Prof. Mussa Assad: Baada ya kuondolewa nafasi yangu kwa dhulma, niliendelea kufanya Dua, na Mungu amejibu

Prof. Mussa Assad: Baada ya kuondolewa nafasi yangu kwa dhulma, niliendelea kufanya Dua, na Mungu amejibu

Huyu anawashwa kweli, amejaa chuki tu. JPM alikuwa sahihi kula kichwa, hauwezi kuwa na mtumishi roporopo namna hii.
Babu yako,baba yako au mjomba wako amewahi kuwa CAG? Au walau kuwa Mwalimu wa chuo kikuu cha Dar es salaam? Una bahati mbaya sana wahenga wako si roporopo lakini hawakufika hata robot ya huyu bwana pamoja kwamba wao ni wameokoka
 
Hivi huyu mzee hajalipwa stahiki zake?

Naona hadi leo moyo wake umekuwa ukiweweseka kwa cheo cha kuteuliwa...
 
SOma vizuri sheria ya CAG na Katiba ndipo ulewe. Zitto anadanganya kuwa hukumu ilikuwa dhidi ya Magufuli klumuondoa CAG kinyume cha Katiba lakini iwapo ulisoma hukumu ile ya mahakama yenyewe ilsema kuwa sheria ya Bunge iliyoweka kifungu kuwa CAG atafanya kazi kwa vipindi vya miaka mitano mitano ndiyo inayokiuka Katiba. Huyu jamaa aliondolewa kwa kufuata sheria hiyo ya Bunge. Na ukisoma vizuri sana utagundua kuwa Katiba ndiyo iliyoandikwa vibaya kwani inasema CAG atafanya kazi hadi afikie miaka 60 ila sheria hiyo ya Bunge iliyotumika kumuondoa yenyewe iliongeza umri huo hadi miaka 65. Kosa la Katiba ni kuwa iwapo mtu atateuliwa kuwa CAG akiwa na miaka tuseme 31 basi atalazimika kuendelea kuwa CAG kwa miaka mingine 30 au 35 kwa mujibu wa sheria hiyo ya Bunge, na sidhani kama hilo ndilo lililokuwa lengo la Katiba hiyo. Hakuna CAG ambaye amewahi kutumika zaidi ya vipindi viwili vya miaka mitano mitano vilivyowekwa na sheria hiyo hiyo ya Bunge; yeye alitumika kipindi kimoja tu ambayo pia ilikuwa chini ya sheria hiyo kwani ilikuwa inaruhusu Rais kumteua tena au kuteua CAG mwingine, ambapo rais aliamua kuteua CAG mwingine.
Kwani hili la CAG ilikuwa mara yake ya kwanza kuvunja katiba na sheria za nchi? Mbona ilikuwa ni kawaida yake tu? Isitoshe, kabla ya kumuondoa CAG alionyesha wazi kukerwa naye. Tunajua kuwa alijaribu hata kwa kutumia Bunge lakini ikashindikana. Na sababu ya kukerwa na CAG ni matumizi ya fedha yasiyozingatia bajeti na taratibu pamoja na hulka ya CAG kujiamini na kutaka kufanya kazi yake kwa uhuru na weledi. Kama Rais bila shaka yoyote alijua kuwa sheria yoyote inayopingana na katiba ni batili na hapaswi kuitumia kufanya uamuzi. Haiyumkiniki pia kuwa hakupata ushauri dhidi ya kumuondoa CAG kwa kutumia sheria hiyo lakini akataa kusikiliza kwa jinsi alivyokuwa na "inflated ego" na jinsi alivyokuwa anahaha kuondondona na kikwazo hicho.
 
Kwamba kalipwa baada ya kifo cha Magu na yeye karudishwa nafasi yake?

Tatizo udini ukikuzidi sana hata kama ni msomi kwa kiwango gani huondoa maarifa na busara.

Yeye angekuwa wa maana dunia ingekuwa imeshamchukua na kumtumia kama kina Mwelle Malecela.

