Kitila Mkumbo hakuwa katika serikali muda huo?
Katika kanuni za "collective responsibility", unapokutana na uamuzi mkubwa ambao hukubaliani nao, una mambo matatu ya kufanya.
1. Unaweza kujenga ushawishi wa hoja kwamba yakataliwe katika uamuzi wa pamoja.
2. Ukishindwa kujenga ushawishi huo, unaweza kuyakubali maamuzi, na ukishayakubali, wewe mwenyewe unakuwa sehemu ya maamuzi. Lawama zozote zinazotokana na maamuzi unastahili kupata, kwa kuwa wewe ni sehemu ya maamuzi pia.
3. Kama unaona mambo haya ni mabaya sana, na huwezi kujenga ushawishi yakataliwe wala kuyakubali, unaweza kujiuzulu cheo chako utike serikalini, ili usiwe sehemu ya maamuzi hayo na uweze kuyapinga kwa uhuru nje ya serikali, au kama backbencher (mbunge asiye waziri, naibu waziri, spika, naibu spika, au AG) bungeni.
Sasa, naomba uhakiki kwa watu wenye rekodi nzuri, Dr. Kitila Mkumbo alikuwapo au hakuwapo serikalini wakati haya madudu ya makinika yanaendelea?
Kama hakuwapo serikalini, aliyapinga lini na wapi?
Kama alikuwapo serikalini, alichukua uamuzi gani kati ya maamuzi matatu hayo hapo juu?