KERO Prof. Mkenda suala la chakula Shuleni, limekuwa mateso na mzigo kwa Wazazi / Walezi, bora kipangwe kiasi fulani cha fedha kwa wote

KERO Prof. Mkenda suala la chakula Shuleni, limekuwa mateso na mzigo kwa Wazazi / Walezi, bora kipangwe kiasi fulani cha fedha kwa wote

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Naunga hoja kipangwe kiwango ,ila watoto lazime wale na asiechangia atandikwe mboko za matako.Haiwezekani mtoto toka amekula saa mbili usiku ugali na fulu aje ale tena kesho saa 11 jioni.Zaidi ya masaa 20 kafunga.Hata rafiki zangu Waislamu ambao nawakubali sana kwenye hiyo sekta wanafunga kwa takribani masaa 12.Ubwabwa oyee .
Waislam hawafungi,bali hubadili ratiba ya kula toka mchana na kuhamishiwa usiku.
Na usiku hukesha wana kula kama viwavi.

Nakubaliana na wewe serikali ifanye cost sharing.
 
Binafsi sijawahi sikia watoto wakichapwa au kufukuzwa shuleni kisa mchango wa chakula, ila nimeona watoto wakishinda njaa kutwa nzima bila msaada kisa hawajachangia chakula.
Wapo wanao chapwa na kufukuzwa, wengine wanaenda na wazazi wao kabisa kujieleza.
 
Mara kadhaa Serikali imesisitiza kuwa suala la malipo ya michango ya ziada ni suala la makubaliano kati ya Shule na Wazazi au Walezi wa Watoto, hilo linaangukia pia kwenye suala la chakula kwa Wanafunzi, ambapo utaratibu ulivyo umekuwa kero kwa wengi wetu.

Utaratibu ulivyo kwa sasa kila shule imekuwa na bei zake, mfano ni Tsh. 1,000 hadi 1,500 kila asubuhi.

- Mwanafunzi anapokuwa hana fedha ambalo siyo kosa lake bali ni ufinyu wa kipato kwa Wazazi/Walezi basi adhabu ya fimbo itamwangukia Mwanafunzi huyo na pengine kukatazwa asihudhurie masomo kisa ameshindwa kutoa fedha ya chakula.

- Kiwango cha chakula wapewacho ni kidogo kiasi kwamba kuna baadhi huwa wanapewa si zaidi ya vijiko vitatu vikubwa vya chakula.

- Upo uwezekano mkubwa kwa hasira ambazo Walimu huwa nazo huu huwa mradi wao, + wapewa tender!

- Serikali ipange kiasi sahihi ambacho Mwanafunzi atatakiwa kukilipa kisichozidi Tsh. 500/- aidha kila Mtoto awe anachangia 10,000 kwa mwezi, ili kupata stock ya Jumla kuliko hivi kwa mafungu ambayo kuna muda mambo yakiwa magumu, unamvuruga mtoto.

- Haya nimeyaona katika shule fulani, yakanisikitisha sana!,

-Vipato vya wazazi wengi havipo sawa kuna, wajane wanasomesha, mama ntilie, wabibi walioyelekezewa wajukuu na wengi tu ndani ya jamii yetu,

-Serikali ije na mwarobaini wa tatizo hili la sivyo Walimu watakuja leta maafa wa watoto wasio na hatia yoyote!

Adios amigo!
 
Hakuna anayepinga bali uwekwe utaratibu bora zaidi na affordable kwa umma wote!
-Tunazungumzia maswala ya umma, hatuzungumzii maswala ya mtu mmoja mmoja!
Suala la chakula ni wazazi ndo wenye maamuzi,ukiona kuna shule wanakula it means wazazi walikaa kakao wakapanga hyo michango yote walimu ni wapokeaji tu na kusimamia tatizo nyie huwa mnawapa mzigo tu walimu,mfano mimi ni mwalimi kwanibwazazi mkiikataa michango ya watotobwenu kula ntapungukiwa nini???
 
Kuna walimu wana mtindio wa ubongo. Sasa unamchapaje mtoto kwa kukosa hela aliyotakiwa apewe na mzazi[emoji2960]
Mfano wewe ndo mwalimu,mmekaa mkakubaliana na wazazi watoe michango,watoto umewaagiza walete michango ama wazazi waje kutoa maelezo hakuna wanachotekeleza unafanyaje!????
 
Wapo wanao chapwa na kufukuzwa, wengine wanaenda na wazazi wao kabisa kujieleza.
Ni kwa sababu wao wazazi ndo walikaaa na kupitisha hyo michango hawakulazimishwa,kama wazazi hawatakubali kutoa michango nafikiri hata walimu pia watakuwa wamepunguziwa majumu ya ziada.
 
Shida ni kuwa ya nyuma ya pazia wengi hatuyajui. Serikali inawalazimisha wakuu wa shule wahakikishe watoto wale chakula shuleni. Mkuu wa shule/mwalimu mkuu hakutani na mzazi moja kwa moja anayekutana nae ni mwanafunzi hicho ndicho kinachotokea. Viongozi wanaweka pressure kubwa kwa hawa walimu juu ya chakula shuleni nadhani suala lingebaki hiari kwa wanaotaka lkn hii ya kulazimishana ndo inapelekea madhila kwa wanafunzi. Lakini pia wanafunzi wenyewe baadhi yao wanapewa lkn hawafikishi
 
Back
Top Bottom