Prof. Kitila Mkumbo: Ushauri wa Kishujaa umesababisha Tanzania ishtakiwe katika Mahakama za Kimataifa. Wasomi wetu waliwadanganya Viongozi

Prof. Kitila Mkumbo: Ushauri wa Kishujaa umesababisha Tanzania ishtakiwe katika Mahakama za Kimataifa. Wasomi wetu waliwadanganya Viongozi

Hizo kesi mbona zimeanza tokea JPM yupo hai. Na Kabudi amewahi kataa ziongelea bungeni eti kuwa akitoa kauli yoyote atahatarisha hoja za serikali kwenye kesi zile.
Abracadabra ni nyingi Ila tusishabikie wakora kuchukua advantage ya kuikamua Nchi ! After all ni kodi zetu na za watoto wetu ndizo zitakazowalipa hao jamaa. !
 
Kwahiyo Kitila naye huko bungeni anachoongea ni kuonyesha chuki yake dhidi ya Magufuli? Mbona mna uwezo mdogo wa kutetea hoja kwa kuchomekea neno mna chuki na Magufuli?!
Hapana sisi wengine tunajaribu kutahadharisha tu kwamba tusishabikie Nchi kunyonywa na Mumiani kwa kisingizio cha jamaa yule alifanya makosa !! Yapo makosa aliyafanya lakini na Wakora huwa wanachukuaga advantage ya kuingiza madudu yao !! Ndicho kitu ninachojaribu kutahadharisha Mkuu !
 
Mkuu wewe ni msomi, extractive industry kama ilivyo commodity market yoyote Ina incur volatility kwenye soko la kimataifa. Hata mauzo ya 2019 ni sababu ya soko kuwa na bei nzuri maana sisi shida yetu haikuwa uzalishaji Bali mgawanyo wa Mapato. Correlation is not causation....
View attachment 2609270
Kwenye madini tukubali au tukatae Ni kwamba “Tunapigwa sana tu “ !!
 
Hapana sisi wengine tunajaribu kutahadharisha tu kwamba tusishabikie Nchi kunyonywa na Mumiani kwa kisingizio cha jamaa yule alifanya makosa !! Yapo makosa aliyafanya lakini na Wakora huwa wanachukuaga advantage ya kuingiza madudu yao !! Ndicho kitu ninachojaribu kutahadharisha Mkuu !
Tatizo la Watanzania huwa wanarukia sentesi moja na kuipa uzito mkubwa badala ya kusoma taarifa nzima inalenga kuzungumzia kitu gani.

Nina hakika Prof. Kitila kaeleweka vibaya kwa sababu, hoja yake hakuzungumzia kesi hizi zimetokana na makosa ya kuwanyang'anya liseni Wawekezaji bali hoja yake ni Ushauri uliotolewa wakati wa kusaini mikataba ya madini miaka ya nyuma na sasa.

Makosa haya ndio yalosababisha leo tuna kesi hizo 3 akilenga uwepo wa madini adimu kabisa ambayo Marekani walienda South katika mkutano wa madini na kueleza malengo yao. Hii ni tahadhali kwetu juu ya maamuzi na Ushauri atakao pewa rais.

Akatahadhalisha zaidi kuwa madini hayo tunayo na tuwe makini sana haswa washauri wa rais wamwelekeze vema na sii kwa Ushujaa wa kibabe tukatoka na ZERO! Mfano wa wasomi wanao disco!

Hizi lawama zote kwa Prof. Kitila sijui kina Paramagamba ni mchepuko wa kuondosha hoja muhimu sana aloweka Prof. Kitila kuhusu mikataba mipya ya madini ambapo alikuwa akiunga mkono bajeti ya wizara ya Madini lakini akiongezea kuwa hizo asilimia 16 za sheria mpya tulonayo hazijatosheleza kabisa mchango wa sekta ya madini nchini.

Hizi kesi 3 kati ya 7 mnazopigia kelele ni mpango mpya wa Wawekezaji hao warudi nchini. I bet, watarudishwa kama ilivyo Symbion na Wawekezaji wengine kina IPTL walofungua kesi zao za madai ndani na nje ya nchi ili wapate kurudi katika Biashara zao.

Hakuna jipya chini ya jua..
 
