Prof. Kitila Mkumbo: Ushauri wa Kishujaa umesababisha Tanzania ishtakiwe katika Mahakama za Kimataifa. Wasomi wetu waliwadanganya Viongozi

Lisu naye alitaka pesa za wazungu tu hakuna la maana

USSR
Ni kwa sababu huna uelewa wowote kuhusiana na masuala ya madini wala sheria.

Yale mambo yalikuwa ya kipumbavu kabisa. Ndiyo maana baadaye ikabidi wao tena wawe watu wa kuwabembeleza Barrick ili wasiabike.

Hiyo ndiyo sababu mkataba ule wa Kabudi na Barrick, ni wa hovyo kuliko hata uliokuwepo awali ambao ulikuwa unaipa Serikali mamlaka ya kuingilia baadhi ya mambo, na ilikuwa na uwezo wa kuishtaki kampuni au kukata rufaa kama Serikali haikurudhika na maamuzi ya mahakama. Leo hata kufanyike nini, mkataba unasema ni marufuku Serikali kuzuia uzalishaji au export ya dhahabu. Mahakama ya biashara ya Singapore ikiamua, ndiyo uamuzi wa mwisho, na hairuhusiwi kukata rufaa.
 
Sikiliza hoja ya kijani mwenzio ndipo uje tena, je tulishtakiwa au hatujashtakiwa?
Lissu aliwatahadhalisha mapema mkamtwanga risasi back mkaja humu ndani kudanganya umma kwamba hatujashtakiwa sasa leo mnaumbuana wenyewe. Oneni hata aibu!
Tumeshtakiwa na makampuni matatu, na hakuna hata kesi moja tuliyoshinda. Tumewabembeleza warudi, tuwape maeneo waliyokuwa wanafanyia kazi, wamegoma. Wanasubiria kukamata mali zanTanzania ziluzopo nje kama hatutawalipa kama mahakama ilivyoamuru.
 
Tazama records ya Uuzaji madini kwa Tanzania. Mwaka 2019 ndio tuliuza dhahabu nyingi tani 55 kwa mwaka, leo tumeshuka hadi tani 43 ni sababu gani ikiwa sheria ni zile zile mbovu..
 
Ujamaa na waamini wa ujamaa ni watu hatari sana, ubabe wa kijinga na hii bado upo sana.

Ila viongozi wa Africa ni watu hatari sana wakikuzunguka... bahati mbaya sana Magufuli hakuwajua wabaya wake.

Walikuwa wanamchekea huku wanafurahia perdiems..
Yeye alikuwa mbaya na hakupenda ushauri. Mshauri mkuu alikuwa musiba na bashite
 
Huyu kijani
Mi nilidhani kijani wote.
Tumeshtakiwa na makampuni matatu, na hakuna hata kesi moja tuliyoshinda. Tumewabembeleza warudi, tuwape maeneo waliyokuwa wanafanyia kazi, wamegoma. Wanasubiria kukamata mali zanTanzania ziluzopo nje kama hatutawalipa kama mahakama ilivyoamuru.
Duu hii hasara Sana kwa taifa iliyotokana na upumbavu wa washamba fulani wazee wa legacy.
 
Dah!...Kina Lissu waliongea sana kuhusu hili ila waliitwa wasaliti, kwa Sasa wasaliti ndio wanaumbuka.
 
Wabaya wa Tanzania sio makampuni ni watanzania wenyewe,umshitaki mtu ambaye bado unamhitaji kuchota Mali kwake na kuneemeka!!!mwenye kichwa kibovu ndo anaweza kuamini. Wapo watanzania nyuma ya haya makampuni .
Hujielewa wala kujitambua.

Ni kampuni gani ya nje iliyoishtaki Tanzania halafu bado ina hamu ya kuendelea kuchota mali za Tanzania? Ninyi ndio mnaojidanganya kuwa eti sisi ndiyo tuna madini mengi ya thamani kuliko nchi yoyote wakati hakuna hata aina moja ya madini ambayo sisi ndiyo tuna reserve kubwa kuliko nchi yoyote Duniani. Madini yote tuliyo nayo ni kwa kiasi kidogo kidogo.

Wajinga utawasikia tuna tanzanite sisi pekee yetu, hawajui kuwa tanzania ni saphire, yenye vanadium. Na saphire zipo kwenye mataifa mengi. Tanzanite ni gemstone, ni jiwe la mapambo ambalo hata lisipokuwepo hakuna kitachoathirika kwenye maisha ya mwanadamu.

Makampuni yote yaliyoishtaki Tanzania yalikwishaondoka nchini, yamebembelezwa yarudi, yafute kesi, yamekataa. Hapo tunatakiwa kulipa fidia approximately a trillion kwa yote matatu.
 
