Prof. Assad: Niliondolewa kazini kinyume na taratibu kwasababu nilikuwa sifuati maelekezo ya Mtu

Prof. Assad: Niliondolewa kazini kinyume na taratibu kwasababu nilikuwa sifuati maelekezo ya Mtu

Assad 3-0 lumumba.
Mzee uwa anapiga kwenye mshono.alafu ni jeshi la mtu mmoja
 
Wewe utakuwa umeanza kufatilia siasa juzi... waulize watu humu Assad aliulizwa mbele ya Rais .....kuhusu hizo trillion 1.5 akasema kabisa hakuna zilizopotea tena hadharani ....labda useme alishikwa uoga lakini ukweli ni kwamba Assad hakuwai kupamba na Magufuli hata mara moja.... Assad alipambana na Ndugai tuuu lakini si Magufuli na wala asingelithubutu.... Tanzania kulikuwa na wanaume wawili tuu Lissu na Magufuli... wengine wameibuka baada ya Magu kufa akiwemo huyo Assad...
Ndugu mbona mambo yako wazi siku hizi? Aliulizwa Dotto na akajibu mheshimu Rais hazina tuko salama. Ndugu tulia fuatilia taratibu hapa hatutafuti mshindi tunakumbushana.
 
Niliondolewa Ofisini kinyume na taratibu kwa sababu nilikuwa nasimamia na kufanya kazi kwa kufuata taratibu na miongozo ya kazi na sio maelekezo ya mtu,kuna mahali viongozi wetu wanashindwa kusimamia wanachokiamini kwa hofu ya kuporwa V8, wanahofu kukosa riziki.

Hili suala la kuniita CAG aliyemaliza muda wake binafsi linaniudhi, katiba ibara ya 144 inatamka wazi muda wa kumaliza na sababu za kukoma kuwa CAG, mimi nilipotolewa ofisini sikuwa nimemaliza muda wangu. Nadhani hatukuwa wazuri katika kusimamia katiba.

Mussa si jina langu, jina alilonipa baba yangu ni Jaffar. Wakati nasoma kulitokea matatizo fulani, ikabidi nitoke sehemu moja kwenda nyingine ili kumaliza masomo na hili jina la Mussa nikalipata huko ila watu wanaonifahamu wananijua kama Jaffar- Profesa Mussa Assad, CAG wa zamani.
kipindi cha mwendazake ulikua usiponafkia au usipo kuwa mnafki hutoboi.

Asad yeye alishindwa kuusoma upepo wa wakati ule na kuendana nao sambamba.
 
Ila ana roho fulani ya ubinafsi ilitakiwa akae atulie hii ya kulia lia katika media inamtia doa kwa kujiona yeye ni bora zaidi ya wengine.

Na hii inaleta tafasri ya kwamba aliumia mno kutumbuliwa 😅
Aendelee kunyamizia uvunjwaji wa makusudi mazima wa katiba, eti ndio uungwana?
 
Kidume nan???yule alijitutumua kumbe ana shot ya umeme????
Analazimisha kuonekana ni mtu msomi anaejielewa ana misimamo.

Bahati mbaya alikutana na Chuma.

Nilichokuwa nampendea yule baba JPM ukijifanya wewe ni wa muhimu sana kwenye hii nchi yeye anakuonesha namna ulivyo takataka tu na nchi inaweza kwenda mbele bila wewe hahahah.

Profesa uliondolewa na kidume sasa unalialia nini!!?
 
This man is a genious aise, halafu ana maisha simple sana kuna kipindi nilipishana nae pale millenium tower akisubiri usafiri wa Uber.
Role number one
"Never outshine the master"
 
Nadhan hujui huyu Mzee alipo sasa hana elimu ya magumashi kama yule iblis wenu
Magu alikuwa sahihi kabisa huyu mzee mara agombane na bunge mara achokonoe mambo ya ikulu...sasa naona maumivu ya kupigwa benchi hayajapona.

Hii ni nchi ukitaka uwa outshine wenye mamlaka lazima upigwe na kitu kizito.
 
Kwa maelezo yake tu huyu mzee ni mwenye kiburi na mwenye kujiabudu (self-worshiping)!
Kama yeye alikua appointed kulikua na shida gani mwenye mamlaka na yeye kuchukua iyo nafasi na kumpa mwingine? Je haoni kua katiba anayojifanya kuisimamia ilipaswa explicitly nafasi ya CAG ilipaswa itangazwe na iwe shindanishi ili kuondoa makandokando yote? Wakati Mkwere anatamba na Mamereta, Escrow na madubwasha mengine hapo mwishoni yeye alikua wapi?
Unafiki ni asili ya mtz..na muoga haachi asili!
Naona wajitahidi kukwepa suala halisi. Katiba ilivunjwa waziwazi kwa makusudi na Jiwe.
Inashangaza sana Jiwe anaposifiwa kwa tabia ya kuvunja Katiba. Waimba mapambio nao
Mkono wa Mungu ndio ulituokoa na udhalimu huu uliyokuwa unakuwa kwa kasi kubwa.
 
Mkuu kama ni kweli huyo MZEE ni mnyenyekevu sana
This man is a genious aise, halafu ana maisha simple sana kuna kipindi nilipishana nae pale millenium tower akisubiri usafiri wa Uber.
 
Back
Top Bottom