Wewe ungeweza kumshauri Magufuli? Ulikuwa unamjua vizuri au unamuona kwenye tv? Kamuulize Mpango atakupa wasifu wake 😄😄
Mimi namfahamu vizuri nimefanya nae kazi nilikuwa simwogopi nilimwambia ukweli akanifukuza nchi kwa kutumia mawaziri wake hakudhubutu kuniambia mwenyewe kwa hiyo alikuwa ananiogopa kwa uwezo wangu na sio upumbavu
 
Sio kweli, kesi iihusiana na shamba la Msouth lilotaifishwa na Serikali.. Mambo mengine jamani acheni chuki zenu muwe wakweli.
Ndege tatu zimeshikiliwa na yote ni makosa ya awamu ya Magufuli tusidanganyane yeye alifikiri akivunja mikataba atafanikiwa kwa ujinga wake kwa hiyo alietia wananchi hasara ni Magufuli na mawaziri wake
 
Mimi namfahamu vizuri nimefanya nae kazi nilikuwa simwogopi nilimwambia ukweli akanifukuza nchi kwa kutumia mawaziri wake hakudhubutu kuniambia mwenyewe kwa hiyo alikuwa ananiogopa kwa uwezo wangu na sio upumbavu
Sasa ulikuwa wapi usimwambie Hadi unasubiria mambo inaharibika?
 
Mimi namfahamu vizuri nimefanya nae kazi nilikuwa simwogopi nilimwambia ukweli akanifukuza nchi kwa kutumia mawaziri wake hakudhubutu kuniambia mwenyewe kwa hiyo alikuwa ananiogopa kwa uwezo wangu na sio upumbavu
Hata Mpango namfahamu tulikuwa nae World bank muulize
 
Mruma na Osoro ndo walisema Tumeibiwa na ACACIA zaidi ya sh Trilion 400
Walilazimishwa waseme hivyo. Niliwahi kuongea nao wote wawili kwa nyakati tofauti Magufuli akiwa hai, nilitaka kujua kama kweli walichokiandika ndicho wanachokiamini. Wote walinijibu kuashiria walilazimishwa. Wakasema, "hivi unamwelewa huyu bwana? Watu wake waliotumwa kwetu walituambia kuwa Rais hataki kusikia neno kuwa hatujaibiwa. Ikabidi report iwe doctored kukidhi matakwa ya Rais.
 
Sasa ulikuwa wapi usimwambie Hadi unasubiria mambo inaharibika?
Hivi nchi gani inaendeshwa na mtu mmoja na ndugu zake na marafiki wake na mahawara wake hiyo ni nchi au ni kichaka cha ujambazi??Alafu mnasema kuna mbunge na mahakama huru??
 
..huko ICSID hatuwakilishwi na mawakili toka hapa Tz.

..kuna taratibu zake za kumpata msuluhishi ambaye anaaminika na kukubalika na pande zote kusikiliza shauri.

..ofisi ya mwanasheria mkuu kazi yake ni kutoa ushirikiano na supporting evidence / documents kutetea upande wa Tanzania.

..tatizo huwa linaanza hapa nyumbani kwa viongozi wetu kujifanya wababe na kukiuka mikataba waliyosaini.

..Matokeo ya ubabe wa viongozi wetu ni kushindwa ktk mashauri mengi yanayopelekwa ICSID.

..Kama tunataka tusipigwe basi tuhakikishe tunatengeneza mikataba inayotulinda, na baada ya hapo tuiheshimu.

..Jambo lingine, ambalo ni gumu, na serikali inaogopa kulifanya, ni kujitoa ktk mikataba inayoelekeza kwamba migogoro na wawekezaji itakwenda ICSID, au uwekezaji hapa nchini italindwa kupitia MIGA. Hali hiyo itaondoa uwezekano wa Tanzania kushtakiwa huko nje.
Na ukojitoa, hakuna mwekezaji atakayekuja Tanzania kwa sababu mahakama zetu hizi za uzalendo wa Rais, haziaminiki.
 
