Prof. Mkumbo: Katiba iliyopo sasa sio ya Demokrasia ya Vyama Vingi

Prof. Mkumbo: Katiba iliyopo sasa sio ya Demokrasia ya Vyama Vingi

Narudia, Mayalla husaidia upinzani Ili wajitambue na wapambane zaidi.

Bt upinzani humuweka P ktk kundi la maadui.

Itafahamika tu.
Mkuu Rabbon , mimi ni kada bonafide genuine ambaye ni mkweli na mpenda haki, wapenda bakit wote tumatanda CCM ishinde kwa haki na nchi iwe na a healthy opposition.
P
 
Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Prof. Kitila Mkumbo amesema Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotumika kwa sasa ni ya demokrasia ya Chama kimoja.

Amesema hali hiyo imechangia kuwa na demokrasia dumavu ambayo inapelekea kuchelewa kwa maendeleo, ambapo amedai kuwa kuna uhusiano wa demokrasia bora na maendeleo

Pia ameshauri kuwa Katiba mpya ni muhimu ili kuwezesha demokrasia ya vingi kustawi ambayo itawezesha wananchi kushiriki ipasavyo.

Amesema kuwa kwa mazingira ya demokrasia ya sasa ni rahisi kutabilika tofauti na ilivyo kwa Kenya, ametoa mfano kuwa ni rahisi kutabili kuwa CCM itashinda uchaguzi 2025 kwenye nafasi ya Urais, amedai kuwa hiyo inachangiwa na takwimu za matokeo ya Urais kwenye chaguzi zilizopita.

Prof. Kitila Mkumbo ameyasema hayo leo Septemba 15, 2022 katika mdahalo ambao umeandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Nchini (LHRC) kwa kushirikiana na wadau wengine, katika siku ya demokrasia duniani ambayo imekuwa ikiadhimishwa kila mwaka.
Kwani Prof Mkandaa anasemaje
 
Narudia, Mayalla husaidia upinzani Ili wajitambue na wapambane zaidi.

Bt upinzani humuweka P ktk kundi la maadui.

Itafahamika tu.
Sasa hapo upinzani wasichoelewa ni nini? We naye una akili ndogo sana.
 
Mkuu Rabbon , mimi ni kada bonafide genuine ambaye ni mkweli na mpenda haki, wapenda bakit wote tumatanda CCM ishinde kwa haki na nchi iwe na a healthy opposition.
P
Sasa Paskal maandiko yako yanabadilisha huo ukweli? Mbona kila kitu kinajulikana
.

Ukweli umeusema ccm sio chama cha siasa. Ni chama dola kinashinda kwa wizi.
 
Maneno yake nayaunga mkono.
Niabu kubwa sana kwa mtu kama Prof kuwa na maneno ya kutapatapa yaani yasiyoaminika mbele ya jamii yetu.
Kama kaona ni kipindi cha kuirudisha heshima yake ni vizuri sana tukumbuke prof ni elimu kubwa ni mbaya kwa prof kudhiakiwa kwa ajili ya Cheo cha kuteuliwa ambayo siyo ya kudumu
Hata kama ni mdangaji wa kisiasa lakini kasema ukweli
 
Kutakuja kutokee changamoto ya maelewano miongoni mwa watu wa tume ya uchaguzi, siku zijazo. Hii itatokana na utaratibu mbaya wa the so called, Demokrasia.
Sio rahisi ccm iko tayari kuwahonga hata rasilimali za Taifa ili waendelee kuwa sapota wao bila mfarakano wowote kati yao.

Mifarakano hutokea pale wanapodhulmiana kwenye ulaji
 
Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Prof. Kitila Mkumbo amesema Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotumika kwa sasa ni ya demokrasia ya Chama kimoja.

Amesema hali hiyo imechangia kuwa na demokrasia dumavu ambayo inapelekea kuchelewa kwa maendeleo, ambapo amedai kuwa kuna uhusiano wa demokrasia bora na maendeleo

Pia ameshauri kuwa Katiba mpya ni muhimu ili kuwezesha demokrasia ya vingi kustawi ambayo itawezesha wananchi kushiriki ipasavyo.

Amesema kuwa kwa mazingira ya demokrasia ya sasa ni rahisi kutabilika tofauti na ilivyo kwa Kenya, ametoa mfano kuwa ni rahisi kutabili kuwa CCM itashinda uchaguzi 2025 kwenye nafasi ya Urais, amedai kuwa hiyo inachangiwa na takwimu za matokeo ya Urais kwenye chaguzi zilizopita.

Prof. Kitila Mkumbo ameyasema hayo leo Septemba 15, 2022 katika mdahalo ambao umeandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Nchini (LHRC) kwa kushirikiana na wadau wengine, katika siku ya demokrasia duniani ambayo imekuwa ikiadhimishwa kila mwaka.
Prof Mkumbo ni mwanaharakati!! Aliingizwa CCM ili kumfumba mdomo!! Baada ya kifumba mdomo (uteuzi) kudondoka chini naona analianzisha!! Huyu ni kama alivyo Polepole!! Alilianzisha la wahuni baada ya kifumba (uteuzi) mdomo kudondoka!! Aliporudishiwa kifumba mdomo (uteuzi) sasa hana habari na wahuni! anaendelea kula kuku kwa mrija huko Malawi!!
 
Baada ya kutemeshwa meza kuu, sasa akili ndio zimeanza kumrudia gwiji huyu wa siasa na zitamkaa vizuri kabisa 2025 baada ya kutemeshwa rasmi jimbo la Ubungo na kulazimika au kurejea darasani kushika chaki, au kujiunga na akina sisi huku kujiweni.

Katiba inatoa haki ya kila Mtanzania kupiga kura kuchagua kiongozi na kuomba kuchaguliwa. Haki ya kuchaguliwa imeporwa na shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa!. Hii ni dhulma kubwa ambayo inatugharimu sana kupitia karma!.

Uchaguzi wetu ni uchaguzi kiini macho kugombea kisu cha makali kuwili, ambapo chama dola kimeshika mpini na vyama makapuku wakishikishwa upande wa makali kuwili!. CCM sio tu ni chama tawala, bali pia ni chama Dola!
P

CCM kwa sasa sio chama cha siasa bali ni kikundi cha dola kilichojivika koti la chama cha siasa. Huyo Kitila anaongea ukweli sasa kwakuwa hayuko kwenye ulaji, na pia aibu ya uchaguzi bora wa Kenya juzi ndio dhamira inamsuta.
 
Kabudi anasemaje kuhusu katiba mpya?
 
Nakubaliana naye katika mengi, ila kwenye ishu ya CCM kushinea nafasi ya urais mwaka 2025 hilo sahau, labda waibe kura!
 
Sikubaliani nae.

Katiba iliyopo sasa sio mbaya kihivyo, tatizo haifuatwi, kama viongozi wetu wangekuwa wanaifuata hii Katiba iliyopo kama ilivyo, hasa kuhusu masuala ya kidemokrasia, kama mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa, hali isingekuwa mbaya kama ilivyo sasa.

Hata hii tume ya uchaguzi, japo Rais ambaye ni mwenyekiti wa chama cha siasa anateua mwenyekiti wake, lakini hakuna popote huyu mwenyekiti na wajumbe wake wameambiwa na Katiba iliyopo waipendelee CCM, ni viherehere vyao tu, sasa kama watandelea na hii tabia ya kiherehere basi hata Katiba Mpya nayo ikija, haitakuja na suluhisho la kudumu.

Ningemuona Kitila ana hoja kama angeanza kwa kuwaambia CCM wenzake kwanza waifuate Katiba iliyopo, baada ya hapo, ndio tuangalie mapungufu yatakayojitokeza ili yakafanyiwe kazi kwenye hiyo Katiba Mpya, lakini kukimbilia Katiba Mpya wakati iliyopo mmeshindwa kuiheshimu ni ujinga.
Ukiona kitu hakifuatwi jua kina mapungufu.Katiba hii iliyopo ingekua nzuri isingetoa hisani kwa mtu kuifuatwa bali lingekua ni takwa kuifuata.Hiyo tume inafanya huo ujinga kwasababu inajua maamuzi yake niyamwisho nailo linaanzia kuanzia upatikanaji wake.nahilo linatokana na katiba yenyewe kutoa huo mwanya.kwahiyo hakuna haja yakujadili kitu chenye mapungufu ambayo tayari yameshaonekana wakati una uwezo na akili zakutengeneza kingine bora.katiba inatakiwa ijisimamie yenyewe sio hadi mtu anapojisikia au kukumbushwa.
 
Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Prof. Kitila Mkumbo amesema Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotumika kwa sasa ni ya demokrasia ya Chama kimoja.

Amesema hali hiyo imechangia kuwa na demokrasia dumavu ambayo inapelekea kuchelewa kwa maendeleo, ambapo amedai kuwa kuna uhusiano wa demokrasia bora na maendeleo

Pia ameshauri kuwa Katiba mpya ni muhimu ili kuwezesha demokrasia ya vingi kustawi ambayo itawezesha wananchi kushiriki ipasavyo.

Amesema kuwa kwa mazingira ya demokrasia ya sasa ni rahisi kutabilika tofauti na ilivyo kwa Kenya, ametoa mfano kuwa ni rahisi kutabili kuwa CCM itashinda uchaguzi 2025 kwenye nafasi ya Urais, amedai kuwa hiyo inachangiwa na takwimu za matokeo ya Urais kwenye chaguzi zilizopita.

Prof. Kitila Mkumbo ameyasema hayo leo Septemba 15, 2022 katika mdahalo ambao umeandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Nchini (LHRC) kwa kushirikiana na wadau wengine, katika siku ya demokrasia duniani ambayo imekuwa ikiadhimishwa kila mwaka.
Soma Tena Nzie ya Mana Donnie Charlie
 
This guy is an hypocrite......Sukumq Ghang sabotaging the Madame President
 
Tatizo la wadai katiba mpya na demokrasia nchini,mtu katoa mawazo sahihi kabisa lakini Cha ajabu badala ya kuungwa mkono na kupush ajenda ashambuliwa kwa matusi Tena.
 
Back
Top Bottom