Private schools (English medium) ada kupanda maradufu 2023. Serikali iingilie kati

Private schools (English medium) ada kupanda maradufu 2023. Serikali iingilie kati

English Medium Schools siyo kwa ajili ya kila mtu.

Nyie wazazi mnaotaka serikali ipeleke pua kule mnataka hizo shule ziwe kama za serikali.
 
Wazazi jikuneni mnapofikia kama una uwezo mpeleke private kama ni apeche alolo mbombo ngafu mlete kidumu na mfagio. Kitu kingine nafikiria mtoto hata ukimleta shule za serikali ukimsimamia na ukawa mfuatiliaji mzuri atafaulu tu.
 
Mtu aliyeelimika vizuri atajiongoza vyema
Hamna kitu hapo; tutapambana nao kwenye hizi nafasi chache za tamisemi; usikubali uingie mtego wa kuwekeza gharama kubwa, ile ni biashara mkuu; wekeza gharama kubwa kama anaenda kusoma chuo cha nje mfano Oxford, Harvard na asome fani technical zenye tija, sio mambo ya history, sociology n.k.​
 
Hamna kitu hapo; tutapambana nao kwenye hizi nafasi chache za tamisemi; usikubali uingie mtego wa kuwekeza gharama kubwa, ile ni biashara mkuu; wekeza gharama kubwa kama anaenda kusoma chuo cha nje mfano Oxford, Harvard na asome fani technical zenye tija, sio mambo ya history, sociology n.k.​
Akili yako imeishia kwenye kuajiriwa...kwa kuwa umepata elimu mbovu
 
Serikali haina budi kufanya lolote liwezekanalo kufanya Shule hizi za private zisipandishe ada kiholela. Zinaweza zikapunguziwa gharama za uendeshaji ili ziwe na nafuu kwa malipo huko serikali.

Baadhi ya Shule vikao vishaanza. Kuna ongezeko la ada la kutisha na wanajiamulia wenyewe kwa utetezi kwamba gharama za maisha zimepanda. Sina shaka na hili kwani sote, ni mashahidi. Vitu havinunuliki.

Njia pekee ni serikali kuzipunguzia Shule hizi mzigo Wa kodi.

Sijui itakuwaje JANUARY!!? Au wazazi wenzangu mnasemaje!? Tupeleke watoto Kayumba!!!
Ipande tu tubaki wachache
 
Mpeleke mtoto shule za serikali na uwe unamkagua na kumfanyia usimamizi, inatosha kabisa.

Wanangu wanasoma Kayumba nawakagua, vitabu vyote nimewanunulia.

Na ratiba ya kusoma nimewapangia kuanzia 7:00 hadi saa 8:30 usiku niwakute mezani. Saa 8:30 hadi saa 9:00 kula.

Saa 9:30 wawe kitandani. Tamthilia wataangalia wiki endi.

Sisi wazazi wao tumesoma shule hizo hizo za St Kayumba na leo tuna masters, na mambo yanaenda.

Wengine wanapeleka watoto huko academy kufuata mkumbo tu. Hasa wazazi wasiosoma shule wazazi wenye elimu ndogo, wazazi vilaza, wanajivunia mtoto kuongea ze ze wanaona ndio mwanao anapaata elimuu.

Hitimisho kama uwezo unaruhusu mpeleke, lakin kama wewe mwenyewe kodi inakushinda halafu unakuja kutupigia kelele hapa.
Kwaio mzee inawezekana haujasimama vizuri kwenye maisha jipange msomeshe mtoto shule bora kua na masters sio hata tija..shule za private mtoto anapata na exposure hawezi kua mzembe mzembe...🤣🤣🤣
 
Nakuelewa lazima ulinde ugali wako.

Safari ya elimu Tanzania wanaofanya vizuri darasani vyuo vikuu huwa wanakutana udsm,mzumbe na Muhas .. haijalishi umesoma kayumba ama shule zenu za kina junior

Nenda udsm hata leo hii kafanye research wangapi wamesoma kayumba primary na wangapi wamesoma shule zenu za kinyonyaji..

Elimu ni content na sylabus sio lugha peke yake....

Mtoto wa shule ya msingi Madenge anafundishwa same sylabus yenye content hizo hizo ambazo wa tusiime primary school anafundishwa tofauti ni lugha ya kufundishia tu.

Sasa why ununue same content kwa bei ya milioni 2. Wakati mwenzako anazipata bure... na mwisho wa siku baada ya kidato cha sita hao wa madenge na tusiime wote wanakutana udsm na kwenye ajira za utumishi na mshahara sawa sawa
Hao wanaonunua syllabus kwa 2m ni sababu wazazi wao wanamudu kulipa..tukija kwenye ajira hao wa private wengi hu opt kwenda private wakati waliosoma shule za umma huamini kwa public employment ndo kila kitu...nkt hao wengine exposure inawawezesha kujua public employment haina issue yoyote...90% ya wanaolalamikia ajira za serikali wamesoma shule za serikali waliopiga private education hawataki hata kuzisikia hizo ajira za serikali za 900k kwa mwezi...🤣🤣😍
 
Mtoto wa shule ya msingi Madenge anafundishwa same sylabus yenye content hizo hizo ambazo wa tusiime primary school anafundishwa tofauti ni lugha ya kufundishia tu.

Sasa why ununue same content kwa bei ya milioni 2. Wakati mwenzako anazipata bure... na mwisho wa siku baada ya kidato cha sita hao wa madenge na tusiime wote wanakutana udsm na kwenye ajira za utumishi na mshahara sawa sawa
Sasa mkuu kama ni same content ...kwanini Private schools ndio zinaongoza mitihani ya kitaifa!!?
 