Walilazimishwa waseme hivyo. Niliwahi kuongea nao wote wawili kwa nyakati tofauti Magufuli akiwa hai, nilitaka kujua kama kweli walichokiandika ndicho wanachokiamini. Wote walinijibu kuashiria walilazimishwa. Wakasema, "hivi unamwelewa huyu bwana? Watu wake waliotumwa kwetu walituambia kuwa Rais hataki kusikia neno kuwa hatujaibiwa. Ikabidi report iwe doctored kukidhi matakwa ya Rais.
Aisee!. Duh
 
Nina hakika Prof. Kitila kaeleweka vibaya kwa sababu, hoja yake hakuzungumzia kesi hizi zimetokana na makosa ya kuwanyang'anya liseni Wawekezaji bali hoja yake ni Ushauri uliotolewa wakati wa kusaini mikataba ya madini miaka ya nyuma na sasa.
Naanza kuhisi hii account ipo hacked!! there's so much misinformation recently!! Kitila was very clear kwamba walishauri leseni zifutwe kwa kuwapa matumaini viongozi wa nchi kuwa "hakuna repurcussions zozote huko mbele".

Ni ajabu sana kauli hizi za spinning kutolewa na great thinker wa calibre Yako.
 
Amesoma kesi zilizopo huko kwenye mahakama za usulihishi na kuishia hapo tu. Angeelezea na sababu za hizo leseni kufutwa pia.

Huko Nachingwea mtu kapewa leseni kafanya utafiti kidogo tu, sijui hana hela eneo kalitekeleza miaka kisa ana mining licence; alitaka serikali imuachie tu eneo kwa utashi wake huyo mwekezaji uchwara.

Hizo leseni zote zilifutwa kwa sababu ya kutoendeleza hayo maeneo, serikali ikaunda kitengo cha kupambana na hizo kesi. Mwamba kafa mmevuruga wizara ya sheria hasa ofisi ya mwanasheria mkuu iliyopewa kazi ya kuangalia kesi zote sasa hivi mnataka kulaumu calculated moves za serikali iliyopita.

Kwanza ni wanasiasa wa Tanzania tu ndio wanatabia hizi nchi zilizoendelea uwezi kukuta wanasiasa wakakosoa maswala ya national Internet either serikali ipo sawa au imekosea; wanasiasa watakuwa upande wa serikali tu kwenye maslahi ya nchi.

Nchi ina waropakaji uwezi tofautisha msomi mwenye Phd na darasa la saba.
 
Hizi kesi 3 kati ya 7 mnazopigia kelele ni mpango mpya wa Wawekezaji hao warudi nchini. I bet, watarudishwa kama ilivyo Symbion na Wawekezaji wengine kina IPTL walofungua kesi zao za madai ndani na nje ya nchi ili wapate kurudi katika Biashara zao.
Mpango upi wakati wanadai cost za damages!! kilichobakia ni utekelezaji wa uhukumu sio kupewa leseni. Yaani miaka 5 Sasa hajachimba kitu Leo alainike kisa amerejeshwa nchini? Zile cost za miaka 5 atazifidia nani?

Haya makampuni kweli ni yakinyonyaji lakini ni CCM wenyewe mmeingia hii mikataba so mnapoivunja msitumie ujuaji maana hela za hongo mmekula alafu mnakiuka makubaliano mnategemea Nini?
 
Amesoma kesi zilizopo huko kwenye mahakama za usulihishi na kuishia hapo tu. Angeelezea na sababu za hizo leseni kufutwa pia
It doesn't matter, makubaliano ni makubaliano. Kama mlijua mkataba wa kihuni kwanini mslisign? Yaani mnakubaliana alafu baadae unakuja kukiuka makubaliano. Lazima ulipe fidia!!
Huko Nachingea mtu kapewa leseni kafanya utafiti kidogo tu, sijui hana hela eneo kalitekeleza miaka kisa ana mining licence; alitaka serikali imuachie tu eneo
Kuna procedure, ni sawa na mtu hajachukua Hela benki miaka 5 waka assume amekufa kumbe yupo nje ya nchi. Siku anarudi anataka Hela zake unadhani hatoshitaki?
Hizo leseni zote zilifutwa kwa sababu ya kutoendeleza hayo maeneo, serikali ikaunda kitengo cha kupambana na hizo kesi
Zimefutwa sababu ya regulations kubadilika na ndio kesi ya msingi Iko hapo. Kwanini ulete sheria mpya alafu unataka compliance kwa leseni ambazo umeshatoa na muda wa kuhuisha bado. Mlikubaliana say standards Fulani alafu baada ya miaka 3 uje na regulations mpya zenye standards mpya then una revoke licence kisa mtu Hana vigezo vipya!! Mahakamani utaanguka tu.
 
Back
Top Bottom