Ni muhimu kwanza kutambua kesi hizo 7 ni za madai gani? Kama mtakumbuka ndege yetu ilizuiwa Canada na South kwa madai ya mwaka 1974. Je, hilo lilikuwa kosa la nani?
Hizo ni kesi za makampuni kufutiwa leseni zao Retention, kwenye madini. Leseni waliwapa wenyewe halafu, siku moja kwa upumbavu tu wakatangaza kuwa eti Tanzania imefuta leseni za retention, na maeneo yote ambayo yalikuwa na Retention licenses ambayo yalikuwa yamefanyiwa utafiti wa madini na makampuni hayo ya nje, tena kwa gharama ya mamilioni ya dola, sasa yamekuwa ni mali ya Serikali.
 
Kabudi alisema hizo 191 billion Usd hazikuwa kweli ila ilikuwa mbinu ya mazungumzo.....labda kuwatia wenge wazungu ili walainike.
 
Tundu Lissu aliyeongea yote haya bila kificho na bado akaonekana msaliti wa nchi, na wakadiriki hata kuidhinisha kupigwa kwake risasi. Miaka 7 iliyopita ilikuwa migumu sana kwa wazalendo halisi wa hii nchi.

Nimeshangaa sana Kitila kuliongelea hili sasa hivi baada ya kusoma upepo wa mama, hii inaonesha hata yeye mwenyewe ni coward tu
 
Ebu zitaje zote au tupe site za madai hayo?
 
Wote wanakuwa na akili wakiwa nje ila wakiwa mle nausomi wao wanasahau kuwa wao ni watu km hao boss zao kila dk ni kusifia tu mtu asichanganyikiwe ajione yy zaidi ya mungu hata mie nakuwa juu ya mungu
 
Ina maana hata kile cheti alichopewa baada ya kazi nzuri ya tume yake alikichana au hakushiriki kwenye yale mazungumzo ?

JokaKuu zitto junior Kiranga
 
Symbion walishtaki sasa hivi wamerudi mtamboni kuzalisha Umeme na sii ajabu hata IPTL umerudi kinyemela..
 
Wewe unaongelea hisia badala ya kuongelea ukweli.

Haya ni makampuni ambayo yalikuwa na leseni za kufanya utafiti.

Utafiti ni gharama kubwa na ni risk kubwa, ndiyo maana hakuna Serikali hata moja Duniani ambayo hufanya utafiti wa madini, mafuta au gas. Ni makampuni yenye mitaji yao ndiyo hufanya kazi hiyo. Uwezekano wa kupoteza pesa kwenye utafiti ni zaidi ya 90%.

Fikiria kampuni kama ya Petra ilikuja Tanzania ilifanya utafiti wa mafuta kwa gharama ya dola milioni 760, mafuta hawakupata, wakaondoka zao. Sasa hapo wewe umenyonywa kitu gani? Au unafikiri Tanzania ina uwezo wa kutenga japo dola bilioni 10 tu kufanya utafiti wa madini, mafuta na gas?

Makampuni ya nje au ya ndani hufanya utafiti kwa kuomba tu leseni, hakuna mkataba wowote, kinachoangaliwa ni sheria tu ya madini inasemaje kwa mtu anayetaka kufanya utafiti wa madini. Akiyapata madini, anataka kuanza uchimbaji, kama mradi utakuwa na mtaji wa zaidi ya dola milioni 100 ndiyo atasaini mkataba na Serikali, na atapewa leseni ya SML.

Kama uwekezaji wako ni chini ya dola milioni 100 ataomba ML, na hakuna mkataba na Serikali, utaongozwa tu na sheria ya madini. Na hiyo haijalishi wewe ni Mtanzania au mgeni. Kama umefanya utafiti, lakini huwezi kuanza ujenzi wa mgodi mara moja, ili eneo ulilolifanyia utafiti liendelee kuwa lako wakati unajiandaa kuomba SML au ML, ukitaka utaomba Retention License. Na Retention License muda wake ni miaka mitatu tu, na hairuhusiwi kurudia kuiomba tena.

Sasa hawa wawekezaji waliomba retention licenses, tukawapa, halafu baada ya miaka miwili, eti Serikali imefuta Retention License kuwa miongoni mwa leseni zinazotolewa na Serikali, na hivyo wote waliokuwa na retention licenses, wamepoteza haki zao zote! Kweli mtu mwenye akili timamu anaweza kufanya hivyo? Ulikuwa ni ukichaa wenye madhara makubwa kwa Taifa.
 
Wabaya wa Tanzania sio makampuni ni watanzania wenyewe,umshitaki mtu ambaye bado unamhitaji kuchota Mali kwake na kuneemeka!!!mwenye kichwa kibovu ndo anaweza kuamini. Wapo watanzania nyuma ya haya makampuni .
Ninyi ndiyo wenye vichwa vya kufugia nywele tu! Kwani hao mnaowaita mabeberu walishtaki kwa kutumia masharti yaliyowekwa na nani? Mikataba waliyosaini iliandaliwa na nani?
Kwa nini kiongozi mwenye akili timamu akiuke kile alichokiwekea masharti yeye mwenyewe huku akijua madhara yake halafu anasingizia mabeberu hawatupendi au eti kuna wasaliti!

Usaliti ni Ujinga wa kiongozi wetu aliyetusababishia hasara ambayo tutailipa miaka Mingi vizazi na vizazi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…