsingi walevi wengi ni wa hasara sema tu walevi huwa na tabia moja; Maumivu na mateso wanayopitia huwa hawapendi yawe wazi, maranyingi hupenda kuonekana wao ni watu wanaofurahia maisha kuliko yeyote hapa duniani na siku zote utawasikia “Basi pombe inamaliza hela ndugu yangu!... Mimi nikiwa hata na elfu kumi nalewa na nnarudi zangu nyumbani”. Weeeee!!!.... usijaribu ndugu yangu hakunaga mlevi wa hivyo na kama rafiki yako mlevi anakuambiaga yuko hivi anakudanganya.
Pombe imebeba mzigo mkubwa sana nyuma yake, usione mtu bar na bia yake mezani akinywa huku akitabasamu pekeake, akipiga story kwa uchangamfu na rafiki zake au akisimama na kucheza kwa furaha ukadhani mtu huyo ni mwenye kufurahia sana maisha na pombe inaishia hapo tu. Elewa kabisa nyuma ya pazia kuna mengi. Uzinzi, ufujaji pesa, kutoa ofa hovyo hata kwa usiowafahamu, kula hovyo (barbeque) hatakama huna njaa na kukopa hovyo ilimradi siku hiyo utimize lengo. Vyote hivi vipo nyuma ya pombe.
***Uko nyumbani kama mgonjwa sababu ya kuwaza pesa uliyoharibu jana kwenye pombe, huna raha kabisa maana unawaza ile pesa uliyochezea ungeweza hata kufanya kitu fulani cha maana. Mara inaingia simu toka kwa swahiba wako mlevi mwenzako.
“We Gee uko wapi?” inasikika sauti ya kilevi.
“Home Mazee” unajibu kinyonge kama mgonjwa sababu upo kitandani huna usingizi ila umelala na kujipindua pindua ukiwa umesongwa na mawazo.
“Aaaaah hahahaaa!!!.... we mjinga umelala nini? Acha ujinga wewe njoo hapa Machakani Lounge tupige vitu” anaongea jamaa yako akionekana mwenye furaha sana huku pembeni ukisikia shangwe la kutosha toka kwa wadau wengine.
Kwakuwa unajua shoo za mdau wako huyu unakurupuka kitandani bafuni fasta piga mswaki unaoga na kuvaa chap huku ukijiliwaza.
“Bora niende huko nipunguze stress maana nikikaa hapa nyumbani nazidi kuchanganyikiwa”
Unatoka ukimuaga mkeo na kumuomba akuazime 20 (toka kwenye hela za matumizi ya nyumbani) maana unaona kwenda mikono mitupu kabisa ni aibu lolote linaweza kutokea.
Unafika bar kweli jamaa wamewaka, vibe la kutosha kwenye meza ya duara kuna watoto wakali kama wanne hivi na washkaji wapo watatu tu, baada ya utambulisho unagundua kabisa mmoja umeachiwa wewe na kawaida ya walevi utasikia;
“We vuta kiti pale, wewe njoo huku alafu huyu akae hapa”
Unasogezewa zigo kiulaini bila hata kutumia nguvu, niwaambie tu jamani walevi maranyingi huwa hawatongozani mambo huwa yanajipanga yenyewe kama game tu. Ukiwa hujalewa vitendo hivi utaona vya kawaida kabisa wala havikuchukulii muda sana tena kuna wakati unajisemea moyoni
“Leo mimi nimekuja kulewa habari za wanawake sitaki, kwanza sina hela kabisa sitaki mambo mengi leo”
Ganzi ikianza kukuingia upuuzi unaanza pia. Dem ulikuwa unamuona wa kawaida mara unaanza kumuona Cleopatra na hivi wakati huo kakulalia pegani kichwa kinakujaa mwanaume unaanza kupiga hesabu kichwani. Mfukoni una 20 tu kuna watu wanakunywa wine hapo, 20 haitoshi. Fasta unamcheki mdau wako wa pesa za moto (za riba umiza) na walivyo hawa jamaa huwa wanaamini sana walevi (wenye vyanzo) hata ukimuomba laki3 wakati huohuo anakuletea, hii inanikumbusha jamaa mmoja aliwahi comment kwenye uzi wangu akisema kwamba alipokuwa mlevi alikuwa hakosi pesa kabisa tofauti na alipoacha. Huu ndio ukweli walevi huwa na mipango mingi ya pesa sema pesa zenyewe huwa za moto[emoji1787] . Mzigo ukifika bata linaendelea....***
Unafikiri asubuhi utaamkaje tena? Juzi umechezea pesa ukaamka unajilaumu, jana rafiki zako wanakushawishi ukanywe unaona ni sawa ili upunguze mawazo lakini baada ya kulewa unajikuta unafuja tena pesa!! Umeamka pombe imeisha na pesa imeisha na deni juu! Kweli pombe ni ganzi yenye maumivu tena maumivu makali sana.
Hii ni sababu kubwa iliyonifanya kuacha pombe, rafiki zangu wengi hawajaamini kama nimeacha na wengine wanafikiri nimetumia dawa au nilipewa dawa na ndungu zangu bila mimi kujua lakini ukweli ni kwamba nimeamua mwenyewe kuacha na InshaAllah sitarudi tena huko. Ili kukaa mbali na pombe nikaamua kuwa karibu na Allah sasaivi nafanya ibada maana ibada hutuweka mbali na maasi. Ukiwa na hofu ya Mungu utafata maamrisho yake.
Makosa yetu na ya watu wanaotuzunguka yawe funzo na si kuzidi kujaza kurasa chafu kwenye kitabu cha maisha yetu.
Wasalaam.View attachment 2210931
[emoji23][emoji23] ndio kauli iliyopo mtaani kwetu mwagilia moyo au palilia moyoMwagilia moyoooo
Umeandika pumba shehe ungejikita kujibu hoja zake na sio hizi taarabu uNazoleta acha ujinga jibu maswalibyake kama unaawezaWewe inaonekana una stress za maisha, inaonekana umefeli shule hadi maisha, nyie ndio mkiwa bar mnatusumbua kuomba bia, na safar hii utapumuliwa sana mbwa wew. Jifunze kusoma na kuelewa hoja za watu sio unakurupuka tu
unachotetea hakieleweki mwishowe unaonekana mpuuzi tu wa mtaani mlevi asiye na mbele wala nyumaAmekudanganya nani? Hayo magonjwa ni life style za binadamu wenyewe, unywe pombe, usinywe pombe mtindo wako wa maisha utakufikisha hapo.
Mtu pombe hunywi halafu unakula hovyo kama nguruwe wewe unadhani kati yako na anayekunywa pombe nani mwenye hatari ya kupata hayo maradhi? Kwanza hicho kisukari ni magonjwa ya kurithi hayo.