Priscus Tarimo vs Ibra Line ni vita ya watoto wa mjini 2025

Priscus Tarimo vs Ibra Line ni vita ya watoto wa mjini 2025

Ndagullachrles

Senior Member
Joined
Jun 20, 2023
Posts
153
Reaction score
161
Kwenye Soka la Bongo hakuna shaka simba na Yanga ndiyo miamba ya soka nchini yenye mamilioni ya mashabiki.

Hata juzi juzi baada ya kuondoshwa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika mjadala umekuwa mkubwa sana hasa aina ya matokeo yaliyopatikana kwa kila timu.

Tuachane na soko,turudi kwenye siasa za bongo ambako mwakani tutashuhudia uchaguzi Mkuu wa wabunge,rais na madiwani.

Joto la kisiasa ni Kali sana katika Jimbo la Moshi mjini ambalo kwa Sasa linashikiliwa na mbunge wake Priscus Tarimo(CCM) aliyerithi mikoba kutoka kwa Jafari Michael wa Chadema Mwaka 2020.

Anqyetajwa kumpa presha Priscus Tarimo ni mfanyabiashara Ibrahim Shayo a.k.a Ibra Line ambaye Mwaka 2020 alitoa upinzani mkali kwa Priscus wakati wa kura za maoni.

Sasa kama ulikuwa haujui ni kwamba mwamba huyo yupo kwenye mawindo ya nguvu kuelekea kura za maoni ndani ya chama chake hapo mwakani.

Taarifa kutoka kwa watu wa karibu kqbisa na Ibra line zinapasha kuwa mwamba huyo analitaka Jimbo kweli kweli na wakati ukiwadia ataweka wazi kila kitu.

"Bro nakuambia kaka wa Jimbo lazima tumpe kura zake na aipeperushe bendera ya chama vizuri na tuko nae bega kwa bega",anasema mtu wa karibu na Ibra Line.

Wapo wanaomini kuwa jimbo la Moshi mjini limepwaya baada ya miaka 25 kuwa chini ya Kambi ya upinzani kabla ya Mwaka 2020 kuchukuliwa na CCM likiwa ni tukio la kihistoria kabisa.

Kwenye mitandao ya Kijamii mjadala ni mkubwa sana juu ya makada Hawa wawili na wapo wnaoamini kuwa kama Ibra line atashinda kura za maoni ndani ya ccm na jina lake likapitishwa na chama chake ,moto utawaka kwa upande wa upinzani.

Kwenye vijiwe vya kahawa na kwenye mikusanyiko ya watu mjadala ni mkubwa sana juu ya makada Hawa wawili japo wapo wengi wanaotajwa kujiwinda na jombo Hilo.

Kwenye matukio yanayohusu shughuli za Kijamii ni nadra sana kutokumuona Ibra Line na hicho ndo kimekuwq kikimuongezea umarufu.

Si hilo pekee,Ibra line amekuwa akitoa vyombo vyake vya usafiri kwa watu wanaopatwa na misiba hasa wenye uhitaji wa kusafirisha miili ya wapendwa wao.

"Kaka nikuhakikishie tu kwamba mwakani moto utawaka kwenye kura za maoni na watu hawataamini hicho kishindo kitakachotokea".

Kwa upande wa wanaomuunga mkono Priscus Tarimo wanaamini kuwa bado anahitajika kutetea jimbo ili aoamilishe ahadi zake kwa wapiga kura wake.

"Sisi tunaamini Priscus bado ananafasi ya kutetea kito chake kuanzia kwenye kura za maoni na mpaka kwenye sanduku la kura"anasema mtu wa karibu na Priscus Tarimo.
 
Ibra Hana nguvu kwenye chama uliza kilicho mkuta 2020 na Tarimo anamtegemea Mosha ila safari hii hata mmoja Hamna atakaye pita na huta amini ccm ni Zaid ya uijuavyo
 
Hao wapori ndio unawaita watoto wa mjini?
 
Tayari umeshavuta chako na kuweka mfukoni . Halafu unakuja JF kumnadi kwetu sisi tuliopo Uvinza, Katoro na Bombambili.

Nenda Moshi ukamnadi huko vijiweni na kwenye club za mbege ambapo ndiyo kuna wapiga kura wenu.
Mangi mimi Niko Moshi tangu 1995 siasa za moshi nazijua sana Mangi tangu enzi ya mbunge wa NCCR-Mageuzi na baadae Baba yetu Philemon Ndesamburo(mwenyezi mungu ailaze roho yake mahali pema peponi)
 
Si tulikubaliana watoto wa mjini ni walio zaliwa Ocean road ,kaliakoo na ilala.
Ama Kuna mabadiriko?
 
Mbunge aliyepo anafanya kazi nzuri achaneni na matapeli watu wa moshi mtakuja kujuta.
 
Back
Top Bottom