Prof. Mkenda, waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza 2023 kutoka shule ya msingi moja wote wamehamishiwa sekondari moja

Prof. Mkenda, waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza 2023 kutoka shule ya msingi moja wote wamehamishiwa sekondari moja

Huu Mfumo ni wa kipuuzi kabisa.

1. Watoto wenye ufauli mdogo kwenye Shule ya Msingi A wanapelekwa wote Shule ya Sekondari A. Hivyo hivyo kwa wale waliofaulu vizuri. Hivyo hivyo kwa waliofaulu. Hapa Sasa tunafanya baadhi ya Shule ziwe Chini na zingine Juu kiufaulu.

2. Wanafunzi pia hatuwasaidii, kwa sababu tunahamisha tabia za Wanafunzi kutoka Shule Moja ya Msingi kwenda Shule Moja Sekondari.

3. Ufundishaji kwenye Shule za Sekondari unakuwa ni mgumu.


Mifumo hii ya kupanga Wanafunzi Shule kutoka Primary kwenda Sekondari ibadilishwe na Wanafunzi wawe wanachanganywa changanywa.
Kumbuka shule za kata hazina boarding, unapomtioa mtoto kutoka shule ya msingi mbali na huna bweni utamuweka wapi?, point kuu hii
 
Huu Mfumo ni wa kipuuzi kabisa.

1. Watoto wenye ufauli mdogo kwenye Shule ya Msingi A wanapelekwa wote Shule ya Sekondari A. Hivyo hivyo kwa wale waliofaulu vizuri. Hivyo hivyo kwa waliofaulu. Hapa Sasa tunafanya baadhi ya Shule ziwe Chini na zingine Juu kiufaulu.

2. Wanafunzi pia hatuwasaidii, kwa sababu tunahamisha tabia za Wanafunzi kutoka Shule Moja ya Msingi kwenda Shule Moja Sekondari.

3. Ufundishaji kwenye Shule za Sekondari unakuwa ni mgumu.


Mifumo hii ya kupanga Wanafunzi Shule kutoka Primary kwenda Sekondari ibadilishwe na Wanafunzi wawe wanachanganywa changanywa.
Hahahahaaaa, hizo ndio 'shule za kata'
 
Mimi labda sijaelewa.

Unakuta shule ya msingi A, ina wanafunzi 123 waliomaliza darasa la saba na wamafaulu wote kuingia kidato cha kwanza mwaka 2023.

Cha kushangaza wanafunzi wote wa hiyo shule ya msingi A wamepangiwa shule moja tu ya sekondari iliyopo kwenye hiyo kata kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2023.

Sasa kwanini wamehamishwa wote kutoka msingi moja kwenda sekondari moja iliyopo kiji hicho hicho na kata hiyo hiyo?

Kwanini wasingebakia hapo hapo msingi waendelee na kidato cha kwanza kwa shule ya msingi kuongezewa madarasa, walimu na vitendea kazi? Kulikuwa na haja gani kujenga shule jirani ya kuhamishia watoto wale wale , wa kijiji kile kile, kata ile ile?

Kulikua na haja gani kukopa mikopo ya Bank ya Dunia kujenga madarasa mapya kibao shule ya jirani na ilipo shule ya msingi kwa ajili ya kuhamishia hapo watoto?

Je Prof, huoni kuwa mitihani ya darasa la saba unaofanyika kwenda kidato cha kwanza sasa ni ya kufutwa na kuboresha shule za msingi ziwe hadi kidato cha nne?

Huoni sasa ni wakati wa shule za sekondari za kata kugeuzwa kuwa vocational training kwa ajili ya wanaomaliza kidato cha nne na kushindwa kuendelea na masomo ya kidato cha tano?
Uko na ideas nzuri ili ziweze kutumika next time safi sana
 
Sasa wakibakizwa hapo na watao ingia la kwanza wakasome wapi?

Wameamua kuwapeleka kata hiyo hiyo ili isiwape wazazi usumbufu wa gharama
Hujaona swala la kuongeza madarasa?
 
