comte
JF-Expert Member
- Dec 11, 2011
- 9,019
- 6,825
Nakubaliana nawe kabisa- ukiongea uzuri unataja na kujuza ubaya pia. Kwa kuzingatia hayo utaona mapungufu ya Mongella kule Arusha ambayo yanalengwa yakatekelezwe na Makonda.Wanabodi,
Jana niliangalia tukio la uapisho wa wateule wapya, Ikulu Dar es Salaam, na nilifarijika sana kuona miongoni mwa waalikwa wa tukio lile, ni Mzee wa Ngomeni, Richard Mwasha kwa jina maarufu la Kuhani Musa.
Nimefarijika sana kumuona Rais Samia akitoa sababu za kumteua kila aliyemteua na kumpa majukumu kwa uwazi kabisa.
Enzi za Kikwete, Tanzania tulisaini ule mkakati wa Open Government Initiative uliokuwa unasisitiza ukweli na uwazi, truth and transparency, JPM alipoingia, aliufuta mkakati huo, hata Bunge live likafutwa, mikutano ya vyama vya siasa ikapigwa marufuku na hata mikutano ya ndani kuzuiwa.
Rais Samia alipoingia, na falsafa yake ya 4R, akafanya mabadiliko mengi makubwa ikiwemo kufungulia mikutano ya siasa.
Kwa mujibu wa katiba yetu ya JMT, Rais wa JMT anaweza kushauriwa na wasaidizi wake, lakini kwenye kufikia maamuzi, rais anafikia uamuzi yeye kama yeye, na halazimiki kufuata ushauri wa yeyote, na hawajibiki kutoa sababu yoyote ya maamuzi yake.
Powers za rais kuteua na kutengua zinaitwa discretion powers, kwa rais kuteua, kutengua au kutumbua bila kutaa sababu yoyote kwa yeyote.
Hivyo kitendo cha Rais Samia kuwa open and transparent kwa kueleza sababu za kumtea fulani mahali fulani na kumpa majukumu kwa uwazi, hii ni hisani kubwa na nzuri kwa mustakabali mwema wa nchi yetu.
Anachokifanya rais Samia kuwa muwazi, open and transparent sababu za kuwateua wateule wake, ni hisani tuu, tena hata uapisho live Mubashara kisha kutolewa hotuba, kumeanza na JPM, zamani hatukuwahi kuwa na hotuba kwenye uapisho, ni kuapa tuu and that was it.
Kitu kizuri zaidi, sio tuu rais Samia anakuambia kwanini amekuteua, bali anaelekeza uende ukafanye nini!. Mfano RC Makonda amepewa special task Arusha, jiji la kitalii, hivyo anapaswa kwenye kukuza Utalii, ila pia kuna maelekezo mengine ya kuyashughulikia na Kuwashughulikia ikiwemo issues za wale machalii wa RChuga na 'cha Arusha".
Yule RC wa Mara ambaye ni mjeshi, kaelekezwa kwenda kushughulikia kijeshi jeshi kile kilimo cha lile zao, (hakulitaja) ambalo Mara ni maarufu na kulivusha mpakani na nchi jirani.
Hiki anachofanya Ras Samia ni sawa na ile Open Government Initiative, kwa mteuliwa kupewa changamoto openly and transparently, akishindwa ku deliver
The public yote itajua hivyo hiki ni kitu kizuri kwa uwajibikaji.
Tanzania tuna sheria ya haki ya kupata habari, au kupata taarifa, the right to information act, hivyo wananchi kuelezwa kila kinachowahusu ni haki yao na sio hisani.
Kwa vile Rais Samia ameisha onyesha njia kwa Kutuhisania, tuwe watu wa shukrani kwanza kwa kumshukuru kwa hiyo hisani tuu kwanza, kisa sasa tumuombe atupe na haki ya kupata taarifa, asiishie kwenye kutupatia taarifa za uteuzi tuu, tupatiwe na taarifa za sababu za utenguzi kwasababu maofisa hao ni watumishi wa umma, wanaolipwa na fedha za umma, hivyo umma una haki zote za kujua kuhusu utendaji wa wateule hao, na sababu za kutenguliwa kwao na kutumbuliwa.
Mfano Paul Makonda, baada ya kuteuliwa Mwenezi wa CCM, amefanya wonders katika kipindi kifupi na kurejesha imani ya wananchi kwa CCM, kwa kuwakimbiza viongozi mchaka mchaka, wengi wakitaraji mchaka mchaka huo ungeendelea hadi 2025, katika uchaguzi Makonda aingie Bungeni, na kupewa Wizara nyeti, lakini mara ghafla Makonda kama Mwenezi, akatumbuliwa!.
Mtu yoyote mwenye cheo kikubwa, akaondolewa na kuteuliwa cheo kidogo ni kutumbuliwa tuu!, hivyo Makonda ametumbuliwa uenezi na kupoozwa na u RC, Dr. Bashiru Ali Kakurwa alitumbuliwa uenezi na kupoozwa na ubunge wa kuteuliwa. DGIS wametumbuliwa mara kadhaa na kupoozwa na ubalozi, wengine wakitumbuliwa wanasugua bench, kama Balozi Liberata Mulamula, Prof. Kabudi, William Lukuvi na wengine wengi, the public has the right to know sababu, na sio kusubiria kuhisaniwa.
Kama ilivyo sifa njema kuteuliwa, mtumishi wa umma akiboronga, the public ielezwe!.
Tena kwa maoni yangu, nafasi za juu zote wakiwemo wakuu wa mihimili, Jaji Mkuu, Spika na wakuu wa zile independent organs zote, nafasi zinapokuwa wazi, Watanzania wenye sifa waombe, washindanishwe tupate the best ndipo rais apelekewe kuteua, na sio huu utaratibu wa sasa wa watu kuokotana, kuteuana na baada ya siku mbili kutenguliwa, haileti picha nzuri sana kwa awamu hii ya Rais Samia.
Nchi nyingi wakiwemo jirani zetu Kenya, Jaji Mkuu, anaomba kazi, anasailiwa, the best amechaguliwa.
Nimalizie kwa kumpongeza tena Rais Samia kwa kutuhisania openness and transparency kwenye teuzi zake, openness hii na transparency hii tuifanye na haki na sio hisani.
Wasalaam
Paskali
Paskal hata hivyo RJMT amesema mabadiliko mengi msingi wake ni kuboresha utendaji akimaanisha hakuna makosa makubwa- ni tactical based reshuffles