Preta njoo nikutongoze, wengine tulieni mjifunze



Jambazi on significant make..

Amazing!
 


Kwamba woote sasa mnatangaza nia ama vipi???

Vampire hunter ni kilietivu alafu hana gilaji...
 
Nafuatilia kwa ukaribu sana.........
Preta toa tamko, mie unikubalie
Zima zote chokochoko, penzi letu walilie
Ardhini kama Choroko, wapotee watitie
Mwingine usimkubalie, hawana nia ya kweli

Upendo wangu wa dhati, moyoni nimekuweka
Umekaa kwenye chati, lala nami kwenye mkeka
Wengine siguse titi, nitachukia hakika
La Azizi maliza ubishi, watoto wakalale

Kwangu wewe kama mboni, ntakupatia ulinzi
Nitakusafisha mtoni, mi nawe nguo na uzi
Kama ni maji pomoni, kipimo cha langu penzi
Achana na hawa wa msimu, mi wako wa kudumu

Nitafugia hata mbwa, kumalizia ghadhabu
Ka hujapika ubwabwa, dogi apewa adhabu
Wewe kamwe hutaguswa, wewe ka safi dhahabu
Wengine mabondia wa wapenzi wao, usiwape nafasi

Nena unikate kiu, kubali tumalizie
Vijana sasa msahau, jaribu tena badae
Mnaula wa kaukau, mchuzi nani kujazie
Sweet maliza kesi, waumbuke na zao pensi
 

Kijana huna kipaji, then wajitangazia ushindi
Hukumbuki kule zenji, yalomkuta yule dingi
Preta ni wangu mi mnyamwezi, nimpe love mingimingi
Wauza mitumba hawawezi, wanachojua fujo nyingi

Preta nkubali mimi, upate raha ya maisha
True love iko kwa mimi, wengine wanakupotosha
Waliku wapi toka zamani, Mpaka thread nimeanzisha
Hao hawana thamani, wanataka kunikwamisha

Hebu njoo utoe msimamo, vijana waache maneno
Tuwazike ndani ya shimo, tuwakate na msumeno
Tuwalambishe ndimu, tuwaache waking'ata meno
Mapenzi yetu yadumu, kikubwa tuwe na msimamo

Sera nshamwaga nyingi, njoo utupe yetu hukumu
Naamini kuna vigingi, wapo radhi wanipe sumu
Ila usijali preta, hawawezi kutudhuru
Wakileta za kuleta, watakimbia ka kunguru
 
Uwanjani mmekimbia, Preta mumeniachia
Mmebaki mnanyatia, moyoni mwenu mwalia
Binti anayevutia, mkonowe mmeachilia
Vimpire_Hunter na Moto, nyie moto wa mabua.

Hamuwezi kuhimili, magumu ya kupitia
Dhaifu yenu miili, hamna ya ukweli nia
Nimewazidi akili, kileleni nafikia
Mwende kimya kimya, msijeanza maneno ya mkosaji.

Uwanja huu ni mpana, mi na Preta meshibana
Bahatisheni kwa Anna, hawezi sema hapana
Ye nami tumeshikana, hatuwezi kuachana
Miss Chagga, Afrodenzi na Lara 1 nao ni wanawake, jaribuni huko.

Preta sio kama Tupa, visu butu kunolea
Mekosa mistari supa, moyoni nachekelea
Mmepata yote mifupa, nje nje amewatolea
Hiyo mistari yenu kajiribuni kwingine

Preta nipe langu Kombe, peke yangu nimesalia
Mzobemzobe nikusombe, achana na masalia
Tuchinje mkubwa ng'ombe, tusiache hata mkia
Kama Sikamona, Zawadi ya Ushindi nipatie.
 
Kama ni ushindi utakuwa ni wako
 
lazima hapa aingie line walahi
 
Dah! Shaaban Robert kafufuka nn maana mnapanga vina balaaa
 
Ntamani niyaone haya mashairi jukwaani jaman
 


Sooth debe tupu mfanowe, bila kutika hilo sio debe,
Mpaka kiboga uliwe, na zikuiishie zako ngebe,
Usilazimishe uchaguliwe, kama denti achuaguavyo mkebe,
Moto nakoleza pambano, Preta ni wangu wa enzi.

Preta ni wangu wa enzi, Vampire anajibaraguza,
Sooth hata unyoe bwenzi, Preta atakuuchuuza,
Hamuwezi nipoka wangu Mpenzi, haitotokea hiyo miujiza.
Miaka Nenda miaka rudi , Preta ndiye wangu laazizi

Preta ndiye wangu laazizi, ndiye wa moyo wangu mahamumu,
Hata kwa ndumba na mizizi, penzi letu katu hamtohujumu,
Hata muwe ving'ang'anizi, atawaona nyoka wa midimu,
Preta ndiye wangu nyonda, nina mtunza tangu enzi,

Tangu enzi nina mtunza, mapenzi na huba Nampatia,
Kutengeza magari nimemfunza, noti na kipato ajipatia,
Nimemnunulia starlet glanza, Sokoni kwa raha ajiondea,
Afrodenzi naye Lara 1, wakufaa wewe Sooth mdandiaji,

Sooth mjaribu miss chagga, huyo ni maji mara moja,
Preta wangu takubwaga, hata u jaribu mara elfu moja,
Misimamoye hakunaga, hata ulie mara elfu Mia moja.
Preta ni mmoja tu, nami moto2012 ndiye wake

Preta ni wangu waridi, mtima wangu ameujaza,
Mwendowe maridadi, tabasamule laniliwaza ,
Hakika sio mkaidi, Sooth kukuachia stoweza,
Preta wangu waepuke, Vampire naye Sooth.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…