Prof. Kabudi na Tundu Lissu wanastahili kuwa kwenye Serikalli ya Rais Samia

Tundu Lissu hawezi kufanya kazi kwenye saluni ya mamakimbo, viongozi wanasengenyana wao kwa wao!
 
Lissu hana uoga anasimama kwenye misimamo yake no matter what hata uko CHADEMA mara kadhaa amekemea wazi wazi maamuzi ya Mbowe mfano suala la maridhiano Lissu alishalikataa kuanzia mwanzo kabisa, kwa mtu ambae sio muoga wa challenge Lissu ni mtu sahihi zaidi wa kufanya nae kazi ingawa sina uhakika kama Lissu atakubali kufanya kazi na CCM na hata akikubali hawatadumu lazima watazinguana tu because Lissu is a man of principles while CCM ili uende nao sawa ni sharti ujizime data kichwani ingawa nina wasiwasi kidogo na uwezo wa Lissu kiuongozi huyu jamaa naona ana-fit zaidi kuwa mwanaharakati. Lakini uyo Kabudi hana misimamo pale ambapo anaona kuna uwezekano masilahi yake yakaguswa tuliona mfano kipindi cha jiwe alifika mpaka hatua ya kusema ameokotwa jalalani, alikunywa mitishamba kudanganya umma ni dawa ya covid19. Kujidhalilisha kote uko ilikua ni kwa ajiri ya kulinda kibarua chake ivyo hawezi kuwa wa tofauti kama mama akitaka kumtumia kwa masilahi binafsi kama alivyotumiwa na jiwe
 
huyu huyu aliekua haamini nchi kuongozwa na mwanamke πŸ’

amekupa kiasi gani?,
mweleze tu ukweli kwamba, kwanza si si mzalendo, ni mbaguzi tena wa kijinsia, aliekusudia kuinajisi katiba.
Kwahiyo haifai kabisa na tamaa zake za madaraka πŸ’

Lakin huyo mwingine, baada ya kufadhiliwa matatizo yake na mabwenyenye na yeye kuwahadaa kwamba ana uwezo wa kua mkuu wa nchi. wamemteka physically and mentally na kumfanya kibaraka wao kwa maleongo yao πŸ’

nae vilevile hafaia na haitawezekana kwa namna yoyote eti apate nafasi ya kutumikia serikali ya Tz kwa maslahi ya mabwenyenye yanayo mtuma πŸ’

bilashaka umeelewa. Hiyo hela waliokupa itumie vizuri na usiwarudie tena πŸ’
 
Kuteuliwa kufanya kazi ya nchi yako siyo kurubuniwa.
Kama taifa linakuhitaji kufanya kazi furani kwa sababu ya uwezo ulionao ni hiyari kukataa ama kuridhia, lakini si kweli kwamba kila anayeteuliwa amerubuniwa.
Huo ni ufisadi wa kumnyamazisha mpinzani wako kwa cheo! Sawa na mwanamke kutoa rushwa ya ngono apate cheo au kazi!
 
Lisu hawezi fanya kazi na mafisi na walafi wasio na chembe za huruma. Zamu yake ipo karibu ya ukombozi wakweli pasipo ushirika na wezi hawa
 
Huyu huyu tunaemheshimu. Eti akafanye kazi kwenye Serikali moja na Konda Boy???
Huyu Dunianui chini ya Jua hakuna kinachi shindikana, Mandela alifanya na watwsi wake na sasa South Africa mambo ni safi ukiwaacha vibaka wanao shambulia ndugu zao waaafrica huko
 
Umeeleza vizuri sana ndugu yangu, ikiwa Mandela aliweza kufanya kazi na watesi wake, hata lissu anawaweza. Ni hilo tu...
 
Umeeleza vizuri sana ndugu yangu, ikiwa Mandela aliweza kufanya kazi na watesi wake, hata lissu anawaweza. Ni hilo tu...
Uyo Mandela hatujui walikubaliana nini na hao watesi wake kule gerezani, something tell me he was a sell out.
 

..Kinachohitajika ni KATIBA MPYA na TUME HURU.

..Hatuhitaji watu kupewa vyeo, na kugeuzwa chawa wa Raisi.

..Prof.Kabudi alikuwa na misimamo yake ya kitaaluma, alipoteuliwa akawa chawa mkubwa wa Magufuli.
 
'Kazi ya uongozi ni ngumu sana'!

Kwani anafanya kazi dependent?

Nadhani maudhui ya mleta mada ni kuwa 'madini' wanayoyamwaga nje ya mfumo, waje wayamwagie ndani ili yalete manufaa.

Uwaziri or whatever unafanyakazi kwa collective responsibilities, kwa hiyo umakame nguvu na dosari zingine za mihemko ya mtu hufichwa na kanuni hiyo.

Nami naungana na mtoa hoja ingawa hajawataja wengi wazuri waliopo nje ya mfumo wanaoweza kulisaisia taifa kuvuka tulipokwama na kusonga mbele.

Uchadema ama Uccm ni matabaka kama matabaka ya dini na ukiwachunguza wote unaona kabisa utofauti wao si wa maslahi kwa nchi bali ni wa kusaka ugali wa kushibisha matumbo yao.
 
Kabudi mzee wa jalalani, arudi tu kwenye jalala, Lissu hana uhakika na anachosema, anaposema fulani alihusika katika shambulio ana uhakika gani? Ataipeleka nchi pabaya.
 
..Kinachohitajika ni KATIBA MPYA na TUME HURU.

..Hatuhitaji watu kupewa vyeo, na kugeuzwa chawa wa Raisi.

..Prof.Kabudi alikuwa na misimamo yake ya kitaaluma, alipoteuliwa akawa chawa mkubwa wa Magufuli.
Katika mpya na tume huru ni hitaji letu pia lakini mada husika haihusiani na katiba wala tume hutu mada iliyopo mezani inahusu namna gani taifa linaweza kunufaika na Lissu na Kabudi kwa kuangalia wasifu wao.
 
Nilimsikia Rais wa zamani wa moja ya nchi za Africa Mashariki,siku za nyuma akisema" SIKU ZOTE AKILI KUBWA NI MALI YA NCHI" mwisho wa kunukuu
 
Mzee mzima kumuita binadamu Mungu ndio unamfagilia, angekuwa kijana sawa tungesema tamaa ya hela na cheo

Kutuletea juice toka Madagascar sijui wapi na kusema inatibu Corona yeye na yule Dorothy please
Kama unataka muendelezo wa kuabudu binadamu sawa
 
Unanikumbusha unyumbu, kuahirisha kufikiri kwasababu ya kujipendekeza ama uoga kwa viongozi na kutumikia kundi Fulani badala ya masilahi ya nchi, herding behavior
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…