Prof. Kabudi: Ndege ya Tanzania, Bombardier Q400 imekamatwa Canada na kesi ipo Mahakamani

Prof. Kabudi: Ndege ya Tanzania, Bombardier Q400 imekamatwa Canada na kesi ipo Mahakamani

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi Kabudi amesema ndege ya Tanzania Bombardier Q400 iliyokuwa iwasili nchini hivi karibuni imekamatwa nchini Canada na kesi ipo Mahakamani

======

NDEGE NYINGINE YA TANZANIA YAKAMATWA CANADA

- Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi amesema ndege aina ya Bombardier Q400 imekamatwa

- Ndege hiyo iliyokuwa iwasili nchini hivi karibuni imekamatwa na kesi ipo Mahakamani

#JFLeo

"Mhe. Rais ndege yetu aina ya Bombadier ambayo ilipaswa ifike Tanzania kutokea Canada imekamatwa na mtu yule yule ambaye aliikamata ndege yetu kule Afrika ya Kusini." - Prof. Palamagamba Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje.

===
Dar es Salaam. Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Profesa Palamagamba Kabudi amesema ndege ya Tanzania aina ya Bombardier Q400 imakamatwa nchini Canada.

Amesema aliyesababisha Bombardier kukamatwa ni Hermanus Steyn, raia wa Afrika Kusini ambaye alifungua kesi ya madai Mahakama Kuu nchini Afrika Kusini akidai fidia ya dola 33 milioni.

Kesi hiyo ilisababisha Mahakama hiyo kuizuia ndege ya Tanzania aina ya Airbus A220-300 kuondoka nchini humo Agosti, 2019.

Steyn, anadai fidia baada ya mali zake kutaifishwa na Serikali ya Tanzania mwaka 1980. Hata hivyo, Septemba 3, 2019 mahakama hiyo iliamuru ndege hiyo iliyokuwa imezuiwa katika uwanja wa ndege wa Oliver Tambo kuachiwa baada ya Serikali kushinda kesi bila kutoa fedha yoyote.

Akizungumza leo Jumamosi Novemba 23, 2019 mjini Dodoma katika hafla ya kuapishwa kwa mabalozi, Profesa Kabudi amesema, “ndege imekamatwa na kesi ipo mahakamani. Aliyesababisha ni yuleyule (Steyn) aliyesababisha ndege yetu kuzuiwa Afrika Kusini.”

Profesa Kabudi amesema kuendelea kwa vitendo hivyo ni hujuma za mabeberu wasiofurahishwa na maendeleo nchini.

Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na Rais wa Tanzania, John Magufuli aliyewaapisha mabalozi hao, Profesa Kabudi amesema, “tulikwenda mahakamani tukamshinda (Afrika Kusini) akakata rufaa na wiki iliyopita tukamshinda tena, huyohuyo sasa amekimbilia Canada amekamata ndege ya Bombardier Q400 ambayo ilikuwa ifike nchini.”

“Jambo linalosikitisha ndege zilizokuwa zinatoka Marekani aina ya Dreamliner mbili hazikukamatwa zimefika lakini kila ndege inapotakiwa kuondoka Canada tunashangaa hao matapeli wanajuaje na ndege zinakamatwa.”
Amesema Balozi wa Tanzania nchini Canada aliitwa nchini na kuelezwa jinsi nchi isivyofurahishwa na kukamatwa kwa ndege zake kila zinapokaribia kuja kuondoka nchini humo.

“Nimemwambia sio tu kwamba tunasikitika bali tunakasirishwa, na tunafikiri mheshimiwa rais kukushauri kama Canada inaendelea kuruhusu vitu kama hivyo sio wao peke yao wanaotengeneza ndege, hatukufanya makosa kununua ndege Canada, hata Brazil wanatengeneza ndege,” amesema Profesa Kabudi.

Amesema wameandaliwa wanasheria kwenda Canada kuipigania ndege hiyo.
Kushikiliwa kwa ndege hiyo kunarejesha kumbukumbu ya ndege nyingine ya Tanzania aina ya Bombardier Q400-8 iliyozuiwa nchini Canada mwaka 2017 kutokana na madai ya Sh87.3 bilioni zilizokuwa zikidaiwa na kampuni ya kikandarasi.

Mabalozi walioapishwa katika hafla hiyo ni Meja Jenerali Anselm Shigongo Bahati (Misri), Mohamed Abdallah Mtonga (Abu Dhabi), Jestas Abouk Nyamanga (Ubelgiji), Ali Jabir Mwadini (Saudi Arabia) na Dk Jilly Elibariki (Burundi).



Chanzo: Mwananchi
Dawa ya Deni Kulipa, ILA NASHAURI, AVAE YALE MANGUO YA JWTZ, apande nayo ndege mpaka CANADA watamuogopa na kuachilia ndege
 
Serikali hii ina hulka ya dhuluma sana hata humu nchini imewadhulumu wazabuni mbali mbali waliokuwa wakiwapa huduma na kwa bahati mbaya jinsi mwenendo wa sheria ulivyowekwa kando kipindi hiki, hawana namna inabidi tu wafirisiwe na mabenki.

Kwa kadri serikali hii itakavyozidi kudhulumu hata haki za raia wake ndivyo watu watakavyozidi kushangilia taarifa kama hizi.

Inatakiwa wajifunze kulipa madeni sio kudhulumu na kwa trend hii watu watastuka sana kupanda hizo ndege kwani hawajui ni muda gani watafaulishwa. Very pathetic indeed.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] unatia huruma balaa

Ni mtazamo wako tu. Lkn kwa mtu ambaye anajua kutumia uwezo wake wa kufikiri vizuri, lazima atajiuliza kwa nini ndege au kitu kingine chochote kikamatwe awamu hii? Je huko nyuma hakukuwa na malimbikizo ya madeni? Fikiria nje ya sanduku la uelewa wako.
 
Tundu Lisu ndio injini behind kukamatwa ndege kanada kupitia kampuni yake ya uwakili aliyoajiriwa.Yeye ndie technocrat wao wa kisheria wa kuikomoa serikali ya Tanzania wa kesi za wadai wa kimataifa wanaoidai Tanzania .Hana uzalendo mjinga mkubwa
 
Daaah hii Sasa imeshakua tabu, tumlipe tu huyu jamaa ili, ndege zetu ziwe na nafasi ya kufanya biashara kimataifa
 
Haya mabaya mengine tunajitakia wenyewe,kwa nini tusilipe madeni ya watu kulingana na makubaliano yaliyoafikiwa tuachane na usumbufu usio wa lazima?
Pia hata kuongea naye tu tuonyeshe ustaarabu kwamba tunalitambua deni Hilo na tunaandaa utaratibu wa kumlipa kidogo kidogo. Kumgeuzia kibao mtu anayedai chake hata huku uswahilini si njia sahihi sana!
 
“Jambo linalosikitisha ndege zilizokuwa zinatoka Marekani aina ya Dreamliner mbili hazikukamatwa zimefika lakini kila ndege inapotakiwa kuondoka Canada tunashangaa hao matapeli wanajuaje na ndege zinakamatwa.”
Sasa mtu muelewa anaweza kuunganisha dots ...sababu ya waziri Kamwelwe kuwaka wakati habari za Dreamliner ya Tanzania kuwasili nchini zilipovuja.
 
Back
Top Bottom