Prof. Assad: Niliondolewa kazini kinyume na taratibu kwasababu nilikuwa sifuati maelekezo ya Mtu

Wewe inaonesha umezaliwa hivi karibuni&umebahatika mapema kupata simu janja,wote tuliosoma zamani kubadilishiwa jina lilikuwa jambo la kawaida
Kwanini abadili jina hao ndio walikua wanabana majina ya wengine enzi zile shule zikiwa chache
 
Huyo kidume aliejifanya ni bora zaidi hata kulilo Mungu yupo wapi

Sent from my TECNO KA7O using JamiiForums mobile app
 
Kwa sheria za nchi huyu hawezi tena kupata cheo kingine serikalini.
Labda mjumbe wa bodi kwenye mashirika
ndiyo nnacho shauri, sheria hiyo ibadilishwe..

mbona mzee baba mlitaka aongoze bila kikomo, na ndugai aliridhia..

kwa assad, nchi inamwitaji kuliko anavyo ihitaji..

apewe hata unakamu wazir mkuu
 
Na Mwamba Assad Yuko zake mjini anadunda tu huku aliyempiga fitina sijui ye Yuko wapi SA hivi [emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]

anadunda na bado analia mpaka leo[emoji3][emoji3]au kudunda kuna maana ngapi??
 
anadunda na bado analia mpaka leo[emoji3][emoji3]au kudunda kuna maana ngapi??

Hahah mwamba yuko mjini anatamba tu aliyejifanya mbabe sijui hata yuko wapi Siku hizi,simsikii sana habari zake teh teh.
 
Profesa uchwara aliyejifanya mhimili wakati mihimili iko 3 tu.

Ajaribu kugombea urais basi labda timu gaidi watamsajili 2025.
Ni kweli asigimbee atachafuka bure kama Watanzania wa wastani ndiyo hawa wanaozungumzia mambo kwa ushabiki!
 
Kiukwel moja ya watu makin ambao hawayumbishwi na mihemko ya wachache wenye nguvu. Mcha Mungu, mtu wa haki
 
Waambie mkuu. Alihoji pesa ya Chattel na mengine mengi maovu. Yule Mungu shetani akamtoa. Ila Mungu ni fundi zaidi. Yako wapi sasa?
Kabla hajaondoka alidai atakuja gombea umalaika mkuu, labda yuko huko.
 
Assad ni profesa gani huyu asiyejua kusoma katiba. CAG anateuliwa kwa kipindi cha miaka mitano, baada ya hapo anaweza kuteliwa tena kwa kipindi cha miaka mitano minge kwa ukomo wa miaka kumi. Yeye anseoma kuwa anatakaiwa awe CAG kwa miaka kumi? Alimaliza kipindi cha miaka mitano, halafu hakupewa kipindi kingine cha miaka mitano. Sasa analialia nini, CAG huteliwa na Rais, hachaguliwi na wananchi.

Kumbe ilimuuma sana, ndiyo maana mara tu baada ya JPM kufariki akaanza kelele; anatumaini mama atamrudisha! Halafu ofisi ya CAG ni taasisi siyo mtu; yeye mwenyewe Assad hakuwa anakagua vitabu bali kuna wakaguzi chini ya ofisi ya CAG. Sasa anataka kutuambia kuwa yeye ndiye aliyekuwa anafanya kila kitu bila kufuata eti "maelekezo;" mpuuzi sana huyu.

Kama kuna wakati hela za umma zilitumika vibaya ni wakati wa Kikwete; kuna kipindi ofisi ya rais ilipewa supplementary budget baada ya kukomba hela zote zilizokuwa zimetengewa kabla ya mda wake.
 
Bahati mbaya tupo nyuma ya Keyboard
Bahati mbaya au nzuri? Unaweza ukawa nyuma ya keyboard lakini ukawa verified user. Kwa hiyo, kuwa anonymous hapa is your choice.
 
Naona kaona upepo umeelekea ufukweni hvyo anajua yoyote yule akiwemo yeye anaweza rudishwa kazini.

Uenda anatest zali kusoma upepo asije teuliwa maneno ikawa mingiii
 
Nimetoa point zangu kama mlipa kodi. kama huzielewi au huzitaki sio lazima uchangie.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…