Hii ipo vyema kwasababu tena hawaendi kutafuta new friends bali akili zinaendelea zilipoishia, hapo ndo wale waliokuwa wanaongoza wanapitwa na waliokuwa mkian elimu bana sijui kwanini
 
Msingi wana muundo tofauti na secondary.
Tukianzia Lugha, nidhamu, namna ya kufundisha, umri, peer group, nk.
Hatahivyo, kuwekwa pamoja hakuna ubaya ila si vizuri kuchanganya watu wenye makundi rika tofauti katika hatua za awali.
Una point lakini haina nguvu sana........kimsingi huu ni UJASUSI unafanywa kwa jamii ya kitanzania na matokeo yake huwezi kuyaona sasa ni baada ya muda kidogo
 
Shule za Serikali ni kwa ajili ya sisi watu wa chini japo sikusoma Dumu Fagio lakini , nimefundisha Dumu fagio niseme tu wanasiasa hawana Huruma
 
Nimeshangaa kwakweli kwa hii style waliyokuja nayo, ingawa kama nadhani na upendeleo bado uko ndani yake. Mfano shule ya Mwanza Sec ambayo ni kongwe ina walimu wa kutosha tena iko katika ya mji tulitegemea wapangwe wanafunzi wa shule za karibu yake kama Bugando Primary n.k , lakn wamepangwa wanafunzi wa kutoka shule za alliance na new alliance na nyinginezo.. ambazo ziko kata ya mbali. Natamani hizi shule kongwe za katika ya mji kama Pamba na Mwanza wangekuwa wanachanganya wanafunzi kutoka sehemu mbalimbali kuliko kuchukua watoto wote wa shule moja kuwahamishia shule nyingine ya sekondari.
Kama una fedha, lolote linawezekana kwa sasa TAMISEMI NA SEKRETARIAT YA AJIRA.

Aliyeshindwa wizara ya madini kapewa TAMISEMI.
ALiyeshindwa TAMISEMI kapewa wizara ya AFYA.
 
Yote tisa kumi, uliofaulu ulikuwa zamani(ingawa wasomi wenyewe ndio tunaleta haya ya kipuuzi) ila sio sasa.

Matokeo yalikuwa yanatoka yakipambwa na neno "PASS" huku ukipangiwa Kantalamba, Galanos, Umbwe, Musoma Tech, Tosa, Malagarasi, Ihungo, Milambo, Minaki, Bihawana, Makuyuni n.k

Siku hiyo hupati usingizi, kijijini unaonekana "King" ushatusua, salamu za pongezi kama zote kutoka kwa wazee.

Kwa sasa Mfumo wetu wa Elimu unahitaji mabadiliko makubwa sana, tunapoteza muda mwingi shuleni lakini tunachokivuna haiionekani.

Nawaza tu huyu kijana wangu sijui nifanyeje aje kuibukia kwenye soccer/football ambapo ukiwa na miaka 16 tayari ushatusua maisha.

Mfumo wetu wa Elimu rubbish kabisa
 
Mimi labda sijaelewa.

Unakuta shule ya msingi A, ina wanafunzi 123 waliomaliza darasa la saba na wamafaulu wote kuingia kidato cha kwanza mwaka 2023.

Cha kushangaza wanafunzi wote wa hiyo shule ya msingi A wamepangiwa shule moja tu ya sekondari iliyopo kwenye hiyo kata kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2023.

Sasa kwanini wamehamishwa wote kutoka msingi moja kwenda sekondari moja iliyopo kiji hicho hicho na kata hiyo hiyo?

Kwanini wasingebakia hapo hapo msingi waendelee na kidato cha kwanza kwa shule ya msingi kuongezewa madarasa, walimu na vitendea kazi? Kulikuwa na haja gani kujenga shule jirani ya kuhamishia watoto wale wale , wa kijiji kile kile, kata ile ile?

Kulikua na haja gani kukopa mikopo ya Bank ya Dunia kujenga madarasa mapya kibao shule ya jirani na ilipo shule ya msingi kwa ajili ya kuhamishia hapo watoto?

Je Prof, huoni kuwa mitihani ya darasa la saba unaofanyika kwenda kidato cha kwanza sasa ni ya kufutwa na kuboresha shule za msingi ziwe hadi kidato cha nne?