Ana mapungufu mno kuliko anavyodhania yupo sahihi. Kiislam huwa wanaamini kila ridhki hupangwa na mwenyezi Mungu ndio maana huwa wanasema kila mtoto anazaliwa na ridhki yake.

Huyu ridhki zake za visasi na husda. Atabaki hapo sana tu.
Kalipwa maana hata aliyemtisha atapelekwa hata na pingu naye yalimkuta ya kumkuta.
 
Kwamba ukishakuwa na wadhifa fulani serikalini hairuhusiwi kusitishwa?

Huyo Mzee asijitoe fahamu..

Hakuna majibu yeyote aliyoyapata,,ameamua kwenda na beat.
 
Ni kitendo kibaya sana kuingilia Uhuru wa C.A.G katika utendaji kazi wake na kutoa taarifa.

Ndiyo maana hatumbuliki kirahisi hadi vikao vya jopo la majaji wa Jumuia ya Madola wajadiliane na kuthibitisha kuwa kukiuka kanuni au kuwa mkosa ndipo anaweza kuondolewa kwa nafasi yake.
 
Kumsakama CAG Kwa namna moja ama nyingine huleta tafsiri mbaya sana na mashaka makubwa kuhusu usalama wa rasilimali za Umma.

Hii inahitajika ufahamu kuweza kuelewa.
 
mwislamu safi mcha Mungu huwezi ukamuona ana sigida. wenye sigida wengi ni wanafiki, wana chuki, roho mbaya na ni wakatili sana. Hata hivyo mbona waarabu hizo sigida hawana? Hata imamu/sheikh mkuu wa maka hana, inakuwaje hawa waswahili wanazo, wanajisugua makusudi?

Uko sahihi kabisa, Nimetembelea mara kadhaa uarabuni, lkn sijawahi ona muarabu akiwa sigida.
Ni hawa tu kina asad ndiyo sijui wameitoa wapi.
 
Ulishawahi kufundishwa na Prof maishani mwako? Au hapo mwalimu Nyerere hakuna maprof?

Shida yako wewe unafikiri kila profesa ni msomi. Kuna wengine hawajaelimika, illiterate professors. Na tunawaona kwa matendo yao, kama hivi anavyojidhihirisha asad.
 
Kwamba kalipwa baada ya kifo cha Magu na yeye karudishwa nafasi yake?

Tatizo udini ukikuzidi sana hata kama ni msomi kwa kiwango gani huondoa maarifa na busara.

Yeye angekuwa wa maana dunia ingekuwa imeshamchukua na kumtumia kama kina Mwelle Malecela.

Ana mapungufu mno kuliko anavyodhania yupo sahihi. Kiislam huwa wanaamini kila ridhki hupangwa na mwenyezi Mungu ndio maana huwa wanasema kila mtoto anazaliwa na ridhki yake.

Huyu ridhki zake za visasi na husda. Atabaki hapo sana tu.
Yaani we jamaa hujielewi kweli, je kama anamsema JOB? kwani job yupo kwenye nafasi yake hadi leo? Pia kwa taarifa yako dunia ilishamchukua kitambo uliza anawafanyia nini SCANDINAVIA COUNTRIES
 
Profesa gani huyu anayelalama kwa ajili ya cheo cha kuteuliwa kwa miaka mitano sasa; inaonekana atalalama hadi kaburini. Ni kama vile alikatishwa mipango yake ya mbeleni kwenye cheo hicho kabla hajaanza kuitekeleza. Labda alikuwa hajaanza kula vya kutosha akanyang'anywa tonge ghafla. Angesoma sheria zote za bunge akawa anazijua. ALitolewa madarakanai kwa kufuata sheria ya Bunge. Mahakama ilisema kuwa sheria hiyo ya Bunge haikuwa halali, lakini ndiyo sheria iliyokuwepo wakati anasimamishwa. Angekuwa na busara ya kutosha angepinga sheria ile kabla haijafanya kazi dhidi yake badala ya kumlaumu mtu aliyeitumia dhidi yake.
Niko upande wa Profesa lakini comment yako hii ni best dhidi yetu, uko sahihi
 
Back
Top Bottom