Sasa mkuu kama ni same content ...kwanini Private schools ndio zinaongoza mitihani ya kitaifa!!?
Ni sawa na kuku wa kienyeji anayejitafutia chakula chake mwenyewe vs kuku wa kisasa anayeletewa chakula; yule wakisasa atanona tu
 
Serikali haina budi kufanya lolote liwezekanalo kufanya Shule hizi za private zisipandishe ada kiholela. Zinaweza zikapunguziwa gharama za uendeshaji ili ziwe na nafuu kwa malipo huko serikali.

Baadhi ya Shule vikao vishaanza. Kuna ongezeko la ada la kutisha na wanajiamulia wenyewe kwa utetezi kwamba gharama za maisha zimepanda. Sina shaka na hili kwani sote, ni mashahidi. Vitu havinunuliki.

Njia pekee ni serikali kuzipunguzia Shule hizi mzigo Wa kodi.

Sijui itakuwaje JANUARY!!? Au wazazi wenzangu mnasemaje!? Tupeleke watoto Kayumba!!!

Ndiyo, huko hakuna ada! Na walimu wengi wanaofundisha Private schools ni hawa hawa wa Kayumba, kwa hiyo tupeleke huko watoto wetu!
 
Na shule nyingi za English medium watoto wengi wanaanza kuaribikia huko na ushoga na usagaji unaanzia huko nimeshaona mifano mingi na mwisho wa siku mzazi unaanzia kulalamika mtoto ameharibika na kumbe wewe ndio chanzo
Kwa hili napinga hii ipo kwa shule zote la muhimu nikuwaombea watoto wetu wawe na hofu ya Mungu na pia kuongea nao... Nina watoto ninao wafahamu wapo shule za kawaida wengine walianza kusagana darasa la 4 mzazi amekuja kugundua mtoto yuko la saba. Walimu wanasema hawana cha kufanya maana watoto wengi katika hiyo shule wako hivyo..
 
Serikali haina budi kufanya lolote liwezekanalo kufanya Shule hizi za private zisipandishe ada kiholela. Zinaweza zikapunguziwa gharama za uendeshaji ili ziwe na nafuu kwa malipo huko serikali.

Baadhi ya Shule vikao vishaanza. Kuna ongezeko la ada la kutisha na wanajiamulia wenyewe kwa utetezi kwamba gharama za maisha zimepanda. Sina shaka na hili kwani sote, ni mashahidi. Vitu havinunuliki.

Njia pekee ni serikali kuzipunguzia Shule hizi mzigo Wa kodi.

Sijui itakuwaje JANUARY!!? Au wazazi wenzangu mnasemaje!? Tupeleke watoto Kayumba!!!
Braza mahindi kilo ni 1500, maharagwe kilo ni 3400, mchele kilo ni 2800.
Mafuta ni 125.000 kwa ndoo, kuni hazishikiki na bado wafanyakazi ulionao na wao inabidi waongezewe mshahara maana tayari na wao wananunua bei hiyo hiyo. Petroli na dizeli ni 3000+ kwa lita. Mchukue mwanao mpeleke serikalini kabla ya mwakani. Hakuna namna vitu havitapanda bei aisee yani hakuna kabisaaaa
 
Wewe uwezo ndo unao kusumbua tu hamna lolote sabb zako hazina mashiko
Sasa mbona mnalalamika wanapandisha Ada huku mna uwezo wa kulipa , sasa lawama za nini c mlipe tu
 
Sasa mkuu kama ni same content ...kwanini Private schools ndio zinaongoza mitihani ya kitaifa!!?

Kabla sijajibu swali lako,

Unaelewa maana ya content ni nini?

Sasa najibu swali lako. Shule za private tena shule chache zinazoongoza mitihani ya kitaifa ni sababu ya factor nyingi mojawapo ni udanganyifu kwenye mitihani. Shule za private zipo zaidi ya 5000 . Je shule zote hizo 5000 huwa zinaongoza mitihani ya taifa ama shule chache kati ya hizo.

Pia Shule za private haziongozi mitihani ya kitaifa miaka yote. Kuna miaka shule za goverment zinaongoza pia.

Swali kwako pia. Je Mtaala wanaofundishiwa shule za private unazozitetea una ubora mkubwa wa maarifa ( knowledge) kuliko mtaala wanaofundishiwa shule za serikali za elimu bure?
 
Serikali haina budi kufanya lolote liwezekanalo kufanya Shule hizi za private zisipandishe ada kiholela. Zinaweza zikapunguziwa gharama za uendeshaji ili ziwe na nafuu kwa malipo huko serikali.

Baadhi ya Shule vikao vishaanza. Kuna ongezeko la ada la kutisha na wanajiamulia wenyewe kwa utetezi kwamba gharama za maisha zimepanda. Sina shaka na hili kwani sote, ni mashahidi. Vitu havinunuliki.

Njia pekee ni serikali kuzipunguzia Shule hizi mzigo Wa kodi.

Sijui itakuwaje JANUARY!!? Au wazazi wenzangu mnasemaje!? Tupeleke watoto Kayumba!!!
Peleka kayumba mkuu , yaani serekali iingilie shule za private wakati serekali yenyewe inasimamia shule zake ambazo Ada ni bure .
Kumpeleka mtoto wako private ni kihere here chako tu, Kama huwezi mpeleke kayumba acha kulalamika , waachie wenye uwezo waende private
 
Kweli kabsa ndugu ada zimepanda mpka zinakalibia juu mbinguni Serikali itusaidie tu kwenye hili
 
Gharama za kuendesha shule ni kubwa sana kwa kweli. Nilitamani nifungue shule ila kupiga gharama za uendeshaji na uwekezaji kwenye miundo mbinu, nikaona mara kumi ni heri ufungue hoteli/ Guest...
 
Back
Top Bottom