Ronal Reagan
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 5,298
- 3,059
Walishtakiwa kipindi kile kile. Hata Kabudi akiwa Waziri wakati Samia alikiri mahali kuwa Acacia wameishtaki Serikali.Mlimtukana Lissu leo mmeanza kushtakiwa na bado.
Ndio maana tunataka na kusisitiza tupate Katiba Mpya...viongozi wetu pia wamelelewa vibaya kiuongozi.
..mfumo umewadekeza sana kwa kuonea wananchi bila kuwajibika au consequences zozote.
..kwa mfano kiongozi anaweza kutoa uamuzi nyumba za wananchi zivunjwe na kusitokee athari zozote kwake. Na wananchi hawana mahali pa kwenda kulalamika kwasababu viongozi wetu wana-control kila kitu ikiwemo mahakama.
..sasa tabia hizohizo wanakwenda nazo ktk kufanya maamuzi dhidi ya wawekezaji. lakini hawa wawekezaji hawana tabia za kinyonge-nyonge kama Watanzania wa kawaida. Pia wawekezaji wana option ya kwenda kutafuta haki zao nje ya nchi ambako viongozi hawana control au mamlaka.
Hapa anazungumziwa Prof Kitila wa CCM!Wewe ni mmoja wa wengi walio mshutumu Lissu alipo waonya kuhusu kuvunja mikataba kiholela.
Mwendazake ataendelea kutia hasara nchi huko alipo.
Walimalizana na mpaka Boss wao akaja Ikulu Dar na inasemekana hao acacia wakakubali watalipa baadhi ya pesa walizotakiwa kulipa !..walifungua kesi wakati yupo hai.
..umesahau ndege zilikamatwa mara ngapi wakati Magu akiwa madarakani?
..umesahau kwamba acacia walifungua kesi wakati Magu akijadiliana na barrick?
Hahahahaha wanamkana Marehemu? Lissu alisema akaitwa kibaraka?Prof. Kitila Mkumbo anadai Tanzania imeshtakiwa na makampuni ya madini, na mashauri hayo yanapelekea serikali kuingia hasara.
Prof anadai Wasomi walitoa ushauri ili kuwafurahisha viongozi badala ya kuwaambia ukweli kuhusu madhara ya kuvunja mikataba ya kimataifa.
Nakumbuka zilikamatwa kwa madai mengine ya mikataba tofauti sio ya madini ! Lakini mimi Twendeni tu mnavyotaka maana kwa sababu ya baadhi ya watu kumchukia Magu basi mpo tayari hata kuwatetea wanyangβanyi wanaotaka kupiga pesa za Nchi bure bure tu eti kwa sababu ya kumkomoa Mwendazake !! Yule alishakwenda harudi tena ! Tuzitetee mali za Nchi angalau watoto wa masikini wa Nchi hii waweze kupata unafuu katika maisha yao. !! Yule alishaenda for good tuache ushabiki wa Simba na Yanga kwenye mali za Nchi πππNdege si zilikamatwa wakati akiwa hai madarakani, au unajizima dat?
Mkiambiwa ukweli mnasema unafiki ππUnafiki tu,unafiki tu wahuniiiii hawa
Huwa sitaki hata kuwaona wakati wowote,ni watu wa mihemko,jazba na wakurupukaji wanaotaka Kuendesha mambo Kwa Imani badala ya facts na analysis..Ujamaa na waamini wa ujamaa ni watu hatari sana, ubabe wa kijinga na hii bado upo sana.
Ila viongozi wa Africa ni watu hatari sana wakikuzunguka... bahati mbaya sana Magufuli hakuwajua wabaya wake.
Walikuwa wanamchekea huku wanafurahia perdiems..
Huna hata uwezo wa kuthibitisha dai lako hata Moja..Wajamaa ni watu wajinga sana nyie.Angalizo tu ni kwamba sasa hivi wanaoitwa wajanja watatengeneza kila aina ya kesi za michongo za kupiga pesa kweri kweri na mwisho wa siku Gari bovu ataangushiwa Mwendazake !! Tutakaoumia ni sisi tulio hai na vizazi vyetu kwa maisha kuwa magumu zaidi na zaidi!
Yule Mwendazake hata kama kweli alikosea lakini yeye alishakwenda na hatorudi tena !! Kwahiyo tusijidanganye kwamba tunamkomoa kwa kuwatetea wanaoitwa wajanja kupiga pesa kwa kuanzisha kesi za michongo michongo!! Tukumbuke mwisho wa siku mzigo wa madeni tutalipa sisi na vizazi vyetu sio Mwendazake !!
Nani alithubutu kusema haya ukiacha Lisu ambae aliponea kifo? Unajizima data si ndio? Inahitaji kujitoa mhanga na sio Kila binadamu ana huo ujasiriHeshima kwako JokaKuu . Huyu jamaa ni wale wale tu. Haya alitakiwa ayaseme wakati yanafanyika na siyo kusubiri baada ya kuona Magufuli and co hawapo kwenye ulaji ndiyo aseme. Nina uhakika hata Magufuli angekuwepo mpaka sasa asingesema haya. Jamaa nimeshamdharau sana huyu na hana tofauti na hao anaowasema.
Wewe ungeweza kumshauri Magufuli? Ulikuwa unamjua vizuri au unamuona kwenye tv? Kamuulize Mpango atakupa wasifu wake ππKwanini hakumshauri Magufuli hivi anakuja kuleta umbeya sasa??
Alipolipwa haraka haraka Symbio mabilioni nikajua tayari mchezo umeshaanza !! Wajanja kazini ! Na watu wanashabikia eti wanafikiri wanamkomoa Mwendazake π π πππSi wanapima upepo yule ameshtaki Amelipwa kwa nini mimi nisishtaki ili nilipwe wanaangalia na aina ya rais na utawala uliopo
π π π πππHuna hata uwezo wa kuthibitisha dai lako hata Moja..Wajamaa ni watu wajinga sana nyie.
Ndio madhara ya kunyima forum watu kuongea ,waliosema kuzuia watu kuongea kunahatarisha usalama wa Nchi sio wajinga..Hii nchi kila mtu husubiri hadi jambo liharibike kisha aanze kunyooshea wengine mkono...
Nilitarajia mtu kama Kitila sasa aoneshe mfano kwa kupigania katiba mpya ili isijetokea tena mtu anayeweza cheza na hatma ya taifa...
Kwa mfano Mpina anajaribu kusimamia ukweli japo amejiandaa Kwa lolote ,so tungekuwa na Wanasiasa wengi wa hivyo ujinga ujinga usingekuwepo.Na niseme wazi, hata nikitofautiana na haya aliyoyasema hapa; ambayo ni sawa na uliyoyasema wewe, haina maana kwamba kuna sehemu tunaweza kubaliana katika jambo hili hili, tukielezana vizuri.
Sasa ngoja nikukumbushe pia, kwa vile nawe umenikumbusha.
Nilishasema humu JF, kwamba hali ya nchi yetu ilivyo sasa, hasa kwa hawa tunaowaita wanasiasa wetu, ni wachache sana kati yao walio na uwezo wa kusimama na kulitetea jambo lolote wakijua kwamba kutetea huko kutawanyiama chakula chao kinachopatikana kupitia kwa ufadhiri wa chama au kiongozi mkuu wa chama.
Naomba mtu yeyote anayeweza kunipa mfano, kwa mfano wa kundi lile la akina Njeru Kasaka kwa sasa hivi, ni nani ndani ya CCM, au hata ndani ya CHADEMA?. Ni nani? Ningemhesabu Lissu katika kundi hilo, lakini hali yake ninaielewa, siwezi kumlaumu.
Na baada ya kuyasema hayo kumhusu huyu Bwana anayeongelewa hapa nikasema kuwa nipo tayari kumsikiliza yeyote anayepaza sauti kwa sasa hivi, bila kujali alifanya nini huko nyuma wakati wa Magufuli, iwe ni kwa woga wakati huo, au iwe ni kwa kutafuta fursa ya uteuzi wakati huu, nipo tayari kumsikiliza mtu huyo kama sauti yake inatetea maslahi ya waTanzania.
Kwa hiyo, kwa sasa hivi, bila kujali anachokitafuta Luhaga Mpina, nitamsikiliza, kwa sababu sisikii sauti nyingine yoyote, na zaidi zaidi kwa masikitiko makubwa hata toka kule kwa CHADEMA, ambayo tulidhani ndio mbadala ttuliobaki nao. Lakini CHADEMA imetekwa, sasa tutafanyaje.
Natumaini nimejieleza vya kutosha.
Kama nimechanganya humo ndani, naomba msamaha, kwa sababu nilitiririka tu, sikurudi nyuma kuhariri chochote.
Nivuteni na miye nije upande wenu kuunga mkono juhudi ! Pengine na mimi nitakuwa mjanja !!Huna hata uwezo wa kuthibitisha dai lako hata Moja..Wajamaa ni watu wajinga sana nyie.
Unawajua Watzn vizuri? Watzn walio wengi kwenye Uongozi Ukiwa unamshauri anaona wewe ni threat kwake Kwa hiyo hawezi fanyia kazi Ushauri wako..Mada za aina hii na hasa wanaozileta zinashangaza kwelikweli.
Huyu Kitila Mkumbo mwenyewe, si anajihesabu kuwa "msomi"? Kaingia serikalini na kawa hadi Waziri, na huko kwenye upinzani yote aliyohusika nayo yanajulikana.
Sasa yeye anayo tofauti ipi na hao wasomi wengine anaowazungumzia hapa.
Hapana, sikatai mada yake, ambayo ni kweli kabisa, ninachokataa ni unafiki wake.. Asijihesabu yeye kwamba anayo tofauti na hao wasomi wengine karibu katika maeneo yote wanakopatikana wasomi hao.
Kama anapokaa nje ya ulaji kidogo akili inamrudia, basi ningemshauri akae chini atazame ni kit/mambo gani hasa yanayovuruga wasomi wetu wasiweze kutimiza wajibu wao kama wasomi walio na uwezo sahihi.
Hapo atakuwa ametoa mchango muhimu kwenye taifa hili. Siyo kulalamikia mambo ambaye hata yeye ni mshiriki mkuu.
Hizi ndio akili za Kitanzania typical ujinga kwamba mtu akikosoa au kushauri jambo unadhani ni mnufaika..Nivuteni na miye nije upande wenu kuunga mkono juhudi ! Pengine na mimi nitakuwa mjanja !!
πkwa sababu ya baadhi ya watu kumchukia Magu basi mpo tayari hata kuwatetea wanyangβanyi wanaotaka kupiga pesa za Nchi bure bure tu eti kwa sababu ya kumkomoa Mwendazake !! Yule alishakwenda harudi tena !