Huoni sasa ni wakati wa shule za sekondari za kata kugeuzwa kuwa vocational training kwa ajili ya wanaomaliza kidato cha nne na kushindwa kuendelea na masomo ya kidato cha tano?
Mbona huo mfumo ni wa muda kidogo tangu kuanzishwa kwa shule za kata, na ikumbukwe shule za msingi ni nyingi kuliko secondari hivyo waliofaulu wote kata husika hupelekwa shule iliyopo/ zilizopo kata husika

Kuna shule teule pia za wilaya na mikoa ambapo wapo wanaopelekwa huko pia

Kuna shule teule kitaifa kama mzumbe kibaha nazo hupokea kutoka mikoa mbali mbali
 
Tatizo lingine kina tunapotoa baadhi ya hoja mfano wetu ni Dar es salaam tuu au mijini, kijijini kuna shule tuu ndani ya kata husika zipo mbali sana na sekondari ya kata, na hakuna mabweni wala daladala za kulipa 200 kama Dar, huyo mtoto umpeleke nje ya kata yake si anaacha shule maana atafikaje KM 20, 30 huko
 
Kwanini wasingebakia hapo hapo msingi waendelee na kidato cha kwanza kwa shule ya msingi kuongezewa madarasa, walimu na vitendea kazi?

Hahahaaaaa
 
Kuna shule za kata alafu kuna shule ya tarafa elewa kwanza hapo

Shule A yenye watoto idadi fulani mfano 90 wakimalaza darasa la saba watoto wachache wenye ufaulu mzuri wataenda shule za vipaji kama kibaha,bwiru,tabora Mara hawa hutoka mwanafunzi mmoja au watatu kwenye shule moja

Then wanafunzi 5-20 hawa hupangiwa shule ya tarafa ni ya vipaji pia

Alafu ndio wanafunzi waliobakia wanapangiwa shule moja ya kata ambayo ipo karibu

KWANINI SERIKALI INAFANYA HIVI
ni kwa sababu wazazi wenyewe ndio walilalamika watoto kupangiwa shule za mbali na kwao hivyo serikali ndio ikaja na huu mkakati na umesaidia saana ufaulu

Huu mkakati ulianza mwaka 2011 kama upo makini kuanzia mwaka huo wanafunzi kwenye daladala walipungua
 
Na wote wapangiwe shule moja so kama ni ujinga na tabia za kijinga wanazihamishia kwenye shule mpya waliyopangiwa
Itakifia mahala. Ukifika la Saba unaanza la Kwanza tofauti ni Jina tu, itaitwa form One iliyokuwa la kwanza.

Maisha yamekuwa zaid ya abunuasi.

Hawa viongozi wanaharibu na kutuona hatuna sisi vichaa
 
Kuna shule za kata alafu kuna shule ya tarafa elewa kwanza hapo

Shule A yenye watoto idadi fulani mfano 90 wakimalaza darasa la saba watoto wachache wenye ufaulu mzuri wataenda shule za vipaji kama kibaha,bwiru,tabora Mara hawa hutoka mwanafunzi mmoja au watatu kwenye shule moja

Then wanafunzi 5-20 hawa hupangiwa shule ya tarafa ni ya vipaji pia

Alafu ndio wanafunzi waliobakia wanapangiwa shule moja ya kata ambayo ipo karibu

KWANINI SERIKALI INAFANYA HIVI
ni kwa sababu wazazi wenyewe ndio walilalamika watoto kupangiwa shule za mbali na kwao hivyo serikali ndio ikaja na huu mkakati na umesaidia saana ufaulu

Huu mkakati ulianza mwaka 2011 kama upo makini kuanzia mwaka huo wanafunzi kwenye daladala walipungua
Mwaka huu alijafanyika hilo kwa shule nyingi mno..kwa mfano wanafunzi wote wa Almuntazir girls wamehamishiwa form one Jangwani,wanafunzi wotee waliofanya mtihani St Augustin primary wamehamishiwa buguruni moto sekondary ukiangalia aina hiyo ya selection haiko sahihi kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom